Nyumba ni ya mwanamke,mume aleta Manzi wake nyumbani in the name of dada wa kambo,kumbe ni mtu wake na tayar wana mtoto
Nianze na swali hili, mwanamke unajua ndugu wote wa karibu wa mume wako? Je,na wewe mwanaume unajua ndugu wa karibu wa mke wako?
Majibu baki nayo mwenyewe msomaji wangu
Ni Nyeri town,kwa road mwanaume na wadada wawili wako road wanatembea,mara paap host huyu hapa kawatokea kwa mbele,story mbili tatu wakafahamiana kidogo
Mume akajitambulisha na kisha akamtambulisha mkewe,halafu akamtambulisha yule mwanamke kuwa ni step sister wake.
Yakapigwa mastory ya maisha pale na ndoa kwa ufupi
Hawa mume na mke ndoa yako ina miaka 7 na wamejaliwa watoto wawili
Kama kawaida ikaja segment ya fichua maovu kupitia simu zao,hii ni test ya kujua uaminifu miongoni mwa wenza,maana kama kuna adui mkubwa wa mahusiano basi ni hiyo simu yako,yes simu yako.
Mke akatoa simu yake ikapitiwa pale,na gud nyuzi ni kwamba wife yupo clean,ikaja zamu ya mume,kwanza mume akajifanya kama alidhani ni simu ya mke tu ndio inapitiwa,anaonekana anakuwa mzito kuitoa simu mfukoni,hata mimi nikajua ehee hapa mikeka imeloa mashekhe wanakula wima leo hahaha!
Host wa kipindi hana baya wala upendeleo akaipitia pale mwisho wa siku yaliyomo yamo,mbaba hayupo clean
Akamwita wife pembeni na yule mdada kama shahidi ambaye kwa sasa anajulikana kama wifi wa mke
Host akafungua mkeka wa meseji,meseji zilionyesha kwamba,mwanaume akiwasiliana na mwanamke ambaye anaitwa Jeny
Na kumfahamisha kwamba ameshaongea na wife,kwahiyo anaweza kuja muda wowote pale nyumbani,Walee mtoto wao na kuendeleza mapenzi yao
Inavyoonyesha huyu mwanamke alikuwa na bwana wake,lakini sijui ilikuwaje wakaachana,ila kutokana na ushahidi wa mazingira inaonyesha chanzo kilikuwa cha huyu mume na mahusiano yake na huyu ambaye alijulikana kwa wife kama wifi yake,huenda mpaka mume au bwana wa huyo wifi wa mchongo akabwaga manyanga
Meseji moja inasomeka kutoka kwa dada wa kambo wa mchongo au wifi wa mchongo ikimwambia mume aje na pedi
Hapo ndio mke akili ikamkaa sawa,akauliza kwani kuna mama Jeny wangapi? Wifi wa mchongo ambaye ndio mama Jeny akasema siyo yeye,hapo wife akasema "hii ni namba yako" je utasemaje hapo
Mume kuona Mv bukoba inazama akajaribu kufanya jambo meli isizame akasema "huyo ni rafiki yangu Peter aliazima simu yangu akawa anachati na mama Jeny
Wife sio boya,akasema " hizo meseji ulichati na huyu mama Jeny kabla hajaja hapa kwetu,kwahiyo Peter hakuwepo huko" mume kimyaa akawa hana ujanja isipokuwa kuiona Mv Bukoba ikizama mbele ya upeo wa macho yake.
Hapo ndio mke akafunguo mafaili ya Dpp (mwendesha mashtaka wa serikali) kwamba "huyu mama Jeny nimemchukulia kama sister wangu,hakuna ninachokula ili yeye hali,hakuna ninachonunua ila yeye simnunulii,hata hapa tumetoka shopping pamoja"
Mke akaendelea kufungua files "hawa wote wanakaa kwenye nyumba yangu niliyoachiwa na baba,halafu kumbe mnakulana humo humo"
Mwanaume huyu ambaye sasa tumuite mbwa baada ya kuona siri zinazidi kuvuja akasema "baby si tutaongee kwa nyumba hapa tupo public kwa tv:
Mke akasema niende wapi wakati mie nipo hapa?
Mke akaendelea kutema nyongo kwamba,asiowaone kwa nyumba ndani ya 2hrs,wawe wamechukua vitu vyao na kusepa
Halafu kibaya zaidi kwenye meseji hizo ilionekana huyu wifi / step sister wa mchongo akimkandia wife wa jamaa kwamba hajui kupika
Maskini wife wa jamaa alikuwa kumbe anapambana kumtafutia kazi wifi wa mchongo ili asikae idle tu nyumbani, what a big love from this cute wife,lakini kumbe huyo anaye mkirimu nyumbani kwake ni nyoka tena black mamba,yani sumu yake nusu saa tu unabadilika jina na kuwa marehemu.
Huyu mbwa wa kiume,akawa anamlaumu host wa show "angalia sasa mambo gani umefanya,huyu.mwanamke ni submissive sana,je nitapata wapi mke kama huyu tena?"
Na huyu mbwa wa kiume akazidi kusema "huyu mwanamke namjua ana msimamo sana akisema amesema" huyu wife atakuwa ndugu yake na mwenye kigoda wa Madecha nini hahaha!
View: https://youtu.be/dhRYKIScJ1Q?si=_HpisC-35TUqVbfk
Somo kubwa hapa,wakati mwingine wabaya wetu hawako mbali sana,kama huyu wifi wa mchongo/step sister wa mchongo,yupo pale ndani na wanashea dudu kama kawa bila wife kujua
Ishi kitaalamu
Siku njema.