Jamani hatuna Serikali tena!

Serikali yababaika
TUHUMA DHIDI YA CHENGE



na Salehe Mohamed, Dodoma na Kulwa Karedia Da



TUHUMA zinazomkabili Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge, anayedaiwa kukutwa na zaidi ya dola za Marekani milioni moja katika akaunti zinazochunguzwa iwapo zina uhusiano wowote na ununuzi wa rada nchini Uingereza mwaka 2002, zinaonekana kuilemea serikali.

Siku moja tu baada ya Chenge mwenyewe kutoa kauli akieleza kushtushwa na tuhuma hizo ambazo aliziita za kuumbiwa na zinazotokana na chuki binafsi, viongozi serikalini wenye dhamana ya masuala ya utawala bora, usalama na uhalifu wameanza kutoa taarifa zinazokinzana.

Akizungumza na Tanzania Daima mjini Dodoma jana, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) Sophia Simba, alisema serikali ilikuwa bado haijaanza kumfanyia uchunguzi Chenge na kwamba suala hilo lilikuwa likishughulikiwa na Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Jinai ya nchini Uingereza ya SFO.

Waziri Simba alisema maofisa wa SFO walifika hapa nchini na kuomba nyaraka na taarifa zote zinazomhusu Chenge na wakazichukua na kurudi kwao ambako wanaendelea na uchunguzi wao.

Aidha, waziri huyo alishindwa kueleza kama serikali ilikuwa imechukua hatua zozote kuchunguza iwapo waziri huyo aliyerejesha nchini juzi akitokea China alikuwa amewasilisha taarifa za kuwa na akaunti ya fedha katika Kisiwa cha Jersey katika Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi..

Waziri Simba, alieleza kuwa, kwa sasa serikali inajikita katika kuandaa utaratibu ambao utaiwezesha kupata fedha ambazo zilitozwa zaidi kuliko gharama halisi ya rada hiyo, iliyonunuliwa mwaka 2002.

“Wale (SFO) ndio wamekuja kutaka mafaili na taarifa kuhusu Chenge na wakapewa halafu wameondoka kwenda kufanya uchunguzi wao, sasa sisi hatuna cha kufanya zaidi ya kusubiri matokeo,” alisema Simba.

Alisema serikali haimtuhumu Chenge kwa kumiliki akaunti yenye fedha nyingi kiasi hicho, bali wale wenye kujua mambo hayo ndio watakaokuwa na jukumu la kufanya uchunguzi husika.

Alisema kifungu cha 6(i) cha Sheria namba 13 ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995, kinabainisha wazi kuwa Kamishna wa Sekretariati ya Maadili ya Viongozi anayo mamlaka ya kuruhusu kufanyika kwa uchunguzi dhidi ya kiongozi wa umma.

Alisema kutokana na sheria hiyo, kamishna aliwaruhusu wataalamu wa SFO kuchukua taarifa kuhusu Waziri Chenge, jambo ambalo mtu yeyote anaweza kulifanya kama kamishna atakubaliana na sababu alizozitoa.

Waziri huyo ambaye hivi karibuni alikaririwa na gazeti moja akionyesha mshtuko wa wazi dhidi ya tuhuma hizo za Chenge hata kufikia hatua ya kuhoji pengine alizipata kwa kuuza ng’ombe wake, alisema taarifa za Chenge kumiliki kiasi kikubwa cha fedha wamezipata kupitia vyombo vya habari.

“Sisi tuna taratibu za kufanya kazi na kufanya uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazowakabili watumishi wa umma. Hatuwezi kufanya uchunguzi wa kila taarifa inayotolewa na vyombo vya habari,” alisema Simba.

Alisema kuwa Rais Jakaya Kikwete alishaweka bayana msimamo wa Tanzania kuhusu suala la ununuzi wa rada ya kijeshi iliyonunuliwa kwa paundi za Uingereza milioni 28.

Alisema kama kuna tatizo lolote kwa mtumishi wa umma kuhusishwa katika tuhuma za rushwa, serikali itaangalia cha kufanya baada ya kupata taarifa za uhakika, baada ya uchunguzi kufanyika.

“Kama kuna ulazima wa kufanya uchunguzi kuhusu kiongozi wetu, tutaufanya, lakini si kwa shinikizo kutoka sehemu fulani au kwa sababu ya maneno ya watu,” alisema Simba.

Wakati Waziri Simba akitoa majibu hayo, Jeshi la Polisi limebainisha kuwa, haliwezi kufanya uchunguzi hivi sasa dhidi ya waziri huyo kwa sababu hadi hivi sasa halijapokea taarifa zozote kutoka serikalini, zinazolitaka kumchunguza.

Akizungumza na Tanzania Daima ofisini kwake Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Manumba, alisema ofisi yake haijapokea taarifa yoyote rasmi ya maandishi kutoka ngazi za juu kwa ajili ya kumfanyia uchunguzi Waziri Chenge.

