Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,813
- 11,991
Kwa sasa Mwanza kuna tabia ya asilimia kubwa ya Daladala kutofika katika ‘ruti’ zao husika walizopangiwa na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) hasa zile zinazotoka Nyashishi kwenda Kisesa, nyingi zinaishia Igoma na wanasema kabisa wanaishia Igoma kama hutaki shuka.
Kwa hivyo, abiria wa Kisesa atakaepanda basi ajue akifika Igoma atafute gari nyingine au usafiri mwingine jambo linalosababisha kero na kuongeza gharama za usafiri kwa raia wa kawaida ambaye anaenda kwenye mizunguko yake ya kila siku.
Nilijaribu kuwasilisha jambo hili kwa mmoja wa maafisa wa usalama barabarani na alinipatia namba ya simu ikitokea nimepata changamoto hiyo.
Pamoja na kuwa mara kadhaa nimempigia kila tunapokutana na changamoto hiyo msaada hauonekani zaidi ya kuniambia ngoja niwasiliane na Askari aliyepo barabarani.
Ukimpigia tena anakwambia askari wote hawapo barabarani licha ya kwamba inakuwa bado mapema saa 11 au 12 Jioni ndio muda ambao kero hii inakithiri.
Tunaomba Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) upande wa Mwanza mtusaidie, tunaoteseka ni sisi Wananchi wa kipato cha chini kwa kulazimika kulipa nauli mara mbilimbili na kupoteza muda mwingi pia njiani.
Kwa hivyo, abiria wa Kisesa atakaepanda basi ajue akifika Igoma atafute gari nyingine au usafiri mwingine jambo linalosababisha kero na kuongeza gharama za usafiri kwa raia wa kawaida ambaye anaenda kwenye mizunguko yake ya kila siku.
Nilijaribu kuwasilisha jambo hili kwa mmoja wa maafisa wa usalama barabarani na alinipatia namba ya simu ikitokea nimepata changamoto hiyo.
Pamoja na kuwa mara kadhaa nimempigia kila tunapokutana na changamoto hiyo msaada hauonekani zaidi ya kuniambia ngoja niwasiliane na Askari aliyepo barabarani.
Ukimpigia tena anakwambia askari wote hawapo barabarani licha ya kwamba inakuwa bado mapema saa 11 au 12 Jioni ndio muda ambao kero hii inakithiri.
Tunaomba Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) upande wa Mwanza mtusaidie, tunaoteseka ni sisi Wananchi wa kipato cha chini kwa kulazimika kulipa nauli mara mbilimbili na kupoteza muda mwingi pia njiani.