Je, Misri imeshaweka jeshi lake sawa mpaka wa Rafah kuijibu Israel ambayo imenuia kuwaua Wapalestina zaidi na watakaobaki kuwasukuma nje?

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,192
10,926
Pamoja na Israel kushindwa kufikia malengo yake ya kivita iliyojiwekea na japo imeshawahamisha wapalestina wa Gaza huku na huko bila mafanikio lakini bado imeweka nia thabiti ya kushambulia eneo la Rafah.

Umoja wa mataifa na kila mmoja wameshatoa angalizo kuwa kushambulia eneo hilo kutasababisha vifo vingi sana kwa wapalestina na kwamba huenda kukaleta mfarakazo mkubwa baina ya Israel na Misri ambao tayari wana mkataba wa kiusalama baina yao unaoheshimiwa kikamilifu na Misri.

Benjamin Netanyahu katika mazungumzo na Anthony Blinken leo amekataa kata kata mapendekezo ya Hamas ya kumaliza vita na akasisitiza kuwa hatosimamisha vita mpaka Israel ipate ushindi ulio wazi dhidi ya Hamas na kwamba ushindi huo uko karibu.

Katika mazungumzo yake mengine Netanyahu amesema ameshatoa amri ya jeshi kushambulia Rafah ambako amedai kuna mahandaki chini yake yanayounganisha na Misri,madai ambayo Misri imekanusha.

Moja ya lengo la wahafidhina wa kiyahudi ni kuwasukuma nje ya Gaza wapalestina na kwa hapo walipo ni kwamba waingie jangwa la Sinai.

Baadhi ya wasemaji wa serikali ya Misri wameshasema kitendo hicho cha Israel kitapelekea kuvunjika kwa mkataba wa Camp David na kwamba hawatoruhusu Israel kudhibiti eneo hilo kama inavyotaka.

Wasemaji wa Israel wamedai tayari Israel imeshaiarifu Misri juu ya kushambulia Rafah na kwamba wasiwe na wasiwasi kwani baada ya mashambulio hayo jeshi la Israel litaondoka eneo hilo.

Madai ya kuarifiwa Misri kuhusu kushambuliwa Rafah yanatiliwa shaka kwani hapo majuzi rais Elsisi alikataa kutpokea simu ya Benjamin Netanyahu kuzungumzia suala lolote lile na tayari Misri imeshatishia kukatisha mahusiano ya kibalozi na Israel.

Pamoja na yote hayo na unyeti wa mashambulio hayo jee Misri imeshapeleka majeshi yake mpakani kujitayarisha na kuzuia athari zake kuingia nchini mwao au kuzuia Israel kudhibiti mpaka huo.

Uzito wa jambo hilo na kauli za kila upande hakuonekani harakati za dhati za Misri kuulinda mpaka huo au kutaka kuzuia janga kubwa zaidi kuwapata wapalestina pindi wakishambuliwa.

Wasemaji wa mashirika ya kibinadamu wamesema kwa huruma kwamba wapalestina hapo walipofika wamechoka kutokana na shida za vita na hata nguvu zimewaishia kukimbia na kuhama kuelekea popote pale kwengine.

Watoto wengi wa kipalestina walio Gaza wametajwa kuwa na mshtuko mkubwa kutokana na vifo vya wenzao waliowashuhudia.Wazee wa kipalestina nao pamoja na uchofu wamejaa huzuni za kupotelewa na watoto na ndugu zao.

1707419011525.png
 
Kwa Misri hakuna jipya
Misri na israhell ndio wale wale tu labda yatokee yalimkuta mubaraq
 
Kwa Misri hakuna jipya
Misri na israhell ndio wale wale tu labda yatokee yalimkuta mubaraq
Insasikitisha sana,
Ingekuwa ni mataifa mengine au Misri haiongozwe na Elsisi basi tayari habari ya Misri kupeleka jeshi mpakani Rafaha ingekuwa ni habari kubwa kwenye vyombo vya habari vya kimataifa.
 
Insasikitisha sana,
Ingekuwa ni mataifa mengine au Misri haiongozwe na Elsisi basi tayari habari ya Misri kupeleka jeshi mpakani Rafaha ingekuwa ni habari kubwa kwenye vyombo vya habari vya kimataifa.
Kabisaaa misri inaongozwa na hao hao wazayuni kwa Misri wala hakuna jipya mzee hakuna
Ila israhell ataua sana atafanya sana unyama ila mwaka huu ama mgogoro huu ndio unaenda kuipa Palestine uhuru wake hakuna namna Palestine kupitia huu mgogoro wasiwe huru
 
Kwa Misri hakuna jipya
Misri na israhell ndio wale wale tu labda yatokee yalimkuta mubaraq

Niliwaambia mpo wenyewe, alla akbar wenu keshakula kona na kukimbia, hakuna wa kuwaokoa, mtaechezea kichapo kote kote, mumejaibu kuomba Mchina, Mrusi lakini hamna lolote, mataifa yote ya kiarabu yameufyata, hata kubwa la magaidi ya uislamu, Iran halina jipya limeufyata.
Mungu wa Wayahudi ni mkubwa kuzidi wenu huyo aliyekimbia mpambano.
 
Ni muda wa hii vita kuisha na watu wazungumze,kuliko kuuana kila uchwao.Risasi haija wahi leta suluhu ya mgogoro.
 
Pamoja na Israel kushindwa kufikia malengo yake ya kivita iliyojiwekea na japo imeshawahamisha wapalestina wa Gaza huku na huko bila mafanikio lakini bado imeweka nia thabiti ya kushambulia eneo la Rafah.

Umoja wa mataifa na kila mmoja wameshatoa angalizo kuwa kushambulia eneo hilo kutasababisha vifo vingi sana kwa wapalestina na kwamba huenda kukaleta mfarakazo mkubwa baina ya Israel na Misri ambao tayari wana mkataba wa kiusalama baina yao unaoheshimiwa kikamilifu na Misri.

Benjamin Netanyahu katika mazungumzo na Anthony Blinken leo amekataa kata kata mapendekezo ya Hamas ya kumaliza vita na akasisitiza kuwa hatosimamisha vita mpaka Israel ipate ushindi ulio wazi dhidi ya Hamas na kwamba ushindi huo uko karibu.

Katika mazungumzo yake mengine Netanyahu amesema ameshatoa amri ya jeshi kushambulia Rafah ambako amedai kuna mahandaki chini yake yanayounganisha na Misri,madai ambayo Misri imekanusha.

Moja ya lengo la wahafidhina wa kiyahudi ni kuwasukuma nje ya Gaza wapalestina na kwa hapo walipo ni kwamba waingie jangwa la Sinai.

Baadhi ya wasemaji wa serikali ya Misri wameshasema kitendo hicho cha Israel kitapelekea kuvunjika kwa mkataba wa Camp David na kwamba hawatoruhusu Israel kudhibiti eneo hilo kama inavyotaka.

Wasemaji wa Israel wamedai tayari Israel imeshaiarifu Misri juu ya kushambulia Rafah na kwamba wasiwe na wasiwasi kwani baada ya mashambulio hayo jeshi la Israel litaondoka eneo hilo.

Madai ya kuarifiwa Misri kuhusu kushambuliwa Rafah yanatiliwa shaka kwani hapo majuzi rais Elsisi alikataa kutpokea simu ya Benjamin Netanyahu kuzungumzia suala lolote lile na tayari Misri imeshatishia kukatisha mahusiano ya kibalozi na Israel.

Pamoja na yote hayo na unyeti wa mashambulio hayo jee Misri imeshapeleka majeshi yake mpakani kujitayarisha na kuzuia athari zake kuingia nchini mwao au kuzuia Israel kudhibiti mpaka huo.

Uzito wa jambo hilo na kauli za kila upande hakuonekani harakati za dhati za Misri kuulinda mpaka huo au kutaka kuzuia janga kubwa zaidi kuwapata wapalestina pindi wakishambuliwa.

Wasemaji wa mashirika ya kibinadamu wamesema kwa huruma kwamba wapalestina hapo walipofika wamechoka kutokana na shida za vita na hata nguvu zimewaishia kukimbia na kuhama kuelekea popote pale kwengine.

Watoto wengi wa kipalestina walio Gaza wametajwa kuwa na mshtuko mkubwa kutokana na vifo vya wenzao waliowashuhudia.Wazee wa kipalestina nao pamoja na uchofu wamejaa huzuni za kupotelewa na watoto na ndugu zao.

Hao wazee ndio walitakiwa wawa onye watoto wao wasianzishe jambo wasilokuwa na uwezo nalo la kutaka vita na Netanyahu jabari lenye kisasi kama nyegele ..............sasa malipo yao ndio hayo...........na kuhusu hao wengine sijui watoto sijui kina mama ..........wenyewe kina mama ndio wanasimamia ujinga wa watoto wao .......mama mkanye mwanao angali mdogo naamini kabisa kama hili jambo lingetumia busara kuanzia ngazi ya familia wapalestina wangekuwa na taifa lao miaka mingi sana sema ujinga fulani fulani hivi ndio unaogharimu na utawagharimu miaka yao yote kama wasipotaka kubadilika
 
Hakuna namna Misri inaweza kwenda kinyume na Israel...... bwana wao ni mmoja
Ni kweli lakini Hamasi kisha wavuruga akili, mnakumbuka Hillary Clinton alisema nini wakati vita vimeanza hakuna kusimamisha vita, akawa na msapoti Netanyau leo analilia huko Netanyau lazima aondoke 😄


View: https://youtu.be/tLR3cwOKui8?si=VlPMBj4hajE4dTO5

Itafika mda Misri atachoko kuwa upande wao, kama alivyo choka Clinton kuwa upande wa Netanyau
 
Ni kweli lakini Hamasi kisha wavuruga akili, mnakumbuka Hillary Clinton alisema nini wakati vita vimeanza hakuna kusimamisha vita, akawa na msapoti Netanyau leo analilia huko Netanyau lazima aondoke 😄


View: https://youtu.be/tLR3cwOKui8?si=VlPMBj4hajE4dTO5

Itafika mda Misri atachoko kuwa upande wao, kama alivyo choka Clinton kuwa upande wa Netanyau


Netanyahu alishasema tangu mwanzo kwamba hivi vita mpaka wafike mwisho wake, Marekani wamejaribu kumshawishi kimya kimya aachie kidogo ila jamaa ameamua kufika mwisho, mlikosea sana kumchezea Myahudi....
 
Kama egypt ameamua kumsaidia ndugu yetu basi hakika amefanya vizuri, na makafiri watasaidiana wao kwa wao, ila bado namashaka na nchi tatu kama hazitamsaidia kafiri nazo ni Qatar, Saudia na Emirates
Mafarisayo mna tabu sana😂, upuuzi mlete nyie halafu mkinyooshwa mnalialia
#resteasyJoshua
 
Niliwaambia mpo wenyewe, alla akbar wenu keshakula kona na kukimbia, hakuna wa kuwaokoa, mtaechezea kichapo kote kote, mumejaibu kuomba Mchina, Mrusi lakini hamna lolote, mataifa yote ya kiarabu yameufyata, hata kubwa la magaidi ya uislamu, Iran halina jipya limeufyata.
Mungu wa Wayahudi ni mkubwa kuzidi wenu huyo aliyekimbia mpambano.
Tumekusikia lakini na wewe huna jipya.
Ushindi wa Hamas na uhuru wa Palestina ni mwaka huu.
Sisi waislamu tunajua vizuri kuwa Allah huwa anaokoa waja wake katika nukta ya mwisho wanadamu wanapoona imeshindikana.
Kiburi cha Netanyahu hakiwezi kuwa juu ya kudra za Mwenyezi Mungu.
Wewe MK254 kaa mkao wa kula usipitwe na matukio.
 
Kabisaaa misri inaongozwa na hao hao wazayuni kwa Misri wala hakuna jipya mzee hakuna
Ila israhell ataua sana atafanya sana unyama ila mwaka huu ama mgogoro huu ndio unaenda kuipa Palestine uhuru wake hakuna namna Palestine kupitia huu mgogoro wasiwe huru
Kumbe kadhia ya tarehe 7/10/23 imeleta matunda kwa Wapalestina kama wote tunavyojionea .
 
Tumekusikia lakini na wewe huna jipya.
Ushindi wa Hamas na uhuru wa Palestina ni mwaka huu.
Sisi waislamu tunajua vizuri kuwa Allah huwa anaokoa waja wake katika nukta ya mwisho wanadamu wanapoona imeshindikana.
Kiburi cha Netanyahu hakiwezi kuwa juu ya kudra za Mwenyezi Mungu.
Wewe MK254 kaa mkao wa kula usipitwe na matukio.

Ushindi upi wakati mumebaki magofu, huo uislamu ndio huwaponza na kuanzisha maugomvi na kila mtu mnaishia kuuawa bure, kiukweli kila mkifuata maagizo ya huo uislamu kufanya maukatili kama mlivyoagizwa mnaishia kuumia nyie tu.
Enzi za leo hayo mauaji aliyokua anafanya huyo 'mungu' wenu muhammad, ukiyafanya utapigwa tu...hili agizo ndio huwa linawaponza sana “Terrorise and behead those who believe in scriptures other than the Koran – 8.12”
 
Back
Top Bottom