Je, Rais Samia kutoa kauli ya "Mwanaume ni yule anayejiamini" ni kijembe Kwa Hayati Magufuli?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,162
Rais Samia ametoa kauli yenye utata mkubwa, wakati wa ziara yake huko Usa River, Arusha, hapo majuzi.

Wakati akitoka kwenye semina elekezi ya viongozi waandamizi huko Arusha, alitoa kauli hii wakati anazungumzia ujio wa Godbless Lema, hapa nchini, kuwa "Mwanaume ni yule anayejiamini" na akaendelea keleza kuwa mwanasiasa huyo wa Chama Cha upinzani Cha Chadema, alimwomba kurudi nchini, lakini akaeleza wasiwasi wake kuwa anaogopa kurudi nchini, kutokana na kuhofia usalama wake, pia aliomba afutiwe kesi nyingi alizo ambazo amebambikiwa na Jeshi la Polisi nchini.

Ndipo Rais Samia, alimuhakikishia mwanasiasa huyo wa upinzani, kuwa aondoe wasiwasi na akamuhakikishia usalama wake na kumweleza kuwa anaweza kurudi nchini na kesi zote zilizoko mahalamani atazifuta.

Akeleza zaidi kuwa baada ya kurudi Mwanasiasa huyo wa upinzani, hakuna baya lolote lililomkuta.

Ndipo akatumbukiza kibwagizo hicho Cha "Mwanaume ni yule anayejiamini"

Ndipo hapo ninapojiuliza, je hiyo kauli ni kijembe kwa Mwendazake?

Kwa kuwa ni katika utawala wake, Hayati Magufuli, ndipo wanasiasa wengi wa vyama vya upinzani, waliomba ukimbizi, nje ya nchi hii, wakiwemo, nikiwataja wachache, Tundu Lissu na Ezekia Wenje.

Kwa kuwa huyo mwanasiasa Lema, aliikimbia nchini mwaka 2020, wakati wa utawala wa Rais wa awamu ya 5, Hayati John Pombe Magufuli, ambaye aliiendesha nchi kibabe Sana, bila kufuata Katiba ya nchi na ndiye aliyepiga marufuku mikutano yote ya vyama vya kisiasa ya vyama vya upinzani nchini.,na alikwenda mbele zaidi, Kwa kuliagiza Jeshi la Polisi, liwabambikie kesi viongozi hao wa upinzani, pale alipojisikia!

Ndipo hapo nimewaza Sana kuhusu kauli hiyo ya "Mwanaume ni yule anayejiamini"

Je alimlenga nani, kama siyo, Hayati Magufuli?

Kwa kuwa ndiye aliyekuwa akiyafanya hayo maovu yote, Kwa kutojiamini kwenye siasa.
 
Jiwe aliyeisigina katiba kwa kuingilia mahakama na kubambikia watu kesi hana tofauti na bi hangaya anayeisigina katiba kwa kuingilia mahakama na kufutia watu kesi.

Kuwa free minded na wachana na double standards.
 
Jiwe aliyeisigina katiba kwa kuingilia mahakama na kubambikia watu kesi hana tofauti na bi hangaya anayeisigina katiba kwa kuingilia mahakama na kufutia watu kesi.

Kuwa free minded na wachana na double standards.
Lakini Kuna tofauti kubwa kati ya kuisigina Katiba, alikokuwa anafanya Mwendazake na anakofanya Rais Samia.

Hayati Magufuli aliisigina Katiba, Kwa kulielekeza Jeshi la Polisi, liwabambikie kesi viongozi wa vyama vya upinzani nchini na Rais Samia, anachofanya ni kurekebisha makosa ya mtangulizi wake Kwa kuwaondolea kesi zote walizokuwa, wamebambikiziwa nazo
 
Jiwe aliyeisigina katiba kwa kuingilia mahakama na kubambikia watu kesi hana tofauti na bi hangaya anayeisigina katiba kwa kuingilia mahakama na kufutia watu kesi.

Kuwa free minded na wachana na double standards.
Sijui kama mnaelewa maana ya kuingilia mahakama.
Mahakama haina kesi maana sio inayoshtaki, bali DPP na idara nyingine kama Polisi, Takukuru nk ndizo zina kua chanzo cha hizo kesi na hawa wako chini ya Executive yaani yeye.
Kwa hiyo hata zile za kubambika ni zake hivyo akiondoa kaondoa kesi sio kaingilia maamuzi (hukumu) ya mahakama.
Msimlinganishe kabisa na Magu aliyetengeneza kesi bila huruma na kutesa watu
 
Kwa kuliagiza Jeshi la Polisi, liwabambikie kesi viongozi hao wa upinzani, pale alipojisikia!
Je hili jukumu batili, kwa sasa halipo kabisa? la watu ( wananchi wa kawaida ) kupewa/ kubambikiwa kesi na Polisi !
 
Mataga mnateseka sana, mama chapa kazi 2030 aje mwingine tusiyemjua maisha yaendelee, kila zama na kitabu chake (Mungu aendelee kumlinda Mzee Mwinyi)
 
Rais Samia ametoa kauli yenye utata mkubwa, wakati wa ziara yake huko Usa River, Arusha, hapo majuzi.

Wakati akitoka kwenye semina elekezi ya viongozi waandamizi huko Arusha, alitoa kauli hii wakati anazungumzia ujio wa Godbless Lema, hapa nchini, kuwa "Mwanaume ni yule anayejiamini" na akaendelea keleza kuwa mwanasiasa huyo wa Chama Cha upinzani Cha Chadema, alimwomba kurudi nchini, lakini akaeleza wasiwasi wake kuwa anaogopa kurudi nchini, kutokana na kuhofia usalama wake, pia aliomba afutiwe kesi nyingi alizo ambazo amebambikiwa na Jeshi la Polisi nchini.

Ndipo Rais Samia, alimuhakikishia mwanasiasa huyo wa upinzani, kuwa aondoe wasiwasi na akamuhakikishia usalama wake na kumweleza kuwa anaweza kurudi nchini na kesi zote zilizoko mahalamani atazifuta.

Akeleza zaidi kuwa baada ya kurudi Mwanasiasa huyo wa upinzani, hakuna baya lolote lililomkuta.

Ndipo akatumbukiza kibwagizo hicho Cha "Mwanaume ni yule anayejiamini"

Ndipo hapo ninapojiuliza, je hiyo kauli ni kijembe kwa Mwendazake?

Kwa kuwa ni katika utawala wake, Hayati Magufuli, ndipo wanasiasa wengi wa vyama vya upinzani, waliomba ukimbizi, nje ya nchi hii, wakiwemo, nikiwataja wachache, Tundu Lissu na Ezekia Wenje.

Kwa kuwa huyo mwanasiasa Lema, aliikimbia nchini mwaka 2020, wakati wa utawala wa Rais wa awamu ya 5, Hayati John Pombe Magufuli, ambaye aliiendesha nchi kibabe Sana, bila kufuata Katiba ya nchi na ndiye aliyepiga marufuku mikutano yote ya vyama vya kisiasa ya vyama vya upinzani nchini.,na alikwenda mbele zaidi, Kwa kuliagiza Jeshi la Polisi, liwabambikie kesi viongozi hao wa upinzani, pale alipojisikia!

Ndipo hapo nimewaza Sana kuhusu kauli hiyo ya "Mwanaume ni yule anayejiamini"

Je alimlenga nani, kama siyo, Hayati Magufuli?

Kwa kuwa ndiye aliyekuwa akiyafanya hayo maovu yote, Kwa kutojiamini kwenye siasa.
Unajitoa ufahamu!
 
Linapokuja swala la kulinda madaraka hakuna anayejiamini.

Hata yeye alimpa za uso Ndugai ,pole pole, lukuvi na prof. Kabudi.

Kalemani nae akala buyu.

Wote hao ni woga tu.

Sisi wenyewe hapa tunaandika tu lakini tunasali yasije tukuta siku moja.
 
Lakini Kuna tofauti kubwa kati ya kuisigina Katiba, alikokuwa anafanya Mwendazake na anakofanya Rais Samia.

Hayati Magufuli aliisigina Katiba, Kwa kulielekeza Jeshi la Polisi, liwabambikie kesi viongozi wa vyama vya upinzani nchini na Rais Samia, anachofanya ni kurekebisha makosa ya mtangulizi wake Kwa kuwaondolea kesi zote walizokuwa, wamebambikiziwa nazo
Mbowe alipewa kesi ya ugaidi na nani?
 
Rais Samia ametoa kauli yenye utata mkubwa, wakati wa ziara yake huko Usa River, Arusha, hapo majuzi.

Wakati akitoka kwenye semina elekezi ya viongozi waandamizi huko Arusha, alitoa kauli hii wakati anazungumzia ujio wa Godbless Lema, hapa nchini, kuwa "Mwanaume ni yule anayejiamini" na akaendelea keleza kuwa mwanasiasa huyo wa Chama Cha upinzani Cha Chadema, alimwomba kurudi nchini, lakini akaeleza wasiwasi wake kuwa anaogopa kurudi nchini, kutokana na kuhofia usalama wake, pia aliomba afutiwe kesi nyingi alizo ambazo amebambikiwa na Jeshi la Polisi nchini.

Ndipo Rais Samia, alimuhakikishia mwanasiasa huyo wa upinzani, kuwa aondoe wasiwasi na akamuhakikishia usalama wake na kumweleza kuwa anaweza kurudi nchini na kesi zote zilizoko mahalamani atazifuta.

Akeleza zaidi kuwa baada ya kurudi Mwanasiasa huyo wa upinzani, hakuna baya lolote lililomkuta.

Ndipo akatumbukiza kibwagizo hicho Cha "Mwanaume ni yule anayejiamini"

Ndipo hapo ninapojiuliza, je hiyo kauli ni kijembe kwa Mwendazake?

Kwa kuwa ni katika utawala wake, Hayati Magufuli, ndipo wanasiasa wengi wa vyama vya upinzani, waliomba ukimbizi, nje ya nchi hii, wakiwemo, nikiwataja wachache, Tundu Lissu na Ezekia Wenje.

Kwa kuwa huyo mwanasiasa Lema, aliikimbia nchini mwaka 2020, wakati wa utawala wa Rais wa awamu ya 5, Hayati John Pombe Magufuli, ambaye aliiendesha nchi kibabe Sana, bila kufuata Katiba ya nchi na ndiye aliyepiga marufuku mikutano yote ya vyama vya kisiasa ya vyama vya upinzani nchini.,na alikwenda mbele zaidi, Kwa kuliagiza Jeshi la Polisi, liwabambikie kesi viongozi hao wa upinzani, pale alipojisikia!

Ndipo hapo nimewaza Sana kuhusu kauli hiyo ya "Mwanaume ni yule anayejiamini"

Je alimlenga nani, kama siyo, Hayati Magufuli?

Kwa kuwa ndiye aliyekuwa akiyafanya hayo maovu yote, Kwa kutojiamini kwenye siasa.

Wa Bongo ni wa Fokonyoko aisee, kila kitu mtafsiri?
 
Rais Samia ametoa kauli yenye utata mkubwa, wakati wa ziara yake huko Usa River, Arusha, hapo majuzi.

Wakati akitoka kwenye semina elekezi ya viongozi waandamizi huko Arusha, alitoa kauli hii wakati anazungumzia ujio wa Godbless Lema, hapa nchini, kuwa "Mwanaume ni yule anayejiamini" na akaendelea keleza kuwa mwanasiasa huyo wa Chama Cha upinzani Cha Chadema, alimwomba kurudi nchini, lakini akaeleza wasiwasi wake kuwa anaogopa kurudi nchini, kutokana na kuhofia usalama wake, pia aliomba afutiwe kesi nyingi alizo ambazo amebambikiwa na Jeshi la Polisi nchini.

Ndipo Rais Samia, alimuhakikishia mwanasiasa huyo wa upinzani, kuwa aondoe wasiwasi na akamuhakikishia usalama wake na kumweleza kuwa anaweza kurudi nchini na kesi zote zilizoko mahalamani atazifuta.

Akeleza zaidi kuwa baada ya kurudi Mwanasiasa huyo wa upinzani, hakuna baya lolote lililomkuta.

Ndipo akatumbukiza kibwagizo hicho Cha "Mwanaume ni yule anayejiamini"

Ndipo hapo ninapojiuliza, je hiyo kauli ni kijembe kwa Mwendazake?

Kwa kuwa ni katika utawala wake, Hayati Magufuli, ndipo wanasiasa wengi wa vyama vya upinzani, waliomba ukimbizi, nje ya nchi hii, wakiwemo, nikiwataja wachache, Tundu Lissu na Ezekia Wenje.

Kwa kuwa huyo mwanasiasa Lema, aliikimbia nchini mwaka 2020, wakati wa utawala wa Rais wa awamu ya 5, Hayati John Pombe Magufuli, ambaye aliiendesha nchi kibabe Sana, bila kufuata Katiba ya nchi na ndiye aliyepiga marufuku mikutano yote ya vyama vya kisiasa ya vyama vya upinzani nchini.,na alikwenda mbele zaidi, Kwa kuliagiza Jeshi la Polisi, liwabambikie kesi viongozi hao wa upinzani, pale alipojisikia!

Ndipo hapo nimewaza Sana kuhusu kauli hiyo ya "Mwanaume ni yule anayejiamini"

Je alimlenga nani, kama siyo, Hayati Magufuli?

Kwa kuwa ndiye aliyekuwa akiyafanya hayo maovu yote, Kwa kutojiamini kwenye siasa.
Jiwe=madman
 
Jiwe aliyeisigina katiba kwa kuingilia mahakama na kubambikia watu kesi hana tofauti na bi hangaya anayeisigina katiba kwa kuingilia mahakama na kufutia watu kesi.

Kuwa free minded na wachana na double standards.
Zile sio kesi ni uhuni tuu wa washamba wasiojiamini waliopata madaraka wakaigeuza nchi kuwa nchi ya giza, namsifu President Samia kwa kufuta ule ushenzi
 
Jiwe aliyeisigina katiba kwa kuingilia mahakama na kubambikia watu kesi hana tofauti na bi hangaya anayeisigina katiba kwa kuingilia mahakama na kufutia watu kesi.

Kuwa free minded na wachana na double standards.
Sidhani kama Chifu Hangaya ameingilia mahakama bali Katiba yenyewe imempa nafasi ya kufuta kesi kupitia Mtendaji wa Serikali anayeitwa DPP..
 
Back
Top Bottom