Jaribio la kutaka kuiangusha serikali ya Nyerere 1982/1983

Mleta mada umenikumbusha utotoni, wakati kesi ikiungurama pale mahakama kuu, sisi tukiwa watoto wa shule ya msingi, tulikuwa tunavizia ifike saa tisa ili tuwaone wale wahaini wakipandishwa kwenye karandinga baada ya siku moja ya kesi kumalizika. Tulikuwa tunakaa upande wa pili wa mahakama kuu, tunavunga kama vile tunaifaidi ile view ya bahari pamoja na kuangalia meli zinavyoingia kumbe lengo letu tuwaone wahaini.
Wakishaingizwa kwenye karandinga ndio sisi taratibu tunarudi nyumbani. Usalama wa nchi ulikuwa kazini enzi zile, ulikuwa huwezi kuongeongea hovyo kama watu wanavyofanya siku hizi.
Huyo wakili Lakha alikuwa mhindi, kichwa fulani cha ukweli.
 
Mimi ni kijana Wa 1990's lakini hii kesi ya uhaini nilikuwa naifuatilia nikiwa mdogo, ilikuwa very interesting na Komandoo Tamim alikuwa Noma sana.!
 
Nashukuru kwa tipp yako na maelezo yako. Ndio najua ile mission ilikuwa baab kubwa. Kungekuwa na uwezekano wa kuiona film yake, basi we acha tu.

Waliokuwa Dar enzi zile ndio walifaidi. Sisi wa mbali kaskazini basi ni kusikia sikia tu wakubwa enzi hizo wakipiga soga kijiweni. Ukiwakaribia wanakufukuza eti sio genge lako hili :). Gazeti huna hela ya kununua. Mjomba ananunua daily news na sunday new ili asiombwe. Redio ipo kwa babu tu na balozi wa nyumba kumi kumi. Huitoa j'mosi mechi simba na yanga. Basi tabu tupu :)
Movie atacheza Ray Kigosi akiwa na hangover ya kutosha ya maji pipa tisa
 
Tamim, nadhani aliuawa pale KINONDONI, au siyo?
Ndiyo pale mkwajuni alipojaribu kuwatoroka maafisa usalama kwa kudadia pickup iliyokuwa ikitokea magomeni. Mtafute Mfalingundi ambaye alikuwa mkuu wa kituo cha salender bridge kwa maelezo zaidi. Bahati mbaya afisa aliyempiga kept Tamimu sasa ni matehemu.
 
Mabibi na Mabwana,

Ningependa sana kupata historia na maelezo juu ya ile kesi ya uhaini. Siukumbuku mwaka ila nadhani ilikua 1982 nilikuwa msingi darasa la tatu hivi. Enzi zile ilikuwa vigumu kuuliza uliza maswali kwa kuogopa unaweza kukamatwa.

Sasa kwa vile sasa mambo yamebadilka ningependa kukumbushwa kidogo pale pamoja na mjadala hapa JF.


Shukran
Vijana wa zamani tulikuwa madhubuti..Pia vijana walifanikiwa kuteka ndege toka dar mpaka London...enzi hizo ....tofauti na hawa wa Dar.
 
Hii ni story nzuri ambayo ingewekwa wazi watu tujifunze pia iwe fundisho kwa kizazi hiki na pia itasaidia tuwe wazalendo nasikitika mpaka leo ni siri sijui ni siri gani isiyokuwa na mwisho
 
Komando kapten Tamim hakuuwawa na makomandoo wenzake bali na maafisa usalama baada ya zoezi la kumkamata mchana kweupe barabarani kuonekana linaelekea kushindwa na jamaa anaweza kutoweka
Na moja wa maafisa usalama aliyekuwepo kwenye hizo kashikashi za kuwakamata makondoo wa jwtz ni Mabere Marando huyu wa chadema, alikuwa ni moto wa kuotea mbali
 
Mawakili Waliotia Fora ni Hussein Muccadam(RIP) Murtaza Larkha, Jadeja Wote walikuwa wa Asia Tarimo, Mwanyika naLamwai Kitabu Cha Kesi Ya Uhaini Kilitoka Mwaka 1985 Kilichokuwa kimeandikwa na Marehemu Mnenge S. Suluja Mhusika Mkuu wa Washtakiwa alikuwa Thomas Lugangira au ‘Uncle Tom’
Wenzake walikuwa ni Hatibu Gandi au ‘Hatty Mac Ghee’, Kapteni Mohammed Tamim, Kapteni Mbogoro, Kapteni Christopher Kadege, Luteni Badru Rwechungura Kajaja na Kapteni Mapunda.
Wengine walikuwa ni Banyikwa na mkewe, Christopher Ngaiza, Zacharia Hans Pope , Kapteni Rodrick Rosham Robert , na Eugene Maganga Wengi nadhani ni Marehemu kwa sasa Lakini Pia Waliowahi kuiitwa Kwa Kuhusika Japo Hawakupatwa na Hatia ni Pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro wakati huo Marehemu John Mhavile(Baba wa Joyce Mhavile wa I TV /Radio One Kingine Kilichokuwa very interested kwenye kesi ni Baadhi wana Usalama kutumia Alphabet kuji indetify Badala ya Majina Yao yani walikuwa Mr. X Kama Mabere marando Dr. Hassy Kitine nadhani pamoja na Mizengo Pinda nk.Washtakiwa 9 Kati ya 16 Walihukumiwa kifungo cha maisha. Na Jaji Nassoro Mzava. Mwaka 1993 Walitoka kwa Sababu ya Tanzania kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi hivyo wafugwa wa kisiasa walipaswa kutoka Lakini Hatty MCghee alitoka akiwa mahtuti na akafariki Hospital MCghee aliwahi kutoroka pamoja na Uncle Tom lakini akadakiwa Horohoro Tanga.
Mwaka 1994 Nikiwa Idara ya uhamiaji makao makuu Nilikutana na zacharia Hans Pope akitafuta passport aende kutibiwa Figo South Africa lakini kaimu Mkurugenzi wa uhamiaji wakati huo Marehemu Peter Hassan Akampa makavu live kuwa huwezi kupewa passports sababu alikuwa chini ya uangalizi agizo kutoka Ikulu Hans Pope alinipa lift siku hiyo mpaka mikocheni pale talk of the town alikuwa na Mgari mbovu zile Land cruser Pick up sura mbaya yeye alikuwa akiishi Mwezi beach njia ya kuelekea Mediterranio hotel
 
Mkuu 1954 sheria ya mtandao nimeikiuka kifungu gani? Niambie niandae utetezi.
Huyo 1954 anajitia hofu bure tu... hakuna sheria yoyote unayovunja kv kila jina utakalotaja litakuwa kwenye kumbukumbu ya mahakama! Tatizo linaweza kuwa pale ambapo mathalani, mtuhumiwa X hakukutwa na hatia lakini wewe ukasema ambao walihusika ni pamoja na X! Lakini ikiwa X alikutwa na hatia na utokaji wake kifungoni ama ulikuwa ni kwa Msamaha wa Rais au kumaliza kifungo; basi sidhani kama kutaja ushiriki wa mtu kama huyo kunakiuka kifungu chochote cha sheria unless kama kifungu hicho kinakusudia kuzima sehemu ya historia ya Tanzania!!

Kwa maana hiyo basi, ningeshauri muendelee kumwaga madini hapa manake ni aibu kwa Taifa wananchi wake kutofahamu historia ya miaka 30 tu iliyopita... ndo kweli tutaweza kufahamu ni nini hasa kilitokea kwa Chief Mkwawa zaidi ya miaka 100 iliyopita!!!!
 
Mawakili Waliotia Fora ni Hussein Muccadam(RIP) Murtaza Larkha, Jadeja Wote walikuwa wa Asia Tarimo, Mwanyika naLamwai Kitabu Cha Kesi Ya Uhaini Kilitoka Mwaka 1985 Kilichokuwa kimeandikwa na Marehemu Mnenge S. Suluja Mhusika Mkuu wa Washtakiwa alikuwa Thomas Lugangira au ‘Uncle Tom’
Wenzake walikuwa ni Hatibu Gandi au ‘Hatty Mac Ghee’, Kapteni Mohammed Tamim, Kapteni Mbogoro, Kapteni Christopher Kadege, Luteni Badru Rwechungura Kajaja na Kapteni Mapunda.
Wengine walikuwa ni Banyikwa na mkewe, Christopher Ngaiza, Zacharia Hans Pope , Kapteni Rodrick Rosham Robert , na Eugene Maganga Wengi nadhani ni Marehemu kwa sasa Lakini Pia Waliowahi kuiitwa Kwa Kuhusika Japo Hawakupatwa na Hatia ni Pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro wakati huo Marehemu John Mhavile(Baba wa Joyce Mhavile wa I TV /Radio One Kingine Kilichokuwa very interested kwenye kesi ni Baadhi wana Usalama kutumia Alphabet kuji indetify Badala ya Majina Yao yani walikuwa Mr. X Kama Mabere marando Dr. Hassy Kitine nadhani pamoja na Mizengo Pinda nk.Washtakiwa 9 Kati ya 16 Walihukumiwa kifungo cha maisha. Na Jaji Nassoro Mzava. Mwaka 1993 Walitoka kwa Sababu ya Tanzania kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi hivyo wafugwa wa kisiasa walipaswa kutoka Lakini Hatty MCghee alitoka akiwa mahtuti na akafariki Hospital MCghee aliwahi kutoroka pamoja na Uncle Tom lakini akadakiwa Horohoro Tanga.
Mwaka 1994 Nikiwa Idara ya uhamiaji makao makuu Nilikutana na zacharia Hans Pope akitafuta passport aende kutibiwa Figo South Africa lakini kaimu Mkurugenzi wa uhamiaji wakati huo Marehemu Peter Hassan Akampa makavu live kuwa huwezi kupewa passports sababu alikuwa chini ya uangalizi agizo kutoka Ikulu Hans Pope alinipa lift siku hiyo mpaka mikocheni pale talk of the town alikuwa na Mgari mbovu zile Land cruser Pick up sura mbaya yeye alikuwa akiishi Mwezi beach njia ya kuelekea Mediterranio hotel
Kulikuwa na Mr.Y. Huyu ndiye aliyewachinjilia baharini watuhumiwa. Alikuwa na kumbukumbu kuanzia mtaa, eneo siku, saa na eneo.

Sasa hivi ni waziri wetu mambo ya kigeni
 
Companero,
Si kweli kwamba Oscar ndiye aliyemwokoa na kumficha Mwalimu katika mapinduzi ya 1964. Huyu mtafiti amekosea. Nadhani Kawawa alikuwa na jukumu kubwa zaidi kumshawishi Mwalimu kujificha kuliko Kambona. Kambona hakujua alipofichwa Mwalimu.
Nyerere na Kawawa walifichwa na mlinzi wa baba wa Taifa ndugu Mbwambwo. Na kiongozi pekee aliyefika Kigamboni kuwaona ni Bhoke Munanka.
 
Wakati wa Uasi wa Tanganyikan Riffles, Aliyekuwa waziri wa Ulinzi na Mambo ya nje Oscar Kambona ndiye aliyeomba msaada wa Waingereza kuzima uasi. Nyerere alikimbilia au tuseme alikimbizwa kufichwa Kigamboni ili asiuawa kwa Maana ilikuwa ni hatari sana.
Nitaweka clip fupi ya mzungu mmoja aliyekuwepo wakati ule.
 
Duh, wewe ni kiboko, umeeleza vema, isipokuwa sina uhakika na hilo jina la LAMWAI. Ila ile incidence naikumbuka sana. Yule TAMIM alikuwa noma sana, kwa mapambano, alikuwa ni komandoo haswa. Sina hakika sana yule jamaa, nadhani alikuwa wa Tanga kama sijakosea, but I am not so sure...ila lile kundi (wahaini) lilikuwa infiltrated sana, wao wenyewe walikuwa hawajui, basi tu hatuwezi kusema mengi humu JF. Ila TISS ya wakati ule ilikuwa kiboko, walikuwa wanachapa kazi kweli kweli, wazalendo, committed to their profession. Walikuwa wanakuwa vetted kweli kweli, lakini siku hizi, aaah, sijui bwana....
Mkuu, Mwalimu alipoambiwa habari za kutaka kupindua serikali yake alipuuzia. Akaondoka kwenda Butiama na kusema hakuna anayeweza kufanya hivyo. Huku watu wakajipanga kweli kweli. Kama ulivyosema TIS ya wakati huo ilikuwa inafanyakazi kizalendo. Watoa habari nao walikuwa wakifanya kazi kizalendo sana. Baada ya kuwa jamaa wamejiandaa sasa kuanza kupanga watu wao kila eneo waliloliona mhimu, mwalimu alipopewa taarifa akiwa huko Butiama kuhusu hali halisi, ilibidi achukue ndege fasta kuja Dar. Ila jaribio hilo lilizimwa kishujaa na kwa weledi mkubwa mno.
 
..kwa mtizamo wangu wahusika wa huu mpango walijaribu ku-recruit wanajeshi ambao walikwenda kutoa taarifa ktk vyombo vya usalama.

..nadhani hicho ndicho kilichopelekea mpango mzima kufeli.

..suala lingine inaelekea pia walikuwa careless na watumiaji wazuri wa pombe. Katika ufuatiliaji wangu wa mwenendo wa kesi na ushahidi uliokuwa ukitolewa inaelekea one of their main guy was talking too much and acting/behaving in a way that made attract the attention of security organs.
 
Back
Top Bottom