CHADEMA iweke mfumo mzuri wa viti maalum

econonist

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
15,766
21,761
Ningependa kukishauri chama Cha CHADEMA kiweke mfumo mzuri wa viti maalum ulio wazi Ili kuepuka Yale ya Covid 19 yasijirudie. Tujifunze kutokana na makosa, la sivyo huko mbeleni litajirudia Tena. Hili la kusema wanawake waliogombea majimboni na kushindwa watapewa nafasi ya mbele kwenye Viti Maalim sio mzuri kabisa.

Akina Halima Mdee walitumia huo mwanya kujiingiza bungeni bila kufuata kanuni na sheria. Inakuaje mnaruhusu mgombea ubunge jimboni akishindwa kwenye Jimbo anapewa nafasi ya viti maalum?

Halima Mdee kagombea Kawe kashindwa na Ask. Gwajima halafu Cha kushangaza anawaacha wote walioshinda viti maalum huko mikoani Dares salaam kwenye chama na kujipeleka bungeni.

Nadhani Ni muda Sasa turuhusu wale waliogombea viti maalum kwenye majimbo au Mkoa ndio wapewe nafasi za viti maalum,baadala ya kuwapa walioshindwa majimboni. Inaondoa maana ya viti maalum

Kwa mfano, Esther matiko aligombea tarime, bulaya aligombea bunda, kaboyoka same, Mdee aligombea kawe, makamba aligombea shinyanga, mwaifunga aligombea Tabora mjini, etc. Lakini wote Hawa na wengine wamechukua nafasi za wale walioshinda viti maalum.

Tuamue moja anayekubali kugombea viti maalum agombee na apewe nafasi na anayegombea jimboni agombee akishindwa ajiandae kwa uchaguzi mwingine.

Pia chama kijitahidi kabla ya uchaguzi kiwe tayari na list yake ya wabunge wa viti maalum, ili wakichakachua kuwepo na rejea ya kupitia majina halali. Sio mpaka uchguzi uishe ndio Tume isubirie majina Hapo ndipo wenye Nia ovu wanatumia kuvuruga chama.
 
Ngumu sana. Kwanza kuna ile mtu anagombea jimboni na pia anagombea viti maalum pia
 
Ningependa kukishauri chama Cha CHADEMA kiweke mfumo mzuri wa viti maalum ulio wazi Ili kuepuka Yale ya Covid 19 yasijirudie. Tujifunze kutokana na makosa...
Unajua kuwa hizo kura zao majimboni zinaleta viti maalum? Pili halima alikuwa mwenyekiti bawacha kwahiyo alikuwa na tiketi tayari ya mjengoni
 
Ningependa kukishauri chama Cha CHADEMA kiweke mfumo mzuri wa viti maalum ulio wazi Ili kuepuka Yale ya Covid 19 yasijirudie. Tujifunze kutokana na makosa...
Mkuu huu uzi wako na ushauri wako vimepuuzwa kwa sababu wewe bado haujasajiliwa katika kundi lao la chawa wa mwenyekiti.

Laiti ungekuwa miongoni mwa chawa wa mwenyekiti basi uzi wako ungejaa Like na Comments mbali mbali za kuusifu uzi wako. Dah pole san mkuu.
 
Hizo kura jimboni husababisha idadi ya viti maalum. Uliwafuatilia viti maalum wa vyama karibu vyote wanachokifanya bungeni ni hawana maajabu.
 
Ningependa kukishauri chama Cha CHADEMA kiweke mfumo mzuri wa viti maalum ulio wazi Ili kuepuka Yale ya Covid 19 yasijirudie...
Sheria zipo wazi kuwa Wabunge viti maalum wanachaguliwa na Kamati kuu then Katibu Mkuu anapeleka majina so hao wamefoji ambacho ni kinyume Cha Sheria. So whether mchakato ungekua wazi au sio wazi obviously kina Mdee Bado tu wangefanya walichofanya coz forgery haihitaji process yoyote ya kisheria ifuatwe.

Kingine CHADEMA iliweka wagombea ubunge zaidi ya 70 wanawake sasa unakuta Jimbo kama Kigamboni 2015 mgombea wa CHADEMA alishindwa ila alikua na kura nyingi kuliko majimbo yote ya Pemba!! Sasa mtu kama huyo utamnyima viti maalum?

Mind you kura za wagombea ubunge ndio zinazaa viti maalum ndio maana licha ya CHADEMA kuporwa majimbo yote Bado ilikua na slots 20 sababu wagombea ubunge walipata kura million 2. So waliochangia Ile pool obviously watapewa kipaumbele viti maalum.

Hii inafanyika Ili BAWACHA iwe strong movement unlike UWT au UVCCM ambapo watu wanaingia kusaka teuzi tu wakikosa huwasikii kwenye harakati.
 
Naunga mkono hoja, pia nashauri kuwa viti maalum ni miaka mitano tu, ukishakuwa mbunge hupaswi kuja kuwa mbunge kupitia viti maalum tena. Na ni vyema uwe viti maalum kama hujafikisha miaka 35.
Hili tayari linafanyika kwa upande wa CHADEMA ukishakuwa viti maalum lazima ukagombee jimboni uchaguzi unaofuata ndio maana viti maalum wote wa 2015-20 waliingia majimboni hawakutakiwa kuomba ubunge wa viti maalum tena kupitia Kura za maoni viti maalum
 
Hili tayari linafanyika kwa upande wa CHADEMA ukishakuwa viti maalum lazima ukagombee jimboni uchaguzi unaofuata ndio maana viti maalum wote wa 2015-20 waliingia majimboni hawakutakiwa kuomba ubunge wa viti maalum tena.

Hii ya kina Halima Mdee, Ester Bulaya, Kaboyoka and the likes ilikuwaje kaka? Check your facts right.
 
Back
Top Bottom