Je, CHADEMA hawaelewi maana ya Lockdown?

Je, CHADEMA hawaelewi maana ya Lockdown?

Kama nchi, Pesa tunazo, na uwezo tunao...

Serikali yetu sikivu ya awamu ya tano haiwezi shindwa ikitoke total lockdown...

Usipotoshe raia na kuifanya serikali yetu ionekane haiwezi... wakati tunajua inaweza...



Cc: mahondaw
 
Unashauri watu kama wachuuzi, bodaboda, wavuvi, mamantilie n.k wakigoma kukaa ndani njia gani itumike kuwafanya wakae ndani?
Tuna serikali inayokusanya matirioni ya shillingi kwa mwezi ,haiwezkusustain watu wake hata kwa mwezi mmoja,au yenyewe ni serikali ya madaraka,ndege,flyover,SGR na vitu vingine vinavyofanana na hivyo?
 
Mawazo mbadala yawe ya kujenga sio kuangamiza jamii. Ukiwafungia watu ndani kwa lazima utaleta taharuki kuliko hiyo ya corona. Hakuna mzazi aliye tayari kuona mwanawe anakufa njaa hapo.
Watu wanatoka nje si kwamba wanapenda. Wenye uwezo walishafungia ndani familia zao muda tu. Ukienda kwa mbowe utakuta vyuku vimejaa kwenye friji, beef, pork na pombe za aina zote na vingine vipo stoo.
Fikiri kuhusu nama lishe, machinga, konda na dereva, muuza matunda.

Sent using Jamii Forums mobile app
Rais alisema ana pesa za kuendesha nchi kwa miezi mitano, Sasa iweje lockdown ya miez miwil iwe tatizo,

Suala ni kwamba waache uongo na kujimwambafai, haya Sasa kumetokea janga tekeleza Ile kauli uliyosema nchi ina pesa za kuitosha miezi mitano, alafu lawama zinapelekwa kwa wapinzani ajabu
 
Tuna serikali inayokusanya matirioni ya shillingi kwa mwezi ,haiwezkusustain watu wake hata kwa mwezi mmoja,au yenyewe ni serikali ya madaraka,ndege,flyover,SGR na vitu vingine vinavyofanana na hivyo?
Sawa, twende hatua inayofuata.
Nieleweshe njia gani ya distribution/ mgawanyo itumike kwa hicho kinachokusanywa kwa yale makundi niliyoyataja pale mwanzo.
 
Tatizo lenu mnadhani Corona ni siasa na eti ni vita vya chadema dhidi ya CCM.

Mawazo duni kabisa. Yaani uzi dhoofu bin hohahahe kabisa kuwahi kuwekwa hapa jamvini.

Hawa wanaopinga lockdown serikali ikitangaza lockdown wataunga mkono juhudi hiyo kwa namna ambayo haijapata kutokea.

JPM alione hili: "Tangaza lockdown mikoa yote iliyothibitika kuwa na wagonjwa utapata 100% ya support nchini".

Najiandaa kumpa mkuu ushauri wa bure: go lockdown, in return you have total support of the nation.

Zawadi ipi kuu kuliko hiyo mkuu unaweza kupata?
Unajua maana yake?

Freeman karantini imemshinda kakimbilia posho mjengoni.......wewe kapuku si ndio utafia nyumbani kwa wazazi kabisa!
 
Rais alisema ana pesa za kuendesha nchi kwa miezi mitano, Sasa iweje lockdown ya miez miwil iwe tatizo,

Suala ni kwamba waache uongo na kujimwambafai, haya Sasa kumetokea janga tekeleza Ile kauli uliyosema nchi ina pesa za kuitosha miezi mitano, alafu lawama zinapelekwa kwa wapinzani ajabu
Kuna tofauti kati ya kuendesha nchi na kuwalisha wananchi bwashee.
 
Mkuu responsibility sio ya mtu moja. Wao hawajafunga kitu chochote na wanaamini njia yao ndio mbadala. Tusubiri tuone, kila nchi ni lazima ifanye vile ambavyo ni sahihi kwa raia wake. Hatuwezi kuiga nchi flani flani kwa sababu kuna tofauti kubwa sana ya maisha kati ya USA na TZ au nchi yoyote ya ulaya. Usiige tembo k*ny*
Well said!
 
Kenya Uganda na Rwanda hakuna mamalishe? Sasa hivi wanaishije?

Hiyo social distance unayoisema ipo?
Pamoja na level seat Dar inafanyika mchana tu usiku watu wanashika bomba kama kawaida. Na Arusha ndio usisiseme. Vipanya vinajaza mpaka kufunga mlango shida.

Mabaa na night club yanaendelea kama kawaida. Kuna mahali tulipita usiku na jamaa yangu akaniuliza kuna korona kweli au ni utani kwa jinsi watu walivyokuwa wamejaa.

Raisi anasema hatuwezi kufunga mipaka kwa sababu tunategemewa na nchi zingine. Kwani Kenya haitegemewi?

Unaongelea umakini tupe mfano wa umakini unaoutaka.

Nairobi kwa siku wanapima watu 350 sisi waziri anatuambia toka janga lilipoanza wamepima watu 600 na ushee.

Sio lazima kufanyike lockdown kama nchi zingine. Wanaweza kusimamia hiyo social distance seriously na usafi kwa nguvu zote. Kwa sababu serikali umelegeza masharti kuna watu wameanza kusema hiyo korona haipo mbona hatuoni? Na wanagoma kunawa mikono.

Korona haijaletwa na CCM sasa inajihami nini kwa kitu ambacho sio makosa yao?

Kosa ambalo ndio litakuwa la CCM na serikali yake ni kutokuchukua hatua madhubuti kudhibiti COVID 19 kusambaa zaidi.

Onyo. Kwa mtazamo wa haraka hao walio kada ya juu ndio watakaoanza kushambuliwa kama tulivyoona Uingereza Iran Ghana Ujerumani Kenya na kwingineko. Viongozi wameonja joto ya jiwe.


*KWA COVID 19 WEKA SIASA PEMBENI.*






Sent using Jamii Forums mobile app
Rwanda wamepelekewa msaada wa chakula na Bakhresa wa Tanzania.

Kenya juzi wananchi walitaka kuuwana kwa kugombea chakula cha msaada!
 
Unafahamu mass testing gharama yake? Je, unavyo vifaa kwa kazi hiyo?

Mkuu, argument yako ni ya kipumba.vu. Hizo ulizozitoa ndio sababu hasa za kwanini tumekuwa hatuna lockdown. Yaani tumeacha ugonjwa uchukue wengine wakati wengine maisha yao yaendelee.

So, waambieni watu “hatutachukua hatua za lockdown kwa sababu hatuna uwezo na lockdown italeta shida kubwa kuliko corona”. Then mkae na mtulie. Hauna tofauti na wale wanaosema “tutumie lugha ya kiswahili elimu ya juu” sababu zao hasa sio kwa sababu kiingereza hakina manufaa, bali ni kwa sababu kiingereza kimewashinda!!

Kuweni wa kweli. Msiseme lockdown haina maana. Semeni hatuna uwezo nayo na turuhusu corona ichukue inaotaka.
 
Back
Top Bottom