Kenya Uganda na Rwanda hakuna mamalishe? Sasa hivi wanaishije?
Hiyo social distance unayoisema ipo?
Pamoja na level seat Dar inafanyika mchana tu usiku watu wanashika bomba kama kawaida. Na Arusha ndio usisiseme. Vipanya vinajaza mpaka kufunga mlango shida.
Mabaa na night club yanaendelea kama kawaida. Kuna mahali tulipita usiku na jamaa yangu akaniuliza kuna korona kweli au ni utani kwa jinsi watu walivyokuwa wamejaa.
Raisi anasema hatuwezi kufunga mipaka kwa sababu tunategemewa na nchi zingine. Kwani Kenya haitegemewi?
Unaongelea umakini tupe mfano wa umakini unaoutaka.
Nairobi kwa siku wanapima watu 350 sisi waziri anatuambia toka janga lilipoanza wamepima watu 600 na ushee.
Sio lazima kufanyike lockdown kama nchi zingine. Wanaweza kusimamia hiyo social distance seriously na usafi kwa nguvu zote. Kwa sababu serikali umelegeza masharti kuna watu wameanza kusema hiyo korona haipo mbona hatuoni? Na wanagoma kunawa mikono.
Korona haijaletwa na CCM sasa inajihami nini kwa kitu ambacho sio makosa yao?
Kosa ambalo ndio litakuwa la CCM na serikali yake ni kutokuchukua hatua madhubuti kudhibiti COVID 19 kusambaa zaidi.
Onyo. Kwa mtazamo wa haraka hao walio kada ya juu ndio watakaoanza kushambuliwa kama tulivyoona Uingereza Iran Ghana Ujerumani Kenya na kwingineko. Viongozi wameonja joto ya jiwe.
*KWA COVID 19 WEKA SIASA PEMBENI.*
Sent using
Jamii Forums mobile app