Jifunze TENSES hapa

" I went to collect the children to the Dar express bus service but they don't their in that bus "

No hivo bro

Sent using Jamii Forums mobile app
' They don't their ina that bus' hapa ndio unamaanisha hawakuwepo kwenye bus?
vipi kuhusu matumizi ya "article" hasa hii ya "The",
mimi huwa inanipa shida wakati mwingine...

Kwa mfano hapa "I went to collect the children..." je ni sahihi kuwepo kwa article kabla ya children?
 
vipi kuhusu matumizi ya "article" hasa hii ya "The",
mimi huwa inanipa shida wakati mwingine...

Kwa mfano hapa "I went to collect the children..." je ni sahihi kuwepo kwa article kabla ya children?
Nadhani haikutakiwa kuwepo ila inategemea na mazingira. Kama mzungumzaji alikuwa anafanya reference kwa maana kwamba msikilizaji tayari alikuwa anajua kuhusu hao watoto au walikuwa tayari wameshawazungumzia, matumizi ya 'the' ni sahihi
 
Nadhani haikutakiwa kuwepo ila inategemea na mazingira. Kama mzungumzaji alikuwa anafanya reference kwa maana kwamba msikilizaji tayari alikuwa anajua kuhusu hao watoto au walikuwa tayari wameshawazungumzia, matumizi ya 'the' ni sahihi
oooh okay,

pia ni muhimu tukijifunza matumizi ya hizi article nyingine pia "a" na "an"

mimi zimenipa shida sana kwenye matumizi kwa mfano nilikua najua tunatumia "article -a" kabla ya nouns/adjectives ambazo zinaanza na consonat...

mfano: she gave me a book.

lkn kumbe pia wanaangalia na jinsi inavyosound hiyo consonant....

mfano: she need to study for "a hour" before she go to lunch.

unaona jinsi hiyo article ilivyokiwa haiendani na hiyo "hour" japo inaanza na Consonant....wataalam sasa wanasema hiyo "hour" sauti yake ukiitamka inasikika "our" ambayo yenyewe inaanza na Vowel...
kwahivyo hapo article sahihi ni "an"

sahihi: she need to study for an hour before she go to lunch.

kumbe sasa tunaona matumizi ya article "a" na "an" zinategemea na suati ya nouns/adjectives,

a - consonat sound
an - vowel sound

hiki ndicho kwenye kiingereza nilijifunza na nikafurahi kuelewa japo kidogo,

ila hii article ya "The" bado sijaridhika...nahitaji kujifunza zaidi.
 
oooh okay,

pia ni muhimu tukijifunza matumizi ya hizi article nyingine pia "a" na "an"

mimi zimenipa shida sana kwenye matumizi kwa mfano nilikua najua tunatumia "article -a" kabla ya nouns/adjectives ambazo zinaanza na consonat...

mfano: she gave me a book.

lkn kumbe pia wanaangalia na jinsi inavyosound hiyo consonant....

mfano: she need to study for "a hour" before she go to lunch.

unaona jinsi hiyo article ilivyokiwa haiendani na hiyo "hour" japo inaanza na Consonant....wataalam sasa wanasema hiyo "hour" sauti yake ukiitamka inasikika "our" ambayo yenyewe inaanza na Vowel...
kwahivyo hapo article sahihi ni "an"

sahihi: she need to study for an hour before she go to lunch.

kumbe sasa tunaona matumizi ya article "a" na "an" zinategemea na suati ya nouns/adjectives,

a - consonat sound
an - vowel sound

hiki ndicho kwenye kiingereza nilijifunza na nikafurahi kuelewa japo kidogo,

ila hii article ya "The" bado sijaridhika...nahitaji kujifunza zaidi.
Umetisha Mr Miller, tuendelee kujifunza
 
hii lugha nataka niachane nayo tu mpango wa kwenda ulaya sina inasumbua sana
 
Habari wakuu ! Natumaini wote ni wazima wa afya , kwa upande wangu niko poa . Sasa twende moja kwa moja kwenye mada yetu .

View attachment 1031445g

Tenses huelezea wakati au muda tendo linafanyika , lilifanyika au litafanyika .

Katika kiingereza kuna tenses ( nyakati ) kuu tatu , ambazo ni :

The present tense ( wakati uliopo)
The past tense ( wakati uliopita )
The future tense ( wakati ujao )

Na kila tense imegawanyika katika sehemu kuu nne ambazo : simple , continous , perfect na continous perfect.

1. PRESENT TENSE ( Wakati uliopo )

I. Simple present tense
II. Present continous tense
III. Present perfect tense
IV. Present perfect continuous tense

2. PAST TENSE ( Wakati uliopita )

I. Simple past tense
II. Past continuous tense
III. Past perfect tense
IV. Past perfect continuous tense

3. FUTURE TENSE ( Wakati ujao )

I. Simple future tense
II. Future continuous tense
III.Future perfect tense
IV. Future perfect continuous tense


Leo tuanze na "simple present tense "

Simple present tense -huu ni wakati ambao unaonyesha vitendo ambavyo vinafanyika kila siku au vya mazoea. Vitenzi ( verbs ) ambavyo vinatumika
katika wakati huu havibadiliki isipokuwa katika nafsi ya tatu umoja .

Zifahamu Nafsi

Nafsi ya kwanza : I ( mimi )
Nafsi ya pili : You ( wewe )
Nafsi ya tatu : He / she / it ( yeye

WINGI

Nafsi ya kwanza : We ( sisi )
Nafsi ya pili : You ( ninyi )
Nafsi ya tatu : They ( wao )

Examples :

I sing songs = > huwa naimba nyimbo

You sing songs = > huwa unaimba
nyimbo

He sings songs = > huwa anaimba nyimbo

She sings songs = > huwa anaimba nyimbo

It sings songs = > huwa anaimba nyimbo

We sing songs = > huwa tunaimba nyimbo

You sing nyimbo = > huwa mnaimba nyimbo

They sing songs = > huwa wanaimba nyimbo

#Kwa nafsi ya tatu umoja , hapa
nazungumzia : ( He , she na it ) ambapo hawa vitenzi vyao vinabadilika vinakuwa vinaongezewa S , ES au IES .

Mfano : take / takes , do / does / fry / fries .

SHERIA YA KUBADILISHA VITENZI ( VERBS ) .

Vitenzi ( verbs ) vingi huwa vinaongezewa " S " tu . Mfano : Seem / seems , look / looks , take / takes .

Kwa vitenzi ambavyo vinaishia na O huwa tunaongezea - ES . Mfano : Go / goes / , do / does , veto / vetoes ) .

Kwa vitenzi ( verbs ) ambavyo vinaishia na - S , - Z , - CH , -SH na - X , hapa huwa tunaongezea " ES " . Mfano : Punch / puches , wash / washes , kiss / kisses , fizz / fizzes , mix / mixes )

Kwa vitenzi ( verbs ) ambavyo vinaishia na sauti ya konsonant alafu mbele zimeishia na - Y huwa tunatoa Y alafu tunaongeza
IES , Mfano : ( Hurry/ hurries , Clarify / clarifies )

Ila kwa vitenzi ambavyo vimeishia sauti ya irabu ( vowel ) huwa tunaongeza " S " tu mbele . Mfano : ( Play / plays , enjoy / enjoys )

KUMBUKA : Kanuni zote za hapo juu zinatumika katika nafsi ya tatu umoja tu ( He , she na It ) .
Kwa nafsi zingine zote vitenzi huwa havibadiliki .

MIUNDO YA SENTENSI KATIKA TENSE HII .

1. Kwa sentensi za kukubali / chanya :

SUBJECT + MAIN VERB

I wake up at 6 AM
( Huwa naamka saa 12 asubuhi )

You wake up at 6 AM
( Huwa unaamka saa 12 asubuhi )

He wakes up at 6 AM
( Huwa anaamka saa 12 asubuhi )

She wakes up at 6 AM
( Huwa anaamka saa 12 asubuhi )

2. Kwa sentensi za kukanusha

SUBJECT + DOESN'T/ DON'T + MAIN VERB

Ufafanuzi :

DOESN'T - inatumika kwa nafsi ya tatu umoja , yani He, she na It .

DON'T - inatumika kwa nafsi

KUMBUKA : Unapotumia DON'T au DOESN'T basi kitenzi kikuu ( main verb ) kinakuwa hakibadiliki ( infinitive ) .

Pia :

Does not = Doesn't
Do not = Don't

KUMBUKA : Unapotumia DON'T au DOES basi kitenzi kikuu ( main verb ) kinakuwa hakibadiliki ( infinitive ) .

Examples :

-I do not wake up at 6 AM
( Huwa siamki saa 12 asubuhi )

-You don't wake up at 6 AM
( Huwa hauamki saa 12 asubuhi )

-He does not wake up at 6 AM
( Huwa haamki saa 12 asubuhi )

-She doesn't wake up at 6 AM
( Huwa haamki saa 12 asubuhi )

- It does not wake up at 6 AM
( Huwa haamki saa 12 asubuhi )

- We do not wake up at 6 AM
( Huwa hatuamki saa 12 asubuhi )

They don't wake up at 6 AM
( Huwa hawaamki saa 12 asubuhi)

3. Sentensi za kuuliza maswali

DO / DOES + SUBJECT + MAIN VERB

Examples :

Do you live here ?
( Je unaishi hapa ? )

Does he like this t-shirt ?
( Je anaipenda fulana hii ? )

Jinsi ya kujibu

-Yes I do .
-Yes he does .
-Yes she does .

Mifano zaidi

She loves her mother
( anampenda mama yake )

He eats banana
( Hula ndizi )

I drive a car
( ninaendesha gari )

You like this movie
( unaipenda muvi hii )

They hate us
( wanatuchikia )

Source : www.englishkona.com

Kwa leo tuishie hapa....tutaendelea .

WhatsApp : 0767329643

NOTE : Huu uzi utakuwa unasasishwa kila mara .
Mkuu huonekani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
oooh okay,

pia ni muhimu tukijifunza matumizi ya hizi article nyingine pia "a" na "an"

mimi zimenipa shida sana kwenye matumizi kwa mfano nilikua najua tunatumia "article -a" kabla ya nouns/adjectives ambazo zinaanza na consonat...

mfano: she gave me a book.

lkn kumbe pia wanaangalia na jinsi inavyosound hiyo consonant....

mfano: she need to study for "a hour" before she go to lunch.

unaona jinsi hiyo article ilivyokiwa haiendani na hiyo "hour" japo inaanza na Consonant....wataalam sasa wanasema hiyo "hour" sauti yake ukiitamka inasikika "our" ambayo yenyewe inaanza na Vowel...
kwahivyo hapo article sahihi ni "an"

sahihi: she need to study for an hour before she go to lunch.

kumbe sasa tunaona matumizi ya article "a" na "an" zinategemea na suati ya nouns/adjectives,

a - consonat sound
an - vowel sound

hiki ndicho kwenye kiingereza nilijifunza na nikafurahi kuelewa japo kidogo,

ila hii article ya "The" bado sijaridhika...nahitaji kujifunza zaidi.

Hii "The" ni matata sana, nakumbuka kitu cha kwamba, kama umeshakizungumzia hicho kitu au muhusika anakielewa unatumia "The" (refer maelezo ya Khantwe pale juu).

Sasa kwa kuanza 'a' na 'an' zitatumika, ulirudia kutumia hiyo pronoun ndipo 'the' inaingia.

Ngoja niende chimbo nitarudi hapa.
 
Back
Top Bottom