Ndugu zangu, mimi baada ya kusikiliza na kutazama matangazo ya hawa jamaa, nimegundua kuwa hawatafuti vazi la Taifa, bali kitambaa......na baada ya kuwasikiliza zaidi, nikafahamu pia kumbe wanazo na hata rangi za hicho kitambaa, ambazo ni rangi ya bendera............... Baada ya kugundua hvyo, nikajiuliza! Sasa kwa nini wanatafuta kitambaa ilihali mabendera yenye rangi wanayoitaka ipo kibao, kwanini wasiende kuchukua hayo na kutuondolea kelele!
Sikuishia hapo lakini nikagundua kuwa Tanzania ni nchi inayoongozwa kwa matukio, kwahiyo hili suala la vazi sasa hivi limekuja ili kuwapoteza WaTz maboya wasiconcetrate kwenye issue muhimu zinazowaumiza kama umeme, mafuta na kupanda kwa gharama za maisha, badala yake wahangaike na huu upupu wa vazi. Sasa hv hakuna babu wa loliondo, no north mara, no maandamano ya cdm, no kafulila, no ajali ya meli, sasa dawa ni kuibua ujinga wa vazi.