Je, Dkt. Kigwangalla amekata tamaa?

Je, Dkt. Kigwangalla amekata tamaa?

Tatizo yule Bwana wa Ikulu mteuzi huwa anayapenda majitu kama haya. Anaweza asichukue hatua yeyote dhidi ya Kigwanga.

Wanaotumbuliwa ni wale wanaojaribu kujiamini kwenye nafasi zao, wanaojaribu kujitegemea kimawazo na wale wanaohisiwa loyalty yao kwa mamlaka ya uteuzi siyo 100%.
 
Kwani anaeongelewa hapa ni dini gani?
images (1).jpeg
 
Kwani anaeongelewa hapa ni dini gani?
(a) Unaelewa kwamba hapakuwa na bado hakuna lengo la kuihusisha Dini ya Mtume Mohammad ( S. A.W) kwenye majadiliano?

(b) Unaelewa pia kwamba matendo na maamuzi yake ndiyo msingi wa majadiliano husika?

(c) Unaelewa athari za muda mfupi na mrefu kufanya mijadala ya masuala muhimu ya kitaifa kwa lenzi ya dini?; na

(d) Unatambua ukweli kwamba kuwa au kutokuwa na dini hakuhusiani moja kwa moja na matendo na mienendo ya mtu katika jamii?
 
Tatizo yule Bwana wa Ikulu mteuzi huwa anayapenda majitu kama haya. Anaweza asichukue hatua yeyote dhidi ya Kigwanga.
Tatizo lenu ni umbumbumbu wa sheria ya ukaguzi. Audit Query siyo wizi au kosa la jinai ndiyo maana ikaitwa query wala siyo misappropriation au theft/fraud na ndiyo maana wizara na idara zinapewa muda wa kujibu query husika na mara nyingi hizo query hufutwa baada ya kupata majibu toka wizara au idara husika. Wizara au idara ikishindwa kujibu hizo Audit Query ndipo Police/PCCB investigations inakuwa initiated ili kujua ukweli kama kuna kosa la jinai ama la.

CAG Audit anaangali kama taratibu za uhasibu zimefuatwa wakati wa malipo husika wakati Police na PCCB investigators wanachunguza kujua kama kuna kosa la jinai limetendeka kwa kuangalia vipengele vya kosa la jinai kama vimetendwa na watuhumiwa.

Hivyo Audit Query ya CAG haina maana kuwa pesa zimeibiwa au kosa la jinai limetendeka. Na ripoti yake siyo conclusive evidence kwa kosa la jinai.

Tatizo la JF ya sasa haina Great Thinkers (GT) kwa kuwa wengi wa GT wameachana nayo tukabaki sisi washabiki wa siasa tu.
 
Hahahaaaaa....... Uongozi ni jalala bwashee.

Ukiona kiongozi anatamka neno " Nimechoka" ujue hapo hamna kiongozi tena!
Kwani neno "Nimechoka" ni lazima litajwe ndipo ionekane hapo hakuna kiongozi tena?

Unaweka vitu vinavyoshawishi ujibiwe hata na watu wasiopenda kujibu. Niachie hapo.
 
Back
Top Bottom