JF Exclusive: The Buzwagi Contract

JF Exclusive: The Buzwagi Contract

1. Mkataba umesainiwa hotelini, huku waziri Karamagi akibeba mihuri ya serikali mfukoni mwake, yote haya yamefanyika kwa siri.

2. Kamati ya uwekezaji ya bunge haikufahamishwa kuhusu haya yote ya waziri Karamagi, ambacho ni kinyume na sheria zetu,

3. Mbunge Zitto, alipoutoboa ukweli wa yaliyofanywa na waziri Karamagi, akakubali bungeni kuwa ni kweli, lakini wananchi hatukuambiwa hiyo part ya waziri kukubali kuwa amefanya makosa.

4. The next thing, mbunge akafukuzwa bungeni, huku waziri Karamagi akiendelea kupeta, sasa mkataba ukaanza kusambazwa, na majuzi tumetishiwa kuwa ukikamatwa na huu mkataba utakiona cha moto!

5. Tumeupata mkataba hapa hapa forum, yaliyoandikwa ndani yake ni kichekesho kitupu, na ndio hasa sababu ya serikali kumfukuza bungeni mbunge Zitto, na kuwa wakali sana na huu mkataba ndio zinaanza kuonekana wazi kuwa ni usaniii wa mwaka,

In the wake of all this, ni justified wananchi kuwa na huo mkataba wa siri za waizi, thank God kuwa na wafadhili wetu wanao pia, maana sasa serikali wanahitaji kutudanganya sisi kwanza halafu wafadhili wetu kama kweli wanaweza!

Mungu Aibariki Tanzania Yetu!
 
Gold in NYSE leo imefikia 700$+ (all time high ilikuwa last week)...sometimes nafikiria bora tungekuwa na wazungu kama part ya raia wetu kama South Africa maana wasingekubali this kind of BS
 
nilikuwa naangalia CNBC last night kipindi cha Jim Crammer...basi anakuambia green(dollar) is getting dumped so the best thing you can do wit ur portfolio ni gold na company to put your money ni XBF yaani Barric Gold maana ni one of the most profitable katika Dow Jones for the last five yrs na reason behind the profit akasema they have a new & huge gold mining somewhere in Africa(mwananangu hapo nikasikia click click click klak klak bongo hiyooooo karamagi katuuza)..kweli tungekuwa makini tungekuwa sawa na South Africa tuu lakini naona tumegeuzwa hapo kama waarabu na record profit in history ya Exxon Mobile kutoka kwa waarabu huku wenyewe wakifa kama kuku,haya mambo wazee sio joke angalieni Sierra Leone mambo ya Diamond,Congo gold,mafuta Nigeria ni kutokana na injustice ya mikataba kama hii ndio maana watu wanaingia msituni,i dont suggest tupigane lakini kutufunga na contract ya 50 yrs huku tukibaki na umaskini uliokithiri na mali ni yetu watu watachoka na kitakachotokea kila mtu anajua
Lakini tufikiri kwa undani zaidi tusiangalie tulipoangukia, tuliangalie tulipojikwaa Waziri Karamagi ni mtu wa mwisho tu, kuna watu wanaitwa wataalamu walioandaa, walionegotiate and eventually ukaandikwa ukapitishwa kwa mwanasheria mkuu,,, nadhani tungekuwa objective kuhoji hawa waheshimiwa! maana tukilinda hii tabia kesho na wewe utakuwa kiongozi utalengeshewa utasaini na mambo yatakuzukia... Karamagi, can not be a Geologist, Financial Accountant, Attorney etc... in fact mimi natamani mikataba isainiwe na makatibu wakuu, sio mawaziri
 
Karamagi, can not be a Geologist, Financial Accountant, Attorney etc... in fact mimi natakami mikataba isainiwe na makatibu wakuu, sio mawaziri

Lakini Karamagi anaweza kwenda hotelini London na mihuri yetu ya taifa mfukoni kutia sahihi mikataba ya taifa letu, bila ya kuwafahamisha kamati ya bunge ya uwekezaji, je haya nayo aliambiwa ayafanye na wataalamu au?

Halafu ni mkataba wa wizara gani ambao unasainiwa na waziri bila ya kupitiwa na kuidhinishwa na katibu mkuu wa wizara hiyo?

