Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 57,101
- 128,716
Wanabodi
Je wajua kuna aina mbili za Malaika na Shetani?. Kuna Malaika wa Mbinguni ambao ni pepo na kuna malaika wa duniani ambao ni watu ni binadamu, na kuna ma shetani wa motoni ambao ni mapepo na kuna mashetani wa duniani ambao ni watu ni binadamu kabisa lakini ni ma shetani!.
Malaika wa Mbinguni ni wale malaika pepo ambao wanatumwa na Mungu mwenyewe, wanaweza kukutokea katika umbo lolote, hata la njiwa, kipepeo, hata mbu!. Na kuna malaika wa duniani ambao ni watu, ni binadamu.
Wale Malaika wa Mbinguni hukaa mbinguni, peponi ambapo shetani mwanzo alikuwa malaika, akaasi ndio akageuka shetani, akafukuzwa peponi na kutupwa motoni!.
Kazi ya malaika ni kutenda mema, na kazi ya shetani ni kutenda maovu.
Malaika akiasi, hugeuka shetani, anafukuzwa kule mbinguni peponi na kutupwa ushetanini ambako ni hapa duniani kuja kuvuna mavuno ya kwenda nayo motoni!.
Malaika wa dunia ni hawa binadamu wa kawaida kabisa wenye roho wa Mungu ndani yao, hivyo wanaotenda matendo mema ya kumpendeza Mungu.
Mashetani wa duniani nao ni hawa binadamu wa kawaida kabisa wenye roho ya shetani ambao ni watenda maovu.
Mtu mwema wa Mungu anaweza kupotea na kuanguka dhambini, akatenda maovu. Kipindi hicho mtu mwema anapoanguka dhambini, anakuwa ni amegeuka shetani na ameingia ushetani kwa kujiunga na shetani na anakuwa anaishi ushetanini kama mtumishi wa shetani na akifanya kazi ya shetani!.
Mtu huyu mwenye roho ya shetani, anakuwa na two options, ama aongoke mwenyewe, atubu madhambi yake, kwa kumkataa shetani na mambo yake yote kuyakataa, anakuwa ameongoka, ameokoka na roho wa Mungu anarejea ndani yake anakuwa ni mtu mwema, anarejea kuwa binadamu malaika mwema.
Asipo ongoka mwenyewe, anaweza kuongolewa kama ilivyo tokea kwa Sauli na kugeuka Paulo, huyu akiongolewa, anakuwa ameongoka unakuwa umeongolewa kutoka ushetanini, then inambidi kubadilika kwa kumkataa shetani na mambo yake yote kuyakataa.
Kufuatia kilicho mtokea Humphrey Polepole, naomba mtanisamehe bandiko hili nalikatia hapa, halitaendelea, limekuwa overtaken by events!.
Samahani sana.
Paskali
Je wajua kuna aina mbili za Malaika na Shetani?. Kuna Malaika wa Mbinguni ambao ni pepo na kuna malaika wa duniani ambao ni watu ni binadamu, na kuna ma shetani wa motoni ambao ni mapepo na kuna mashetani wa duniani ambao ni watu ni binadamu kabisa lakini ni ma shetani!.
Malaika wa Mbinguni ni wale malaika pepo ambao wanatumwa na Mungu mwenyewe, wanaweza kukutokea katika umbo lolote, hata la njiwa, kipepeo, hata mbu!. Na kuna malaika wa duniani ambao ni watu, ni binadamu.
Wale Malaika wa Mbinguni hukaa mbinguni, peponi ambapo shetani mwanzo alikuwa malaika, akaasi ndio akageuka shetani, akafukuzwa peponi na kutupwa motoni!.
Kazi ya malaika ni kutenda mema, na kazi ya shetani ni kutenda maovu.
Malaika akiasi, hugeuka shetani, anafukuzwa kule mbinguni peponi na kutupwa ushetanini ambako ni hapa duniani kuja kuvuna mavuno ya kwenda nayo motoni!.
Malaika wa dunia ni hawa binadamu wa kawaida kabisa wenye roho wa Mungu ndani yao, hivyo wanaotenda matendo mema ya kumpendeza Mungu.
Mashetani wa duniani nao ni hawa binadamu wa kawaida kabisa wenye roho ya shetani ambao ni watenda maovu.
Mtu mwema wa Mungu anaweza kupotea na kuanguka dhambini, akatenda maovu. Kipindi hicho mtu mwema anapoanguka dhambini, anakuwa ni amegeuka shetani na ameingia ushetani kwa kujiunga na shetani na anakuwa anaishi ushetanini kama mtumishi wa shetani na akifanya kazi ya shetani!.
Mtu huyu mwenye roho ya shetani, anakuwa na two options, ama aongoke mwenyewe, atubu madhambi yake, kwa kumkataa shetani na mambo yake yote kuyakataa, anakuwa ameongoka, ameokoka na roho wa Mungu anarejea ndani yake anakuwa ni mtu mwema, anarejea kuwa binadamu malaika mwema.
Asipo ongoka mwenyewe, anaweza kuongolewa kama ilivyo tokea kwa Sauli na kugeuka Paulo, huyu akiongolewa, anakuwa ameongoka unakuwa umeongolewa kutoka ushetanini, then inambidi kubadilika kwa kumkataa shetani na mambo yake yote kuyakataa.
Kufuatia kilicho mtokea Humphrey Polepole, naomba mtanisamehe bandiko hili nalikatia hapa, halitaendelea, limekuwa overtaken by events!.
Samahani sana.
Paskali