Je, Wachagga na Wamasai ni ndugu moja?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,200
12,691
Nilikuwa nasoma kitabu Desturi za Wachagga, by S. J. Ntiro, 1953. Jisomee mwenyewe.

MLANGO WA 5

ASILI YA WACHAGGA

Wachagga ni kabila lenye mchanganyiko wa makabila mengi sana. Makabila haya yameingia katika nchi ya Kilimanjaro katika nyakati tofauti. Makabila mengi yameingia Kilimanjaro yakikimbilia mwinuko wa nchi ili yaweze kuwaepuka maadui wao. Makabila mengi yalivutwa na rutuba ya nchi. Kwanza walijenga nyumba zao porini, lakini baadaye walipanda milima na kushika mahali kulikokuwa na vyakula zaidi. Iliwapasa kuwaheshimu wakubwa wa nchi ili wawaruhusu kuingia katika nchi. Makabila mengine yaliwafuata watu waliokuwa wakiishi katika nchi kwa kusudi la kuwanyang'anya mali, kama ng'ombe, mbuzi, na kondoo zao. Mara kwa mara mapigano yalitokea. Wenyeji waliwakimbilia kwa mikuki na marungu kuwazuia wasichukue mali zao. Wakati mwingine makabila yaliyoingia yalishindwa na wenyeji, lakini wakati mwingine ilikuwa kinyume. Kwa ufupi, hizi ndizo sababu kubwa zilizovuta makabila mbalimbali yaliyoingia Kilimanjaro.

Lugha za Kichagga ni uthibitisho mmoja mkubwa wa kuonyesha kuwa asili ya Wachagga ni makabila mengi. Nchi nzima ya Kilimanjaro imegawanyika katika sehemu ndogo ndogo 22 za watu wasemao lugha tofauti za Kichagga. Maneno ya sehemu moja ni tofauti na maneno ya sehemu nyingine kwa namna wanavyotamka ijapokuwa mtu wa sehemu moja anaweza kuelewa asemayo mtu wa sehemu nyingine. Tofauti ya namna hii katika sehemu za kabila moja si nzuri kwa sababu ni rahisi kuleta matangamano katika nchi.

Sehemu kubwa ya asili ya kabila la Kichagga ni Masai. Masai ni watu wapendao ng'ombe. Waliingia Kilimanjaro wakapigana na wenyeji na kuwanyang'anya ng'ombe na mbuzi na kondoo: kila wakati Masai walipokuja ilikuwa vita. Wengi wa Masai walifukuzwa na kurejea maporini ambako wanaishi mpaka leo, lakini wengi wao walibaki katika nchi wakageuka kuwa Wachagga. Kupata wanawake lilikuwa kusudi lingine lililowafanya Masai kupigana na watu waliokaa Kilimanjaro. Baada ya vita ambazo Masai walishinda, waliwachukua wanawake mateka Masaini. Tangu zamani za kale desturi ya kuwavizia wanawake na kuwaiba inaendelea mpaka hivi leo kidogo kidogo maporini. Siyo kwamba Masai wanawatesa wanawake hawa ila waliwapeleka kuzidisha kabila lao.

Wasambaa, Wapare, Wameru na Wakilindi ni makabila yaliyoingia Kilimanjaro katika nyakati mbalimbali. Makabila haya manne yaliingia kwa upole na utaratibu kuliko Masai. Mpaka leo hivi Wapare wanaingia Kilimanjaro ya mashariki kwa wingi.

NB. Kitabu kinapatikana ndani ya maktabaapp

Desturi za wachagga cover.png
 
Mkuu wachaga ni Eastern Bantu. Eastern Bantu ni Wachagga, Meru Tanzania, Wapare, Wagweno na makabila yote ya Tanga. Pia Eastern Bantu ni wakikuyu, Wakamba meru Kenya, Embu, Taita. Walisafiri pamoja kutoka kongo zamani sana ila hao Eastern Bantu wa Tanzania wakaamua kusettle permanently Tanzania na wale wengine wakaendelea kusonga mbelw na kusettle mlima Kenya na huko kwa wakamba na Taita.

Masai siyo Bantu hawana undugu kabisa na wachaga. Masai ni plain nilotes asili yao ni southern Ethiopia. Wanaundugu na wasamburu na makambila ya southern nation Ethiopia kama Hamer.
 
