Je, Wabunge Viti Maalum ni wa kubebwa? Mnaonaje iwe ni awamu moja tuu kisha waendeni jimboni, kupisha wengine, au waendelee kubebwa tu?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,468
113,583
Wanabodi,

Kwanza angalieni hii picha
More than 60% of Rwanda’s parliamentarians are women. Photo: Sam Ngendahimana
More than 60% of Rwanda’s parliamentarians are women. Photo: Sam Ngendahimana

Nimesoma kwenye Ripoti ya WB, Bunge la Rwanda ndilo Bunge linaloongoza Dunia kwa gender equality baada ya kuwa na asilimia kubwa ya wabunge wanawake kuliko wanaume, wakati Bara la Africa likiongoza duniani kwa kuwa na maspika wengi wanawake kuliko mabara yote.

Hii maana yake ni gender equality is possible ila pia nafasi za upendeleo kwa wanawake vikiwemo viti maalum, dhumuni lake sio kuongeza tuu idadi ya wanawake bungeni, bali ni kuwajengea uwezo wabunge wanawake walioteuliwa, yaani empowerment, kuwa empower.

Hilo kwa Rwanda limewezekana kwasababu ubunge wa viti maalum kule ni kwa awamu moja tuu, awamu ya pili wanakwenda majimboni na kupisha wengine.

Mnaonaje na sisi Tanzania tukafuata mfumo huo?.

Japo sio neno zuri kulitumia lakini ndio ukweli wenyewe, Ubunge wa Viti Maalum ni ubunge wa kubebwa. Sasa kama wewe Mbunge mwanamke umebahatika kubebwa, ukaukwaa ubunge wa Viti Maalum, na ukakaa Bungeni miaka 5, maana yake umeisha kuwa empowered, huhitaji kubebwa tena kumendea ubunge kupitia Viti Maalum, sasa unakuwa umeiva kustahili kwenda kugombea jimboni.

Kama umekuwa Mbunge Viti Maalum miaka mitano na bado huwezi kwenda jimboni, then wewe utakuwa hufai, hata ukirudi Bungeni utakuwa huna jipya!, hivyo ni bora upumzishwe, wapewe nafasi wengine wenye uwezo wa kujiongeza kwasababu kiukweli kabisa kuna baadhi ya hawa wabunge wa viti maalum huwasikii wakichangia mjadala wowote zaidi ya kuupara na kutokelezea, hadi watu humu kuwabatiza jina la Wabunge wa "Vitu Maalum".

Ukibebwa, bebeka, haiwezekani mtu ubebwe mara ya kwanza, uvushwe mto mpaka ng'ambo ya pili, halafu baada ya kufika upande wa pili, badala ya kushuka na kutembea mwenyewe, wewe bado unang'ang'ania mgongoni uendelee kubebwa!. Kitakacho fuata hapo ni wewe kubwaga tuu chini puu!, unless huyo anayekubeba, naye anapata uroda fulani kukubeba,maana kiukweli ukibeba chochote nimzigo kwako,ila kama mzigo huo unafaida kwako, japo ni mateso kuendelea kuubeba, utaendelea kuubeba tuu.

Mnaonaje wanabodi, hawa wabunge wa kubebwa kupitia Viti Maalum, wawekewe ukomo wa miaka 5 tuu au kwa sababu kubebwa ni raha, na kula uroda hivyo wabebaji wanapenda kuendelea tuu kubeba na wabebwaji wanaona uroda kubebwa?.

Ukibebwa bebeka, na next time jibebe, usibwete, na kupenda kuendelea kubebwa tuu, oneni aibu!. Tuweni kama Rwanda!.

Vipi wajameni, wa kubebwa waendelee kubebwa tuu au wajibebe, na wasipojibeba wabwagwe?

Paskali
 
Rwanda in nchi ya kidikiteita Africa na labda inaongoza kwa udikiteita. Si ajabu hao wote wameingizwa kwa njia kama ya uchaguzi wa Serikali za mitaa wa hapa ili kupunguza nguvu ya kuhoji bungeni. Na nadhani hiyo mbinu ya serikali za mitaa, Jiwe ameikopi toka Rwanda. Hivyo hoja yako haina mashiko.

Ingelikuwa picha hiyo ni ya say Sweden, Norway, Denmark and the like, ningelikupa like.
 
Kati ya fursa zinazotumika kudhalilisha wanawake ni ubunge wa upendeleo (wenyewe wanaficha na kuita viti maalum)!

Huu ni utaratibu wa kipuuzi wenye lengo la kuimarisha mfumo dume! Ni either wanasogezwa karibu wakaliwe au wanapewa fursa za kuthibitisha kuwa bila wanaume kuwabeba au kuwapa fursa wasingezipata!

No such a thing as free lunch. Ukweli utawaweka huru! Kama wanataka Uhuru kamili wakachuane majimboni!!

Vinginevyo hawana tofauti na wale wanawake wanaosimama barabarani kusubiria fursa za upendeleo usiku wa manane!

Hongera na heshima tele kwa wanawake wabunge waliochuana majimboni kupata nafasi zao...!
 
Paskali,
1. huwa ninasikitika na kufadhaishwa sana Tanzania inapolinganishwa na Rwanda.

2. Hakuna ubunge mugumu kuupata kama ubunge wa vitu maalumu, hao akina mama huwa wanahangaika sana, wanatembea mkoa mzima kuwaona wapiga kura wao wakati wabunge wa majimbo wanatemblea vikata vichache.

3. utaratibu wa vitu maalumu unaakisi mfumo dume katika jamii yetu- utaisha pale mfumo dume utakapo isha. nina hakika wanaume hatukubali mfumo dume ufe kwani unatufaidisha sana.

4. Tuuundeleze utamaduni huu wa viti maalumu; tukiufuta na wanawake ambao ni wengi wakiamua hilo bunge watakuwa wao tu.

5. so wanaumeeeeeeeeeeeeeee SHSSSSS msiwaamshe wanawake ni jeshi kubwa.
 
Hatuna cha kujifunza toka Rwanda, Kagame anapenda hao wanawake kwakua ni rahisi kuwaendesha, yes huo ndio ukweli. Na hata akitoka madarakani atamwachia mwanamke ili yeye aendelee kuwa rais kutokea nyumbani kwake.
 
Watawala wetu ndio wanaweza kuamua hilo kama wakiona lina tija kwao.

Sisi raia wa kawaida hata kama tukitaka hivyo viti visiwepo na watawala wanavitaka hatuwezi kubadilisha chochote.
 
Kwa taarifa yako kutokana na mwenendo wa Magufuli kuchezea box la kura, hata bunge lijalo iwapo hakutakuwa na tume huru ya uchaguzi, bunge zima litakuwa la viti maalum maana wote watapita bila kupingwa. Kwa hiyo hii hoja yako kwa mazingira haya tayari ni hoja mfu.
 
Pascal Mayalla,
Dawa ilikuwa ndani ya katiba ya Warioba. Ilikuwa haina viti maalum lakini ililazimisha uchaguzi wa wabunge wanawake na wanaume kwa lazima, kwa pamoja. Sitta aliyejidai kuwa ni samaki aliyerudi majini akajikuta hana muelekeo na Bunge lake. Aibu tupu!

Hata wakijaa Bungeni haisaidii kueleza gender equality maana vijijini bado wanawake wanahangaika. Bahati mbaya hili akina Pompeo hawalioni na badala yake wanahangaika na mambo ya mashoga,
 
inajulikana wazi dunia nzima toka kuumbwa kwa ulimwengu wanawake ni dhaifu dhidi ya wanaume kwa nchi za ki afrika ambazo zinaongozwa ki dikiteta kuwa na wabunge na Maspika wengi wanawake ni fursa tosha kwa Mtawala. Wanawake wengi duniani kwenye uongozi ni ndio Mzee!
 
wakagombee majimboni, na hao walioko majimboni waende wapi? majimbo yako machache, kwanza wabunge wa viti maalum ni wachache inafaa waongezwe, kila jimbo inafaa liwe na mbunge wa viti maalum idadi iwe sawa
 
Back
Top Bottom