“Kwa kweli suala hili nimelisoma kwenye magazeti tu… naomba tuwe na subira,” alisema DCI Manumba katika mahojiano na gazeti hili jana.

Alisema kama ofisi yake ikipokea taarifa ya kumfanyia uchunguzi Chenge, haitasita kufanya hivyo kwa vile kazi yake kubwa ni kushughulikia matatizo kama hayo.

“Tutafika hata huko anakodaiwa kuweka fedha hizo kuchunguza, kwa vile hivi sasa kuna njia nyingi za mawasiliano,” alisema Manumba.

Hata hivyo, alisema kulingana na aina ya suala lenyewe, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ndiyo yenye dhamana kubwa ya kuendesha uchunguzi.

DCI, ambaye hakutaka kuingia kiundani juu ya suala hilo, alisema taasisi nyingi za serikali zimegawana majukumu kwa mujibu wa sheria.

“Wenzetu wa TAKUKURU naamini hivi sasa wako katika nafasi nzuri zaidi ya kulizungumzia hili, mimi hapa nakupa tu hali ilivyo ya mgawanyiko wa majukumu yetu,” alisema.

Tanzania Daima haikuweza kuwasiliana na TAKUKURU kutokana na ukweli kwamba, iwapo ingekiri kumchunguza waziri huyo basi sheria ingelizuia gazeti hili kuandika taarifa hizo.

Jumamosi ya wiki iliyopita, gazeti linaloheshimika nchini Uingereza, la The Guardian liliandika kuwa katika uchunguzi huo wa SFO iligundulika akaunti moja inayohusishwa na Chenge ikiwa na zaidi ya dola za Marekani milioni moja katika akaunti moja, katika Kisiwa cha Jersey.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, SFO inamchukulia Chenge kuwa mtu anayeweza akawa shahidi muhimu katika uchunguzi mzima wa zabuni ya ununuzi wa rada kutoka Kampuni ya BAE ya nchini Uingereza.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, SFO inatarajia kuanza upya kufanya uchunguzi kuhusu fedha hizo ili kuangalia iwapo zina uhusiano wowote na zile zinazoaminika kutolewa kwa njia ya rushwa wakati Tanzania iliponunua rada ya kijeshi kutoka nchini humo kwa paundi milioni 28, ambazo ni sawa na shilingi bilioni 70, mwaka 2002.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, inaaminika kwamba, uchunguzi huo wa SFO unatarajiwa kuanza katika kipindi cha wiki sita zijazo.

Kwa mujibu wa habari hizo, uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba, moja ya mambo yanayofuatiliwa ni kujua iwapo fedha hizo zinazoaminika kuwa za Waziri Chenge zilizowekwa katika akaunti moja iliyoko katika Kisiwa cha Jersey zina uhusiano wowote na zile zilizotoka katika Kampuni ya BAE System inayotuhumiwa kuinyonya Tanzania kwa kuiuzia rada hiyo kwa bei kubwa kuliko ilivyotakiwa.

The Guardian katika habari yake hiyo iliyowekwa katika mtandao wa intaneti, linaripoti kuwa, taarifa hizo zinakuja ikiwa ni miaka mitatu sasa tangu Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) kwa kushirikiana na SFO na taasisi za uchunguzi za Uswisi na Jersey zilipoanza kuchunguza kuhusu kashfa nzima ya ununuzi wa rada.

Gazeti hilo lilimkariri Waziri Chenge akikiri kwamba fedha hizo ni zake na akatumia fursa hiyo kukanusha kuwapo kwa uhusiano wowote kati ya fedha hizo na kashfa nzima ya ununuzi wa rada, uliofanywa wakati yeye akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

“Jambo la wazi linalotaka kuonekana hapa ni kwamba mimi nilipokea kwa lengo la kujinufaisha mwenyewe fedha za rushwa kutoka BAE. Huu ni uongo,” alisema Chenge.

Aidha, gazeti hilo lilimkariri Chenge akisema kuwa, wakati rada hiyo ilipokuwa ikinunuliwa yeye alihusika kwa kiwango kidogo sana katika mchakato mzima, kwani jambo hilo lilishughulikiwa na wizara nyingine na uamuzi ukaidhinishwa na Baraza la Mawaziri.

Mbali ya hilo, gazeti hilo lilimkariri mwanasheria wa Chenge anayeishi Cleveland, Ohio, nchini Marekani, J Lewis Madorsky, akikanusha kwa niaba ya mteja wake huyo, kuwapo kwa uhusiano wowote kati ya fedha zake na tuhuma zozote.

