Jiji la Mwanza halina taa za barabarani

Jiji la Mwanza halina taa za barabarani

Mimi mtoa post siyo CHADEMA wala sina chama chochote ila penye ukweli lazima tuseme. Pitia post zangu zote uone kama mimi ni CHADEMA
Chadema ni wazee wa kutengeneza uwongo, wajiandae October
 
Acheni propaganda zilizokufa wakuu, barabara ya kutoka sabasaba kwenda hadi Buswelu ni ya lami na inawaka taa mwanzo mwisho, barabara ya kutokea Pasiansi kwenda hadi Nyakato Buzuruga kupitia Kiloleli Nyasaka maduka 9, Nyasaka center kote huko taa zinawaka, barabara yote kutokea mjini kati kuelekea Igoma taa zinawaka, sasa wewe mleta unaongelea Mwanza ya wapi
Barabara ya kutoka nyegezi kona hadi malimbe ina taa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inasikitisha kuona kwamba Mwanza jiji la pili kwa ukubwa nchini Tanzania halina taa za barabarani mitaa yote, katikati ya Jiji ni giza tupu, barabara zote kuu tatu za kutoka na kuingia Jijini (Nyerere, Kenyatta na ile iendayo uwanja wa ndege) zote ni giza tupu.

Inafikia mtu unajiuliza hivi uongozi wa Jiji hili na ule wa Manspaa ya Ilemela unakwama wapi? Mbona miji midogo kama Geita na Kahama kwa sasa sina taa za barabarani?

Kwa kweli ni aibu kwa Jiji kama hili kukosa taa hizi hata maeneo nyeti kama stendi kuu ya mabasi Nyegezi n.k. Nadhani wakati umefika sasa wa viongozi wa mkoa, jiji na Manspaa ya Ilemela kuondoa kero hii.
Unaongelea mwanza ipi ndugu, au kuna mwanza ingine sio ninayoijua
 
Wewe usidanganye watu. Barabara ya Kutoka mjini kwenda Igoma ni giza tupu. Aidha katikati ya Jiji ni giza totolo, wewe unakaa Mwanza ipi ? Kawadanganye wasioijua Mwanza.
So barabara moja ikiwa giza ndo mwanza hakuna taa. Noncense kabisa. Halafu ile barabara ina taa nafikiri zinaishia nyakato pale sheli ama veta sijachunguza
 
Mleta mada inaonekana hauna muda mrefu tangu uingie jijini, hilo tatizo umechelewa sana kuling'amua.
 
Mleta mada inaonekana hauna muda mrefu tangu uingie jijini, hilo tatizo umechelewa sana kuling'amua.
Nimezaliwa Mwanza na sasa ninaishi Mwanza. Haya sema jingine mkuu
 
Nimezaliwa Mwanza na sasa ninaishi Mwanza. Haya sema jingine mkuu
"Nadhani wakati umefika sasa wa viongozi wa mkoa, jiji na Manspaa ya Ilemela kuondoa kero hii". Napata mashaka na hii kauli yako kwa nini umeitaja Ilemela kwa upekee?
 
"Nadhani wakati umefika sasa wa viongozi wa mkoa, jiji na Manspaa ya Ilemela kuondoa kero hii". Napata mashaka na hii kauli yako kwa nini umeitaja Ilemela kwa upekee?
Jiji la Mwanza ni wilaya ya Nyamagana. Wilaya ya Ilemela ni Manspaa ya Ilemela, hivi ndivyo TAMISEMI ilivyogawa
 
Back
Top Bottom