Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,504
- 113,618
- Thread starter
-
- #81
Mkuu Joka Kuu, heshima mbele...Tafadhali Pascal Mayalla..tafadhali sana.
..wewe una heshima hapa JF.
..vijana wanakuamini ktk mabandiko yako.
..sasa siyo vizuri ukawapoteza namna hii.
..mgogoro wa Julian Asange unahusu KUDUKUA na kusambaza mawasiliano nyeti ya SEREKALI ya Marekani.
..ungewatendea haki vijana hawa wanaokuheshimu kama ungefafanua alichofanya Julian Asange, halafu ukalinganisha kama waTz tuna uhuru wa kufanya jambo linalokaribiana na alichofanya.
..au kwanini usituletee clip za MAHOJIANO kati ya VIONGOZI wa nchi za wenzetu na VYOMBO VYA HABARI halafu tuone kama na sisi tuko HURU na tuna WELEDI kiasi gani.
Kipindi cha JK Kubenea alipata wapi taarifa za Ikulu?mbona alitetewa kuwa ni uhuru wa habari?kwanini huyu jamaa akamatwe na watu waliomtetea Kubenea?Kweli me naona Mayalla usifananishe issue ya Julian aisee Yale sio level ya Africa, kwavyovyote yule anatumia hackers kitu ambacho ni kosa la jinai. Kwa hacking tu unaweza kuiba hata Banks ndo maana kukawa na mifumo ya Security. Hizo habari anazo zisema mayala ni uchunguzi wa kuhoji sources lkn huwezi kuvunja na kufungua vilivyofungwa bila ruhusa ya wahusika huo ni ujambazi, ndo alipoangukia Julian.
Web ya NAO iko hewaniVipi kuhusu Bunge kuto publish vitabu baadhi, na website ya Nao kuwa shutdown?
Assange amekamatwa kwa kupublish "classified" information sio kwa kumziba mdomoIko wapi "freedom of speech, expression etc" wanazosema hao wazungu?
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Ndege John, kwanza nakubaliana na wewe, kwenye media hatuwezi kujilinganisha na Kenya, wametuacha mbali.
Lakini kwenye hili la Makonda kuwataja watu majina was not right, na hiyo ya 70% ya rushwa kuwasafisha pia sikubaliani na wewe kwa sababu ili kupata% ni lazima kuwe na data, hiyo data ya hadi kufikia 70% imepatikanaje?.
Yes rushwa ipo kila mahali, ila nakuomba usichanganye na vile vibahasha vyetu halali mkaviita rushwa
PWaandishi wa Habari na Bahasha: Sio Kila Bahasha ni Rushwa
Mkuu The Boss, bahasha ni dunia nzima mpaka Ikulu inatembeza bahasha, hiyo PCCB yenyewe na mpaka Polisi wanatembeza bahasha halali kama wanavyotembezewa!. dunia nzima kivipi? waandishi wa kenya wanapokea bahasha? marekani? uingereza? south africa?????www.jamiiforums.com
Pascal, wote sasa hivi si wanaandika kwa kumsifia Magufuli, watashitakiwa kwa lipi? Waandishi nyinyi mnaongoza kwa uoga baada ya Azory kupotea.wa hivi karibuni sijawahi kusikia Mwandishi wa habari wa Tanzania kukamatwa na kushitakiwa kwa alichoandika
Uchungizi haukuonyesha km kubenea alihack information inawezekana kuna mtu alivujisha taarifa zikamfikia kubenea. Sidhani km hilo ni kosa la mwandishi, hilo ni tatizo la maafisa wa usalama kuwa taarifa hazitoki nje. Lkn Julian anakiuka sheria za kimtandao ambazo mataifa yote wanaheshimu. Majasusi huwa wana hack baadhi ya information kwa matumizi yao ya kiusalama, huwa hawapublish. Hata zile email za Hilary, sio km alikua anaziaccess peke yake, mashirika mengi ya kijasusi huwa yanazipata ila hawawezi kuanika kwa raia wa kawaida.Kipindi cha JK Kubenea alipata wapi taarifa za Ikulu?mbona alitetewa kuwa ni uhuru wa habari?kwanini huyu jamaa akamatwe na watu waliomtetea Kubenea?
Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli kabisa, watu wanadhani Assange kaonewa, kusengekuwa na sheria mitandao ingeleta shida duniani. Kunavitu watu wanatamani kufanya lkn sheria haziruhusuAssange amekamatwa kwa kupublish "classified" information sio kwa kumziba mdomo
Sent using Jamii Forums mobile app
Sidhani Pascal ila mazingira ya kuandika habari za kiuchunguzi yamebinywa. Kumbuka wakati Ndugu Ulimwengu alipoanza kuandika makala zake za uchunguzi, akifuatiwa na Mwana halisi, na wengine nini kiliwakuta??. Pia kumbuka kukua kwa aina fulani ya uandishi ni mazingira na kama mazingira hayaruhusu huwezi ona kukua kwa aina hiyo ya uandishi.Nimeuliza jee Tanzania ni hatuna uhuru wa kuandika, au ni hatuna waandishi wa kuandika habari za uchunguzi?.
Ili kuhalalisha media tunatishwa media ziandike basi mambo mazito tuone serikali inaigopa. Ripoti ya CAG imetoka ikiibua madudu kibao, media gani imekwenda deep, nakutolea mfano mdogo tuu wa Vote 20?
P
Karibumkuu "njaa" kuna mambo mengi unaweza post yenye manufaa kwa taifa ukianza na
tasnia yako ambayo iko hoi
Wanabodi,
Media za Tanzania tuna kilio kikubwa cha kulakamikia kuminywa au kunyimwa uhuru, "freedom of the press", na wananchi wetu wanakosa haki ya kupata habari, "the right to information" mfano kuyajua mahela ya vote 20 ambayo kila Ripoti ya CAG ikiibuka, inaibuka nayo, na kila siku tunawaangalia waandishi wa nchi za wenzetu haswa UK na US kuwa wako huru zaidi.
Baada ya Asange kudakwa, Marekani inaitaka Uingereza iwakabidhi Asange ili wao ndio washughulike nae, somo kubwa la kujifunza hapa ni kufuatilia kwa makini, nini kitamkuta Asange, jee Uingereza itamkabidhi kwa Marekani washungulike nae au itamkingia kifua katika kulinda na kutetea uhuru wa habari?.
Ripoti ya CAG imetoka ikiibua madudu kibao, ya matumizi mabaya ya fedha za umma, tungekuwa na serious media, by now, tungeishajua for sure ile 1.5B ilikwenda wapi na imefanyia nini!, au hata kujua tuu hizi fedha zinazochotwa kila siku hazina bila idhini ya Bunge na kutumbukizwa kwenye Vote 20, mule huwa zinakwenda kufanyia nini?. Inamaana hiyo Vote 20, wao hawana mpango kazi, kila siku wanafanya kazi kwa zimamoto, then serious media ingeonyesha basi hata huo moto uliozimwa isije kuwa ni mchwa tuu anatafunia Vote 20?.
Jumamosi Njema
Paskali
Mkuu Capt Tamar ,Naendelezea hapahapa~~chochote chenye public interest kina mawazo na maamuzi yanayotoka kwa watu kwa ajili ya watu,mwenyekiti wa ccm ndiye anejigeuza kuwa mwenyekiti wa Tanzania,yeye ndiye anayeamua nini kiwe for public interest na kipi kisiwe,alipomtimua mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali baada ya mkaguzi huyo kusimamia public interest wewe Pascal Mayalla hukumgombeza magufuli au kumkumbusha kuwa pesa iliyopotea ni ya umma,na mkaguzi ndiye jicho la umma,unamshangilia mwizi halafu unaongea habari za public interest,fool
Asante,
Ubarikiwe
Japo sina uhakika, kwavile siwezi kusoma mabandiko ya watu wote humu, lakini humu JF, mimi ni miongoni mwa tuliomuongelea sana CAG, Ofisi ya CAG na Ripoti za CAG!.
