FairPlayer
JF-Expert Member
- Feb 27, 2006
- 4,145
- 731
Yaani hii management fee itakuwa badala ya kodi!
yaani technical services or management services ndizo zipi?
Technical services au management fees au group fees kama inavyiitwa na makampuni kadhaa ni ile hela unayolipa group company (kampuni inayokumiliki), mara nyingi ni asilimia kadhaa ya mauzo au uzalishaji wenu. Kuna tatizo la kodi la hiki kifungu kwani wengi wana gross up (kama tech fees calculated ni 100 basi wenyewe wanataka 100, withholding tax ya 15% mnailipa wenyewe) kwahiyo badala ya kulipa 85% (100-15% withholding tax) mnalipa 100, kwahiyo grossup ya 115 inaonekana ni expense kwa kampuni badala ya 100, kodi ya Corporate tax inakuwa imekwepwa kwa asilimia 30% ya asilimia 15% iliyoongezwa!
TRA walishagundua hili, wana fight sasa hawa jamaa wemeshtuka wameliweka kwenye mkataba wazi.
Jamani hizi tax evasion zinazogeuzwa tax avoidance sio nzuri.
Kwa asiyeelewa aulize.