JamiiForums Issues an Official Responce to CCM allegations: (Press Release)

JamiiForums Issues an Official Responce to CCM allegations: (Press Release)

Status
Not open for further replies.
Sawa nisiwakatishe tamaa mawakili wenyewe wa JF ni akina nani Pasco, MsandoAlberto na Gurudumu au nimekosea, angalizo tu adui mnayemwendea msim underestimate ana uwezo hata wa kuwaazima silaha bila nyie kutambua siku mkitaka kufyatua zikawa hazina risasi nafikiri umenielewa.
Quinine, naomba niweke record clear, japo nimesoma sheria UD, naomba kukiri wazi, mimi sio wakili na wala sifanyi shughuli yoyote inayohusiana na sheria. Professional yangu ni nyingine, nimesoma law just for the love of it, sijawahi kuitumia popote, na more surprising, huwezi amini, (baada ya kumaliza, nilijitimkia zangu mitaani,) mpaka leo, hata hiyo transcript wala degree yenyewe, sijaichukua toka UD, japo niiweke tuu kabatini kwangu.
Pasco
 
Kama na Pasco nae ni miongoni mwa mawakili basi hii kesi tumeshashindwa kabla haijaanza.
Matola, hoja yako hii ni kweli kwa asilimia 100% kwa sababu Pasco sio wakili, na uthibitisho ni huu!.

Naomba niweke record clear, japo nimesoma sheria UD, naomba kukiri wazi, mimi sio wakili na wala sifanyi shughuli yoyote inayohusiana na sheria. Professional yangu ni nyingine, nimesoma law just for the love of it, sijawahi kuitumia popote, na more surprising, huwezi amini, (baada ya kumaliza, nilijitimkia zangu mitaani,) mpaka leo, hata hiyo transcript wala degree yenyewe, sijaichukua toka UD, japo niiweke tuu kabatini kwangu.
Pasco
 
Mzee Mwanakijiji, hili lina ukweli ndio maana ile miswada miwili ya huduma za habari (Media Services bill 2007 ) na haki ya kupata habari, (The Right to Information Bill, 2007)kwanza ilikuwa miwili, sasa itaunganishwa na kuwa mswada mmoja tuu Media Bill, ulishapita hatua zote mpaka baraza la mawaziri, lakini mpaka sasa hakuna kinachoendelea.

Mkuu Pasco;

This is very useful . . . .

Je unafahamu chochote juu ya Cyber Law ya Tanzania?

SM
 
Ndiyo maana nikasema mpinzani tunayetaka kumwendea anauwezo wa kutuazima silaha, silaha yenyewe ikaja kutoa maji kama ya kinjekitile.
Quinine, nadhani kwenye bold, ulimaanisha wakili na sio mpinzani!.
 
Asanteni sana JF crew.
Isingekuwa busara kuliacha hili lipite bila kusemewa. Huu ungekuwa mtandao wa chama fulani cha siasa basi ungekuwa ushakufa siku nyingi!
Ni vizuri wanasiasa wakawa wakweli na sio kuficha vichwa vyao ndani ya mchanga.
 
Pasco, please kachukue transcript na LL.B yako wajukuu waje wajivunie! Ichukue si kwa ajili yako bali kwa ajili ya vizazi vijavyo! Na ipo siku (siku sio nyingi) tutihitaji pia. UN wanatabia ya kutaka vyeti vya maofisa wanaoteuliwa kwenda kuwakilisha huko.
 
mwanakijiji,

kuna tuhuma nzito zinafufuka huku tuliko kwamba umenunuliwa na chadema baada ya pesa yako ya dhamana kwenye kesi yako kuishi marekani bila visa.

chadema kupitia mbowe na slaa na wafuasi wa mengi walilipia dola 5000.

kwa sisi wengine huo ni mgongano wa maslahi. ghafla umeanza kuwa nape wa chadema.

tuthibitishie ni chadema wamelipa udhamini wako.

imekuwaje mtu unajifanya mtetea ufuataji wa sheria unaishi nchi za watu ukivunja sheria.


Kwa kifupi hujui ulisemalo, kama huna mchango wowote kwenye mada husika basi tupishe kaa pembeni, inaonekana wewe haujawahi kutoka nje ya nchi yako, yaani hata Nairobi haujuwi inafananaje. hapa sio sehemu ya majungu, wenzio huwa wakituhumu wanaleta na supporting docs za kukazia kile wanachotuhumu. hivi akitokea member mwingine wa kiume akasema alikesha guest house na wewe tumuamini! mwanakijiji sio malaika, ila kama unamtuhumu lete evidence hapa in details kutoka US immigration Department. otherwise uzushi wako peleka kwenye vikao vya kitchen pati.
 
Mwanakijiji / Maxence / Wanasheria wanachama wa JF / Wana JF

Je; Inawezekana kuiburuza CCM mahakamani na kudai Damages / Fidia kwa habari za:

1. Uongo
2. Kuivunjia Heshima na Hadhi JF
3. Kuwasababishia wanachama usumbufu, kuwapa wasiwasi na kuwaumiza kisaikolojia?

We dare to talk openly and we can also dare to DO openly.

JF should not take any "Bullshit" from CCM nor any Party nor the Government. We are simply a social network.

Why dont we give them a lesson? Tunaogopa nini au tunamwogopa nani?

mkuu mi nashauri na tulishashauri mara nyingi kuwa kama CCM wanahoja,wabonyeze REGISTER waingie Jf tushindane kwa hoja si vitisho! Hamna kuwashtaki ccm wanatafuta mtu wa kufa nae,waache ccm ife peke yake. Binafsi sijui kama Jf ni ya chadema/upinzani maana tunao watu humu wanaoleta hoja kibao za ccm na kukashifu cdm/au slaa,iweje wakimbile mtaani kulalama? Nakuhakikishia,JF ni mahakama ya fikra,kila mtu huleta utetezi wake na kila member ni jaji ambako uruhusiwa kutoa hukumu akibonyeza REPLY. Kiukweli mi ntaichukia Jf kama ina uchadema unless iweke wazi,lakini as far as kila mtu ujisalimisha mwenyewe jf,sidhani kama kuna lengo ila kama wanaoneemeka na ccm hawaoni haja ya kuja hapa kujadili msitakabali wa taifa,basi isiwe tabu wacha wenye uchungu tuendelee kujuzana! Siku njema,karibu nec,cc,msekwa hapa Jf tukaangane!
 
Madai ya CCM si ya kupuuzwa kuna jambo la msingi hapa katika Forum ambalo kwa hakika linahitaji kutazamwa kwa jicho la tatu:
1. kuwa critical thinkers haimaanishi kukosoa kila jambo, nimewahi kulisema hili katika moja ya thread zangu baada ya kupokea changamoto ambazo kwa kweli ukipima huoni msingi wa hoja ulikuwa wapi zaidi ya ushabiki.

2. Kuna mabadiliko makubwa katika mwenendo wa uchangiaji katika forum, nimelitazama hili kwa muda sasa mpaka wakati mwingine nasita kuomba fikara za watanzania kwa kuwa utaishia kupokea michango iliyojaa matusi na kejeli isiyotoa hoja za kitaalam na zilizotafitiwa. Ushahidi mzuri soma thread zote za wiki hii uchuje mwenyewe.

3. Kinadharia na mlengo wa Hoja nyingi ambazo hazitoi mizani sawa katika uchambuzi zinaweza kujenga hoja ya nguvu kwa madai ya CCM.

4. Inawezekana wapo wanajamii wenye mlengo wa wastani na wahafidhina ambao kamwe mawazo yao ni sahihi kuliko ya wengine.

5. Hii ni forum yenye heshma na msaada mkubwa katika jamii, tutumie taaluma na hoja zenye kuleta mabadiliko ya kweli katika kuleta ustawi wa maisha ya Mtanzania. Nilipendezwa sana na Hoja ya Mwanakijiji last week kuhusu hoja ya CHADEMA na ukosoaji wa Utawala. Ilijaa mantiki na yenye kutoa taswira sahihi ya Upinzani na mabadiliko.

6. Haya ni mawazo binafsi na si msimamo wa Taasisi yoyote wala kipindi chochote katika chombo chochote cha habari.

Yahya M

Huwezi kuweka constraints (vikwazo) kwa mawazo ya mwanadamu kuhusu suala lo lote. Kwa ni fursa nzuri kuruhu uwezekano wa fikra zote zijitokeze ili uziweke kwenye mizani. Sikubaliani na wewe kwa hoja yako. Kwa saikolojia ya ualimu kazi kubwa ni kuibua fikra za mwanafunzi kwa sababu akiweza kuzitoa kwa uhuru ataweza kukabiliana na mitihani ya darasani na ya dunia.

CCM walishaamua kufikiri, kuamua na kutenda watakavyo badala ya kila mtanzania wala siyo kwa naba ya mtanzania
 
Nsiande, kina Kabwe na Slaa hawakukaribishwa; kwanini tuwape huo umuhimu hao watu wa sekretariati ya CCM? kwa ujiko gani walionao. Wanajua anuani ya JF - https://www.jamiiforums.com kuna mahali pale juu panasema "register"...

Kwa hili natofautiana kabisa na kiongozi wangu. Mimi ni mwanachama hai wa CCM sijawahi kupata kikwazo chochote kujiunga hapa JF wala kikwazo katika kutoa maoni na kubishana na lile ninalo amini linazungumzwa tofauti. Isitoshe hata hao CHADEMA kama hii Forum ni yao kwa ajili ya wanachama wao mbona basi hawana control kabisa na mambo yao? mbona wanaruhusu mijadala inayotoa maoni tofauti na chama chao?
 
Mkuu Pasco;

This is very useful . . . .

Je unafahamu chochote juu ya Cyber Law ya Tanzania?

SM
Super Man,
Kwanza nakupongeza sana kwa juhudi zako kuhakikisha jf, inapata haki dhidi ya shutuma hizi.

Naunga mkono asilimia 100%, kwenda mahakamani kudai fidia, lengo letu likiwa sio kupata mafao ya tozo, bali kulinda heshima yetu.
Tanzania hatu legistalation yoyote ya cyber law. Sheria zetu zote, zimetokana na sheria za Mwingereza, comon law ambazo walizikopi na kuzipeleka Afrika kusini ilipopata uhuru wake 1912, na baadaye India ikazikopi ilipopata uhuru wake 1948, na Tanzania tocacopy zile sheria za India para-material (neno kwa neno bila kubadili kitu). Wenzetu India, wameshazibadili za kwao na kujumuisha cyber law, sisi bado.

Pamoja na kutokuwa na specific cyber law, tumeshapitisha vifungu kadha wa kadha vyenye kuruhusu prosecution ya cyber crimes kupitia several The Written Laws (Miscellaneous Amendments) na pia kupitia baadhi ya shria mpya tulizoshinikizwa ikiwemo anti-terrosism act.

Wanasheria wamegawanyika sehemu nyingi, wale wenye kushughulikia kesi mbalimbali za madai ya mahakamani, wanaitwa wanasheria waitwa wanasheria wa litigations, na miongoni mwa kesi zinazosumbua mahakamani kuliko kesi nyingine zote, ni kesi za madai ya defamation na libel, zinapoteza muda mrefu na nyingine huishia kutoshinda. Mawakili wa kesi za namna hii nchi za wenzetu, wanatumia mtindo unaitwa 'No Win No Fee', yaani wakili atalipwa tuu baada ya kushinda kesi, ila mgao wake unakuwa ni mkubwa hadi kufikia kugawana nusu kwa nusu (fifty fifty).

Kinachazifanya kesi hizi ziwe sumbufu, ni jinsi ya kuthibitisha umeumizwaje kiuchumi, mfani JF ikidai fidia ya bilioni 100, inatakiwa kuthibitisha kwanza thamani yake, is it woth 100 bilions?, pili kuthibitisha njia za mapato za jf zinatirisha mabilioni hayo, halafu ndipo una prove kuwa matamshi yale yameiangusha jf kimapato hivyo kustahili fidia husika.

Kwa vile lengo letu sio kupata faida ya kuichumi, bado tunaweza kufungua kesi kama ya Mengi na Manji, ambayo Manji anadai Shilingi Moja Tuu (1/=) ili kumthibitishia Mengi, lengo sio mafao bali kulinda heshima.

Gharama za wakili, sio issue sana, mimi naamini kuna mawakili watajitolea kyuibeba hii kesi free of charge. Kwa wenzetu ulaya, ili uweze kujenga jina, mawakili wanaochipukia, hujitolea kubeba complex cases wakishinda ndipo wanapotokea.

Mimi binafsi, sikuwahi kuwa na mpango wa kuwa wakili, lakini jf, ime ni inspire sana, mpaka nimetamani, ningekuwa wakili, ningeibeba hii kesi free of charge, na ninaamini kwa asilimia 100 tungeshinda!.
 
Pasco, please kachukue transcript na LL.B yako wajukuu waje wajivunie! Ichukue si kwa ajili yako bali kwa ajili ya vizazi vijavyo! Na ipo siku (siku sio nyingi) tutihitaji pia. UN wanatabia ya kutaka vyeti vya maofisa wanaoteuliwa kwenda kuwakilisha huko.
MsandoAlberto, asante sana kwa ushauri huu, japo sitarajii uwakilishi wowote UN, profession iliyotangulia ilinipa access kuripoti UN General Assembly kwa miaka 4 mfufulizo. Nitaifuatia hiyo transcript kwa sababu, huu ndio mwaka wa mwisho, kwa sisi tuliosoma zamani ku petition, baada ya sasa, wanaofuatia wote, lazima wapite Law School, hivyo lets hope for the best, I'll eventually join the bar this year!.
 