Nakutakia Jumapili Njema
P
Mkuu snow snow , karibu na mitaa hii .Brightone Chonjo
Snowden amuomba Trump amuachie Julian Assange kizuizini nchini United Kingdom kabla hajahukumiwa.
Snowden ni mdukuzi (Hacker) ambaye alikuwa ameajiriwa na serikali ya marekani kitengo cha ujasusi yani (CIA) alifukuzwa kazi baada ya ku kopi na kusambaza habari za siri za marekani na ndipo alipo kimbilia Russia walipo mpa hifadhi mpaka sasa, amemuomba raisi anae maliza muhula wake Trump kumuachia Assange ambaye huyu ni ni raia wa Australia ambaye kazi yake ni mwandishi wa habari lakini anauwezo wa kuhariri na kutoa kwa uma na bado ni mwanaharakati hasa kwa mabo ya marekani .
Ambapo aliweka hadharani habari za vita mauaji na matumizi ya silaha mbalimbali za marekani kwenye magazeti ya marekani kama washington post na new york times ambapo kikawaida hilo ni kosa kubwa sana la kiusalama wa taifa (National security ), yani kwa tanzania tukute habari za jeshi zile nyeti kwenye Nipashe hahaha, sasa ukiangalia hapa maana yake Snowden alikuwa anadukua anampa rafiki yake Assange anaweka kwenye magazeti , ufahamu kuwa Assange alisha shikwa kwa makosa mengine ya kiudhalilishaji wa kingono na sweden alipo achiwa akapata hifadhi UK na ndipo alipo shikwa na serikali ya kule baada ya marekani kutoa tamko kuwa anamadai ya kuweka hadharani habari nyeti hapo ikiwa ni 2016 kwenye uchaguzi wa marekani ambapo WikiLeaks waliposti baadhi ya habari hizo....lakini 23 may 2019 ndipo alipo kamatwa UK uchunguzi ukiendelea na endapo atagundulika na makosa atafungwa miaka 175.
mwezi uliopita patna wake stella ali post picha za watoto wake wawili twiter kwamba wanamhitaji nyumbani.
#wikileaks #snowden #FreeAssange #Classfiedinformation #Confidential #Russiatoday
Wanabodi,
Yule Mwandishi Julian Asange wa WikiLeaks, ametiwa nguvuni nchini Uingereza kwa kutakiwa na Marekani, sasa sisi Tanzania, tujifunze kwa kitachompata, tukitumie kujifanyia tathmini ya Press Freedom yetu, usikute sisi tuna press freedom kubwa kuliko UK na US, zaidi ya magazeti kufungiwa na vituo vya TV kutozwa faini, kwa hivi karibuni sijawahi kusikia Mwandishi wa habari wa Tanzania kukamatwa na kushitakiwa kwa alichoandika, ukiondoa enzi zile za Adam Mwaibabile "Mwana".
Media za Tanzania tuna kilio kikubwa cha kulakamikia kuminywa au kunyimwa uhuru, "freedom of the press", na wananchi wetu wanakosa haki ya kupata habari, "the right to information" mfano kuyajua mahela ya vote 20 ambayo kila Ripoti ya CAG ikiibuka, inaibuka nayo, na kila siku tunawaangalia waandishi wa nchi za wenzetu haswa UK na US kuwa wako huru zaidi.
Baada ya Asange kudakwa, Marekani inaitaka Uingereza iwakabidhi Asange ili wao ndio washughulike nae, somo kubwa la kujifunza hapa ni kufuatilia kwa makini, nini kitamkuta Asange, jee Uingereza itamkabidhi kwa Marekani washungulike nae au itamkingia kifua katika kulinda na kutetea uhuru wa habari?.
Kwa upande wa sisi media ya Tanzania, tunalalamika kuwa hatuko huru wakati waandishi wenyewe wa type ya Asange, wa kuibua ma vitu kama Stan Katabalo, hatuna!, sisi wengi wa waandishi wetu, tunakalia kuandika habari za mikutano, warsha, seminar, na makongamano na kuzikunja zile brown ..., badala ya kuandika investigative stories, sasa uhuru wa habari tunaoutafuta ni uhuru gani?.
Ripoti ya CAG imetoka ikiibua madudu kibao, ya matumizi mabaya ya fedha za umma, tungekuwa na serious media, by now, tungeishajua for sure ile 1.5B ilikwenda wapi na imefanyia nini!, au hata kujua tuu hizi fedha zinazochotwa kila siku hazina bila idhini ya Bunge na kutumbukizwa kwenye Vote 20, mule huwa zinakwenda kufanyia nini?. Inamaana hiyo Vote 20, wao hawana mpango kazi, kila siku wanafanya kazi kwa zimamoto, then serious media ingeonyesha basi hata huo moto uliozimwa isije kuwa ni mchwa tuu anatafunia Vote 20?.
Kama UK inayojitapa kwa Press Freedom sasa inamshikilia Asange, sisi kwetu kuna Mwandishi gani amewahi kushikiliwa kwa maandishi yake ukiondoa kifo cha Daudi Mwangosi, na kupotea kwa Azory Gwanda na Ben Saanane wetu humu jf, jee kuna Mwandishi gani au media gani inaripoti investigative stories za kuhalalisha kutaka uhuru zaidi?.
Somo la kukamatwa kwa Asange kutupe funzo usikute sisi Tanzania tuna press freedom kubwa kuliko ya UK na US ila tumekosa waandishi wa kuitumia hii freedom kikamilifu.
Jumamosi Njema
Paskali
Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari mjini Morogoro, JamiiForums ndani ya Nyumba
Wanabodi, Mei 3 kila mwaka, ni siku ya kimataifa ya kusherehea siku ya Uhuru wa Habari, Media Freedom Day, ambapo hapa nchini, kitaifa siku hii inasherehekewa kwa muda wa siku 2, mjini Morogoro toka katika hoteli ya Nashera ambapo Jamiiforums pia inashiriki, na tayari nimeishamuona Mkuu Max...www.jamiiforums.com
Serious Media inaweza kuwabaini "wasiojulikana" Deo Masakilija
Wanabodi, Naangalia kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari kinachorushwa na Star TV, ambapo mwandishi Mkongwe, Deo Masakilija, amealikwa. Dotto Bulendu ameanza kwa hoja 'Je media imetimiza wajibu wake ipasavyo katika kuwabaini hawa watu wasiojulikana wanaohusika na matukio ya utekaji, utesaji...www.jamiiforums.com
Media kuikosoa Serikali: Je, Tanzania tuna Strong Media au Strong Journalists wenye Uwezo huo?
Wanabodi, Declaration of Interest: mwanzisha mada ni mwandishi wa habari mstaafu ambaye amehudumu kwenye tasnia hii as active media kwa zaidi ya miaka 27, hivi sasa ni mstaafu akiendelea kuhudumu as passive media kama mwandishi/mtangazaji was kujitemea kupitia kampuni ya PPR. Serikali zote...www.jamiiforums.com
Uhuru wa Habari Tanzania: Je, Vyombo Viko Huru? Je, Waandishi wa Habari wako huru? Wanathaminiwa?.
Wanabodi Leo ni Siku ya Kimataifa ya kuadhimisha Uhuru wa Habari. Kwa Tanzania, maadhimisho rasmi yanafanyikia jijini Mwanza, katika kuadhimisha siku hii kwa Tanzania tunaadhimisha nini haswa?. Wakati tukiadhimisha hicho tunachoadhimisha, hakuna ubaya tukitafakari baadhi maswali haya... 1.Jee...www.jamiiforums.com
Waandishi wa Habari na Bahasha: Sio Kila Bahasha ni Rushwa
Mkuu The Boss, bahasha ni dunia nzima mpaka Ikulu inatembeza bahasha, hiyo PCCB yenyewe na mpaka Polisi wanatembeza bahasha halali kama wanavyotembezewa!. dunia nzima kivipi? waandishi wa kenya wanapokea bahasha? marekani? uingereza? south africa?????www.jamiiforums.com