peno hasegawa
JF-Expert Member
- Feb 24, 2016
- 16,029
- 26,231
Ukiona manyoa,ujue kaliwa!Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida lakanusha taarifa zinazozambaa kuwa limemkamata na kumshikilia Shekhe Zuberi Nkokoo (53) mwalimu wa dini ya Kiislam kutoka Taasisi ya Islamic Foundation ambaye aliripotiwa kupotea Juni 02, 2025 majira ya saa 5:30 usiku akiwa karibu na Sheli ya Lake Oil iliyopo Mtaa wa Misuna, Manispaa ya Singida.
Jeshi la Polisi Singida linaendelea kufanya uchunguzi wa kubaini mahali alipo mtu huyo ili kujua kama amekamatwa au ameshikiliwa, mhusika ni nani na sababu za kushikiliwa kwake.
Aidha, Jeshi la Polisi Singida linawashikilia watu watatu kwa mahojiano ambao ni Abdul Ally (58), Mfanyabiashara na Mkazi wa Muriet mkoani Arusha, Shabani Ramadhani Ikenga (54), Mfanyabiashara na Mkazi wa Kisaki Manispaa ya Singida, na Maulid Mussa (52), Mfanyabiashara na Mkazi wa Muriet mkoani Arusha.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida linawataka wananchi kupuuza taarifa za uzushi na za uongo zinazozenezwa kwa nia ya kuleta taharuki kwa jamii na badala yake watoe ushirikiano kwa Jeshi la Polisi ili kubaini wapi alipo kiongozi huyo wa dini.
View attachment 3358145
CC: kifo ni kifo TU.
By saa100