Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,337
- 113,178
- Thread starter
- #81
Mkuu Joka Kuu, heshima mbele...Tafadhali Pascal Mayalla..tafadhali sana.
..wewe una heshima hapa JF.
..vijana wanakuamini ktk mabandiko yako.
..sasa siyo vizuri ukawapoteza namna hii.
..mgogoro wa Julian Asange unahusu KUDUKUA na kusambaza mawasiliano nyeti ya SEREKALI ya Marekani.
..ungewatendea haki vijana hawa wanaokuheshimu kama ungefafanua alichofanya Julian Asange, halafu ukalinganisha kama waTz tuna uhuru wa kufanya jambo linalokaribiana na alichofanya.
..au kwanini usituletee clip za MAHOJIANO kati ya VIONGOZI wa nchi za wenzetu na VYOMBO VYA HABARI halafu tuone kama na sisi tuko HURU na tuna WELEDI kiasi gani.
Amini usiami kwa Tanzania tatizo ni letu sisi waandishi, wala usiende mbali hadi ulaya kwa Asange, nenda tu hapo jirani zetu Kenya kwa Mohammed Amin na Jicho Pevu, sisi tunashindwa nini?.
Nimesema waandishi wetu wengi ni reporters tuu kazi kubwa ya media zetu ni kuripoti matukio na pressvm conferences, mikutano, semina, warsha na makongamano. Hutuzami deep na hatuna competent team za kufanya IJ.
Tangu awamu ya 5 imeingia madarakani, fungu la Vote 20, ndilo linaloongoza kuchota fedha hazina bila ya idhini ya Bunge na bila kuidhinishwa na CAG, this time limechota zaidi ya bilioni 900. Tungekuwa na serious media, zamani wangeshutumia IJ kujua hizi fedha za vote 20 ambazo hazikuidhinishwa na Bunge, zinafanyia nini?.
Kabla Lissu hajadhambuliwa , kuna mtu alisema kuhusu tunadukua simu mtu fulani, intelligence agencies zote duniani zinadukua sio simu tuu, hata tailing, emails hadi private lives, lakini haya mambo huwa hayasemwi.
Akakamilisha kwa kumuita mdukuliwa ni msaliti na kusema msaliti hawezi kuachwa hivi hivi akasurvive na kutolea mfano usaliti vitani huwa wanafanywa nini.
Baada ya muda mfupi Lissu kashambuliwa. Tungekuwa na serious media, aliyemtaka maneno hayo angeulizwa alimaanisha nini
Serious Media inaweza kuwabaini "wasiojulikana" Deo Masakilija
Wanabodi, Naangalia kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari kinachorushwa na Star TV, ambapo mwandishi Mkongwe, Deo Masakilija, amealikwa. Dotto Bulendu ameanza kwa hoja 'Je media imetimiza wajibu wake ipasavyo katika kuwabaini hawa watu wasiojulikana wanaohusika na matukio ya utekaji, utesaji...
www.jamiiforums.com
Ninachosema hapa kama hizi serious media zipo, zifanye tuone.
Kwa vile hatuna then inawezekana kabisa sisi tuko huru kuliko UK na US ila hatuna competent person who can do some serious stuff.
P