Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 11,618
- 20,556
Maneno haya yaliandikwa kabla ya uhuru, 1953
BIASHARA NA WAHINDI
Haiwezekani kufikiria biashara ya nchi ya Kilimajaro bila kuwakumbuka Wahindi. Wahindi wamejiingiza katika biashara ya Kilimanjaro kuliko kabila lingine lo lote. Wahindi wananunua na kuuza karibu kila kitu Wachagga Wanachonunua. Wamejenga majumba makubwa na wamezuia biashara yote ya nchi.
Zaidi ya hayo wanapata karibu fedha zote za biashara na wanazipeleka India.
Njia iliyopo ni Wachagga kujiunga na kufanya biashara kwa umoja. Kama maduka makubwa ya umoja yakifunguliwa kwa msaada wa serikali kwa maonyi na uongozi mwanzoni, faida nyingi itapatikana ambayo itatumiwa kwa njia nyingi zitakazohitaji fedha siku hizi.
Sisemi Wahindi ni watu wabaya na kwa hiyo wafukuzwe kwa nguvu. Wahindi tangu walipoingia Kilimanjaro wamekwisha fanya kazi ya manufaa kwa nchi; hapakuwako duka hata moja walipokuja. Ni vizuri Wachagga watoe ahsante kwao. Lakini wakati umekuja sasa ambao ni lazima Wachagga wafanye biashara ya nchi yao na kuanza kushindana na Wahindi katika biashara polepole.
BIASHARA NA WAHINDI
Haiwezekani kufikiria biashara ya nchi ya Kilimajaro bila kuwakumbuka Wahindi. Wahindi wamejiingiza katika biashara ya Kilimanjaro kuliko kabila lingine lo lote. Wahindi wananunua na kuuza karibu kila kitu Wachagga Wanachonunua. Wamejenga majumba makubwa na wamezuia biashara yote ya nchi.
Zaidi ya hayo wanapata karibu fedha zote za biashara na wanazipeleka India.
Njia iliyopo ni Wachagga kujiunga na kufanya biashara kwa umoja. Kama maduka makubwa ya umoja yakifunguliwa kwa msaada wa serikali kwa maonyi na uongozi mwanzoni, faida nyingi itapatikana ambayo itatumiwa kwa njia nyingi zitakazohitaji fedha siku hizi.
Sisemi Wahindi ni watu wabaya na kwa hiyo wafukuzwe kwa nguvu. Wahindi tangu walipoingia Kilimanjaro wamekwisha fanya kazi ya manufaa kwa nchi; hapakuwako duka hata moja walipokuja. Ni vizuri Wachagga watoe ahsante kwao. Lakini wakati umekuja sasa ambao ni lazima Wachagga wafanye biashara ya nchi yao na kuanza kushindana na Wahindi katika biashara polepole.