Mkuu heshima mbele kwa kujaribu kuwa-objective, ila ni vizuri tu huyu waziri akajiuzulu now, badala ya kuendelea kuharibu sifa ya chama chetu CCM, maana ni kikubwa kuliko Karamagi!
 

Wasiwasi wangu ni kwamba Serikali yetu kuu, kwa niaba ya wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeingia mkataba mzuri/mbaya sijui, kwa sababu terms za negotiation sizijui, lakini imeingia mkataba na Mwekezaji tena sio mwekezaji wa mfukoni hapani ni kampuni linalotambulika ulimwenguni...

Serikali imeingia mkataba na kampuni ya Pangea minerals LTD ambayo ni subsidiary ya Barrick Gold Corporation hivi serikali yetu bado haijajifunza miaka yote hii kuingia mikataba na kampuni uchwara. Kwa nini wanaingia na sub-sidiary kampuni badala ya kuingia mkataba na kampuni mama? Huoni hapo kuna uhuni?
wakati huo tujue hatumtendei haki mwekezaji ambaye hana hatia yoyote...

Mwekezaji yupi? Pangea? Je yeye anatutendea haki gani hapa kwenye huu mkataba?
Ningekuwa mwekezaji ambaye nataraji kuja hapa,,, ningefikiria mara mbili kama mikataba itakuwa inafanyikwa kama tunavyofanya, naombeni sana tuangalia mambo kwa mbali zaidi, tusiangalie kwa nia ya kuongoza nchi, kesho itakuwa UDP, CHADEMA etc... lakini taifa ni hili hili

Ndio sababu wewe sio mwekezaji, wawekezaji makini wapo wengi wanataka kuja Tanzania. Hatuongelei mambo ya vyama hapa bali mkataba bomu.
 
Lakini tufikiri kwa undani zaidi tusiangalie tulipoangukia, tuliangalie tulipojikwaa Waziri Karamagi ni mtu wa mwisho tu, kuna watu wanaitwa wataalamu walioandaa, walionegotiate and eventually ukaandikwa ukapitishwa kwa mwanasheria mkuu,,, nadhani tungekuwa objective kuhoji hawa waheshimiwa! maana tukilinda hii tabia kesho na wewe utakuwa kiongozi utalengeshewa utasaini na mambo yatakuzukia... Karamagi, can not be a Geologist, Financial Accountant, Attorney etc... in fact mimi natamani mikataba isainiwe na makatibu wakuu, sio mawaziri

...acha acha kabisa na the ball stop to karamagi ambaye aliweka mkwaju kwenye hizo karatasi, ana wasaidizi million kidogo wanaolipwa kumfanyia kazi yeye sasa unataka kuleta excuse gani hapa? ...ndio yale yale unamwambia hakimu nilikuwa sijui kama ni kosa.
 
Mkuu heshima mbele kwa kujaribu kuwa-objective, ila ni vizuri tu huyu waziri akajiuzulu now, badala ya kuendelea kuharibu sifa ya chama chetu CCM, maana ni kikubwa kuliko Karamagi!

FMES,

I would like that to happen, however if there is no already laid down procedures which don't allow a government official to sign a contract outside the government premises... then we go not have grounds to force him to resign, we will have to pray for him for him to decide on resignation on his own, or HE. President to ask him to do so!
 
Gold in NYSE leo imefikia 700$+ (all time high ilikuwa last week)...sometimes nafikiria bora tungekuwa na wazungu kama part ya raia wetu kama South Africa maana wasingekubali this kind of BS


Kwani nani amekwambia sisi tunakubali huu ujinga? Huoni mawaziri wanavyopata tabu huko mikoani? Usitake kuleta utumbo mwingine hapa tafadhali.
 
[/size]

Kwani nani amekwambia sisi tunakubali huu ujinga? Huoni mawaziri wanavyopata tabu huko mikoani? Usitake kuleta utumbo mwingine hapa tafadhali.

...kijana huna hoja sasa unaleta vioja.
 
Gold in NYSE leo imefikia 700$+ (all time high ilikuwa last week)...sometimes nafikiria bora tungekuwa na wazungu kama part ya raia wetu kama South Africa maana wasingekubali this kind of BS

Koba
Nadhani hapo ndio kuna possibility ya US Congress kulifumbia macho suala hili kama Zitto ata bahatika kukutano nao..........seems like hizo hits za gold ndio life line kwa sasa.
Wallahi sijawahi kupata uchungu na Tanzania kama nilionao sasa...........Mazee kama unao mkataba watume hao wakina Cramer kwenye "MAD MONEY" tuone atafanyaje!!!!. Kama ni mtu fair, let say akiongelea hii issue kwenye show nadhani itakuwa poa sana!!!!.......labda watu wanaweza ku-boycott stocks za Barrick kuwa pressurize kinamna, mambo ya guilty conscious ya wazungu...who knows.
 
FMES,

I would like that to happen, however if there is no already laid down procedures which don't allow a government official to sign a contract outside the government premises... then we go not have grounds to force him to resign, we will have to pray for him for him to decide on resignation on his own, or HE. President to ask him to do so!

...nafikiri unahitaji upigwe bomu la kichwa tuu na wala sio bunduki upotelee mbali maana mkuu point zako ni kali kweli kweli lakini ujumbe tutawafikishia wananchi kwamba tumuombee Karamagi...mpuuzi kweli kweli wewe!
 
I would like that to happen, however if there is no already laid down procedures which don't allow a government official to sign a contract outside the government premises...

Hapana mkuu nafikiri tunayo sheria inayomtaka waziri kuiarifu kamati ya bunge ya uwekezaji, kuwa ataenda chumbani London hotelini kusaini mkataba wa madini, huku akiwa amebeba mihuri ya serikali yetu mifukoni mwake!

Mwinyi, alipojiuzulu akiwa waziri wa mambo ya ndani, hakuombwa na mtu yoyote ilikuwa tu ni ustaarabu on his part, ambao tunauomba kwa waziri Karamagi, lakini anweza kuendelea kuwa waziri ila kwa gharama ya nani na this kind of mikataba?
 
Koba
Nadhani hapo ndio kuna possibility ya US Congress kulifumbia macho suala hili kama Zitto ata bahatika kukutano nao..........seems like hizo hits za gold ndio life line kwa sasa.
Wallahi sijawahi kupata uchungu na Tanzania kama nilionao sasa...........Mazee kama unao mkataba watume hao wakina Cramer kwenye "MAD MONEY" tuone atafanyaje!!!!. Kama ni mtu fair, let say akiongelea hii issue kwenye show nadhani itakuwa poa sana!!!!.......labda watu wanaweza ku-boycott stocks za Barrick kuwa pressurize kinamna, mambo ya guilty conscious ya wazungu...who knows.

...mkuu hawa mabepari watapiga kelele kama hawana interest hapo lakini kwa hili hata kukusikiliza hawatakusikiliza ...waulize Iraqis na demokrasi ya mafuta under the name of war on terror maana hata Greenspan kasema kwenye kitabu chake Iraq war is nothing but oil
 
Lakini tufikiri kwa undani zaidi tusiangalie tulipoangukia, tuliangalie tulipojikwaa Waziri Karamagi ni mtu wa mwisho tu, kuna watu wanaitwa wataalamu walioandaa, walionegotiate and eventually ukaandikwa ukapitishwa kwa mwanasheria mkuu,,, nadhani tungekuwa objective kuhoji hawa waheshimiwa! maana tukilinda hii tabia kesho na wewe utakuwa kiongozi utalengeshewa utasaini na mambo yatakuzukia... Karamagi, can not be a Geologist, Financial Accountant, Attorney etc... in fact mimi natamani mikataba isainiwe na makatibu wakuu, sio mawaziri

Kill,
Upo sahihi ni bureaucracy yote imeoza...........bila kuwapigia kelele hawawezi kubadilika!!. lukuki la makaratasi kibao na fine prints ni psychological tactic ya western cooperates kwani wanajua kuna tendency ya uvivu wa kusoma.........i really doubt kama waziri alisoma hii kitu vizuri, au ndio kaingizwa king na wasaidizi wake.
 
Hebu Acheni wivu huko!


Hamjasoma Tamko la Serikali kuhusu maendeleo ya Sekta ya Madini? Maswali yenu yote yamejibiwa.

Hii yote sababu ya CCM:

Chama Cha Mafisadi.......CCM
Chama Cha Majambazi......CCM
Chama Cha Malaya.........CCM
Chama Cha Mataahira......CCM
Chama Cha Majambazi......CCM
Chukua Chako Mapema......CCM
Kwa Ari Nguvu na Kasi Mpya.....ANGUKA!

Nimewamiss Asha mie
 
Hapana mkuu nafikiri tunayo sheria inayomtaka waziri kuiarifu kamati ya bunge ya uwekezaji, kuwa ataenda chumbani London hotelini kusaini mkataba wa madini, huku akiwa amebeba mihuri ya serikali yetu mifukoni mwake!
Kwa faida yangu mimi slow learner na kwa faida ya watu kama mimi, unaweza kunielekeza kwenye hiyo sheria walau niisome kidogo ingawa lugha ya sheria wakati mwingine inanipiga chenga? wawezanipatia wewe au mh. mwingine yeyote?

Mwinyi, alipojiuzulu akiwa waziri wa mambo ya ndani, hakuombwa na mtu yoyote ilikuwa tu ni ustaarabu on his part, ambao tunauomba kwa waziri Karamagi, lakini anweza kuendelea kuwa waziri ila kwa gharama ya nani na this kind of mikataba?

Hapa ni bahati tu tulipata, na bahati ati haiji mara mbili, kwani ni miongo (decades) ngapi zimepita hatujawahi bahati na hali kama ya mzee Ruhsa?
 
Hebu Acheni wivu huko!


Hamjasoma Tamko la Serikali kuhusu maendeleo ya Sekta ya Madini? Maswali yenu yote yamejibiwa.

Hii yote sababu ya CCM:

Chama Cha Mafisadi.......CCM
Chama Cha Majambazi......CCM
Chama Cha Malaya.........CCM
Chama Cha Mataahira......CCM
Chama Cha Majambazi......CCM
Chukua Chako Mapema......CCM
Kwa Ari Nguvu na Kasi Mpya.....ANGUKA!

Nimewamiss Asha mie

Haya mama, naomba uombe toba ndani ya mwezi huu mtukufu wa Ramadahani maana hicho chama kina watu wengi ndani yake wako waumini wa dini mbalimbali, na pia wamo watu wazuri tu, ni kwa bahati mbaya kuna watu unatamani uwatukane lakini isingekuwa vyema uwatukane wana-CCM wote, dhambi kwa Mungu bi. Asha,,, naomba usali usiku huu kwa kosa ili,,,

Inshallah mwenyezi Mungu akuongoze na kukupa hekima ya kupeleka ujumbe kwa unapokusudia bila kutukana
 
Kill,
Upo sahihi ni bureaucracy yote imeoza...........bila kuwapigia kelele hawawezi kubadilika!!. lukuki la makaratasi kibao na fine prints ni psychological tactic ya western cooperates kwani wanajua kuna tendency ya uvivu wa kusoma.........i really doubt kama waziri alisoma hii kitu vizuri, au ndio kaingizwa king na wasaidizi wake.

..hapo mzee you nail it,tendency ya uvivu wa kusoma,rushwa na kufanya mambo kwa kulipua wanaijua iko sana kwa waafrica ndio maana wanatuingiza mikenge kama hii kwa hizo weakness
 
...mkuu hawa mabepari watapiga kelele kama hawana interest hapo lakini kwa hili hata kukusikiliza hawatakusikiliza ...waulize Iraqis na demokrasi ya mafuta under the name of war on terror maana hata Greenspan kasema kwenye kitabu chake Iraq war is nothing but oil

Mazee,
watu just need to get it, this is worse beyond words!!!!!!!!!.Ukianza ku-connects dots hapa kichwa kinaweza ku-explode, ndio maana yule Mkwere kaja hapa wakawa wanamvisha viremba vya ukoka...........kwa maneno mengine money maker kwasasa Wall Street ni Barrick, kisa ni limkataba la Buzwagi,Tanzania......Yaani somebody in smallville,USA anahit jackpot kwa gold ya Bongo!!!!!11.
 
Back
Top Bottom