Inaendelea sehemu ya 03
********************************************
Basi wakati nikiwa pale kitandani nawaza mariamu alipomaliza kufanya usafi na kupika akanikaribisha chakula kiukweli ni mwanamke anaejua kupenda sana akaniambia mume wangu mbona kama leo una mawazo sana kuna nini??
Nikamjibu hapana nipo kawaida basi tukala chakula ulikuwa wali na samaki lakini mariamu muda mwingi alikuwa akiniangalia sana anasema leo sina raha nawaza nini kwani? Wakati tupo tunakula ikabidi nimuulize mariamu hivi kwanini ulinidanganya?
Swali lililompa mshangao akanijibu nimekudanganya nini?
Nikamwambia ww unakaa wapi maana unajua sielewi jana nimekutana na asha nimemuuliza kuhusu ww amesema hakujui ww unakaa wapi niambie tu ukweli?
Mariamu akacheka sana akasema nikwambie kitu naona hauniamini haya leo nataka nikupeleke kwetu halafu asha alikudanganya sijui anakutaka nini ?
Nikamjibu basi tukishamaliza kula leo nataka nipajue kwenu basi tulipomaliza kula tukanya sex na mariamu kiukweli ni mwanamke flan mtamu sana na anaejua mapenzi alikuwa akinipa upendo wa kutosha mno na alipenda kuakikisha namaliza haja zangu zote then tulipomaliza basi tukaenda kuoga leo kwa mara ya kwanza ndio naiona sura ya mariamu tukiwa bafuni ni mtoto mmoja mrembo sana alikuwa ana nywele za kiarabu ana nywele ndefu mno kiukweli ni mrembo haswa hadi nikawa najisemea kimoyoni huyu mwanamke mbona mzuri kupindukia,
Basi baada ya kuoga nae akavaa hijabu lake na nguo zake na mimi nikavaa tukaondoka kuanza safari ya kwenda kwa kina mariamu sasa nilipofika njiani nikakutana na wanangu wakawa wananiambia kaka mbona spidi spidi unaenda wapi hapo nipo na mariamu nikawaambia npo na shemeji yenu hapa namsindikiza kwake? Wakasema ww siku hizi umeanza kuvuta bangi nn mbona upo pekeeako shemeji yupo wapi? Swali lililonishtua kumbe mariamu alikuwa hawamuoni wao mimi ndie ninaemuona tu lakini cha ajabu eti fikra ikaja kichwani kuwa labda washikaji wananitania tu nikawajibu haya bhana nikamvuta mariamu na kuanza kwenda nae sasa baada ya mwendo wa mda mrefu tukafika hadi pale pale kwa kina asha kwa bibi kazikale sasa cha ajabu asha alisema hamjui mariamu akatoka ndani na kumkumbatia mariamu na kumwambia dada kumbe ulienda kwa huyu bibi alikutafuta sana,
Ghafla mariamu akaniuliza sasa umeniamini???
Wakuu nitaendelea kesho