JF Exclusive: The Buzwagi Contract

JF Exclusive: The Buzwagi Contract

Na kama ningekuwa waziri karamavi, leo ningeomba kuondoka nchini kwani naamini kuwa hasira hizi za wananchi kuna siku nwatakuja kumtoa .......kama anacho.....
 
Haoni uchungu na nchi hii na haswa rasilimali zake kwani watoto wake pamoja na wajukuu wake wataweza kuwa nje ya nchi,hivyo haoni haja ya kutokusaini,na kusema bungeni kuwa alikuwa na haraka ya kuusaini kwani taifa lingepoteza dili hilo.

NAKULILIA NCHI YANGU, TANZANIA.
 
Ukitimiza wajibu wako kama kiongozi huna hofu ya kuwaogopa wananchi! kwani wananchi watakukinga. Ila ukifanya na kutenda kana kwamba umesimikwa na mbingu na kutawazwa na malaika kuwa kiongozi basi wananchi wanaweza kukutoa madarakani!
 
kwa mujibu wa kipengele hicho ni kwamba hiyo kampuni (Barrick) wamekubali kwamba watatoa kodi yao serikalini kwa kufuata sheria ya Income tax Act No:11 of 2004 (nadhani hilo liko wazi)

sasa tuangalie hiyo sheria ya Income tax inasemaje?:

kwanza twende kwenye Legal key definitions

"PERSON"-means an individual or entity (ukurasa wa 21)

"entity"-means a partnership,trust or corporation (ukurasa wa 16)

ukiangalia ukurasa wa 130 wa (pdf) ya hiyo act No 11 ya 2004 kuna kifungu cha 3-
kinazungumzia" Rates of income tax for entities"

kinasema hivi "

Kwa hiyo ni dhahiri kwamba kama Barrick wamekubali kwamba watalipa kodi based on the ACT NO. 11 ya INCOME TAX YA
2004 basi kipengele hicho kinawafunga Barrick kutoa 30 percent ya income per year.

kwa hiyo nadhani hiyo 30 percent ambayo watu wanaitaka iko pale pale (niko tayari kukosolewa)


Hapo ndipo unagongana na tatizo jingine, kama kuna kipengele kinachosema kwenye mkataba huo huo kuwa kodi haitatokana na mapato, faida, n.k utawezaje kutoza kodi hiyo kwa kutumia sheria hiyo ya 2004?
 
Ukisoma mahojiano kati ya rais na jarida la economist ambalo mwanakijiji ameweka hapa utaona kuwa yeye anaridhika na hizo pesa tunazopata sasa hata tukimtaka karamagi ajiuzulu ili haki iweze kupatikana hatakubali kwani boss wake anaona hakuna tatizo hapo,.
 
Mwanakijiji najua utakuwa unarejea kipengele cha 4.2 kujenga conclusion yako
ambacho kinasema:

4.3 Local Government rates and taxes shall not be:

4.3.1 in excess of those generally applicable on Tanzania, or

4.3.2 based on profit, turnover, sales or output from mining operations, or

4.3.3 based on the value of land used for the mine, mining infrastructure or installations,
provided that the aggregate of such local Government rates and taxes charged shall not exceed United States Dollars Two Hundred Thousand (US$ 200,000) in any one calendar year.

Lakini nilivyoelewa mimi ni kwamba kipengele hicho kinafafanua au kwa lugha nyingine ni kwamba kinaweka mipaka
ya kodi itakayotozwa na SERIKALI ZA MITAA ambako mgodi huo wa Buzwagi upo,kwa maana hiyo Income tax ya asilimia 30 inayotozwa na SERIKALI KUU Iko pale pale ipo
 
Gamba la Nyoka, biashara gani nyingine Tanzania ambayo ipo katika eneo la Tanzania ambayo hailipi kodi nyingine zote isipokuwa kodi ya mapato peke yake? Na kodi ya mapato kwa mkataba wa Buzwagi inaanza kulipwa lini na mapato (income) inaanza kuhesabiwa lini?
 
MK, why are U wasting ur time with Gamba la I don't know what??

Just let him answer the following::

1) Is there any Mine in Tz where this hypothetical 30% tax has ever been paid??

2) Is there any grace period where by all taxes are exempted for say 5-10 yrs??

3) Is the tax paid after deductions?? Ok then if U carry the costs of the mines to the yr after exemption period, how long will it take for (revenue- mine cost) to be in positive territory??

4) Who authored the mkataba to begin with?? What, Barrick, no wonder
 
Ameeeeen,

Wamefanya wanachotaka for a long time na sasa wana-take things for granted! imefikia point wananchi wamechoka. Hali za maisha ni ngumu na wao wanatumbua tu na kuuza nchi!..........

Inasikitisha kwa kweli, masoko ya pesa ulimwenguni yanazidi kushamiri, kampuni zinazoongoza kwenye masoko hayo na mzunguko wa pesa duniani kote unaelemea zaidi kwenye mlundikano wa dhahabu. Barrick na kampuni nyingine chache kubwa ndiyo zinaaminika, dhahabu yenye faida kwenye makampuni haya nyingi tu inatoka Tanzania, wananchi wa Tanzania wanaachiwa mashimo tu...halafu viongozi wetu wanaona wako kwenye 'win win' situation, what.... to me with regard to the underpinnings in this contract is factual defecation on the faces of Tanzanians at large, inauma na ina uma kikweli kweli.

Hata kijana wa kidato cha nne anaweza kusoma huo mkataba akauelewa na kuona kuwa hauna uwiano sawa bali ni matusi ya kukudhalilisha kama vile wewe unaye saini hauna kisomo chochote... hivi kwanini wana saini vitu kama hivi?! Greedy greedy greedy driven ****** (mind you i could swear worse than this, only wouldn't do so and be against JF rules)!

Dhahabu yetu ilikuwepo miaka milioni iliyopita, kuichimba kama biashara pekee bado kwa kweli katika nchi yetu kutokana na utaalam tulio nao kuwa hafifu. Tuache hizo dhahabu, kutokana na maendeleo ya teknolojia kuongezeka kwa kasi duniani katika muda mfupi, si punde nasi tutaweza kuchimba hii maliasili yetu. Badala yake tunaita mtu wa nje aje achimbe na kutuachia mashimo baada ya kupewa peremende chache. Hapa nakumbuka story za jinsi wa misionari walivyokuwa wanakuja na gololi kibao na kuwapatia machifu kama fadhila za wao kupata almasi.

Kadri haya makampuni yanavyochimba ndivyo kadri jinsi nchi yetu inavyo lemazwa, kwani kinachochimbwa ni maliasili ambayo haiwezi kurudishwa, inachimbwa kwa wingi kiasi kwamba siye tunaachwa walemavu wa kudumu, maana hata baada ya miaka 30 tukisha kuja kuwa na teknolojia ya kuchimba, maliasili hii itakuwa imeshatoweka. Ila hizo nchi na makampuni yake yanayochimba yatakuwa bado yamehifadhi vipande hivi vya dhahabu kama yakinishi la utajiri wao na hivyo kuwa na control kwetu na shilingi yetu. Sasa huyu baba wa watu anasahau kuwa kusaini mkataba kama huu ni sawa na kuwa **** wajukuu zake indirectly!

Niko tayari kuishi maisha duni hadi kifo changu kuliko kuona niko raped by multinational corporations by receiving meager conditional rewards (as per contract seen) on my own wealth. Bora tufe masikini kuliko kujiuza kinamna hii, I'm sure vizazi vijavyo vitakuwa na teknolojia nzuri tu ya kuweza kuchimba dhahabu hizi, na si kung'ang'ania kuchimba through watu wengine wanao tutusi katika mikataba. What an idiot, unaingia mkataba utafikiri kama vile dhahabu ina expire kesho kutwa, eti kuharakishia chance otherwise tunge lose out...

Mbona wasiharakishe kujenga mabarabara na viwanda vya kusindika mazao, maana wanaweza kutoza kodi na kufarijika kupitia 'win win situation' kama kweli wana nia njema wakati Taifa letu bado mhimili wake ni kilimo na ufugaji... kwa nini wasiwekeze huku kwanza maana ndiyo kwenye haraka la sivyo 'tutakufa na njaa', instead wanakimbilia madini, kwani wanajua kabisa kuwa wakichimba leo na kuweka hazina hiyo ya dhahabu kwenye mabenki yao huko Ulaya, basi watakuwa wamepata kitu madhubuti cha kuendelea kutugandamiza sisi katika mfumo wa pesa duniani. Fikiria Tanzania ingeweza kuweka dhahabu kama hazina yake katika mabenki ya pesa duniani, shilingi yetu ingekuwa inateleleka namna hii?!... hata dhahabu tu zinazochimbwa kienyeji zinaweza kutuokoa tusiwe na fedha inayoyumba kila siku, badala yake, tuna i blackmail shilingi yetu sisi wenyewe through these bunch of crack heads.


SteveD.
 
Gamba la Nyoka, biashara gani nyingine Tanzania ambayo ipo katika eneo la Tanzania ambayo hailipi kodi nyingine zote isipokuwa kodi ya mapato peke yake? Na kodi ya mapato kwa mkataba wa Buzwagi inaanza kulipwa lini na mapato (income) inaanza kuhesabiwa lini?

Lakini ukiachilia mbali hiyo income tax ya asilimia 30
itabidi walipe malipo yafuatayo katka SERIKALI KUU kwa mujibu wa kipengele cha 4.1


4.1 The Company shall pay to the Government:

4.1.1 a royalty at the rate of 3% on the Net Back Value of all minerals produced from the Contract Area, other than diamonds, in respect of which the royalty shall equal 5% of the Net Back Value; and

4.1.2 stamp duty under the Stamp Duty Act No. 20 of 1972, as in effect on the Fiscal Stabilization Date.

4.1.3 for each year of production the amount of US$ 125,000 by 31st December of each calendar year a contribution to the Empowerement Fund
lakini hata ukichunguza kipengele chenye utata cah 4.3 utagundua kwamba bado kuna kodi Barrick watalipa

4.3 Local Government rates and taxes shall not be:

4.3.1 in excess of those generally applicable on Tanzania, or

4.3.2 based on profit, turnover, sales or output from mining operations, or

4.3.3 based on the value of land used for the mine, mining infrastructure or installations, provided that the aggregate of such local Government rates and taxes charged shall not exceed United States Dollars Two Hundred
Thousand (US$ 200,000)
in any one calendar year.

Kwa hiyo ukichunguza utaona kwamba watalipa local government taxes lakini "HAITA EXCEED THOSE GENERALLY APPLICABLE IN TANZANIA"

Watalipa hiyo tax ya value ya ardhi(mine),miundombinu(infrastructure or installations) lakini (AGGREGATE OF SUCH LOCAL GOVERNMENT RATES AND CHARGES HAITA EXCEED DOLA 200,000)

Kwa mujibu wa kipengele hicho cha 4.3 kodi ambayo barrick hawatalipa kwa
"LOCAL GOVERNMENT" SIYO (CENTRAL GOVERNMENT) Ni ile kipengele cha 4.3.2 kinachosema "based on profit,turnover,sales or or output from mining operations"
 
Haoni uchungu na nchi hii na haswa rasilimali zake kwani watoto wake pamoja na wajukuu wake wataweza kuwa nje ya nchi,hivyo haoni haja ya kutokusaini,na kusema bungeni kuwa alikuwa na haraka ya kuusaini kwani taifa lingepoteza dili hilo.

NAKULILIA NCHI YANGU, TANZANIA.

Jamani,
Peremende tamu sana ilibidi asaini hivo hivo asizikose!!
 
Lakini ukiachilia mbali hiyo income tax ya asilimia 30....

lakini hata ukichunguza kipengele chenye utata cah 4.3 utagundua kwamba bado kuna kodi Barrick watalipa

4.3 Local Government rates and taxes shall not be:

4.3.1 in excess of those generally applicable on Tanzania, or

Ina maana gani kukataa kulinganisha kodi na mahali ambapo hapana madini?

4.3.2 based on profit, turnover, sales or output from mining operations, or
Sasa wanatumia kipimo gani kutoza hiyo kodi?

4.3.3 based on the value of land used for the mine, mining infrastructure or installations,
Kama huwezi kupima kodi kwa kuzingatia thamani ya vitu hivyo (kama biashara nyingine wafanyavyo) unatumia kigezo gani?

provided that the aggregate of such local Government rates and taxes charged shall not exceed United States Dollars Two Hundred Thousand (US$ 200,000) in any one calendar year.

Kama hujaweka kigezo cha kodi na badala yake unaamua kuwa jumla ya "kodi hiyo" haitazidi dola laki mbili. Ina maana wanaweza kulipa dola laki moja au dola mia tano!!

Kwa hiyo ukichunguza utaona kwamba watalipa local government taxes lakini "HAITA EXCEED THOSE GENERALLY APPLICABLE IN TANZANIA"
tell me why not? Kwanini walinganishe kodi ya hapo na kodi ya kijiji cha Buzuruga, au kule Pangani, au Undali, Unyanyembe n.k alimradi haitazidi kodi za sehemu hizo? Sehemu nyingine wameweka kodi zao kwa kuangalia raslimali zao, iweje mahali ambapo pana thamani kubwa isitozwe kodi kubwa kidogo, kwanini ilingane na kodi ya miji ambayo haina raslimali kubwa na zenye thamani?

Watalipa hiyo tax ya value ya ardhi(mine),miundombinu(infrastructure or installations) lakini (AGGREGATE OF SUCH LOCAL GOVERNMENT RATES AND CHARGES HAITA EXCEED DOLA 200,000)
back to square one!

Kwa mujibu wa kipengele hicho cha 4.3 kodi ambayo barrick hawatalipa kwa
"LOCAL GOVERNMENT" SIYO (CENTRAL GOVERNMENT) Ni ile kipengele cha 4.3.2 kinachosema "based on profit,turnover,sales or or output from mining operations"
Hivi local tax inatokana na vigezo gani?
 
Peremende!
Peremende hizi jamani zimetufikisha hapa..
Peremende....aliyekuumba ni nani hadi unaleta kilio kikuu hivi?
Peremende una utamu gani kuliko vitu vingine?
Peremende humwonei huruma hata anayekutafuna
Peremende! umemlevya waziri wetu, hadi akaweka maslahi ya taifa pembeni ili asikukose
Peremende! tukupe nini ili uacha kuwapumbaza watawala wetu1
Peremende! ona, IPTL, Richimonduli,, TtCl, Dawa si sisco, kote huko umepitapita!
Peremende! Ipo siku utamu wako tutaukomesha, utamu wako utageuka kilio kikuu...na hapo ndipo wale wote uliowalevya, huku ukikaa pembeni na kucheka, watalia na kusaga meno!
 
Hey guys..

It is friday afternoon in the US, weekend ndio hivyo inaingia.

Articles na parts zaidi za huu mkataba zitaendelea kuwekwa hapa randomly but accordingly no matter how long it takes. Naamini kuwa wale ambao hawajaupata huu mkataba wanafuata hiyo link hapo especially ya bongoradio kujipatia copy zao.

Tanzania itakombolewa na Watanzania wenyewe kutoka mikononi mwa hawa wezi na wakoloni mamboleo.....

Viva JF... walisema mkataba ni siri... na bila wao kujua kila mtu hata wasioishi bongo wataupata huu mkataba...

Viva JF.... The best of you is YET to come..

Viva JF.
 
Wazee wa JF,
Naomba kuwekwa sawa hapa kidogo, leo nimeongea na nyumbani na kuna mtu kanambia kwamba huko darisalama kuna mikataba kama hii zaidi ya mitatu!!!..........jamaa anasema kuna ule aloona gazetini, kwenye vijiwe vya CUF na mwingine kwenye nyumba flani flani za ibada na yote hii inatofautiana!!! N.B hayo ni mawazo yake.........sasa swali langu je kutokana na source zenu hasa waliopo nyumbani, jee hii ni kweli,udaku au janja ya CCM kuchanganya watu vichwa!!???.
Kwa ujumla natoa hongera kwa wanaJF kwani naona mambo ni mpwitompwito na yanakwenda yakiongezeka!!.Mafisadi wana i-feel hii heat ya wadanganyika.
 
Wazee wa JF,
Naomba kuwekwa sawa hapa kidogo, leo nimeongea na nyumbani na kuna mtu kanambia kwamba huko darisalama kuna mikataba kama hii zaidi ya mitatu!!!..........jamaa anasema kule ule aloona gazeti, kwenye vijiwe vya CUF na mwingine kwenye nyumba flani flani za ibada na yote hii inatofautiana!!! N.B hayo no mawazo yake.........sasa swali langu je kutokana na source zenu hasa waliopo nyumbani, jee hii ni kweli,udaku au janja ya CCM kuchanganya watu vichwa!!???.
Kwa ujumla natoa hongera kwa wanaJF kwani naona mambo ni mpwitompwito na yanakwenda yakiongezeka!!.Mafisadi wana i-feel hii heat ya wadanganyika.

Of course ccm watakuambia kuwa kuna mikataba hata kumi wakitaka na wanaweza kutengeneza yao feki ili kuchanganya raia...

Whatever they do.... huu mkataba unastinck ndio maana hawakuwa tayari kabisa kuanzisha kamati ya bunge kuuchunguza na wakafanya haraka kumfukuza zitto bungeni!

Cha moto watakiona mwaka huu.... Mtanzania asiyejulikana jina ameamua kuvujisha huu mkataba huku akiweka maisha yake, kazi, na familia yake on the line kwa ajili ya maisha ya Watanzania..

Tumwombe MUNGU amlinde huyu mtanzania jasiri kwani hatujui nini kitampata huyu......

VIVA JF..... The best of you is YET to come.....
 
Back
Top Bottom