Je, Sheria inasema nini kuhusu ardhi ya mtu binafsi kutumika kwa ajili ya manufaa ya Umma?

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
1607934448586.png

Sheria ya Utwaaji wa Ardhi ( Land Acquisition Act Cap. 118 R.E. 2002 katika kifungu chake cha 3 imempa nguvu na madaraka Rais ya kuchukua ardhi inayomilikiwa na mtu binafsi kwa ajili ya manufaa ya umma.

Rais anaweza kufanya hivi endapo tu ataona au watu wanataka ardhi hiyo kwa ajili ya manufaa ya umma kwa ujumla.

Lakini pia sheria hii imetoa ulinzi kwa watu ambao ardhi zao zitachukuliwa kwa manufaa ya umma.
Ulinzi huo ni kama ifuatavyo:

1. Lazima wapewe Taarifa ya awali (Notice) ya lengo la kuchukua ardhi yao. Kifungu cha 6 cha sheria hii inataka Waziri anayehusika na mambo ya ardhi atoe taarifa ya lengo la kuchukua ardhi kwa mtu anayemiliki ardhi hiyo. Na taarifa hiyo kutoka kwa Waziri inatakiwa itolewe si chini ya muda wa wiki 6 kabla ya kuanza mchakato wa kuchukua ardhi hiyo.

2. Lazima Fidia itolewe kwa wale wote ambao ardhi yao imechukuliwa. Kifungu cha 11 cha sheria hii inataka watu wote waliochukuliwa ardhi zao kwa lengo la manufaa ya umma wapewe Fidia juu ya ardhi yao.

Na tathimini ya Fidia itafanywa na Waziri husika au Mahakama, na kiwango cha Fidia itakuwa sawa kama ambavyo ilikuwa thamani ya ardhi husika wakati inachukuliwa na pia usumbufu alioupata mtu ambaye ardhi yake imechukuliwa.

Ingawa sheria hii haijampa mtu haki ya kujipigia tathimini juu ya Fidia anayotaka kulipwa lakini kifungu cha 13 kinampa mtu haki ya kwenda mahakamani kupinga kiwango cha Fidia atakacholipwa kama hajaridhika nacho.

Hivyo, ulinzi huu aliopewa mmiliki wa ardhi ni wa kuzingatiwa, endapo hajapatiwa kimoja wapo kati ya hivi au vyote basi uchukuaji huo wa ardhi utakuwa batili na mtu anaweza kwenda mahakamani kushitaki ili mahakama izuie zoezi hilo la uchukuaji wa ardhi au kurejesha ardhi hiyo kama tayari ilishachukuliwa.
 
Kw
Kwa hali tunayokwenda nayo upinge ardhi yako kuchukuliwa wewe ni nani. Ukishapewa taarifa na waziri wewe kusanya vilago vyako ulale mbele
Comment yako niliisoma jana nikaipotezea, leo nimerudi baada ya kuona taarifa ya habari ya ITV ya mkazi wa Inyala Mbeya nyumba yake kuvunjwa mbele ya usimamizi wa RC Mbeya na DC huku akifungwa pingu, kwahiyo kipengele cha mahakama hata hakijazingatiwa hapa maana hajapewa nafasi
 
Comment yako niliisoma jana nikaipotezea, leo nimerudi baada ya kuona taarifa ya habari ya ITV ya mkazi wa Inyala Mbeya nyumba yake kuvunjwa mbele ya usimamizi wa RC Mbeya na DC huku akifungwa pingu, kwahiyo kipengele cha mahakama hata hakijazingatiwa hapa maana hajapewa nafasi
Mahakama Ni mhimili wa dola, unaemshitaki Ni.....

