Kumpenda mtu haimaanishi yeye ndio awe sehemu ya kila kitu cha maisha yako
Kama kuna watu ambao wanaumia zaidi baada ya mapenzi kuisha au baada ya kuachwa ni wale watu ambao mapenzi yao kwa wenza huwa ndio kila kitu kwao
Watu hawa huwa hawana kipaumbele kingine chochote zaidi ya mpenzi wake tu,wakishaanza kupenda basi wanaweka kila kitu nyuma yao kana kwamba wameacha kuishi kabisa
Hapa marafiki watakuwa hawana dili tena,hana tena muda wa kuwa na rafiki zake kama hapo awali,kuna mambo alikuwa anafanya na rafiki Zale now hafanyi tena
Alikuwa mtu wa mazoezi au akishiriki kwenye michezo fulani lakini baada ya kuwa in love basi tena kila kitu kinasimama
Alikuwa anajipa muda wa peke yake sometime na kureflect maisha kwa ujumla wake lakini now inaonekana kana kwamba hana cha kufikiria zaidi ya mpenzi wale tu
Guys you have maisha mengine baada ya mapenzi, usiache kufanya mambo ambayo ulikuwa unayafanya hapo awali kwasababu tu now uko in love
You deserve to have a time for your own, kutana na marafiki zako kama mna ratiba za kufanya hivyo,engage kwenye mambo ya kijamii na watu wako wa karibu
Furahia mambo mengine ambayo ulikuwa unadili nayo hapo kabla maadamu tu hayaleti athari kwenye mahusiano yenu
Point hapa ni kwamba mapenzi sio kifungo au gereza la kukufanya usiishi tena, una maisha ya kuishi na unastahili hilo
Kuna wengine hapa huwa mpaka mnapigana mikwala kwamba hakuna tena kushiriki kwenye mitindao ya kijamii
Nakumbuka kuna mtu huko nyuma aliwahi kusema baada ya kumpata mrembo hapa jf sasa akataka kumpiga stop asishiriki tena hapa mtandaoni,sasa haya unaweza kuita ni mapenzi au adhabu za mapenzi hahaha!
Wengine hupiga mikwala wenza wao wasitumie tena pm,anahofu kwamba kwakuwa yeye alimpata baby kupitia pm so anahofia huenda kuna wengine watapitia huko huko
Sasa haya nayo ni mapenzi au adhabu za kupendana?
Mapenzi mazuri huwa hutufanya tuwe bora zaidi,hutufanya tupate thamani zaidi na nguvu ya kusonga mbele,sasa ukiona mapenzi kwako yanakuwa sehemu ya kukufanya usiwe bora na uwe mtu wa majuto kila kikicha basi hapo unakuwa sio sehemu ya mapenzi bali unakuwa sehemu ya adhabu ya mapenzi
Mtu ambaye pamoja na kuwa In love lakini bado akaendelea kuishi maisha yake,kufanya au kufuata ratiba zake kama hapo awali,huyu hata ikitokea bahati mbaya mapenzi yamefikia mwisho bado atakuwa anazungukwa na marafiki ambao watakuwa faraja kwake,atashiriki michezo na mambo mengine kama kawaida na kumsaidia kupunguza upweke wa kuachwa
Ila tofauti na yule mtu ambaye yeye baada ya kuwa in love,kila kitu katika dunia yake kilisimama na fokasi yake ikawa kwa mpenzi wake tu,huyu akiachwa au mapenzi yakiisha,ndio huona dunia yote imemuangukia,hana pa kushika,anapata upweke wa kufa mtu,mwisho wa siku wanakuwa na option moja tu ya kupoteza uhai,kwao wao wanaona hawana mtu tena wa kuwapa bega waegemee na leso ya kufutia machozi
Kuwa in love yes lakini usijtenge kabisa na maisha yako uliyoyazoe maadamu hayaleti sintofahamu kwenye mahusiano yenu
Alamsiki!