“Wakati tukitambua kuwa masuala hayo yalitokea muda mrefu uliopita, tunaweza tu tukathibitisha kuwa, tuhuma zozote za ukiukwaji wa sheria, ukiukwaji wa maadili, kutenda isivyo sawa na mambo mengine ya hivyo dhidi ya mteja wetu ni mambo ambayo kimsingi tunayakanusha kwa nguvu kubwa,” alisema mwanasheria huyo wa Chenge.

Hata hivyo, gazeti hilo liliandika kuwa uchunguzi huo dhidi ya Chenge unamfanya yeye kuwa tu shahidi muhimu, kwani wanaielenga zaidi BAE ambayo inadaiwa ilimlipa wakala mmoja wa Tanzania mamilioni ya fedha ili kujenga ushawishi wa rada iliyokuwa ikiiuza kununuliwa.

Wakala huyo ambaye amekuwa akitajwa kwa muda mrefu na ambaye sasa anaaminika kukimbia nchini na kutafutwa na polisi wa kimataifa ni, Shailesh Vithlani.

Akizungumza baada ya kurejea nchini juzi, Waziri Chenge aliwataka wananchi kuwa na subira kuhusu uchunguzi huo na kile alichokiita vijisenti ambavyo vinatakiwa kujulikana vilipatikanaje.

Alikiri kwamba tuhuma hizo dhidi yake ni nzito na zilizomshtua, na akakataa kuelezea chochote kwa undani kuhusu kuwa na fedha hizo au njia alizozipata, na iwapo kulikuwa na uhusiano wowote kati ya tuhuma hizo na kashfa ya ununuzi wa rada ya kijeshi.

Hata hivyo alisema amekuwa kiongozi serikalini kwa muda mrefu, akishika nyadhifa tofauti, akiwa ameshika nafasi ya Uanasheria Mkuu wa Serikali kwa miaka 10, hivyo fedha alizokuwa akilipwa zilikuwa halali.

“Tuhuma za ufisadi dhidi yangu ni nzito mno… inabidi nipate muda wa kukaa na kutafakari kwanza, na ukweli wa mambo utajulikana baada ya vyombo vya dola vilivyopewa kazi ya kunichunguza kumaliza kazi yake na hapo nitakuwa na muda wa kujibu,” alisema Chenge juzi.


Source: Tanzania Daima


aliyo guku oyaga gete ituja ya ntuzu!ulindoshi sana guku!i bariadi a banhu balilya milenda na bugali ubebe bilion moja ulihaya vijisenti aliyo ulindoshi sana!
 
Serikali yababaika
TUHUMA DHIDI YA CHENGE



na Salehe Mohamed, Dodoma na Kulwa Karedia Da



TUHUMA zinazomkabili Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge, anayedaiwa kukutwa na zaidi ya dola za Marekani milioni moja katika akaunti zinazochunguzwa iwapo zina uhusiano wowote na ununuzi wa rada nchini Uingereza mwaka 2002, zinaonekana kuilemea serikali.

Siku moja tu baada ya Chenge mwenyewe kutoa kauli akieleza kushtushwa na tuhuma hizo ambazo aliziita za kuumbiwa na zinazotokana na chuki binafsi, viongozi serikalini wenye dhamana ya masuala ya utawala bora, usalama na uhalifu wameanza kutoa taarifa zinazokinzana.

Akizungumza na Tanzania Daima mjini Dodoma jana, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) Sophia Simba, alisema serikali ilikuwa bado haijaanza kumfanyia uchunguzi Chenge na kwamba suala hilo lilikuwa likishughulikiwa na Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Jinai ya nchini Uingereza ya SFO.

Waziri Simba alisema maofisa wa SFO walifika hapa nchini na kuomba nyaraka na taarifa zote zinazomhusu Chenge na wakazichukua na kurudi kwao ambako wanaendelea na uchunguzi wao.

Aidha, waziri huyo alishindwa kueleza kama serikali ilikuwa imechukua hatua zozote kuchunguza iwapo waziri huyo aliyerejesha nchini juzi akitokea China alikuwa amewasilisha taarifa za kuwa na akaunti ya fedha katika Kisiwa cha Jersey katika Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi..

Waziri Simba, alieleza kuwa, kwa sasa serikali inajikita katika kuandaa utaratibu ambao utaiwezesha kupata fedha ambazo zilitozwa zaidi kuliko gharama halisi ya rada hiyo, iliyonunuliwa mwaka 2002.

“Wale (SFO) ndio wamekuja kutaka mafaili na taarifa kuhusu Chenge na wakapewa halafu wameondoka kwenda kufanya uchunguzi wao, sasa sisi hatuna cha kufanya zaidi ya kusubiri matokeo,” alisema Simba.

Alisema serikali haimtuhumu Chenge kwa kumiliki akaunti yenye fedha nyingi kiasi hicho, bali wale wenye kujua mambo hayo ndio watakaokuwa na jukumu la kufanya uchunguzi husika.

Alisema kifungu cha 6(i) cha Sheria namba 13 ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995, kinabainisha wazi kuwa Kamishna wa Sekretariati ya Maadili ya Viongozi anayo mamlaka ya kuruhusu kufanyika kwa uchunguzi dhidi ya kiongozi wa umma.

Alisema kutokana na sheria hiyo, kamishna aliwaruhusu wataalamu wa SFO kuchukua taarifa kuhusu Waziri Chenge, jambo ambalo mtu yeyote anaweza kulifanya kama kamishna atakubaliana na sababu alizozitoa.

Waziri huyo ambaye hivi karibuni alikaririwa na gazeti moja akionyesha mshtuko wa wazi dhidi ya tuhuma hizo za Chenge hata kufikia hatua ya kuhoji pengine alizipata kwa kuuza ng’ombe wake, alisema taarifa za Chenge kumiliki kiasi kikubwa cha fedha wamezipata kupitia vyombo vya habari.

“Sisi tuna taratibu za kufanya kazi na kufanya uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazowakabili watumishi wa umma. Hatuwezi kufanya uchunguzi wa kila taarifa inayotolewa na vyombo vya habari,” alisema Simba.

Alisema kuwa Rais Jakaya Kikwete alishaweka bayana msimamo wa Tanzania kuhusu suala la ununuzi wa rada ya kijeshi iliyonunuliwa kwa paundi za Uingereza milioni 28.

Alisema kama kuna tatizo lolote kwa mtumishi wa umma kuhusishwa katika tuhuma za rushwa, serikali itaangalia cha kufanya baada ya kupata taarifa za uhakika, baada ya uchunguzi kufanyika.

“Kama kuna ulazima wa kufanya uchunguzi kuhusu kiongozi wetu, tutaufanya, lakini si kwa shinikizo kutoka sehemu fulani au kwa sababu ya maneno ya watu,” alisema Simba.

Wakati Waziri Simba akitoa majibu hayo, Jeshi la Polisi limebainisha kuwa, haliwezi kufanya uchunguzi hivi sasa dhidi ya waziri huyo kwa sababu hadi hivi sasa halijapokea taarifa zozote kutoka serikalini, zinazolitaka kumchunguza.

Akizungumza na Tanzania Daima ofisini kwake Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Manumba, alisema ofisi yake haijapokea taarifa yoyote rasmi ya maandishi kutoka ngazi za juu kwa ajili ya kumfanyia uchunguzi Waziri Chenge.

“Kwa kweli suala hili nimelisoma kwenye magazeti tu… naomba tuwe na subira,” alisema DCI Manumba katika mahojiano na gazeti hili jana.

Alisema kama ofisi yake ikipokea taarifa ya kumfanyia uchunguzi Chenge, haitasita kufanya hivyo kwa vile kazi yake kubwa ni kushughulikia matatizo kama hayo.

“Tutafika hata huko anakodaiwa kuweka fedha hizo kuchunguza, kwa vile hivi sasa kuna njia nyingi za mawasiliano,” alisema Manumba.

Hata hivyo, alisema kulingana na aina ya suala lenyewe, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ndiyo yenye dhamana kubwa ya kuendesha uchunguzi.

DCI, ambaye hakutaka kuingia kiundani juu ya suala hilo, alisema taasisi nyingi za serikali zimegawana majukumu kwa mujibu wa sheria.

“Wenzetu wa TAKUKURU naamini hivi sasa wako katika nafasi nzuri zaidi ya kulizungumzia hili, mimi hapa nakupa tu hali ilivyo ya mgawanyiko wa majukumu yetu,” alisema.

Tanzania Daima haikuweza kuwasiliana na TAKUKURU kutokana na ukweli kwamba, iwapo ingekiri kumchunguza waziri huyo basi sheria ingelizuia gazeti hili kuandika taarifa hizo.

Jumamosi ya wiki iliyopita, gazeti linaloheshimika nchini Uingereza, la The Guardian liliandika kuwa katika uchunguzi huo wa SFO iligundulika akaunti moja inayohusishwa na Chenge ikiwa na zaidi ya dola za Marekani milioni moja katika akaunti moja, katika Kisiwa cha Jersey.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, SFO inamchukulia Chenge kuwa mtu anayeweza akawa shahidi muhimu katika uchunguzi mzima wa zabuni ya ununuzi wa rada kutoka Kampuni ya BAE ya nchini Uingereza.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, SFO inatarajia kuanza upya kufanya uchunguzi kuhusu fedha hizo ili kuangalia iwapo zina uhusiano wowote na zile zinazoaminika kutolewa kwa njia ya rushwa wakati Tanzania iliponunua rada ya kijeshi kutoka nchini humo kwa paundi milioni 28, ambazo ni sawa na shilingi bilioni 70, mwaka 2002.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, inaaminika kwamba, uchunguzi huo wa SFO unatarajiwa kuanza katika kipindi cha wiki sita zijazo.

Kwa mujibu wa habari hizo, uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba, moja ya mambo yanayofuatiliwa ni kujua iwapo fedha hizo zinazoaminika kuwa za Waziri Chenge zilizowekwa katika akaunti moja iliyoko katika Kisiwa cha Jersey zina uhusiano wowote na zile zilizotoka katika Kampuni ya BAE System inayotuhumiwa kuinyonya Tanzania kwa kuiuzia rada hiyo kwa bei kubwa kuliko ilivyotakiwa.

The Guardian katika habari yake hiyo iliyowekwa katika mtandao wa intaneti, linaripoti kuwa, taarifa hizo zinakuja ikiwa ni miaka mitatu sasa tangu Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) kwa kushirikiana na SFO na taasisi za uchunguzi za Uswisi na Jersey zilipoanza kuchunguza kuhusu kashfa nzima ya ununuzi wa rada.

Gazeti hilo lilimkariri Waziri Chenge akikiri kwamba fedha hizo ni zake na akatumia fursa hiyo kukanusha kuwapo kwa uhusiano wowote kati ya fedha hizo na kashfa nzima ya ununuzi wa rada, uliofanywa wakati yeye akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

“Jambo la wazi linalotaka kuonekana hapa ni kwamba mimi nilipokea kwa lengo la kujinufaisha mwenyewe fedha za rushwa kutoka BAE. Huu ni uongo,” alisema Chenge.

Aidha, gazeti hilo lilimkariri Chenge akisema kuwa, wakati rada hiyo ilipokuwa ikinunuliwa yeye alihusika kwa kiwango kidogo sana katika mchakato mzima, kwani jambo hilo lilishughulikiwa na wizara nyingine na uamuzi ukaidhinishwa na Baraza la Mawaziri.

Mbali ya hilo, gazeti hilo lilimkariri mwanasheria wa Chenge anayeishi Cleveland, Ohio, nchini Marekani, J Lewis Madorsky, akikanusha kwa niaba ya mteja wake huyo, kuwapo kwa uhusiano wowote kati ya fedha zake na tuhuma zozote.

“Wakati tukitambua kuwa masuala hayo yalitokea muda mrefu uliopita, tunaweza tu tukathibitisha kuwa, tuhuma zozote za ukiukwaji wa sheria, ukiukwaji wa maadili, kutenda isivyo sawa na mambo mengine ya hivyo dhidi ya mteja wetu ni mambo ambayo kimsingi tunayakanusha kwa nguvu kubwa,” alisema mwanasheria huyo wa Chenge.

Hata hivyo, gazeti hilo liliandika kuwa uchunguzi huo dhidi ya Chenge unamfanya yeye kuwa tu shahidi muhimu, kwani wanaielenga zaidi BAE ambayo inadaiwa ilimlipa wakala mmoja wa Tanzania mamilioni ya fedha ili kujenga ushawishi wa rada iliyokuwa ikiiuza kununuliwa.

Wakala huyo ambaye amekuwa akitajwa kwa muda mrefu na ambaye sasa anaaminika kukimbia nchini na kutafutwa na polisi wa kimataifa ni, Shailesh Vithlani.

Akizungumza baada ya kurejea nchini juzi, Waziri Chenge aliwataka wananchi kuwa na subira kuhusu uchunguzi huo na kile alichokiita vijisenti ambavyo vinatakiwa kujulikana vilipatikanaje.

Alikiri kwamba tuhuma hizo dhidi yake ni nzito na zilizomshtua, na akakataa kuelezea chochote kwa undani kuhusu kuwa na fedha hizo au njia alizozipata, na iwapo kulikuwa na uhusiano wowote kati ya tuhuma hizo na kashfa ya ununuzi wa rada ya kijeshi.

Hata hivyo alisema amekuwa kiongozi serikalini kwa muda mrefu, akishika nyadhifa tofauti, akiwa ameshika nafasi ya Uanasheria Mkuu wa Serikali kwa miaka 10, hivyo fedha alizokuwa akilipwa zilikuwa halali.

“Tuhuma za ufisadi dhidi yangu ni nzito mno… inabidi nipate muda wa kukaa na kutafakari kwanza, na ukweli wa mambo utajulikana baada ya vyombo vya dola vilivyopewa kazi ya kunichunguza kumaliza kazi yake na hapo nitakuwa na muda wa kujibu,” alisema Chenge juzi.


Source: Tanzania Daima


aliyo guku oyaga gete ituja ya ntuzu!ulindoshi sana guku!i bariadi a banhu balilya milenda na bugali ubebe bilion moja ulihaya vijisenti aliyo ulindoshi sana!


Itakuwa kama Bot, EPA, mikataba , IPTL , na mengine mengi na Watanzania hatutaona ndani .NI wale wale unategemea nini ?
 
Huyu mama amedhibitisha ambacho kiliwahi kuongelewa hapa kuwa uwezo wake ni questionable, anawajibika kutoa majibi ya kulidhisha kwa Watanzania badala ya kutoa majibu kama ya chenge na baadhi ya viongozi wa CCM.
JK anakazi kubwa maana yeye mwenyewe anaonekana hafai sasa na mawaziri wake nao wameanza kuchemsha.
 
Are these really prudent Tanzanian leaders?
Kwa nini waseme hizi ni habari walizosikia kwenye magazeti na kunyamaza kimya wala wasiwapatie wananchi majibu yanayohusu pesa yao??.

Basi upo mfumo mbovu sana wa utendaji ktk serikali,tena wa kuogopana na kulindana katika maovu,hatima yake ni kufuga bomu ambalo itafikia mda litalipuka.

Namuuliza mheshimiwa Waziri na mkurugenzi wa makosa ya jinai,ina maana hayo magazeti yamezusha??Basi yafungieni,yasitolewe tena maana yanapotosha umma wa Watanzania kwa habari ambazo ni uzushi na zinazoweza kuhatarisha amani na usalama wa Taifa hili.

Na hizi habari kama ni kweli basi hamjui mlitendalo ni vema mkae kimya kama kawaida yenu na kutumia ile falsafa ya mimi si msemaji wa hili na lile,kuliko kujichafua kwa kitu ambacho ni dhahiri.

Naililia Tanzania yangu maana hatima yake siijui.

Hawa jamaa ni wasanii na wamekaa kulindana tu - hawastahili kuitwa viongozi bali MAFISADI. Ati habari wamezisikia katika gazeti hawawezi kuzichuklia hatua - mangapi wanayasikia na wanachukua hatua haraka na kama ni challenge hebu iandikwe katika gazeti kama wananchi wanataka kufanya maandamano kupinga ufisadi wao uone nini kitatokea.

Wanatufanya wajinga - sasa inabidi kutubadili mikakati kwani kusema tumesema hadi koo zimekauka.
 
JK alishawaambia kwamba ikidhihirika kwamba BAE waliiuzia Tanzania Radar kwa bei mbaya, yeye ataomba arudishiwe hela zilizozidi. Sikutegemea kusikia kauli kama hiyo kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliye makini na ana dhamira ya kupambana na rushwa na ufisadi.

Nilitarajia kwamba angesema PCCB kwa kushirikiana na Idara nyingine Polisi na TISS watachunguza ili kuona kama kulikuwa na rushwa. Maajabu ni kwamba yeye alinawa mikono na kuwaachia SFO wachunguze na wakithibitisha yeye ndiyo adai change, what a joke!

Yaani watu ambao siyo hela yao wakufanyie uchunguzi wewe wakati unaendelea kuwakumbatia walioshiriki kwenye hayo manunuzi na huwachunguzi ili kujua kama kweli kuna harufu ya rushwa ama hakuna, kweli Tanzania tuna Rais ambaye hajapata kutokea.

Kwa hiyo alichofanya Mama Sofia Simba ilikuwa ni kuongea along the lines za Boss wake (JK). Kwa hiyo Mchungaji Kishoka yuko sahihi kabisa kwamba hatuna serikali.

Kama Boss anacheza karata kwenye PC kila siku unategemea walio chini yake watafanya nini? Majibu ya Waziri Simba ni reflection ya msimamo wa serikali nzima kuanzia kwa JK na hasa nikirejea kauli ya kusema atakuja kudai chenji.

The whole government is not serious, tunahitaji kuwa na watu serious kuanzia Ikulu mpaka ngazi za chini. Kama Mkuu wa Kaya akiwa serious na kazi hakuna watu watacheza makida makida huko kwenye wizara na hata kwenye idara za serikali na taasisi/mashirika ya umma.
 
Yaani hii serikali kwa kweli sijui inatakiwa iwajibike kwa nani. Ni upuuzi mtu Waziri mzima unapojibu eti "SFO walikuja kuomba mafaili ya Chenge na kuondoka nayo na serikali inasubiri uchunguzi" Grrrrrrrrrrrrrrriii....... Mie sipingi dhana ya uchunguzi lakini ina maana serikali ilitoa original files za Chenge bila kubaki na KOPI?????????? Ina maana kama hizo faili zikipotea au kurasa zikanyofoka na kupotea kwa bahati mbaya basi habari za Chenge ndo zimepotea kabisa. Mmmh inachekesha sana, pamoja na teknolojia yetu nyembamba Bongo lakini serikali haijawa na uwezo wa kuwa na HARD DRIVES (I don't buy Hon. Simba's response)
Nyie mnaona bora kuwaficha watanzania waliowapa hiyo dhamana na kuficha utumbo wenu. The day is coming.......not too far. Everyone needs to come out and clean to be counted, I SAID IT, YES NOW.
 
...mambo ya ajabu kabisa,lakini people deserve leaders they elect,acha wapiga kura wapate walichochagua,inasikitisha sana lakini wa kulaumu ni hao wapiga kura na sijui kwa nini nione huruma,ni kweli napenda nchi yangu na ningefanya chochote kusaidia lakini kwa mwendo wa huu wa CCM kushinda kila uchaguzi sina la kusema.
 
...huu ni usenge wa hali ya juu,lakini people deserve leaders they elect,acha wapiga kura wapate walichochagua,inasikitisha sana lakini wa kulaumu ni hao wapiga kura na sijui kwa nini nione huruma,ni kweli napenda nchi yangu na ningefanya chochote kusaidia lakini kwa mwendo wa huu wa CCM kushinda kila uchaguzi sina la kusema.

naona watakupasua kichwa mkuu !
 
My final conclusion ni kuwa, hiki chama CCM - CHAMA CHA MAJANGILI. Hawa viongozi hewa wamezidi kuihujumu nchi kwa nguvu mpya, ari mpya na kasi mpya. They need to tell UMMA wa Watanzania the truth and give back all the money they stole from the people.
 
Tume ya maadili na viogozi iko wapi? wanajaribu kufanya mazingaombwe gani? Ni tume ya Kuwaamsha viongozi warudi kwenye ASILI yao, maadili ya utu, utu katika uongozi! Ni tume ya kuwakumbusha kila mara viongozi wapi wameukana utu ndani ya uogozi wao! Viogozi wetu wanahitaji kukarabatiwa upya kabisa. Lakini sasa hawa wa utawala bora nao ndio hawa ...what a bad news? Tunakwenda wapi? Basi hawa wa "maadili ya uongozi" wako wapi?

Hii tume sijui Sekretarieti ipo tu kwa kumyonya Mtanzania. Shughuli hasa ni nini????? Yaani natamani nimuume mtu sikio maana hawasikii hawa. Juzi haoa tumeambiwa na Mh. Marmo tena ndani ya Bunge kuwa Hakuna kiongozi yeyote ambaye akutwa na makosa by hiyo sekretarieti. Baada ya siku 3 tunasikia haya ya Chenge. Kwa maana hiyo huyo Marmo kwa niaba ya serikali kalidanganya Bunge na wananchi wote. Cha ajabu Kiongozi huyo sijasikia akiomba SAMAHANI mbele ya chombo alichotumia kuwadanga watanzania. So what next??????? Hii Sekretarieti ivunjwe na Marmo aachie ngazi maana ni yeye ndiye alikuwa na dhamana katika hiyo sekretarieti kwenye baraza la kwanza la Mawaziri wa JK. Yeye anajua kabisa kuwa kuna baadhi ya viongozi walidanganya kuhusu mali zao na still wakadanganya Bunge.
Kuna mtu anatakiwa kuwajibika.
 
Mi nadhani hapa ni lazima turudi nyuma kidogo na kujiuliza kwa nini tunashangaa kwamba serikali hatuna - yaani kwamba mawaziri na watendaji wakuu ni useless. I think it is essential kwamba tuangalie kwanza nani amewaweka katika nafasi yao?

Mawaziri wote ni wabunge waliopigiwa kura na wananchi wa majimbo yao. Swali: kwa nini watanzania tunateua viongozi kama hao? Maana mawaziri kama hawa hawastahili hata kuwa wabunge! Alfu tuje kwa mtendaji mkuu, na yeye amepigiwa kura na wananchi. Hata ubunge haumfai!

So the system of selecting viongozi ni MBOVU! After that I can only say, until politics become truly free and fair with level playing field, hatutakuwa na uongozi imara! And believe me it is getting worse as we progress!
Jamani 2010 tufanye kweli! Iwe ABC Anyone But CCM!
 
Poor Tanzania. wanamsubiri Kikwete aseme ndio wapate msimamo na wao. Natamani kama angelikuwa Nyerere wakati huu.

Hivi hakuna uwezekano wa kuajiri shirika kama SFO kukomboa fedha zetu zilizoko kwenye mabenki ya nje kutoka kwa mawaziri wote wa awamu ya tatu; including Mkapa?
 
Serikali ipo!Labda kielezwe serikali iliyopo madarakani ni serikali ya aina gani!serikali hakuna Sonalia.Tanzania ina serikali ina Jeshi ni dola kamili.
Kama hakuna serikali basi mmoja wenu aende Ikulu aingie kama atakavyo aone kiatacho msibu!Aende polisi atukane polisi aone!aene kushini atukane!Mijitu mingine ipo hapa JF imekuwa ipo huru kuandika watakacho wamefikia hatua ya kusema hakuna serikali kwani nchi inatawalia na nani?
Kama yapo mapungufu katika serikali hilo linazungumzwa basi waziujuzullu serikali nzima nyie mlioko hapo JF mujipange mje mtawale!
 
Kwa mtu mwenye busara ukishaona mambo yanaenda kombo unastep down.
Kwa mwendo huu hawa CCM naona ata iyo 2010 ni mbali waitishe referendum wajijue wako ktk hali gani.
Namsuport Steve D unaweza ukana utaifa wako kwa upumbavu unaoendelea.
 
Naomba kujua hivi JK mna hakika huwa anasoma hizi comments za humu????

Mkuu Tuandamane ni vigumu kujua kama JK anasoma hizi threads au sivyo, otherwise uwe Mnikulu au wale wa usalama.

Hata hivyo najua anapata taarifa juu ya mambo muhimu yanayojadiliwa kila siku katika vyombo vya habari. Alishalisema hili katika hotuba yake moja kwamba anafuatilia habari na Serikali yake inawasikiliza wananchi.
 
Itakuwa kama Bot, EPA, mikataba , IPTL , na mengine mengi na Watanzania hatutaona ndani .NI wale wale unategemea nini ?

Hata kama lakini sasa hivi tumeamka wao wanadhani sisi tumelala kumbe wao ndio waliolala. Bora wanunue silaha mapema kabla ya uchaguzi wasije fanya kama zimbabwe maana 2010 wakichukua wakiweka waaa patakuwa hapatoshi, patachimbika.
 
Serikali ipo!Labda kielezwe serikali iliyopo madarakani ni serikali ya aina gani!serikali hakuna Sonalia.Tanzania ina serikali ina Jeshi ni dola kamili.
Kama hakuna serikali basi mmoja wenu aende Ikulu aingie kama atakavyo aone kiatacho msibu!Aende polisi atukane polisi aone!aene kushini atukane!Mijitu mingine ipo hapa JF imekuwa ipo huru kuandika watakacho wamefikia hatua ya kusema hakuna serikali kwani nchi inatawalia na nani?
Kama yapo mapungufu katika serikali hilo linazungumzwa basi waziujuzullu serikali nzima nyie mlioko hapo JF mujipange mje mtawale!

Taratibu mkuu,
kama hipo mbona hatuioni au unafikiri kusikia majina inatosha, lazima waact wakati unapoitajika, au wanasubiri wafadhili wagome kwanza ndo na serikali yetu itaact juu ya maswala mbalimbali yanyoisumbua nchi sasa.
Comment za Waziri Sofia umeziona lakini, au umesema chungulia comment kwanza wenzio wote wamekaa kuimya.
 
Just imagine that Mheshimiwa Simba or Kikwete are being confroted by a BBC, CNN, Economist, Business Weekly, Financial Times, Wall Street Journal, The Herald, New York Times and even East African are at press conefernce and the QA session goes like this.

Q. Mr. President, you country is being accused of purchasing an over priced radar equipment that covers just a third of your country and it is being speculated that your then attorney general Mr. Chenge was recipient of a commision to facilitate the purchase, what is your government stand on this?

A. Our government has not started its own investigation on this matter, we are waiting for the British government investigations to be completed, then we will take action. We have submited our formal complain with British government demanding a refund for over pricing of the radar. BAE has to refund our money, it is unfair they sold us an over priced radar.

Q. Mr. President, it is being alleged that you government ignored the plea from some members of British Government and donor countries that advised your country not to purchase this radar..

A. We needed the radar after 9/11 to secure ourselves againts threats and air collision of two jumbo jets! We have right as a sovereign nation to decide what we want!

Q. Mr. President, it has now been discovered that Mr. Change has more than $6 million in offshore accounts all over the world, is this possible for a person who has worked in your country in government to have such vast amount of money?

A. As I have stated before, SFO came asking about Chenge and we gave them a file. I am surprised just like you that Chenge has such amount of money. However we are going to wait for SFO and British government findings before we start our investigations.

Q. Did your government start its own investigation after SFO inquired about Chenge? Didn't that sound odd to you that your cabinet member is being investigated by SFO and British government on corruptions charges?

A. SFO came and ask for the file and we gave them permision to do its investigations so that we could get our refund back!

Q. Is your government going to seize and freeze Mr. Chenge's accounts and fully investigate him and his role not only on the Radar issue but so is IPTL and current BOT scandal of dubious government company Meremeta?

A. Ehh, we will wait for the British to complete their investigations and if it is seem fit, then we will start our own investigations. Let me say this, our government has just read these allegations in newspapers and until we have sufficient evidence, from the British and SFO, then we will start our internal investigation.

Imagine the embarrasment of identifying yourself to a British or American that you are from Tanzania!
 
Back
Top Bottom