Ni sawa na kesi ya mahindi unampelkea ngedele
 
Comment yako niliisoma jana nikaipotezea, leo nimerudi baada ya kuona taarifa ya habari ya ITV ya mkazi wa Inyala Mbeya nyumba yake kuvunjwa mbele ya usimamizi wa RC Mbeya na DC huku akifungwa pingu, kwahiyo kipengele cha mahakama hata hakijazingatiwa hapa maana hajapewa nafasi
Kuna mihimili imeota mizizi imejichimbia kwenda chini ndio inalisha mihimili mingine ( hizi comment haziko waziwazi kulingana na wakati tulionao )
 
Comment yako niliisoma jana nikaipotezea, leo nimerudi baada ya kuona taarifa ya habari ya ITV ya mkazi wa Inyala Mbeya nyumba yake kuvunjwa mbele ya usimamizi wa RC Mbeya na DC huku akifungwa pingu, kwahiyo kipengele cha mahakama hata hakijazingatiwa hapa maana hajapewa nafasi
Ndiomaana maskini wa kihindi hawajengi..unafungwa pingu kisa nyumba yako....
 
Jimbo la Texas nchini Marekani lilipitisha sheria ya kuzuia matumizi ya kunyang'anya ardhi ya mtu mmoja binafsi na kumpa mtu binafsi mwingine "kwa manufaa ya umma". Sheria ikitumika kutumia ardhi ya mtu binafsi kwa manufaa ya umma, basi umiliki uhame kutoka binafsi kwenda umma. Sheria hiyo inataka matumizi ya thamani ya soko kutumika kama kigezo cha fidia.
 
Unasemea watu wa kimara sio ?
Kimara origibnal owners walishalipwa siku nyingi wakaondoka zao miaka ya sabini kukabaki pori watu wakaanza kuvamia na kuuziana !!! Ni kama VINGINGUTI lile eneo ni mali ya shirika la Reli TRC lilikuwa lijenge stesheni yake kubwa pale wahame pale walipo mjini sababu padogo wakachelewa kujenga watu wakavamia kujigawia na kuuzia wengine!! Sipati picha siku serikali ikiamua kutwaa lile eneo bila fidia nini kitatokea!!
 

Sheria ya Utwaaji wa Ardhi ( Land Acquisition Act Cap. 118 R.E. 2002 katika kifungu chake cha 3 imempa nguvu na madaraka Rais ya kuchukua ardhi inayomilikiwa na mtu binafsi kwa ajili ya manufaa ya umma.

Rais anaweza kufanya hivi endapo tu ataona au watu wanataka ardhi hiyo kwa ajili ya manufaa ya umma kwa ujumla.

Lakini pia sheria hii imetoa ulinzi kwa watu ambao ardhi zao zitachukuliwa kwa manufaa ya umma.
Ulinzi huo ni kama ifuatavyo:

1. Lazima wapewe Taarifa ya awali (Notice) ya lengo la kuchukua ardhi yao. Kifungu cha 6 cha sheria hii inataka Waziri anayehusika na mambo ya ardhi atoe taarifa ya lengo la kuchukua ardhi kwa mtu anayemiliki ardhi hiyo. Na taarifa hiyo kutoka kwa Waziri inatakiwa itolewe si chini ya muda wa wiki 6 kabla ya kuanza mchakato wa kuchukua ardhi hiyo.

2. Lazima Fidia itolewe kwa wale wote ambao ardhi yao imechukuliwa. Kifungu cha 11 cha sheria hii inataka watu wote waliochukuliwa ardhi zao kwa lengo la manufaa ya umma wapewe Fidia juu ya ardhi yao.

Na tathimini ya Fidia itafanywa na Waziri husika au Mahakama, na kiwango cha Fidia itakuwa sawa kama ambavyo ilikuwa thamani ya ardhi husika wakati inachukuliwa na pia usumbufu alioupata mtu ambaye ardhi yake imechukuliwa.

Ingawa sheria hii haijampa mtu haki ya kujipigia tathimini juu ya Fidia anayotaka kulipwa lakini kifungu cha 13 kinampa mtu haki ya kwenda mahakamani kupinga kiwango cha Fidia atakacholipwa kama hajaridhika nacho.

Hivyo, ulinzi huu aliopewa mmiliki wa ardhi ni wa kuzingatiwa, endapo hajapatiwa kimoja wapo kati ya hivi au vyote basi uchukuaji huo wa ardhi utakuwa batili na mtu anaweza kwenda mahakamani kushitaki ili mahakama izuie zoezi hilo la uchukuaji wa ardhi au kurejesha ardhi hiyo kama tayari ilishachukuliwa.
Bado sheria haisemi mtu atatakiwa kulipwa ndani ya kipindi kisichozidi muda gani
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom