Sijui nn sasa we ndo ujui Mungu wetu ni mmoja na alisema Samehe saba mara sabini,.. Nyie na matakbir yenu mnaleta shida dunia nzima sio kila jambo unatakiwa ulipize kwa damu, vingine vya kukaa mezani yanaisha,mnajiita chinja chinja
Mbona una hofu mkuu? Uko miongoni mwa watu wasiojulikana nini? Albadir haina mchezo, inatembea haswa na inatafuta, kila aliyehusika inamchukua.
Iliwahi kusomwa Tanga miaka ya nyuma na sharifu ilikuwa balaa, watu walitafutana.
Ni baada ya mwenye shamba la minazi kuingia shambani kwake na kukuta makumbi tu ya nazi, wezi walisafisha shamba zima.
Akatangaza kwa siku tatu, aliyehusika ajitokeze mwenyewe, watu wakakaa kimya, baada ya siku tatu kupita, sharifu akaenda kuisoma, ilikuwa ni kutafutana haswa kupita kiasi.
Punda aliyebeba nazi alikufa, chuma kilichofulia nazi kilimong'onyeka, wezi wote walikufa, kila aliyekula zile nazi alikufa, iliacha gumzo kubwa Tanga miaka na miaka, yoyote aliyeshiriki katika hizo nazi alikufa.