Kama mwenyekiti wa chama cha magamba alimkimbia mgombea mwenzake wa urais Dr Slaa kwenye midahalo ya wazi, unadhani ndani ya chama hicho kuna watu wenye uwezo wa kujenga hoja na kuzisimamia? wao kazi yao ni kuingia humu nakuwa upande wa Guests basi, na ndio maana hata makuwadi wao wanaowatumia kuja humu hawaji na hoja yoyote, zaidi ya kuvuruga mada za msingi wanazojadili watu. wao siasa zao ni Dr Slaa tu. kumbe kama kuna mtu wanaotakiwa kumuogopa sana kwa sasa ni Tundu Lissu.

Mi sidhani kama wanaingia kama guests. Hivi mnafahamuje kama MS, Mhadhir, Kupeng'e, Kibunango, Kashaga, nk sio miongoni mwa sekretariet ya CCM?
 
Melo na mwenzake Mushi walishawai kamatwa na kuhojiwa na police. Tundu lisu chadema ndio mwanasheria wao. Utakataaje kama si mtandao wa chama. Mijadala iwe ya busara si matusi wala uchochezi ulivyo sasa. Hakuna uhuru bila mipaka.
Zhu, fani ya uwakili ina kitu kinaitwa client charter, yule ni mteja, kama zilivyo profession nyingine zozote, hata wewe ukiwa ni Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo, na ni kada wa CCM, akija Dr. Slaa kutibiwa moyo, utamtibu kwa uadilifu ule ule ambao utamtibu JK atakapo hitaji huduma yako.

Ndio maana Mabere Marando ndio wakili wa Manji, wakati Manji ni CCM.

Hata mimi ni mmiliki wa a small production house, wakati wa uchaguzi, kampuni yangu ilipewa tenda ya kuandaa vipindi vya kuhubiri amani, na kutoingiza udini katika siasa. Wadau wakuu wa vipindi hivyo walikuwa viongozi wa Dini ambao ni ma pro-CCM, kampuni ilifanya bili kuingilia conflict of interest na msimamo wangu binafsi wa kutofungamana na chama chochote, bali ni mkereketwa wa demokrasia ya kweli ndani ya bunge.
 
I know CCM like my "naked glorious body" They are as predictable as spring rains!

lol. If u did, your Chadema could be in power right now. Lets be honest baab, you are making a living off CCM being in power. Otherwise, your megaphone is impotent.

I remember perusing JF right before election and reading this space you would think Chadema will win a landslide, they ended up losing big. Reading it right now you would think Chadema will take over a country in 3 weeks.

Someni Tanzania literature, Kezilahabi, Mtobwa na wengine ili mupate uelewa wa society ya WaTanzania tulivyo. We are all talk. Read anthropology work in Tanganyika. Heck, even Germany East Africa had to be subsidized from Berlin, the colony was not making any monies. British didn't even bother messing with Tanganyika. Read David Landes' masterpiece on why countries are rich and others a poor.

Throngs of threads about CCJ came and go. At that time you would have thought it was Qiyama for CCM.

InshaAllah November 2015 we will be here. Millions threads will be read and forgotten, and you will probably author few thousands. You candidate will loose. And the society will be better off. Jamii Forum and family will continue to cash up "donors' money.

Life goes on.
 
Walishindwa siku nyingi sana kuhusu fikra mpya na sasa wanatafuta mchawi ila ukweli ni kwamba Jamii forum ni kisima cha chemchem pevu
 
Wameshindwa na sasa wanatafuta mchawi ila kwa hili ni jambo nzuri sana na wao wasijue kuwa Tanzania bado ipo kwenye ujamaa na ujima wa mifumo wa kale
 
Juzi mwanasheria mkuu wa serikali Ndg. F. Werema, alikuwa Channel ten ambapo alijibu maswali ya moja kwa moja.

Kuna mtu mmoja aliuliza swali tokea Zanzibar kuhusu muswada wa kukusanya maoni ya katiba mpya. Aliyeuliza swali alijitambulisha kama "Junius", na alipokuwa akijibu, Jaji Werema alianza kwa kusema hadhani kama huyo aliyeuliza swali, 'Junius' ni jina lake halisi...

Nilipotafakari nikajiuliza hivi ametumia kigezo gani kujua Junius sio jina halisi la mhusika?

Nililazimika kudhani kuwa pengine anamfahamu na labda pale studio namba inadisplay, au alimwambia awali kuwa nitakuuliza swali na kudanganya kuwa naitwa Junius.

Lakini probability kubwa zaidi nilidhani ni kuwa Werema anatembelea na pengine ni member wa JF.

Kama tunavyojua, kuna member wa JF anatumia jina Junius, na mara nyingi amekuwa na hoja za kutetea Zanzibar.

Kama mwanasheria mkuu yupo huku, namwomba asijifiche, ajitambulishe na sisi tutampa nafasi yake kama mwanasheria mkuu tunapojadili mada mbalimbali...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom