Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 7,200
- 12,691
Nilikuwa nasoma kitabu Desturi za Wachagga, by S. J. Ntiro, 1953. Jisomee mwenyewe.
Wachagga ni kabila lenye mchanganyiko wa makabila mengi sana. Makabila haya yameingia katika nchi ya Kilimanjaro katika nyakati tofauti. Makabila mengi yameingia Kilimanjaro yakikimbilia mwinuko wa nchi ili yaweze kuwaepuka maadui wao. Makabila mengi yalivutwa na rutuba ya nchi. Kwanza walijenga nyumba zao porini, lakini baadaye walipanda milima na kushika mahali kulikokuwa na vyakula zaidi. Iliwapasa kuwaheshimu wakubwa wa nchi ili wawaruhusu kuingia katika nchi. Makabila mengine yaliwafuata watu waliokuwa wakiishi katika nchi kwa kusudi la kuwanyang'anya mali, kama ng'ombe, mbuzi, na kondoo zao. Mara kwa mara mapigano yalitokea. Wenyeji waliwakimbilia kwa mikuki na marungu kuwazuia wasichukue mali zao. Wakati mwingine makabila yaliyoingia yalishindwa na wenyeji, lakini wakati mwingine ilikuwa kinyume. Kwa ufupi, hizi ndizo sababu kubwa zilizovuta makabila mbalimbali yaliyoingia Kilimanjaro.
Lugha za Kichagga ni uthibitisho mmoja mkubwa wa kuonyesha kuwa asili ya Wachagga ni makabila mengi. Nchi nzima ya Kilimanjaro imegawanyika katika sehemu ndogo ndogo 22 za watu wasemao lugha tofauti za Kichagga. Maneno ya sehemu moja ni tofauti na maneno ya sehemu nyingine kwa namna wanavyotamka ijapokuwa mtu wa sehemu moja anaweza kuelewa asemayo mtu wa sehemu nyingine. Tofauti ya namna hii katika sehemu za kabila moja si nzuri kwa sababu ni rahisi kuleta matangamano katika nchi.
Sehemu kubwa ya asili ya kabila la Kichagga ni Masai. Masai ni watu wapendao ng'ombe. Waliingia Kilimanjaro wakapigana na wenyeji na kuwanyang'anya ng'ombe na mbuzi na kondoo: kila wakati Masai walipokuja ilikuwa vita. Wengi wa Masai walifukuzwa na kurejea maporini ambako wanaishi mpaka leo, lakini wengi wao walibaki katika nchi wakageuka kuwa Wachagga. Kupata wanawake lilikuwa kusudi lingine lililowafanya Masai kupigana na watu waliokaa Kilimanjaro. Baada ya vita ambazo Masai walishinda, waliwachukua wanawake mateka Masaini. Tangu zamani za kale desturi ya kuwavizia wanawake na kuwaiba inaendelea mpaka hivi leo kidogo kidogo maporini. Siyo kwamba Masai wanawatesa wanawake hawa ila waliwapeleka kuzidisha kabila lao.
Wasambaa, Wapare, Wameru na Wakilindi ni makabila yaliyoingia Kilimanjaro katika nyakati mbalimbali. Makabila haya manne yaliingia kwa upole na utaratibu kuliko Masai. Mpaka leo hivi Wapare wanaingia Kilimanjaro ya mashariki kwa wingi.
NB. Kitabu kinapatikana ndani ya maktabaapp
MLANGO WA 5
ASILI YA WACHAGGA
ASILI YA WACHAGGA
Wachagga ni kabila lenye mchanganyiko wa makabila mengi sana. Makabila haya yameingia katika nchi ya Kilimanjaro katika nyakati tofauti. Makabila mengi yameingia Kilimanjaro yakikimbilia mwinuko wa nchi ili yaweze kuwaepuka maadui wao. Makabila mengi yalivutwa na rutuba ya nchi. Kwanza walijenga nyumba zao porini, lakini baadaye walipanda milima na kushika mahali kulikokuwa na vyakula zaidi. Iliwapasa kuwaheshimu wakubwa wa nchi ili wawaruhusu kuingia katika nchi. Makabila mengine yaliwafuata watu waliokuwa wakiishi katika nchi kwa kusudi la kuwanyang'anya mali, kama ng'ombe, mbuzi, na kondoo zao. Mara kwa mara mapigano yalitokea. Wenyeji waliwakimbilia kwa mikuki na marungu kuwazuia wasichukue mali zao. Wakati mwingine makabila yaliyoingia yalishindwa na wenyeji, lakini wakati mwingine ilikuwa kinyume. Kwa ufupi, hizi ndizo sababu kubwa zilizovuta makabila mbalimbali yaliyoingia Kilimanjaro.
Lugha za Kichagga ni uthibitisho mmoja mkubwa wa kuonyesha kuwa asili ya Wachagga ni makabila mengi. Nchi nzima ya Kilimanjaro imegawanyika katika sehemu ndogo ndogo 22 za watu wasemao lugha tofauti za Kichagga. Maneno ya sehemu moja ni tofauti na maneno ya sehemu nyingine kwa namna wanavyotamka ijapokuwa mtu wa sehemu moja anaweza kuelewa asemayo mtu wa sehemu nyingine. Tofauti ya namna hii katika sehemu za kabila moja si nzuri kwa sababu ni rahisi kuleta matangamano katika nchi.
Sehemu kubwa ya asili ya kabila la Kichagga ni Masai. Masai ni watu wapendao ng'ombe. Waliingia Kilimanjaro wakapigana na wenyeji na kuwanyang'anya ng'ombe na mbuzi na kondoo: kila wakati Masai walipokuja ilikuwa vita. Wengi wa Masai walifukuzwa na kurejea maporini ambako wanaishi mpaka leo, lakini wengi wao walibaki katika nchi wakageuka kuwa Wachagga. Kupata wanawake lilikuwa kusudi lingine lililowafanya Masai kupigana na watu waliokaa Kilimanjaro. Baada ya vita ambazo Masai walishinda, waliwachukua wanawake mateka Masaini. Tangu zamani za kale desturi ya kuwavizia wanawake na kuwaiba inaendelea mpaka hivi leo kidogo kidogo maporini. Siyo kwamba Masai wanawatesa wanawake hawa ila waliwapeleka kuzidisha kabila lao.
Wasambaa, Wapare, Wameru na Wakilindi ni makabila yaliyoingia Kilimanjaro katika nyakati mbalimbali. Makabila haya manne yaliingia kwa upole na utaratibu kuliko Masai. Mpaka leo hivi Wapare wanaingia Kilimanjaro ya mashariki kwa wingi.
NB. Kitabu kinapatikana ndani ya maktabaapp