Jamii yashauriwa kuacha tabia ya kumeza dawa bila kupima, hali hiyo inatengeneza usugu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Medard Beyanga.jpg

Dkt. Medard Beyanga

Mkurugenzi wa Maabara ya Taifa ya Afya ya Jamii, Dkt. Medard Beyanga ameshauri jamii kuwa na kawaida ya kufanya vipimo kuanzia katika hatua za awali za ugonjwa na kuacha kujichukulia maamuzi ya kwenda kununua dawa bila kuwa na utaalam wa daktari.

Amesema jambo la kwanza la kufanikiwa kumaliza changamoto ya ugonjwa au Magonjwa ya Mlipuko ni kufanya vipimo vya maabara mapema kwa kuutambua ugonjwa husika ili kujua njia rasmi na sahihi za kuutibu.

Kutumia dawa bila vipimo, hufanya Vimelea vya Ugonjwa kuwa sugu na unaweza usipone tatizo.

Ameeleza kuwa anatoa wito kwa jamii kufanya vipimo katika sehemu sahihi kwa kuwa kufanya hivyo kunarahisisha njia za kukabiliana na changamoto husika, kwa kuwa kuendelea kutumia dawa bila kupima kunasababisha usugu ndani ya mwili na baadaye hali hiyo inaweza kuathiri mwili wakati wa matibabu rasmi.

“Mtu anapopata changamoto za awali kabisa anatakiwa kwenda kuanzia ngazi ya Zahanati kama ataona ni jambo dogo, lengo la kufanya hivyo ni kuwa hata anapotokea ugonjwa husika ni mkubwa kuliko sehemu aliyoenda kupata matibabu basi watampa mwongozo wa nini akifanye au kumpeleka katika ngazi za juu zaidi.

“Kufanya hivyo kunaweza kupungua hata magonjwa ya maambukizi, kuna wakati kumekuwa kukitokea changamoto za maambukizi kusambaa kwa kasi kwa kuwa tu hatua muhimu hazikuchukuliwa mwanzoni.”

Ametoa mfano maambukizi ya Ugonjwa wa Marburg yaliyotokea Mkoani Kagera miezi ya hivi karibuni, akieleza kuwa yaliripotiwa mapema na ndio maana hata matibabu yake yalidhibitiwa mapema pia.


Pia soma - Wizara ya Afya: Mtumishi mmoja wa Afya alifariki kwa Ugonjwa wa Marburg Virus
 
Mkumbushe tu Kuna watu wapo huko singida vijijini hata Ela ya kupeleka nafaka kusaga au kukoboa hawana wanasaga na mawe na kukoboa kwa kutwaga kwenye kinu
Uko sahihi mkuu.

Nimeishi kwenye hayo mazingira naelewa sana ulichosema.

Huyu Dkt alete ushauri mzuri aache kugeneralize hivi
 
Anawazungumzia watu kipato Cha Kati ila watz most of them, they can't even Afford to pay for painkillers .



Fanya vipimo goverenmet viwe free of charge

Dawa ziwe free of charge

Then alete hizo hoja zake
 
Niseme ukweli tu nina tabia ya kujinyea dawa bila kupimwa kila ninapojisikia naumwa naenda famasi kununua panado na dawa yeyote ninayohisi nimepata ugonjwa wake kama malaria, typhoid, UTI, maumivu mengine. Kuna wakati nilikunywa Chloromphenicle zikaniletea madhara ya kukosa hamu ya kula kwa muda mrefu, panado ndio nazikimbilia sana kuzinywa hata sijui naumwa ugonjwa gani. Haya mazoea ni mabaya sana bora niwe napimwa kwanza na kuandikiwa dawa na daktari kuliko kunywea dawa kiholela kuepuka madhara
 
Ukiachana na watu wenye hali duni na kushindwa kumudu gharama za hosp huku mtaani wengi wanajinywea tu dawa kwa kuoanisha dalili za ugonjwa uliopita na wa sasa
 
Back
Top Bottom