January Makamba: CCM imeshashinda majimbo 176 mpaka sasa

January Makamba: CCM imeshashinda majimbo 176 mpaka sasa

sasa NEC wanahangaika nini kutoa nusunusu?si waende kwa "genius" January Makamba awape matokeo?
 
Huu mchezo wa saikolojia ambao makamba hawezi. Majimbo gani hayo??? Tume ina kigugumizi cha kutangaza matokeo hata ya hapo dar??? Isitoshe tume na jeshi la polisi wanatoa kauli gani kwa kura zinazokamatwa kwenye magari ya serikali??? Kura feki zimezagaa mpaka bar, zimetoak wapi???

Kwa hali hii ya kujitangazia matokeo natoa wito kwa viongozi Wa ukawa nao kutujia na matokeo waliyoyajumlisha maana uvumilivu umefika kikomo
 
Hamna namna nyingine bali ni jukumu la UKAWA nao kututangazia matokeo maana wenzetu uvumilivu umeshawashinda, ya nini kujifanya busara wakati unafanyiwa dhihaka ya kiwango hiki
 
Tume haitangazi matokeo ya Ubunge! Matokeo ya Ubunge yanatangazwa na Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya, miji, manispaa na Majiji. Kila mtu mwaka huu anajifanya kushabikia siasa ila wengine weledi nil. Kwa kuwa Chadema ndo mlijifanya mna kura nyingi mkatoa wazo la kubandikwa matokeo vituoni ili mjumlishe, uwezekano ni mkubwa kwa anayosema January Makamba. Kwani CCM haina watu wanaojua hesabu za kujumlisha na huku walikuwa na mawakala kila kituo Nchini? Tumesikia Reporters wa Radio 1 huko Mikoani , majimbo mengine kati ya Kata 28, CCM imeshinda udiwani Kata zote! Hapo unategemea nani Kashinda Ubunge na kuongoza Urais?. TAFAKARI!!

You are right, wengi humu ni wageni wa siasa. Siyo kazi ya tume kutangaza matokeo ya ubunge
Pia kuna mmoja kasema CCM imepoteza majority wakati 166 ni sawa na 66.2% of 266 (More than two third). Na hii itapanda watakapo ingia viti maalum na walw 10 wa Rais
 
Hakuna kitu kama hicho cha kushughulikiwa. Sisi ni taifa moja na tofauti za miezi miwili ya kampeni haiwezi kutufarakanisha. Vijana tuungane tujenge nchi yetu, sasa NI SAA YA MABADILIKO YA KAZI. KWA MAGUFULI NI KAZI TUU!

Wewe na nani? Kamwe siwezi kuchangamana na yeyote aliye shabiki wa ccm, wewe kwangu daima ni adui, hivi ndivyo nitakavyowakuza na watoto wangu. Bora shetani kuliko ccm
 
CCM ilishashinda huu uchaguzi kabla ya hata uchaguzi wenyewe.

CCM wanaumbuka mwaka huu kwasabbau Ukawa wana uthibitisho toka kwenye vituo.

Sasa huo ushindi wameutoa wapi?

Hiyo ni 'mind game' wanachezewa watu.

Mkikubali wanatangaza, mkikomaa January anaumbuka.
 
Tundu Lissu, Mbowe, Prof Safari, Gwajima, Prof Baregu, utafiti wenu umeifikisha hapo Chadema mlipewa onyo lakini tamaa ya pesa imewazika.

kila kitu ni tamaa ya pesa? hao wanaogombea hawataki pesa? watatumikia bure taifa
 
Ajabu watu hawaoni tofauti ya Makamba na Maalim Hamad. Makamba anaongelea matokeo ya majimbo ambayo tayari NEC kupitia kwa Wakurugenzi waliokasimiwa madaraka, wametangaza matokeo.

Maalim Sharif Hamad anazungumzia matokeao ya urais ambayo kwa mujibu wa sheria lazima yatangazwe na NEC au ZEC. Hiyo ndiyo tofauti. Kama sheria si nzuri, hilo suala lingine. Njoo Katiba ya Warioba!!!
 
Ukawa mkajaribu tena 2020 na msisahau kuendelea kumuhudumia Lowassa ili Mungu amjalie aje tena kugombea 2020
 
Akiongea na waandishi wa habari muda huu January Makamba amesema kwa mujibu wa taarifa rasmi za mabandiko ya Tume ya uchaguzi katika vituo vya matokeo, ni kuwa CCM mpaka sasa imeshinda majimbo 176 kati ya majimbo 264 na imekomboa majimbo 12 kutoka upinzani.

Aidha amesema Maalim seif Hamad kutangaza matokeo ya ushindi wa ZNZ ni mzaha

=============================


Ina maana mpaka dakika hii hamna uhakika wa matokeo ya Urais? Kama mmepata kujua kuwa mmeshinda kwa majimbo nayo it means mnajua matokeo ya urais kwa uhakika.......nadhani matokeo yenu yanawaambia mmepigwa chini, mnasubiri huruma ya tume!
 
Ajabu watu hawaoni tofauti ya Makamba na Maalim Hamad. Makamba anaongelea matokeo ya majimbo ambayo tayari NEC kupitia kwa Wakurugenzi waliokasimiwa madaraka, wametangaza matokeo.

Maalim Sharif Hamad anazungumzia matokeao ya urais ambayo kwa mujibu wa sheria lazima yatangazwe na NEC au ZEC. Hiyo ndiyo tofauti. Kama sheria si nzuri, hilo suala lingine. Njoo Katiba ya Warioba!!!
Emu tupe chanZo cha NEC ikithibitishaa kutangaza walau jumla ya majimbo 150 ukiachana na 176 ya makamba
 
NEW UPDATES OF THE CONSTITUENCIES RESULTS:
CCM has succeeded to win the following constituencies;
1. Chalinze- Ridhiwani J. Kikwete
2. Kibaha Mjini- Sylvester Francis Koka
3. Gairo-Ahmed Shabiby
4. Mvomero-Suleiman Ahmed Saddiq
5. Chemba- Juma Selemani Nkamia
6. Bahi-Omar Ahmed Badwel
7. Kibakwe-George Boniface Simbachawene
8. Mpwapwa-George Malima Lubeleje
9. Mtera- Livingstone Joseph Lusinde
10. Dodoma Mjini-Antony Peter Mavunde
11. Geita Mjini-Costantine John Kanyansu
12. Geita Vijijini- Joseph Lwinza Kasheku
13. Nzega Mjini- Husein Bashe
14. Nzega Vijijini- Dk Hamis Kigwangala
15. Iramba Mashari- Mwigulu Mchemba
16. Singida Kaskazini- Lazaro Nyalandu
17. Musoma Vijijini- Prof. Sospeter Muhongo
18. Musoma Mjini- Vedastus Mathayo
19. Kisarawe- Suleiman Jafo
20. Ilemela- Angelina Mabula
21. Kahama- Jumanne Kishimba
22. Nanyamba- Abdalah Chikota
23. Morogoro Mjini- Mohamed Abod
24. Tunduru Kusini- Eng. Ramo Makani
25. Bumbuli- January Makamba
26. Ilala- Musa Hasan Zungu
27. Nachingwea- Hasan Elias Masara
28. Nkasi Kaskazini- Ally Mohamed Kessy
29. Muleba Kaskazini-Charles John Mwijage
30. Mpanda Mjini-Sebastian Simon Kapufi
31. Mpanda Vijijini -Moshi Selemani Kakoso
32. Katavi -Issack Aloyce Kamwele
33. Nsimbo -Richard Philip Mbogo
34. Kavuu-Dkt. Pudenciana Wilfred Kikwembe
35. Songea Mjini-Leonidas Tutubert Gama
36. Nyasa-Eng. Stella Martin Manyanya
37. Tunduru Kaskazini-Ramo Matala Makani
38. Tunduru Kusini-Daimu Iddi Mpakate
39. Peramiho-Jenister Joakim Mhagama
40. Madaba- Joseph Kisito Mhagama
41. Mbinga Mjini- Sixtus Raphael Mapunda
42. Nkenge -Diodorus Buberwa Kamala
43. Kongwa - Job Y. Ndugai
44. Kondoa -Sanda Edwin
45. Kondoa Vijijini-Dkt. Ashatu Kijaji
46. Mlalo-Rashid Abdakkag Shangazi
47. Pangani -Jumaa Hamidu Aweso
48. Kilindi-Omari Mohamed Kigua
49. Mkinga-Danstan Luka Kitandula
50. Handeni Vijijini-Mboni Mohamed Mhita
51. Muheza-Adadi Mohamed Rajabu
52. Korogwe Mjini-Mary Pius Chatanda
53. Korogwe Vijijini - Stephen Hillary Ngonyani (Maji Marefu)
 
kweli nyani haoni kundule,
yani Sief kutangaza matokeo ni mzaha ila Makamba kutangaza matokeo ni ushujaa??

Sasa kujitangaza kua ameshinda urais we unaona yupo sawa?kuna tume toka makao makuu ndo watatangaza na kama ameshinda hakuna wasi wasi
 
Emu tupe chanZo cha NEC ikithibitishaa kutangaza walau jumla ya majimbo 150 ukiachana na 176 ya makamba

Chanzo cha NEC? Mkurugenzi wa Halmashauri aliyemtangaza Nassari kwa mfano amefanya hivyo kwa niaba ya NEC. Hayo tayari ni matokeo rasmi ya NEC kisheria.

Kwenye urais ni habari nyingine.
 
Makamba mwongo, sana sana anajaribu kupima upepo je goli la mkono liyapokelewaje?
Amepiga hesabu ya theluthi mbili exactly ya wabunge wa ccm! Hilo goli la mkono liko wazi mno, Malaika watashughulika na makamba wananchi tulieni!
 
Back
Top Bottom