Mkuu wachaga ni Eastern Bantu. Eastern Bantu ni Wachagga, Meru Tanzania, Wapare, Wagweno na makabila yote ya Tanga. Pia Eastern Bantu ni wakikuyu, Wakamba meru Kenya, Embu, Taita. Walisafiri pamoja kutoka kongo zamani sana ila hao Eastern Bantu wa Tanzania wakaamua kusettle permanently Tanzania na wale wengine wakaendelea kusonga mbelw na kusettle mlima Kenya na huko kwa wakamba na Taita.

Masai siyo Bantu hawana undugu kabisa na wachaga. Masai ni plain nilotes asili yao ni southern Ethiopia. Wanaundugu na wasamburu na makambila ya southern nation Ethiopia kama Hamer
Inasemwa pia Wachagga wana damu ya Waoromo kutoka Ethiopia. Inawezekana kiini chao, na wenye lugha ya kichagagga walikuwa ni hao Eastern bantu. Lakini baadaye watu wengi waliingia uchagani na hata kumeza Wachagga wabantu. Sura hiyo inasema sehemu kubwa ya mchanganyiko huo ni Wamasai.
 
Inasemwa pia Wachagga wana damu ya Waoromo kutoka Ethiopia. Inawezekana kiini chao, na wenye lugha ya kichagagga walikuwa ni hao Eastern bantu. Lakini baadaye watu wengi waliingia uchagani na hata kumeza Wachagga wabantu. Sura hiyo inasema sehemu kubwa ya mchanganyiko huo ni Wamasai.
Hapana Oromo, Somali na Borana ni Cushites. Wachagga ni Bantus pure Bantus kutoka Congo/Cameroon karne na karne huko
 
Miaka mingi nyuma kulikuwa na vitabu vya shule 'Oxford English Course for East African Students'. Vitabu hivi vya primary schools vilikuwa na hadithi za watu wa East Africa na moja ya hadithi ilikuwa inazungumzia 'A chagga boy and a Kisii boy (sikumbuki exactly ilikuwa inazungumzia nini nakumbuka title na picha tu). Picha iliyochorwa ilionyesha kijana wa kichaga amevaa na kusuka kama mmasai na mimi kwa siku nyingi nikidhania hawa watu wamefanana makabila.
 
Hili suala la utofauti wa lugha mbona lipo sehemu nyingi.

Mgogo wa mpwapwa anatofautiana kimatamshi na baadhi ya maneno na mgogo wa Bahi.

Uwezekano wa makabila kujichanganya uchagani upo , maana nimeshasikia wakisimulia mila za kuwakubali watu katika ukoo.

Pia hata wale waliokuwa wanachukuliwa kufanya kazi za kilimo na wakoloni walizamia Moshi na kuchanganyikana na wachagga.

Vilevile rutuba iliyopo mlimani ni kivutio kwa watu wengi , kwahiyo sishangai kama kuna wamasai watakuwa walihamia hapo na kuwa assimilated.
 
Nilisikiaga wazee wakisema kuwa

"Sisi baba yetu mzaa babu alikua ni mmasai .....na alioa wanawake wengi na kila kaya ilikua ni wafugaji na wanamiliki aina Fulani ya mifugo, , ....'''
 
Nilisikiaga wazee wakisema kuwa

"Sisi baba yetu mzaa babu alikua ni mmasai .....na alioa wanawake wengi na kila kaya ilikua ni wafugaji na wanamiliki aina Fulani ya mifugo, , ....'''
Hivyo nazani kulingana na majadiliano ya wadah kadhaa hapo juu,,, kwa wachaga walioko saivi Kuna mchanganyiko wa Nilotes na wabantu
 
Nilikuwa nasoma kitabu Desturi za Wachagga, by S. J. Ntiro, 1953. Jisomee mwenyewe.

MLANGO WA 5

ASILI YA WACHAGGA

Wachagga ni kabila lenye mchanganyiko wa makabila mengi sana. Makabila haya yameingia katika nchi ya Kilimanjaro katika nyakati tofauti. Makabila mengi yameingia Kilimanjaro yakikimbilia mwinuko wa nchi ili yaweze kuwaepuka maadui wao. Makabila mengi yalivutwa na rutuba ya nchi. Kwanza walijenga nyumba zao porini, lakini baadaye walipanda milima na kushika mahali kulikokuwa na vyakula zaidi. Iliwapasa kuwaheshimu wakubwa wa nchi ili wawaruhusu kuingia katika nchi. Makabila mengine yaliwafuata watu waliokuwa wakiishi katika nchi kwa kusudi la kuwanyang'anya mali, kama ng'ombe, mbuzi, na kondoo zao. Mara kwa mara mapigano yalitokea. Wenyeji waliwakimbilia kwa mikuki na marungu kuwazuia wasichukue mali zao. Wakati mwingine makabila yaliyoingia yalishindwa na wenyeji, lakini wakati mwingine ilikuwa kinyume. Kwa ufupi, hizi ndizo sababu kubwa zilizovuta makabila mbalimbali yaliyoingia Kilimanjaro.

Lugha za Kichagga ni uthibitisho mmoja mkubwa wa kuonyesha kuwa asili ya Wachagga ni makabila mengi. Nchi nzima ya Kilimanjaro imegawanyika katika sehemu ndogo ndogo 22 za watu wasemao lugha tofauti za Kichagga. Maneno ya sehemu moja ni tofauti na maneno ya sehemu nyingine kwa namna wanavyotamka ijapokuwa mtu wa sehemu moja anaweza kuelewa asemayo mtu wa sehemu nyingine. Tofauti ya namna hii katika sehemu za kabila moja si nzuri kwa sababu ni rahisi kuleta matangamano katika nchi.

Sehemu kubwa ya asili ya kabila la Kichagga ni Masai. Masai ni watu wapendao ng'ombe. Waliingia Kilimanjaro wakapigana na wenyeji na kuwanyang'anya ng'ombe na mbuzi na kondoo: kila wakati Masai walipokuja ilikuwa vita. Wengi wa Masai walifukuzwa na kurejea maporini ambako wanaishi mpaka leo, lakini wengi wao walibaki katika nchi wakageuka kuwa Wachagga. Kupata wanawake lilikuwa kusudi lingine lililowafanya Masai kupigana na watu waliokaa Kilimanjaro. Baada ya vita ambazo Masai walishinda, waliwachukua wanawake mateka Masaini. Tangu zamani za kale desturi ya kuwavizia wanawake na kuwaiba inaendelea mpaka hivi leo kidogo kidogo maporini. Siyo kwamba Masai wanawatesa wanawake hawa ila waliwapeleka kuzidisha kabila lao.

Wasambaa, Wapare, Wameru na Wakilindi ni makabila yaliyoingia Kilimanjaro katika nyakati mbalimbali. Makabila haya manne yaliingia kwa upole na utaratibu kuliko Masai. Mpaka leo hivi Wapare wanaingia Kilimanjaro ya mashariki kwa wingi.

NB. Kitabu kinapatikana ndani ya maktabaapp

View attachment 2510854
Ni kweli Kuna wachagga wengi wenye asili ya kimasai! Mm Babu yetu WA ukoo alikua mmasai kabisa na jina alotumia Leo linatumika umasaini tena wale wamasai wa Kenya ! Sisi wenyewe ukoo wetu maana yake inadhihirisha tulikua wamasai na kazi kubwa ilikua ufugaji
 
Mkuu wachaga ni Eastern Bantu. Eastern Bantu ni Wachagga, Meru Tanzania, Wapare, Wagweno na makabila yote ya Tanga. Pia Eastern Bantu ni wakikuyu, Wakamba meru Kenya, Embu, Taita. Walisafiri pamoja kutoka kongo zamani sana ila hao Eastern Bantu wa Tanzania wakaamua kusettle permanently Tanzania na wale wengine wakaendelea kusonga mbelw na kusettle mlima Kenya na huko kwa wakamba na Taita.

Masai siyo Bantu hawana undugu kabisa na wachaga. Masai ni plain nilotes asili yao ni southern Ethiopia. Wanaundugu na wasamburu na makambila ya southern nation Ethiopia kama Hamer.
Sahihi
 
Lakini angalia Wachagga wengi wao. Ni kweli lugha yao ni ya kibantu, lakini features zao unaona ni kama wabantu wengine? Wamekaa kinilotic na kikush hivi.
hamna kitu.
Unataka kutuambia zile zisizoonekana na wamama wa Kichanga na vile vitambi kama gunia ndo maumbo ya wakushi na Wanilotiki??
 
Ni kweli Kuna wachagga wengi wenye asili ya kimasai! Mm Babu yetu WA ukoo alikua mmasai kabisa na jina alotumia Leo linatumika umasaini tena wale wamasai wa Kenya ! Sisi wenyewe ukoo wetu maana yake inadhihirisha tulikua wamasai na kazi kubwa ilikua ufugaji
Kiruu! hebu nenda kuleee!
 
Wamasai na wachaga sijawahi kusikia walikuwa na significant conflicts ardhi ya wachaga haifai kwa ufugaji so logically sio kweli kuwa wachaga walikuwa na mifugo mingi.....
Wachaga ni wabantu na wamasai nilotics hakuna ukaribu hata kidogo hapa
 
Back
Top Bottom