Umesoma kitabu

Umesoma kitabu

Mwl Mwakujonga

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2023
Posts
377
Reaction score
739
Mwaka 2026 unaelekea robo ya nne ya oktoba hadi Desemba, tukiwa tumemaliza wiki 37 kati ya wiki 52 za Mwaka.

Umefanikiwa kusoma kitabu gani? Biblia ina vitabu 66 kati ya hivyo vitabu kuna kotabu unaweza kusoma dk 2 na ukamaliza

Mara nyingi tumekuwa ni watu wa visingizio mara hohoho muda sina, mada mambo ni mengi, lakini ukweli mchungu hatutaki kusoma biblia.

Kama umeweza kuamka asubuhi na kuingia mitandao ya kijamii ukatumia hata dk 10 kusoma habari na jumbe mbalimbalia ujue muda unao sema hautaki kusoma

Inawezekana haujui faida ya kusoma biblia lakini faida moja wapo unaposoma neno la Mungu linakuongoza njia sahihi unayotakisa kuendeka

Biblia sio kwa ajili ya kwenda mbinguni tu ila ni kwa ajili ya kukupa maelekezo ya kuishi hapa duniani.

Watalaamu wa dini wanasema biblia ni muongozo wa Mungu kwa mwanadamu namna ya kuishi duniani

Sio lazima uanze kusoma vitabu vingi anza na vile vidogo somo kitabu cha Yuda , obadia, hagai , Yohana nk

Wakati nimeanza kusoma biblia nilikiwa mtu wa hasira sana, lakinj kadri nilivyosoma biblia nilijua namna ya kupambana na hasira

Nilijua hasara ya hasira na nilijua kwanini hasira inaweza kukukwamisha katika safari yako na Mungu, kwa hiyo biblia imekuwa msaada mkubwa sana wa kupambana na hasira

Sio tu hivyo ni mambo Mengi nimejifunza ikiwemo kusamehe na kusahau, katika maisha ya dunia hii lazima ujifunze kusamehe na kusahau na kucontrol hasira lasivyo utakuwa na changamoto sana

Kitabu cha mithali nilitabu kizuri sana cha kukusaidia namna ya kuishi vizuri na watu na Mungu.

Nilitabu ambacho Mfalme Sulemani ambaye alijaliwa kuwa na hekima kuliko wanadamu wote wa kipindi kile ametuachia tujifunze mahali alipopitia

Tuna na tabia ya kusoma vitabu sio tu biblia hata vitabu vingine vyenye maarifa mbalimbali

Je umesoma kitabu chochote mwaka huu? Ni kitabu gani ? Na umejifunza nini karibu
 
Kitabu cha kutoka!!!
Mungu atatupigania na atatuokoa,

Kitabu cha Hesabu!!!
Tusikate tamaa kurudi, maisha ya dhambi hata kama hatuoni tumaini mbele yetu...bali tumuamini MUNGU!

Na vingine vya kuongezea maarifa!!!
(Adam na eva,
Enock,
The story of redemption,
Councel on mental health,
Temperance,) Egw
N.k
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom