Je, Kiusalama na Kiulinzi hiki ninachokiona sasa huku nchini Puerto Rico si hatari kwa Rais wetu?

Ni kawaida kwa sababu Rais amalindwa kwa gharama yoyote ila sema Kwa Tanzania tumeishazoea wale PSU kuliko hao PSG!
 
Je Kiusalama na Kiulinzi ni ' afya ' kwa Kiongozi yoyote yule wa nchi kulindwa na askari waliobeba silaha kali na nzito popote pale anapokuwa au hasa akiwa katika halaiki ya Watu? Na kama ni sahihi je hawa Walinzi wanaoonekana wamebeba hizi ' silaha ' nzito wanaaminika vipi na Wenzao waliopo kuwa labda hawawezi ' kugeuka ' nyuma au wale waliopo nyuma hawawezi ' kumshambulia ' Kiongozi wetu?

Nitafurahi sana endapo nitajibiwa haya maswali yangu kwani kwa siku za hivi karibuni namuona sana Rais wa huku nilipo nchini Puerto Rico ' akilindwa ' namna hiyo hivyo nikaona si vibaya nikiwauliza ' Wabobezi ' wa masuala ya Kiulinzi na Kiusalama mliopo huko Tanzania mnisaidie kunifafanulia Kitaaluma na Kiueledi kabisa.

Nawasilisha na karibuni mno nchini Puerto Rico wana JF.
Swali zuri sana, nijuavyo siyo silaha zote zinakuwa na risasi,nyingi ni tupu tu,ila moja au mbili ndo zinakuwa na risasi hasa kwa wale walinzi walioaminiwa hasa.
 
Nasikia huko potoriko ni udikteta tuu.


Daini tume chama cha mapotoriko kitoke.
 
Hii Puerto Rico inayozungumzwa hapa siyo nchi ya wadanganyika kweli maana mkuu wa nchi ile juzi kwenye maonyesho ya tisatisa alikuwa full maaskari wenye masilaha.

Kiufupi hili jambo lina faida na madhara yake,tena makubwa!!
Kwa maelezo hayo nnauhakika umemuelewa mwenzetu alieko Puerto Rico. Puerto Rico anayoiongelea ndo hiyohiyo unayoidhania.
 
Kweli bongo vilaza wengi , yani wanashindwa kuielewa nch ya "Puerto Rico" mtoa mada aliyoimaanisha.

Mkuu hata mimi naish Puerto Rico , nilijiuliza swali hili nikakosa jibu, labda ni maagizo ya mwenyew kiongoz wetu Puerto Rico.
Madhara ya kutosoma yale masomo yanayodharaulika
 
Kuna mtu mmoja namjua hua anatembea kaning'iniza funguo ya gari kwenye lux ya suluali yake na hana hata baiskeli ni mpanda dala dala na msaga sole ya viatu.yote hiyo ni aina ya kutaka kuaminika mjini au kutaka kutapeli mahala.

JAH RASTAFARI MORNING AFRICA
 
Hivi kupost link yako ni kinyume na taratibu za JF? Sijazisoma sheria zote za JF ila toka nimejiunga JF nimekuwa nikipitia post nyingi sana japo sichangii na nimeona wadau wengi tu wakiweka link za website au matangazo mbalimbali na hawapewi ban labda kuna kingine nyuma ya pazia

Ila kwa tabia hii JF inaanza kupoteza ladha kama watu tuliozoea kusoma post zao kama THE BOLD wanapigwa ban Mara kwa Mara hivi. Nadhan hii ni Mara ya tatu kama sijakosea
Mkuu ndio wanasema hivyo lakini hata mimi nilishangaa iweje ale BAN kwa maana kuna wengine huwa wanapost link lakini hawapigwi BAN..sikuelewa kiundani sana mkuu hii ishu imekaaje
 
ulitaka tujue uko puetarico

1416073233148-jpg.202681


Njia hii ukiifuata utafika sehemu moja inatwa Kiabakari. Hapo ndio Puerto Rico.

Na ukiambaa ambaa na Mto Mara ukafika Wilaya ya Serengeti, ingia kata ya Kisaka. Kuna kijiji zamani kiliitwa Nyibokho, sasa hivi kinaitwa Costa Rica. Kule tunakula Kware wa porini na miwa, vitoga na kambale...raha sana Costa Rica
 
Je Kiusalama na Kiulinzi ni ' afya ' kwa Kiongozi yoyote yule wa nchi kulindwa na askari waliobeba silaha kali na nzito popote pale anapokuwa au hasa akiwa katika halaiki ya Watu? Na kama ni sahihi je hawa Walinzi wanaoonekana wamebeba hizi ' silaha ' nzito wanaaminika vipi na Wenzao waliopo kuwa labda hawawezi ' kugeuka ' nyuma au wale waliopo nyuma hawawezi ' kumshambulia ' Kiongozi wetu?

Nitafurahi sana endapo nitajibiwa haya maswali yangu kwani kwa siku za hivi karibuni namuona sana Rais wa huku nilipo nchini Puerto Rico ' akilindwa ' namna hiyo hivyo nikaona si vibaya nikiwauliza ' Wabobezi ' wa masuala ya Kiulinzi na Kiusalama mliopo huko Tanzania mnisaidie kunifafanulia Kitaaluma na Kiueledi kabisa.

Nawasilisha na karibuni mno nchini Puerto Rico wana JF.
Mambo ya usalama mimi siyajui nakumbuka wakati wa Nyerere kulikua hakuna mambo haya yule alikua Raisi kipenzi cha watu na alikua anajumika nao bila silaha kali. Sijui hawa wa sasa nini kimetokea
 
Back
Top Bottom