Je, Wajua kuwa wimbo wa MB DOG "Mapenzi Kitu Gani" Ubeti wa kwanza ulikuwa unasifia na kutoa shukrani kwa Radio na Sio mapenzi kama wengi wadhaniavo

DR Mambo Jambo

JF-Expert Member
May 10, 2012
8,598
17,727
Kama ulibahatika kuwa Kijana au kuwa na umri wa utambuzi miaka hiyo Utakumbuka Zaidi Nyimbo Mojawapo iliyokuwa Gumzo miaka hiyo ni Mapenzi kitu gani ya MB DOG..

sasa leo Nataka kukuletea Story kidogo kuhusu Nyimbo hiyo kuwa Nyimbo hyo kwa 90% haikuzungumzia Mapenzi bali ilitoa Sifa na Shukrani kwa vipindi vya Refia pamoja na Redio zilizokuwa zinafanya vizuri wakati huo...

Ntanukuu versi hiyo...

Huamini miujiza mchumba,
Sauti ya nyuki inasikika,
Sogea karibu baby,
Times zishafika,
Unipe uhuru dear,
Ni kiss ninapotoka,
Toka mlimani dear,
niwe free ndani ya kopa,
Penzi kwa fujo my buu,
Moyo wangu ushauteka,
Raha ya Africa RTD mimi ndo one nasikika.
Hiv kwann dear moyo wangu unautesa,
Hivi hushoboki dear,
inavyonipenda East Africa....,


_______________
_______________

Zilizokuwa Bold hapo juu ni Radio na wadau wa kipindi hicho....
  • Miujiza (Magic Fm)
  • Sauti ya Nyuki -"Nyuki Djs" (Hawa walikuwa maDj wanajiita Nyuki Djs kina Steve B,Dj Too Shot,Dj Fetty,Mully B,Pitter Moo,DJ Venture pamoja na Dj Nelly na wengi wao walikuwa wakifanya kazi Mawingu Fm baadae Clouds FM..
  • Times (Times Fm)
  • Uhuru (Radio Uhuru)
  • kiss (Kiss Fm)
  • mlimani (Mlimani Fm)
  • free (RFA-Radio Free Africa)
  • kwa Fujo - kwa fujo Djs
  • RTD (Radio Tanzania Dar es salaam) ambayo sasa ndo TBC
  • One (Radio one Fm)
  • East africa (East Africa Radio )

Wasanii wa zamani walikuwa wabunifu sana ilikuwa inachukua Muda sana kujua Ujumbe aliowasilisha...

Kwa wasioijua nyimbo 👇👇👇


_____________________
___________<<<<
Shukrani Cannabis kwa interview Clip..

 
Aisee Asante sana mkuu leo ndio nimejua na pengine hata mwenyewe mb Dog hajui na aliltewa aimbe tuu kumbe ili kuwa ni praise and worship ili aweze kuishi!
Hufuatilii mambo, hilo jambo aliliongea mwenyewe mb dog kwenye interview yake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom