Ukisema hakuna kabila lenye wanawake wazuri kuliko Wasukuma hili ni dai la jumla ambalo haliwezi kuthibitishwa kwa maoni binafsi kiongozi. Na ukisema nenda ukaone, bado hujathibitisha hilo. Umenialika nikakubaliane na maoni yako.
Kwa mfano mtu wa kabila jingine angeleta kauli hiyo hiyo akiwatetea watu wake, ungeikubali bila ushahidi au ungeona ni mtazamo wake tu?
Na tatizo si ushahidi wako. Tatizo ni kwamba madai yako hayawezi kuwa fact. Yanaweza kuwa mawazo yako au yangu binafsi tu.
Kama angeandika hivi:
Kwa maoni yangu, Wasukuma wana wanawake wazuri kuliko makabila mengine.
Hapo wala kusingekuwa na tatizo kwasababu hayo ni maoni yake.