Januari Makamba: Wanaozuia bomba la mafuta lisijengwe ni wanafiki. EWURA yatoa kibali cha kuanza Ujenzi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987


Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetoa kibali cha Ujenzi wa Bomba la Mafuta kutoka Mtukula hadi Tanga lenye urefu wa km 1147.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), James A. Mwainyekule amesema EWURA imetoa kibali cha Ujenzi wa Bomba la mafuta ghafi kwa EACOP.

Kibali hicho ni cha kujenga Bomba la mafuta ghafi kuanzia Mtukula Mkoni Kagera hadi Chongoleani Mkaoni Tanga.

James A. Mwainyekule, amesema Bomba hilo litapita katika Mikoa nane ambayo ni Kagera, Tanga, Manyara, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga na Geita.

Naye Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Waziri wa Nishati, Januari Makamba amesema Wanaozuia bomba la mafuta gafi lisijengwe ni Wanafiki. Kayasema hayo wakati Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (#EWURA) ikitoa kibali cha ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) kutoka Mtukula Mkoani Kagera hadi Chongoleani, Tanga lenye urefu wa KM 1147.

amesema “Kuna maneno mengi kuhusu bomba, wenzetu Ulaya wakidai halistahili kujengwa, hata Bunge la Ulaya limetoa Azimio ambalo ni maneno tu, wenzetu Nchi za Afrika na zinazoendelea kuna unafiki tena mkubwa sana, msingi wa maendeleo yao ilikuwa ni uvunaji wa rasilimali kama hizi mfano makaa ya mawe na gesi.”

Makamba amesema tahadhali zote za kimazingira zimechukuliwa kwani baada ya bomba kujengwa, juu yake tutapanda miti kiasi kwamba hutajua kama bomba limepita.

Bomba hilo litapita Mikoa 8 ambayo ni Kagera, Tanga, Manyara, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga na Geita.

Naye Omary Mgumba, Mkuu wa Mkoa wa Tanga akiongea kwa niaba ya Wakuu wa Mikoa nane ambayo bomba limepita amesema hali ya Usalama ni nzuri. Wanaendela kufundisha wanavijiji ambapo bomba linapita ili walinde miundombinu kabla, wakati na baada ya mradi kumalizika.

Pia ameomba Serikali kuongeza Vituo vya Polisi kwenye Vituo sehemu bomba linapita.

Makamba: Juu ya bomba la mafuta kutapandwa miti

Kuna maneno kuwa linapita kwenye mbuga za Wanyama, vyanzo vya maji, watu wataathirika, hizo ni propaganda.

Kuna kazi kubwa imefanyika kulinda mazingira, bomba litakapopita patapandwa miti juu yake kiasi kwamba itakuwa ngumu kujua kama kuna bomba limepita.

Watu 9,898 wataguswa na mradi na kati yao watu 390 tu ndio ambao ardhi yao itachukuliwa na wamepewa fursa kama wanataka kujengewa nyumba nyingine au kulipwa, hakuna vurugu wala nguvu iliyotumika.

85 wameamua kujengewa nyumba, tumelipa fidia Tsh. Bilioni 29 kwa wale ambao bomba litapita katika maeneo yao, kazi ya kulipa inaendelea.

Kuhusu haki za binadamu zimezingatiwa, NEMC walitoa maelekezo ya nini cha kufanya, mradi pia utatoa ajira na manufaa ya kiuchumi.

Makamba: Kazi kubwa imefanyika kulinda mazingira na Haki za Bnadamu

Akizungumzia ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Kagera hadi Tanga amesema kuna kazi kubwa imefanyika kulinda mazingira sehemu ambapo litapita.

Amesema “Watu 9,898 wataguswa na mradi, kati yao Watu 390 ndio ambao ardhi yao itachukuliwa na wakapewa fursa kuchagua kujengewa nyumba nyingine au kulipwa, 85% wameamua kujengewa, pia tumelipa fidia Tsh. Bilioni 29 kwa ambao bomba litapita katika maeneo yao na zoezi la kulipa linaendelea.”

Aidha, amesema Haki za Binadamu zimezingatiwa kwa kuzingatia muongozo wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).
 


Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetoa kibali cha Ujenzi wa Bomba la Mafuta kutoka Mtukula hadi Tanga lenye urefu wa km 1147.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), James A. Mwainyekule amesema EWURA imetoa kibali cha Ujenzi wa Bomba la mafuta ghafi kwa EACOP.

Kibali hicho ni cha kujenga Bomba la mafuta kuanzia Mtukula Mkoni Kagera hadi Chongoleani Mkaoni Tanga.

James A. Mwainyekule, amesema Bomba hilo litapita katika Mikoa nane ambayo ni Kagera, Tanga, Manyara, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga na Geita.

-------------------


Waziri wa Nishati, Januari Makamba amesema hayo wakati Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (#EWURA) ikitoa kibali cha ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) kutoka Mtukula Mkoani Kagera hadi Chongoleani, Tanga lenye urefu wa KM 1147.

amesema “Kuna maneno mengi kuhusu bomba, wenzetu Ulaya wakidai halistahili kujengwa, hata Bunge la Ulaya limetoa Azimio ambalo ni maneno tu, wenzetu Nchi za Afrika na zinazoendelea kuna unafiki tena mkubwa sana, msingi wa maendeleo yao ilikuwa ni uvunaji wa rasilimali kama hizi mfano makaa ya mawe na gesi.”

Bomba hilo litapita Mikoa 8 ambayo ni Kagera, Tanga, Manyara, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga na Geita.
Wanatoa vibali Mara ngapi Mbna Dr John pombe Joseph magufuli ameshatoa kibali enzi za utawal wake leo huyu wa ewura nae anatoa kibali mkataba ulishasainiwa kwa pande zote na kukubalika na mashart yote ila SAS bado Kuna ucheleweshaji mkubwa wa kuanza kwa mradi huu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 


Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetoa kibali cha Ujenzi wa Bomba la Mafuta kutoka Mtukula hadi Tanga lenye urefu wa km 1147.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), James A. Mwainyekule amesema EWURA imetoa kibali cha Ujenzi wa Bomba la mafuta ghafi kwa EACOP.

Kibali hicho ni cha kujenga Bomba la mafuta kuanzia Mtukula Mkoni Kagera hadi Chongoleani Mkaoni Tanga.

James A. Mwainyekule, amesema Bomba hilo litapita katika Mikoa nane ambayo ni Kagera, Tanga, Manyara, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga na Geita.

-------------------


Waziri wa Nishati, Januari Makamba amesema hayo wakati Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (#EWURA) ikitoa kibali cha ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) kutoka Mtukula Mkoani Kagera hadi Chongoleani, Tanga lenye urefu wa KM 1147.

amesema “Kuna maneno mengi kuhusu bomba, wenzetu Ulaya wakidai halistahili kujengwa, hata Bunge la Ulaya limetoa Azimio ambalo ni maneno tu, wenzetu Nchi za Afrika na zinazoendelea kuna unafiki tena mkubwa sana, msingi wa maendeleo yao ilikuwa ni uvunaji wa rasilimali kama hizi mfano makaa ya mawe na gesi.”

Bomba hilo litapita Mikoa 8 ambayo ni Kagera, Tanga, Manyara, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga na Geita.

Waliosema kujenga bwawa la NYERERE kuwa littaharibu mazingira miti ikikatwa hawakuwa WANAFIKI?

Anyway wanaopinga Kutoka nje ya nchi Si WANAFIKI, ni VITA ya UCHUMI kutafuta maslah kama uncle alivyosema.
 
Wanatoa vibali Mara ngapi Mbna Dr John pombe Joseph magufuli ameshatoa kibali enzi za utawal wake leo huyu wa ewura nae anatoa kibali mkataba ulishasainiwa kwa pande zote na kukubalika na mashart yote ila SAS bado Kuna ucheleweshaji mkubwa wa kuanza kwa mradi huu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Kivipi? Mambo ya kitaalam ni tofauti na mambo ya kisiasa. Kujenga bomba la mafuta au la maji, lazima upate kibali(license or permit) kutoka kwa mdhibiti(regulator).
 
Kigingi ni

Good Governance
Environmental conservation
Transparency

Both two sides Uganda and Tanzania

Hutoboi bila kutii vigezo hapo juu...especially no 3
 
Wanatoa vibali Mara ngapi Mbna Dr John pombe Joseph magufuli ameshatoa kibali enzi za utawal wake leo huyu wa ewura nae anatoa kibali mkataba ulishasainiwa kwa pande zote na kukubalika na mashart yote ila SAS bado Kuna ucheleweshaji mkubwa wa kuanza kwa mradi huu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Mkuu kuna Mbuyu wanauzunguka....
 
Kwamba wengine wana bomba la tangu miaka ileeee, haimaanishi kuwa bomba hilo linalotaka kujengwa siyo environmentally friendly. Tuna upepo wa kutosha - windmill; tuna jua la kutosha - solar; na maji kiasi - hydro; tungekazania hivyo kuliko kugang'ana na mifuta ambayo wenzetu wenye mambo ya miaka ile wanaangalia jinsi ya kujinasua tukielekea net zero!
 
Salaleh yaani ata hao waganda wenye mafuta yao na wabia kwenye main contract sidhani kama wamefanya shughuli za hadhara kwenye huu mradi kama watanzania walioingia kwa njia ya ‘deal kuona’.

Mkutano wa fursa
Sijui local context
Mara mkutano wa oil and gas kwa wanasheria
Mara hadhara ya ku sign sijui nini

Yaani kila siku EACOP utadhani ni mafuta yetu na ndio wenye mkataba badala ya TOTAL/CNOOC/Uganda.

Tuna viherehere kushinda waganda wenyewe ambao mambo mengine wanafanya private tu maofisini sisi kutwa kujitapa kwenye majukwaa.

Alitambua juhudi za hayati kupigania hilo bomba lipite Tanzania au hizi ni jitiahada za Samia pia.

Ni aina ya watu ambao awaoni aibu kuchukua credit za watu wengine na kujifanya zao hadharani.
 
Aitambua juhudi za hayati kupigania hilo bomba lipite Tanzania au hizi ni jitiahada za Samia pia.

Ni aina ya watu ambao awaoni aibu kuchukua credit za watu wengine na kujifanya zao.
I knew where you were heading to!! Ulitaka tu JPM atajwe uridhike no wonder umeonyesha chuki zako wazi kisa ni January ndio anapata credit sio JPM!!

You can do better than this
 
Wanatoa vibali Mara ngapi Mbna Dr John pombe Joseph magufuli ameshatoa kibali enzi za utawal wake leo huyu wa ewura nae anatoa kibali mkataba ulishasainiwa kwa pande zote na kukubalika na mashart yote ila SAS bado Kuna ucheleweshaji mkubwa wa kuanza kwa mradi huu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Hiyo ndio Tanzania ya ulambaji asali bwana. Ni vichekesho haya yalishafanywa kipindi hivyo haya ya Leo ni yapi Tena??!
 
I knew where you were heading to!! Ulitaka tu JPM atajwe uridhike no wonder umeonyesha chuki zako wazi kisa ni January ndio anapata credit sio JPM!!

You can do better than this
Kwani kuna ubaya gani si miaka michache tu Uganda walikuwa back and forth wakijiuma uma ilo bomba lipite Tanzania au Kenya; na nchi zote mbili zikipeleka arguments kwanini lipite kwao.

Ata Museveni mwenyewe alipokuwa Chato aliweka wazi, Magufuli ndio aliemshawishi zaidi kuamua lipitie Tanzania. Sasa kuna shida gani akisema mtu alietumia nguvu hilo bomba kupitishwa Tanzania.

Yaani ata kwenye mradi wa bwawa la Nyerere bila ya soni uso mkavu anataka kuondoa credit za mtu alieasisi mradi.
 
I knew where you were heading to!! Ulitaka tu JPM atajwe uridhike no wonder umeonyesha chuki zako wazi kisa ni January ndio anapata credit sio JPM!!

You can do better than this
Mbona kama nawe huna tofauti kubwa nae, ulitaka Magufuli asitajwe? why asitajwe kama yeye alikuwa mwanzilishi wa huu mradi?

Kwanini unaingiza habari za chuki kwa Makamba kwa jambo lililo wazi kama hilo? huyo Makamba mwenyewe unayemtetea ameshaonesha chuki kwa Magufuli mara nyingi tu, tena mpaka baba yake...

Haya mambo kuweni makini nayo, huu ulimbukeni wa kutengeneza timu sioni kama una maana yoyote.
 
Back
Top Bottom