Jeshi la Polisi lakanusha kumshikilia Sheikh Zuberi Nkokoo Mkoani Singida

Jeshi la Polisi lakanusha kumshikilia Sheikh Zuberi Nkokoo Mkoani Singida

Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida lakanusha taarifa zinazozambaa kuwa limemkamata na kumshikilia Shekhe Zuberi Nkokoo (53) mwalimu wa dini ya Kiislam kutoka Taasisi ya Islamic Foundation ambaye aliripotiwa kupotea Juni 02, 2025 majira ya saa 5:30 usiku akiwa karibu na Sheli ya Lake Oil iliyopo Mtaa wa Misuna, Manispaa ya Singida.

Jeshi la Polisi Singida linaendelea kufanya uchunguzi wa kubaini mahali alipo mtu huyo ili kujua kama amekamatwa au ameshikiliwa, mhusika ni nani na sababu za kushikiliwa kwake.

Aidha, Jeshi la Polisi Singida linawashikilia watu watatu kwa mahojiano ambao ni Abdul Ally (58), Mfanyabiashara na Mkazi wa Muriet mkoani Arusha, Shabani Ramadhani Ikenga (54), Mfanyabiashara na Mkazi wa Kisaki Manispaa ya Singida, na Maulid Mussa (52), Mfanyabiashara na Mkazi wa Muriet mkoani Arusha.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida linawataka wananchi kupuuza taarifa za uzushi na za uongo zinazozenezwa kwa nia ya kuleta taharuki kwa jamii na badala yake watoe ushirikiano kwa Jeshi la Polisi ili kubaini wapi alipo kiongozi huyo wa dini.

View attachment 3358145
Ukiona manyoa,ujue kaliwa!
CC: kifo ni kifo TU.
By saa100
 
Wanabalance ili ionekane hata waislamu nao wanatekwa.
Watekaji hawajahi kuwa na akili
Kwani mdude ni mkristo ?! Na marehemu Ally Kibao je ?! Acheni fikra za udini! Yaani mnatia aibu saa nyingine! Udini, udini , udini, haya semeni mdude ni muumini wa kanisa gani ?!
 
Back
Top Bottom