Dodoma one
JF-Expert Member
- Apr 23, 2012
- 326
- 29
Nzuri sana hiyo
Tamimu si aliuwawa?Mimi ni kijana Wa 1990's lakini hii kesi ya uhaini nilikuwa naifuatilia nikiwa mdogo, ilikuwa very interesting na Komandoo Tamim alikuwa Noma sana.!
Hakuna cha upiganaji wala nini,alisaidiwa na ndugu zke walioko Canafa na Australia.walimpa malori ya mizigo ndo kilichomtoa.mdogo wake yeye walipoachiwa na Mwinyi 1995 aliondoka zake nchini.Huyu ni mpiganaji asilia
Hadithi za kutengenezwa huwa tamu sana!! Hivi waasi waliokuja kuachiwa na mzee Mwinyi ni kina nani?Japo historia haisemi wazi juu ya mambo mengi sana Tanganyika na Tanzania ya leo, lakini Mwalimu Nyerere tangu awe kiongozi wa nchi hii amenusurika mapinduzi MATATU,
Moja ni la mwaka 1964, lapili ni la mwaka 1970 na la mwisho ni la mwaka 1980 (Sina uhakika sawa na hiyo miaka)
Jaribio la kwanza ndilo lilipelekea kuundwa kwa JWTZ na lilizimwa kwamsaada wa Malkia wa Uingereza aliyetuma makomandoo maalumu na wakafanikiwa, Jaribio la pili ndilo lililopelekea kuundwa kwa Usalama wa Taifa na kikosi maalumu cha ulinzi wa Rais,
na jaribio la mwisho ndio lilipelekea kubadili sera ya usalama wa Taifa kwa kuwapandikiza kila kwenye sekta na kuwa kila mtu ni mlinzi wa nchi hii (usalama)
Sikumbuki vema lakwanza kama liliongozwa na nani lakini Kambona ndie alimficha Mwalimu, lapili sikumbuki vema, lakini la mwisho liliongozwa na baadhi ya wanajeshi wa kikosi cha Anga cha Ukonga Banana,
Na mipango yao iliharibikia palepale Banana baa baada ya mmoja wao kulewa na kuanza kuongea hovyo hasa akisema yeye anataka cheo cha uwaziri mkuu!
Enzi hizo 1980+ mmoja wa makamanda wa usalama wa taifa aliyeongoza kuwadhibiti waasi hao ni Mabere Marandu,
Na alifanikiwa kuongoza oparesheni za kumsaka na kumuua mmoja wa makomandoo ambae alikuwa ameandaliwa rasmi kumuua Nyerere,
Mapambano yalikuwa ni makubwa kutoka airport hadi kinondoni ulipo ubalozi wa Marekani sasa ndipo walipofanikiwa kumuua!
Jambo la kuwashangaza waasi wale (wanajeshi) wote Mwalimu aliwaita ikulu,
akamwambia kiongozi wa mapinduzi yale (simkumbuki) kuwa
"Shika bunduki uniue wewe mwenyewe kwamkono wako ili uwe rais wa nchi hii"
jamaa aliomba radhi huku akitambaa kisha mwalimu akasema
"nimewasamehe wote"
na aliwapa vyeo na kazi, wengi walikwenda kuwa mabalozi wa Tz nchi za nje!
Sisi hapa tunasema kama porojo tu, lakini yapo mengi sana nyuma ya pazia!
Watawala wanahisi kuyataja ni kama kuharibu sifa ya Tanzania na wengine wanaona kama itaharibu sifa ya Mwalimu.
Mimi binafsi nafikiri kama yatasemwa hadharani yataongeza sifa ya Mwalimu Nyerere na utawala wa ccm ya kale!
Atakuwa ni kiongozi pekee barani afrika na duniani aliyenusurika majaribio matatu ya uasi,
Atakuwa ni kiongozi wa kwanza duniani kuwasamehe waasi kwa mda huohuo wa uasi (baada ya kuwakamata) na kuwapa kazi nyingine za kitaifa
Atakuwa ni kiongozi pekee duniani aliye ng'atuka kwa amani na kwenda kuishi kijiji tena bila hata ulinzi, akitembelea land rover ya shamba miaka mitano tu baada ya jaribio kali la mapinduzi ya Banana Ukonga!
Hizo zote zilikuwa ni sifa zake ambazo watawala wa leo kwa makusudi ama kwakujua au kutojua wamefifisha nyota ya mwana wa Afrika mbele ya uso wa mataifa!
Na kwakuwafahamisha tu ni kuwa mmoja ya wanajeshi hao walioasi ni Meja Gen Hans Popi yule mwenye Sams Super Store pale Mbezi Makonde!
Kwakifupi hayo ndiyo ninayafahamu,
Bongoyo island na mbudya island.Ndio ni Mabere Marandu huyu wa Chadema,
Nigeria walisaidia sana kuja kuleta amani, tulitawaliwa karibu mwaka mmoja!
Wengi wa waasi walisamehewa, lakini makomando na baadhi waliuawa na wengine kupelekwa Gwantanamo ya Afrika, hicho ni kisiwa kidogo kinachomilikiwa na Tanzania kipo kata ya Zanzibar na Tanganyika,
Sina uhakika kama badoo kinatumika ama kinatumika kwa siri zaidi!
Najiuliza sana kwa nini hili swala hawafundishwi watoto mashuleni? Nani wakumfunga paka kengele? Nani wakusimama juu ya zile winchi pale bandari na kupenyeza target pale magogoni?Nashukuru sana mkuu