Je, jina lako/ID unalotumia JamiiForums lina maana yoyote?

Mkuu japo Uzi ni wa muda mrefu, tangu 2009, Nadhani bado ninayo nafasi kuchangia, ili wanachama wenzagu ndani ya JF, wapate kujua ni kwa nini natumia jina/id ya ya Mgodo visa.

Ilikuwa ni 1992, nakumbuka nilikuwa moja ya Madarasa (ningeomba nisitaje) katika shule ya Msingi Kibasila.

Kwa ufupi, nilikuwa ni mtu wa Story nyingi za Vituko na Matukio, nilikuwa ni moja ya watu wachekeshaji na nisie kaukiwa na Vibweka (yote hii ilisababishwa na Mzee wangu kumiliki Runinga mapema).

Siku moja katika Maongezi, ilitokea ndani yake badala ya kutamka neno MDOGO, mimi nikatamka MGODO...

Basi hapo ndipo kama jina lilizaliwa.
Kila mmoja anajua, pale unapo jifanya mjuaji, na bahati mbaya UKACHAPIA..

Jina lilinibamba, watu Mgodo...Mgodo..na wengine wakaongezea neno Visa.. (likazaliwa Mgodo visa)

Bahati nzuri/mbaya nikaenda/nikachaguliwa Elimu ya Sekondari, shule moja na baadhi ya class mate, jina Mgodo visa likaendelea...kutokana na kuendelea na Vituko au mbwembwe.

Wanafunzi wengine wakaona jina hilo limekaa mahala pake....yaani acha tu wana JF, Jina langu halisi, mpaka ndugu zangu wenyewe wameshaa lisahau..but life goes on, jina ni utambulisho tu, no matter ni zuri au baya.

Ndio maana yupo na MASUDI KIPANYA..
obama-laugh-US-worlds-funniest.jpg
 
Dah! We mtu ulipotea humu. Ilibidi nihakikishe hili bandiko lako si la miaka chungu nzima iliyopita. Good to see you again Mkuu.
Nipo mkuu.
Nikipata chance huwa nachangia, ila mara nyingi nimegeuka mtazamaji tu.
Hivi zile JF re-union parties hazipogo tena?
Pamoja sana mkuu.

Mapendo,
TANMO.
 
Sijazisikia tena Mkuu labda hii hali ya uchumi pia imechangia. Haya uwe unazuka mara moja moja nafasi ikiruhusu Mkuu.

Nipo mkuu.
Nikipata chance huwa nachangia, ila mara nyingi nimegeuka mtazamaji tu.
Hivi zile JF re-union parties hazipogo tena?
Pamoja sana mkuu.

Mapendo,
TANMO.
 
Good thread! Big up Mkuu BAK.
Kwa kuasisi hii thread.

ID yangu inamaanisha MPWA kwa kikabila chetu.
Nimeamua kuwa na hii Id kwa sababu tangu utotoni nimelelewa na my Auncle hadi na kanisapoti kielimu hadi nimefika chuo kikuu.
Auncle akiwa ananitambulisha kwa watu lazima aseme huyu ni Mpwa wangu, kwahiyo nimeamua kuwa na Id ya hivi kama kumkumbuka na kumuenzi kwa fadhila alizonifanyia.

Id yako kwa kihehe maana yake "Mnakufa"
 
Id yangu maana yake ni Kompyuta. Nilichagua ID hii ili kuenzi lugha ya Kiswahili hasa ukizingatia majina mengi ya vitu vya kisasa watu wanayatamka kwa kiingereza
 
Mm enzi nasoma seminari ile ikifika muda wa likizo nikienda mtaani, basi wana wananiambia kunae demu mkali kahamia mtaani. (Si unajua waseminari tulvyo na ugwadu)
Sasa kuna kipindi alihamia mwarabu mmoja tajiri mnoo. Alkua na watoto wakike watatu na ni wazurii kupita maelezo. Ukionekana unaongea nae, be ni sifa tosha. Bc bna mkora nmetoka seminari nakumbuka nlkua form four ndo nmemaliza. Bc nkaanza jipendekeza kwao, maana mzee wao alkua mfanyabiashara. Afu naongea English sio ya nchi hii kudadeQ. Bahati nzuri mwarabu mmoja akanielewa. Nkawa naenda nae mazoezini,ananishangilia. Bc maraia wakadai "we jamaa una sumu knoma" Mpk huyu mwarabu umemfanikisha?!! Unae effect kwelii. Braza mmoja kwa uchungu akasema "Hyu k*** ni ma-effect"
Bc ndo jina ikaanzia hapo.
Afu huyo mwarabu hamuezi amini ni mke wa celebrity flani "Mbana Pua"
Maisha haya bana
 
Back
Top Bottom