mayala luswetul
Member
- Jun 2, 2008
- 40
- 0
Bila kumsahau michael Katembo mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi
wakuu mnakumbuka maigizo ya Mzee Jangala usiku saa tatu???, never miss.
enzi hizo kwanza mwasikiliza wadhamini CHIBUKU!!, ..chibuku oyeee, chibukuuu hongera hongeraa hongeraaa...!, duh.
Kweli ndugu
unakumbuka kipindi cha uhamiaji? mikingamo?
Kulikuwa pia na Abdul-Omar Masoud, na kile kipindi cha Michezo. Wakati fulani akadokeza ule mziki wa kuanzia na akaukata kwa hafla na kwa furaha akasema- Lisemwalo lipo kama halipo laja- Yanga Bwanga aingia Yanga.kipindi kilicho kuwa kinaendeshwa na mkurugenzi Mzee David Wakati. halafu kulikua na external service huko ndo kulikuwa na nyimbo za kizungu na kilikuwa chaendeshwa kwa ung'eng'e. na nikikumbuka watangazaji kama akina Sekioni Kitojo, Ahmed Jongo, Charles Hilary, Abisai Steven Ben Kiko (huyu alivuma sana wakati wa vita vya uganda .
Mimi mpaka leo nataka kujua aliyepiga zile nyimbo za MAJIRA,MCHANAMWEMA na MICHEZO na wapi ntapata records zile.Alipuliza trumpet vizuri and drums arrangement zilikuwa bomba.
umenikumbusha adili na nduguze,Mama na mwana, kwa ambao kipindi tulikuwa watoto.
Michezo ya kuigiza pwagu na pwaguza, mzee jongo na bi nyakomba.:lol: