Jaribio la kutaka kuiangusha serikali ya Nyerere 1982/1983

Alichoandika Yericko eti Nyerere aliwasamehe waasi wa 1980s eti akawapa ubalozi sijui blah blah ni kamba mtupu.

Mmoja kati ya hao waasi ali-share kwenye magazeti hii story yake miaka haizidi sita iliyopita.

Jamaa yeye alitorokea Kenya na alikamatwa na kurudishwa Tz na wakafungwa lakini walitolewa baadae na huyo muasi msimuliaji aliachiwa akiwa gereza la Butimba na walikuwa wanajeshi vyeo vya chini tu.

Kipindi anatoa makala zile jamaa alikuwa Tabora akiwa choka mbaya hana chochote.

Ngoja nizitafute hizo makala.
 
Ni Januari 9 , 1982 siku ya Mapinduzi ambayo kamwe hayakufanikiwa matokeo yake. Akiwa katika gereza la Butimba lenye ulinzi wa hali ya juu, utaratibu wa mahabusu na wafungwa akiwemo Eugene Maganga kwa miaka miwili ulikuwa ni kuamka mapema mwishoni mwa wiki. Kwa sababu fulani hata hivyo, Jumamosi asubuhi ya Oktoba 22, 1995 aliamkamapema na alipowasha radio yake ndogo ulikuwa wakati muafaka kwake kupata taarifa fupi zikisema kwamba Rais Ali Hassan Mwinyi alitoa msamaha kwa wafungwa akiwemo yeye pamoja na wafungwa wengine wengi. Huu ni wakati ambapo kundi la watu wanane walikuwa wakiusubiri, kwa miaka kumi ambayo wamekuwa kifungoni wakitumikia kifungo cha maisha kwa uhaini.Kamwe hawakuweza kupoteza matumaini. " Wafungwa katika jela mbalimbali ambao pia walisikia habari hizi walianza kushangilia ,"anasimulia Maganga." Cha kushangaza sikufurahia kwa sababu nilikuwa naisubiri siku kama hii kwa muda mrefu. Mara zote ilikuwa inatisha kufikiria kuwa ningeweza kutumia maisha yangu yote gerezani. "

Maganga na watu wengine saba - Suleiman Kamando , Zakaria Aspopo , Vitalis Mapunda, Mbogolo, Kajaji Badru, Hatty MacGhee na Christopher Kadego walitiwa hatiani mwaka 1985 kwa ajili ya mpango uliopangwa miaka miwili iliyopita kuipindua serikali ya Rais wa kwanza nchini Julius Nyerere. mtu wa tisa, Mohamed Tamimu aliuwawa katika mapambano ya risasi na polisi wakati wa kukamatwa kwao.

Siku ya Jumatatu Oktoba 24, 1995, siku mbili baada ya habari kufika kwenye redio, Maganga alitangazwa kuwa mtu huru. Anakumbuka vizuri siku hiyo alipovuka milango ya gereza kwa uhuru. Ilikuwa ni majira ya saa saba mchama. "Tulikaribishwa nje ya gereza na ndugu zangu wenye furaha pamoja na wale wa mfungwa mwenzangu Hatty MacGhee . Hisia zangu zilikuwa juu kiasi kwamba ni vigumu sana kuelezea kwa sasa ," anasema Maganga. Wafungwa wengine sita wa uhaini waliachiwa siku mbili baadae kutoka Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam. Wakati wa kutolewa kwao, Maganga alikuwa amezungushwa katika magereza kadhaa ikiwa ni pamoja na Ukonga jijini Dar es Salaam na sehemu yake ya mwisho ilikuwa Butimba jijini Mwanza. Licha ya matatizo waliyovumilia gerezani, Maganga anasema hakuna hata mmoja wao aliyewahi kujuta kwa kujaribu kuipindua serikali. "Tunajutia tu kushindwa mapinduzi lakini hatujutii kupanga mapinduzi".

Kabla ya wao kuja na wazo la kuipindua serikali, Maganga na Kadego walifanya kazi katika jeshi kwenye kikosi cha mizinga . Maganga alikuwa Luteni wakati Kadego alikuwa kapteni. Maganga alikuwa na umri wa miaka 26 na alikuwa ndio kwanza amerudi kutoka London ambapo alitumia miezi minne kuongeza ujuzi wake wa kijeshi kabla ya kuitwa kwenda kupambana katika vita vya Uganda mwaka 1978. Kama mmojawapo wa askari waliokuwa mstari wa mbele, Maganga anaamini Tanzania ilishinda vita kwa sababu Uganda ilikuwa na jeshi dhaifu. Lakini hawezi kusamehe misingi ambayo vita ilijengwa . "Rais Nyerere alitumia vibaya rasilimali za nchi kupigania maslahi ya rafiki yake wa karibu Milton Obote ili aweze kurudi madarakani". Endapo sababu za kutoelewana zilizosababisha vita zilikuwa za msingi, Maganga anasema diplomasia ingesaidia kutatua tatizo kirafiki. Badala yake walipendelea kampeni ya kijeshi. Mara baada ya vita hii , Mei 1980, Maganga alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kujifunza Uhusiano wa Kimataifa na Utawala wa Umma . Kamwe hakuwa na furaha kutokana na aina ya maisha ambayo Watanzania walikuwa wakiishi, anasema walikuwa maskini na walikuwa wakilazimishwa kuishi katika vijiji vya Ujamaa .

Kundi hili lilijenga hoja kwamba vita kati ya nchi hizo mbili ilikuwa si lazima na ilisababisha matumizi mabaya ya fedha za umma. "Vita haikuwa kati ya nchi mbili bali ilikuwa ni kati ya Nyerere na Idi Amin".
Maganga anaeleza zaidi kuwa pia walilichukulia suala la hali ya hamasa katika jeshi ambayo ilikuwa imeshuka hasa baada ya Meja Jenerali Mrisho Sarakikya Mkuu wa kwanza wa Majeshi ya Ulinzi (1964-1974) na timu yake kujiuzulu. Wapangaji wa mapinduzi pia walihisi kuwa Rais alikosa imani kwa watu wa kaskazini kwasababu walikuwa wame elimika nje ya nchi hivyo aliogopa kuwa wangejaribu kumpindua.“ Watu ambao walikuwa na elimu ndogo walichukua nafasi za juu na hapo ndipo mambo yalipoenda vibaya,”, anasema Maganga. Askari hawakupandishwa vyeo kutokana na sifa kwa kuwa Rais alikuwa na nia ya kujenga jeshi lenye watu ambao hawakuweza kuleta changamoto yoyote dhidi yake. Anasema baadhi ya maafisa walipandishwa mara mbili kwa juma moja. “Sisi tulitaka kuleta mabadiliko lakini aina ya watu tuliotaka kufanya nao kazi hawakuwa tayari kujitolea . Hata hivyo, sisi hatukukata tamaa juu ya nia yetu ya kuleta mabadiliko”. Wakiwa bado wanajadili jinsi ya kukamilisha mipango yao, Maganga na wenzake, walikutana na marehemu Pius Rugangira (Uncle Tom) ambaye alikuwa mfanyabiashara wa Tanzania aliyejiimarisha nchini Kenya.

Baba yake Rugangira hakuwa na uhusiano mzuri na Rais Nyerere, kwamujibu wa Maganga, naye alikuwa amekwenda kuishi na kufanyakazi nchini Uganda. Na kwasababu yakuwa Uganda, Rugangira alishtakiwa kuwampelele zitoka Uganda, shutuma ambazo zilisababisha mtafaruku na serikali. Kwaujumla, yeye pia aliona kuwa Watanzania hawakustahili kulipa bei ya vita iliyopangwa na ndio sababu aliamua kuwasikiliza wapangamapinduzi. Rugangira alijitolea kugharamia shughuli zao, Maganga na maafisa wengine wa jeshi ambao waliokubaliana kufanya kazi pamoja, walianza kupata matumaini. "Sisi wote tulikuwa vijana na hatukuwa na imani yeyote na afisa wa cheo cha juu jeshini kwa sababu walikuwa wameridhika na jinsi mambo yalivyokuwa". Ingawa kuna ukimya kuhusu mipango yao ya mapinduzi ya kijeshi, Maganga anasita kuonyesha wazi jinsi walivyokuwa wamepanga kutekeleza mpango wao. Anasema tu kuwa bado hiyo "ni siri" ingawa walitarajia kutumia uzembe uliokuwepo jeshini ili kufikia malengo yao .

Mpanga mapinduzi mwingine ambaye alikuwa katika kundi la Maganga wakati wa mahojiano lakini hakutaka jina lake litajwe, anasema watu wengi wanaamini kundi lilipewa fedha nyingi kufanya mapinduzi lakini kwa kweli fedha kidogo walizopata kutoka kwa Rugangira zilikuwa kwa maana tu ya kushughulikia dharura ndogo. Anasisitiza haikuwa fidia kwa ajili ya kufanya mapinduzi . "Kama sisi tulililipwa fedha , hakuna hata mmoja wetu ambaye angekuwa maskini leo". anasema. Askari mmoja mstaafu anaongeza kwamba walitaka kujenga demokrasia ya vyama vingi ambayo watu wangekuwa na uhuru wa kutoa maoni yao na kuchagua rais wao wenyewe . "Tulitoa mapendekezo kwamba Rugangira angekuwa Waziri Mkuu lakini kwa sharti kwamba asingegombea urais katika uchaguzi ambao ungefanyika baada ya miaka mitano baadaye". Siku tatu kabla ya mapinduzi yaliyopangwa hayajafanyika , Rugangira aliripotiwa kuwauliza kuwa walitaka wapewe nafasi gani katika serikali mpya lakini walijibu kuwa hawataki chochote.

Wakati mipango yote ilipokuwa tayari ,walisubiri kuwasili kwa rais ambaye alikuwa katika ziara nje ya nchi. Kwa mujibu wa Maganga, rais alirudi Januari 1982 baada ya kukaa miezi miwili nje na akaenda kijiji nyumbani kwake Butiama ."Sababu ya kutaka kuipindua serikali wakati yeye akiwa nchini ni kwamba tulikuwa na nia ya kumuua". Maganga anasema. Alikuwa Rugangira aliyepinga mpango huo na badala yake alipendekeza kumkamata rais. Nyerere bila kutarajia alitumia muda mwingi akiwa Butiama na alikuwa bado kurudi Dar es Salaam siku mbili kabla ya siku mapinduzi yalipopangwa ilikuwa siku ya Jumatatu Januari 9, 1982. Ijumaa kabla yake Januari 6, waalikuwa wamepanga kukutana kwa mara ya mwisho kabla ya mapinduzi kufanyika lakini baadhi ya wenzao hawakutokea kwenye mkutano. Mohamed Tamimu alikuwa miongoni mwa wale ambao hawakuja . "Tulikuwa na wasiwasi na tuliamua kutuma mmoja wetu Kinondoni Mkwajuni kuuliza lakini tulishtuka kuona kwamba polisi walikuwa wamevamia nyumba yake na aliuawa katika mapambano yaliyodumu saa mbili akifukuzwa kutoka uwanja wa Leaders, alipofika Kinondoni eneo maarufu la sinema (ubalozi wa Marekani leo) alizidiwa nguvu na kuuawa na kikosi cha majasusi kilichokuwa kikiongozwa na jasusi na mwanasheria nguli Mabere Nyaucho Marandu". anasema Maganga. Katika hatua hiyo, walijua utambulisho wao na mipango yao haikuwa siri tena. Tamimu, kwa mujibu wa wenzake, alikuwa na utamaduni wa kutunza kumbukumbu za mikutano na majina ya washirika. Ilikuwa ni suala la muda tu kabla hawajakamatwa.Tamimu alipangwa kuwa mdunguaji maalumu kwaajili ya kumuua rais Nyerere aliyekuwa akirejea toka nje ya nchi.

Hisia zao zilikuwasa hihi. Polisi walikuwa kila mahali kusaka kikundi. Kadego na Maganga waliamua kutoroka kupitia Tanga na Mombasa hadi Nairobi ambako walikaa kwa miezi kumi kama wakimbizi wa kisiasa. "Hatujui nini kilichotokea kwa watu wengine ambao tuliwaacha Dar es Salaam lakini hatukukata tamaa tulipofika Nairobi. Tulitaka kujipanga tena na kurudi kuipindua serikali , "anasema Maganga .

Kamwe hawakuweza kulaumiana wao kwa wao kwa kushindwa kufanya mapinduzi ingawa Maganga anaamini bahati yao iliondoka kwa sababu MacGhee alikuwa raia wa kawaida na hakujua jinsi ya kutunza siri . Anamtuhumu MacGhee kwa kuvujisha taarifa kwani karibu watu wote walijua kabla ya kukakimilka kwa mpango. Maganga pia anahisi kuwa Tamimu alijua kwamba MacGhee hakuwahi kuwa askari wa Marekani kama alivyokuwa akidai lakini hakuwaambia . " Tuligundua baadaye kwamba jina lake halisi alikuwa Hatibu Hassan Gandhi na alikuwa rubani wa Tanzania " Mjini Nairobi , hawakuwa na ajira na walikuwa wanaishi chini ya msaada wa Tume ya Umoja wa Mataifa kwa Wakimbizi. Maganga anasema walikuwa na baadhi ya mawasiliano na ubalozi wa Marekani mjini Nairobi ambako waliomba udhamini na kuanza msingi upya jijini Nairobi ambapo wangeweza kujipanga vizuri na kupanga kwa ajili ya mapinduzi mengine ."Walisema walikuwa na shughuli nyingi zinazofanana na wasingeweza kutuunga mkono". anasema.

Siku chache baadaye Maganga na Kadego wakizunguka katika mitaa ya Nairobi, ghafla waliingia kwa mpanga mapinduzi mwenzao Uncle Tom na MacGhee waliyekuwa wamemwacha Dar es Salaam . Wawili hao walikuwa wamekimbia toka gereza la Keko jijini Dar es Salaam ambako walikuwa wamewekwa baada ya kukamatwa kwao.

Ingawa walikuwa huru na maisha yao mjini Nairobi Rugangira aliamua kusafiri kwenda London kuangalia namna ya kuingia Malawi. Alikuwa na mashaka kuwa serikali jijini Nairobi na Dar es Salaam zinaweza kula njama na kuwakamata. Wote nane walikuwa kwa namna fulani wameweza kutoroka kwenda Nairobi.

Hakika, kabla Rugangira kurudi kutoka London, kundi hili lilikamatwa na mamlaka jijini Nairobi na kubadilishana na Senior Lance Koplo Ochuka na Sergeant Pancras Oteyo ambaye pia alifanya majaribio ya kuipindua serikali ya Rais Daniel Arap Moi mwaka 1982 na walikimbilia Tanzania .

"Tulifungwa sana pingu na kufunikwa macho na kupelekwa gereza la Isaka lenye ulinzi wa hali ya juu mjini Dodoma ambako tulikaa kuanzia Novemba 1983 hadi Oktoba 1984", anasema Maganga .
Juu ya kuwasili huko, walikuta kuta za mahabusu gerezani zimepakwa kinyesi. Walifungwa minyororo kwenye ardhi, walitumia siku tatu bila kuoga. Mkuu wa gereza aliagiza walinzi gerezani wasizungumze na wafungwa au hata kuwa karibu nao kwa kuogopa kwamba wafungwa wangejaribu kuwashawishi wasimamizi wa sheria na usala wa jela kujiunga pamoja nao na kutoroka. Maganga anasema hata hivyo watu waliokuwa wanawalinda hawakuwa wote wabaya na kuna wakati mmoja wao alisaidia wafungwa kusafirisha barua kwenda Ubalozi wa Marekani. Walitaka dunia ijue kwamba walikuwa jela kwa sababu hakuna mtu alikuwa anafahamu hili kwa wakati huo. Barua waliyokuwa wameandika, Maganga anasema, ilisababisha Kamishna wa Umoja wa Mataifa kwa Wakimbizi kutembelea Tanzania na kushinikizwa serikali kupeleka kesi mahakamani. Kesi ilianza Januari 1985 na Desemba ya mwaka huo na walihukumiwa kifungo cha maisha .

Wanasisitiza kwamba kimsingi hawajutii kuhusu kupanga njama ya mapinduzi, lakini Maganga anasema anakatishwa tamaa tu ni kwa namna maisha yao yalivyogeuka. Baada ya kuwekwa huru, waligundua kuwa baadhi ya marafiki na jamaa walikuwa wamegeuka kuwa maadui wao na hata kutotaka kuonekana karibu au pamoja nao. Wote Kadego na Maganga hawakuwahi kuoa na Maganga anasema sehemu ngumu sana labda si miaka kumi waliyotumikia jela lakini kuanza tena upya wakati hawana chochote. "Serikali ilihakikisha kwamba hatuwezi kupata ajira mahali popote na baadhi yetu walibaki bila ajira hadi leo hii, " anasema. Baadhi yao ambao familia zao zilikuwa bora wameweza kujipenyeza katika biashara. " Kadego na mimi tunaishi mkono kwa mdomo . Kwa kweli Kadego ni mmachinga , " Maganga anasema. MacGhee alikufa wiki moja baada ya kutolewa wakati baadhi wao walijaribu kujiunga na vyama vya upinzani lakini waliamua kuacha. Waliona vyama vilikuwa havijajipanga na watu ambao waliwaongoza walionekana wabinafsi. "Katika uchaguzi wa mwaka 1995, mimi niligombea kiti cha ubunge katika jimbo la uchaguzi Tabora lakini nilipoteza . Sitaki kujihusisha katika siasa tena, " Maganga anasema.

Maganga ana watoto wawili kutoka kwa mama tofauti na anasema hakuna mtu aliyejali kuwapeleka katika shule nzuri wakati alipokuwa jela. Yeye bado ana matumaini ya kuwapatia elimu nzuri lakini hana mapato, mipango yake imeanza kuonekana kama ndoto. Alijaribu kujiunga na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kujifunza Sheria mwaka 1999 lakini alishindwa kuendelea katika mwaka wake wa pili kutokana na ukosefu wa ada. "Si marafiki zangu wote wanajali kuhusu matatizo yangu. Baadhi hujaribu kunifikiria mimi wakiwa na kitu cha kunipa , "anasema. Pamoja namna mambo yalivyokwenda hivi sasa, yuko tayari kufanya kazi yoyotte anayoweza kupewa. Hata hivyo, maisha yake binafsi hayamsumbui kabisa kama vile kile anachokiita' mawazo ya Watanzania. "Wanalalamika karibu kila kitu lakini hakuna hata mmoja wao aliyewahi kuchukua hatua yoyote. Wanatoa lawama kwetu kwa kujaribu kuipindua serikali wakati wengi wao bila hata kuthubutu," anasema. Akasema alikuwa anaenda kulala usiku bila chakula chochote lakini hakuwa mnyonge, isingekuwa mara ya kwanza. Ni wakati yeye anasema, "Nchi hii ... Nyerere kapotosha mawazo ya watu . Watu wachache sana wanaweza kufikiri na kuchukua hatua, " kwa hiyo hujikatia tamaa, Maisha ya mbwa.

Wakiwa gerezani walipata taabu sana hasa kwa wafungwa wa kisiasa kama wao. Walikuwa hawaruhusiwi baadhi ya marupurupu ambayo walikuwa na haki kuyapata, na waliweza kushuhudia maovu kadhaa ambayo yaliishia chini ya paa za magereza . Maganga anakumbuka kushuhudia wafungwa vijana kulawitiwa . Kulikuwa na ndoa za jinsia moja, wachuuzi wa madawa ya kulevya na baadhi ya wafungwa waliweza hata kuandaa ‘mashindano ya urembo’ ambapo wanaume walionyeza mambo yao.

"Wafungwa waliosimamia wengine walilala na wale ambao walishinda mashindano ya urembo na wakawapa neema kidogo kama zawadi, kwa mfano, kuwatetea kutofanya kazi ngumu na kuruhusu kwao anasa ya kuoga kwa sabuni. Ilikuwa ni uzoefu mbaya na unaochukiza machukizo ambayo bado yanaendelea katika mawazo yangu , "anasema Maganga . Kabla ya kupelekwa gerezani Maganga anasema alidhani kuwa jela zilisimamiwa na maafisa ustawi lakini kwa mshangao wake hakukuwa na mtu yoyote katika magereza ambayo yeye aliwahi kutumikia adhabu yake.
Aidha, maafisa magereza waliwezesha uuzaji wa madawa ya kulevya katika magereza na hata walishiriki katika kuuzia wafungwa vijana wafungwa wengine. walinzi hawa pia walishuhudia wafungwa dhaifu wakibakwa na wafungwa wenye nguvu bila kujaribu kuingilia kwa namna yoyote .

Maganga hata hivyo ana furaha kwa mabadiliko madogo yeye na wenzake waliyoweza kuleta katika magereza yote waliowahi kutumikia . Pamoja na James Christopher mshirika wa karibu wa Kadego , walikuwa muhimu katika kuimarisha shughuli za michezo na kutetea haki za wafungwa wengine katika gereza la Ukonga . "Hatukuweza kamwe kumvumilia mtu yeyote ambaye alijaribu kukiuka haki za wengine” Kwa sababu ya jitihada zao za kuwatetea, baadhi ya wafungwa wenzao hawakusherehekea kutolewa kwao, kwani sasa wangeachwa na kujilinda wao wenyewe .
....................................................................

Makala hii inapatikana katika kitabu kiitwacho Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi kilichoandikwa na member mwenzetu hapa jf Yericko Nyerere
 
SIRI YA UASI WA 1964

Na comred Mbwana Allyamtu

MLINZI mkuu zamani wa Baba wa Taifa, Julius Nyerere, Peter Bwimbo (87) ameandika kitabu kwa mara ya kwanza akiweka wazi jinsi Mwalimu alivyotoroshwa kutoka katika mikono ya wanajeshi walioasi katika Maasi ya Jeshi ya mwaka 1964.

Kitabu hicho: “ Peter D.M Bwimbo: Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere ” kimechapwa mwaka huu nchini na Kampuni ya Mkuki na Nyota na kina jumla ya kurasa 131 zinazoeleza mambo mbalimbali ambayo hayakuwahi kuelezwa waziwazi na yeyote.

Kwa mfano, kitabu hicho; zaidi ya kueleza namna Nyerere alivyotoroshwa –kimeeleza pia namna aliyekuwa Waziri Mkuu, Rashidi Kawawa, alivyonusurika kufa kwa kuvuta hewa chafu nchini Misri kwenye miaka ya 1960 na namna Mwalimu pia alivyoamua kutopanda ndege iliyokuwa imeandaliwa na mwenyeji wake, aliyekuwa Rais wa Zaire, Mobutu Seseseko, kutokana na hofu za kiserikali.

Ilivyokuwa wakati wa maasi

Januari 20, mwaka 1964, askari wa Kiafrika waliokuwa ndani ya Jeshi la KAR waliasi kwa madai kwamba ingawa Tanganyika ilikuwa imepata Uhuru, bado jeshi hilo lilikuwa chini ya Waingereza na wanajeshi wengine wenye asili ya Kiasia.

Katika kitabu hicho, Bwimbo ameandika kwamba maasi hayo yalitokea ghafla pasipo mipango hiyo kufahamika hata kwa Idara ya Kikachero ya wakati huo (Special Branch) na kwamba wahusika hawakufahamika mapema mpaka walichopanga kilipokamilika na hatimaye maasi kuanza.

Ni maasi hayo ndiyo yaliyosababisha KAR kuvunjwa na hatimaye kuundwa kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) pamoja na Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) kama inavyofahamika sasa.

Operesheni Magogoni

Bwimbo anasema katika kitabu hicho kwamba aliipachika kazi ya kumwokoa Mwalimu na Kawawa wasitekwe na waasi waliokuwa wamevamia Ikulu jina la Operesheni Magogoni, kwa vile kivuko kilichotumika kuwaondoa viongozi hao kutoka Ikulu na kuwapeleka Kigamboni kilikuwa kinafahamika kwa jina la Magogoni.

“ Nilipigiwa simu majira ya saa 8 usiku na ofisa wa kitengo chetu aliyekuwa mkuu wa zamu usiku huo hapo Ikulu, Leon Kazimili, kwamba kuna taarifa kuwa katika kambi ya Calito (Lugalo) palikuwa na dalili kuonyesha kuwa imevamiwa na majeshi ya kigeni usiku huo; Januari 20, 1964.

“ Niliamka haraka kuelekea Ikulu nikiwa na gari langu kwa sababu Ikulu ndiko mahali walipokuwa Rais pamoja na Waziri Mkuu ambaye nyumba yake ilipakana na Ikulu upande wa Kaskazini. Leon Kazimili sasa ni marehemu. Niliwasili Ikulu kutoka nyumbani kwangu Upanga majira ya saa 8:20 usiku. Wakati huo, tayari watu wa usalama walikuwa wamewaamsha Rais na Waziri Mkuu kuwaeleza kuhusu kilichotokea Calito.

“ Nilipanga haraka akilini mwangu hatua za kuchukua katika hali ya dharura kama hiyo kutokana na mafunzo niliyokuwa nimeyapata nchini Marekani mwaka 1963. Nilitoka nje ya viwanja vya Ikulu kwa nyuma upande wa baharini kwa miguu kama majira ya saa 8:45 usiku huo nikiwa na Nyerere na Kawawa, bila wasiohusika kufahamu.

“ Mkurugenzi wangu (Mkuu wa Special Branch) pamoja na Kamishina wa Polisi (sasa IGP) walibakia katika eneo la Ikulu. Ni muhimu kupotosha ukweli katika mazingira haya ya dharura ili maadui au wasiohusika wasifahamu kinachoendelea wakati huo.

“ Nilikuwa na askari polisi wawili wenye sare waliokuwa wanalinda uwanja wa Ikulu siku hiyo. Nilitumia usafiri nilioukuta kwenye kivuko cha serikali cha Magogoni baada ya kuwaeleza wafanyakazi waliokuwa wanaendesha pantone siku hiyo kuwa nilitaka kuwawahisha viongozi hao wawili kwenye kikao maalumu kilichopangwa kufanyika katika Chuo cha Kivukoni.

“ Wafanyakazi hao wawili penye kivuko ambao kutokana na mazingira ya usiku huo sikuweza hata kuchukua majina yao, walikubali kutuvusha baada ya kuona kwa macho yao sura za viongozi hao wawili (Nyerere na Kawawa). Tulipovuka, tuliwaambia wale wafanyakazi kuwa wasikirudishe kile kivuko Magogoni kwa sababu viongozi wangetaka kurejea Ikulu mara tu baada ya kumalizika kwa kikao chao. Lengo lilikuwa ni kuhakikisha kuwa hata kama maadui wangebaini kuwa Rais na Waziri Mkuu wameondoka, wasingeweza kuja Kigamboni kwa wakati huohuo,” ameandika.

Kwa sababu hakukuwa na maandalizi ya kumpokea Mwalimu na Kawawa, Bwimbo ameandika kwamba ilibidi watembee kwa mguu kutoka Kigamboni hadi katika kijiji cha Salanga katika usiku huo wa manane wa kihistoria na kwamba njiani walikuwa wakitishwa na mbwa kutoka katika nyumba walizokuwa wakizipita.

Bwimbo ambaye anasema alipata mafunzo mbalimbali ya masuala ya ukachero katika nchi za Uingereza na Marekani, alisema alikuwa na lengo la kuwapeleka viongozi hao katika nyumba ya kupumzikia viongozi iliyokuwepo eneo la Mji Mwema lakini sababu kulianza kukucha, waliamua kulala kwenye nyumba ya msamaria mwema, Sultan Kizwezwe, ambaye aliwapokea vema na wala hakuwasaliti kwa adui.

Kitabu hicho kinachopatikana katika duka la Tanzania Publishing House (TPH) lililopo mtaa wa Samora jijini Dar es Salaam, kimeeleza namna mlinzi huyo alivyokuwa akiwakatia mapapai viongozi hao na kula nao; katika wakati ambapo askari waasi walikuwa wakiwatafuta kwa lengo la kuwadhuru au kuwadhalilisha.

Mzee Kizwezwe sasa ni marehemu na Bwimbo alieleza kuwa ingawa Mwalimu Nyerere alitaka kumjengea nyumba kama shukrani zake kwake; msamaria huyo alikataa zawadi hiyo na badala yake alikubali zawadi ya baiskeli.

Katika wakati huo ambao Mwalimu alikuwa akiishi Salanga, ni kiongozi mmoja tu; aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, hayati Bhoke Munanka, ndiye pekee aliyepata fursa ya kupafahamu alikofichwa Mwalimu na kuzungumza naye.

Kwa mujibu wa mtunzi wa kitabu hicho, kilitakiwa kichapwe mapema kuliko mwaka huu lakini kwa sababu ya unyeti wa taarifa za mwandishi huyo, ilibidi kwanza kihakikiwe na vyombo vya ulinzi na usalama nchini.

Kitabu hiki cha Bwimbo ambaye ana asili ya Ukerewe, Mwanza, ni cha kwanza kuandikwa na mtumishi mstaafu wa TISS; mojawapo ya taasisi ambazo usiri ni mojawapo ya sababu za kuwepo kwake.

Kitabu hicho kina simulizi mbalimbali za matukio ya kiusalama ambazo hazikuwahi kuwekwa hadharani; ikiwamo kuhusu siku Bwimbo alipotaka kumpiga Nduli Iddi Amin katika mojawapo ya vikao vya wakuu wa Nchi za Afrika (OAU) kilichofanyika jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Baada ya Mwalimu kubaini nia ya Bwimbo kumchapa Iddi Amin, mwalimu alimwambia; “Mbe Petro, acha bwana”.

KUTOKA KWENYE KITABU CHA MLINZI

Kitabu hicho: “ Peter D.M Bwimbo: Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere” kimechapwa mwaka huu nchini na Kampuni ya Mkuki na Nyota na kina jumla ya kurasa 131 zinazoeleza mambo wana”.
 
SIRI YA UASI WA 1964

Na comred Mbwana Allyamtu

MLINZI mkuu zamani wa Baba wa Taifa, Julius Nyerere, Peter Bwimbo (87) ameandika kitabu kwa mara ya kwanza akiweka wazi jinsi Mwalimu alivyotoroshwa kutoka katika mikono ya wanajeshi walioasi katika Maasi ya Jeshi ya mwaka 1964.

Kitabu hicho: “ Peter D.M Bwimbo: Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere ” kimechapwa mwaka huu nchini na Kampuni ya Mkuki na Nyota na kina jumla ya kurasa 131 zinazoeleza mambo mbalimbali ambayo hayakuwahi kuelezwa waziwazi na yeyote.

Kwa mfano, kitabu hicho; zaidi ya kueleza namna Nyerere alivyotoroshwa –kimeeleza pia namna aliyekuwa Waziri Mkuu, Rashidi Kawawa, alivyonusurika kufa kwa kuvuta hewa chafu nchini Misri kwenye miaka ya 1960 na namna Mwalimu pia alivyoamua kutopanda ndege iliyokuwa imeandaliwa na mwenyeji wake, aliyekuwa Rais wa Zaire, Mobutu Seseseko, kutokana na hofu za kiserikali.

Ilivyokuwa wakati wa maasi

Januari 20, mwaka 1964, askari wa Kiafrika waliokuwa ndani ya Jeshi la KAR waliasi kwa madai kwamba ingawa Tanganyika ilikuwa imepata Uhuru, bado jeshi hilo lilikuwa chini ya Waingereza na wanajeshi wengine wenye asili ya Kiasia.

Katika kitabu hicho, Bwimbo ameandika kwamba maasi hayo yalitokea ghafla pasipo mipango hiyo kufahamika hata kwa Idara ya Kikachero ya wakati huo (Special Branch) na kwamba wahusika hawakufahamika mapema mpaka walichopanga kilipokamilika na hatimaye maasi kuanza.

Ni maasi hayo ndiyo yaliyosababisha KAR kuvunjwa na hatimaye kuundwa kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) pamoja na Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) kama inavyofahamika sasa.

Operesheni Magogoni

Bwimbo anasema katika kitabu hicho kwamba aliipachika kazi ya kumwokoa Mwalimu na Kawawa wasitekwe na waasi waliokuwa wamevamia Ikulu jina la Operesheni Magogoni, kwa vile kivuko kilichotumika kuwaondoa viongozi hao kutoka Ikulu na kuwapeleka Kigamboni kilikuwa kinafahamika kwa jina la Magogoni.

“ Nilipigiwa simu majira ya saa 8 usiku na ofisa wa kitengo chetu aliyekuwa mkuu wa zamu usiku huo hapo Ikulu, Leon Kazimili, kwamba kuna taarifa kuwa katika kambi ya Calito (Lugalo) palikuwa na dalili kuonyesha kuwa imevamiwa na majeshi ya kigeni usiku huo; Januari 20, 1964.

“ Niliamka haraka kuelekea Ikulu nikiwa na gari langu kwa sababu Ikulu ndiko mahali walipokuwa Rais pamoja na Waziri Mkuu ambaye nyumba yake ilipakana na Ikulu upande wa Kaskazini. Leon Kazimili sasa ni marehemu. Niliwasili Ikulu kutoka nyumbani kwangu Upanga majira ya saa 8:20 usiku. Wakati huo, tayari watu wa usalama walikuwa wamewaamsha Rais na Waziri Mkuu kuwaeleza kuhusu kilichotokea Calito.

“ Nilipanga haraka akilini mwangu hatua za kuchukua katika hali ya dharura kama hiyo kutokana na mafunzo niliyokuwa nimeyapata nchini Marekani mwaka 1963. Nilitoka nje ya viwanja vya Ikulu kwa nyuma upande wa baharini kwa miguu kama majira ya saa 8:45 usiku huo nikiwa na Nyerere na Kawawa, bila wasiohusika kufahamu.

“ Mkurugenzi wangu (Mkuu wa Special Branch) pamoja na Kamishina wa Polisi (sasa IGP) walibakia katika eneo la Ikulu. Ni muhimu kupotosha ukweli katika mazingira haya ya dharura ili maadui au wasiohusika wasifahamu kinachoendelea wakati huo.

“ Nilikuwa na askari polisi wawili wenye sare waliokuwa wanalinda uwanja wa Ikulu siku hiyo. Nilitumia usafiri nilioukuta kwenye kivuko cha serikali cha Magogoni baada ya kuwaeleza wafanyakazi waliokuwa wanaendesha pantone siku hiyo kuwa nilitaka kuwawahisha viongozi hao wawili kwenye kikao maalumu kilichopangwa kufanyika katika Chuo cha Kivukoni.

“ Wafanyakazi hao wawili penye kivuko ambao kutokana na mazingira ya usiku huo sikuweza hata kuchukua majina yao, walikubali kutuvusha baada ya kuona kwa macho yao sura za viongozi hao wawili (Nyerere na Kawawa). Tulipovuka, tuliwaambia wale wafanyakazi kuwa wasikirudishe kile kivuko Magogoni kwa sababu viongozi wangetaka kurejea Ikulu mara tu baada ya kumalizika kwa kikao chao. Lengo lilikuwa ni kuhakikisha kuwa hata kama maadui wangebaini kuwa Rais na Waziri Mkuu wameondoka, wasingeweza kuja Kigamboni kwa wakati huohuo,” ameandika.

Kwa sababu hakukuwa na maandalizi ya kumpokea Mwalimu na Kawawa, Bwimbo ameandika kwamba ilibidi watembee kwa mguu kutoka Kigamboni hadi katika kijiji cha Salanga katika usiku huo wa manane wa kihistoria na kwamba njiani walikuwa wakitishwa na mbwa kutoka katika nyumba walizokuwa wakizipita.

Bwimbo ambaye anasema alipata mafunzo mbalimbali ya masuala ya ukachero katika nchi za Uingereza na Marekani, alisema alikuwa na lengo la kuwapeleka viongozi hao katika nyumba ya kupumzikia viongozi iliyokuwepo eneo la Mji Mwema lakini sababu kulianza kukucha, waliamua kulala kwenye nyumba ya msamaria mwema, Sultan Kizwezwe, ambaye aliwapokea vema na wala hakuwasaliti kwa adui.

Kitabu hicho kinachopatikana katika duka la Tanzania Publishing House (TPH) lililopo mtaa wa Samora jijini Dar es Salaam, kimeeleza namna mlinzi huyo alivyokuwa akiwakatia mapapai viongozi hao na kula nao; katika wakati ambapo askari waasi walikuwa wakiwatafuta kwa lengo la kuwadhuru au kuwadhalilisha.

Mzee Kizwezwe sasa ni marehemu na Bwimbo alieleza kuwa ingawa Mwalimu Nyerere alitaka kumjengea nyumba kama shukrani zake kwake; msamaria huyo alikataa zawadi hiyo na badala yake alikubali zawadi ya baiskeli.

Katika wakati huo ambao Mwalimu alikuwa akiishi Salanga, ni kiongozi mmoja tu; aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, hayati Bhoke Munanka, ndiye pekee aliyepata fursa ya kupafahamu alikofichwa Mwalimu na kuzungumza naye.

Kwa mujibu wa mtunzi wa kitabu hicho, kilitakiwa kichapwe mapema kuliko mwaka huu lakini kwa sababu ya unyeti wa taarifa za mwandishi huyo, ilibidi kwanza kihakikiwe na vyombo vya ulinzi na usalama nchini.

Kitabu hiki cha Bwimbo ambaye ana asili ya Ukerewe, Mwanza, ni cha kwanza kuandikwa na mtumishi mstaafu wa TISS; mojawapo ya taasisi ambazo usiri ni mojawapo ya sababu za kuwepo kwake.

Kitabu hicho kina simulizi mbalimbali za matukio ya kiusalama ambazo hazikuwahi kuwekwa hadharani; ikiwamo kuhusu siku Bwimbo alipotaka kumpiga Nduli Iddi Amin katika mojawapo ya vikao vya wakuu wa Nchi za Afrika (OAU) kilichofanyika jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Baada ya Mwalimu kubaini nia ya Bwimbo kumchapa Iddi Amin, mwalimu alimwambia; “Mbe Petro, acha bwana”.

KUTOKA KWENYE KITABU CHA MLINZI

Kitabu hicho: “ Peter D.M Bwimbo: Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere” kimechapwa mwaka huu nchini na Kampuni ya Mkuki na Nyota na kina jumla ya kurasa 131 zinazoeleza mambo wana”.
tupe na bei mkuu..
 
Back
Top Bottom