A
Anonymous
Guest
- Thread starter
- #1
Hali ya sintofahamu imezidi kutanda ndani ya Halmashauri ya Mpimbwe mkoani Katavi baada ya aliyekuwa DMO kutajwa kuhamishwa ghafla kutoka Halmashauri ya Mpimbwe kufuatia tuhuma nzito za ukusanyaji wa fedha za vituo vya kutolea huduma za afya zinazodaiwa kufikia zaidi ya shilingi milioni 60, ambapo fedha hizo alidai ameagizwa na Mkurugenzi kwa ajili ya matumizi ya ujio wa Mwenge tarehe 27/09/2025, jambo ambalo si kweli.
Kwa mujibu wa taarifa zinazozunguka miongoni mwa watumishi wa halmashauri hiyo, fedha hizo zinadaiwa kukusanywa kwa utaratibu wenye utata.
Kila incharge wa kituo ambacho kina mapato makubwa alipewa maelekezo ya kutoa pesa mbichi nje ya mfumo, huku kazi ya ukusanyaji akipewa mtumishi mwingine ambaye fedha hizo zinadaiwa kuwekwa kwenye akaunti binafsi inayohusishwa na mke wa mtumishi huyo.
Kinachozua maswali makubwa kwa watumishi ni hatua ya mamlaka kuishia kumhamisha mtuhumiwa mkuu wakati uchunguzi wa vyombo mbalimbali, ukiwemo wa TAKUKURU, ulidaiwa kuanza kufanyika kabla ya hatua hiyo ya uhamisho.
TAKUKURU walishafika na kuhoji watumishi wote waliohusika katika kupokea maelekezo ya kutoa pesa hizo, na kuna watumishi walikiri kuingiziwa pesa na kuombwa zirudishwe na DMO huyo.
Watumishi wengi sasa wanahoji:
1. Je, kuhamishwa ndio adhabu mpya ya matumizi mabaya ya fedha za umma?
Wengine wanaamini kuwa uhamisho huo wa haraka unaweza kuwa njia ya kuzima mjadala huku ukweli wa tuhuma hizo ukiachwa gizani bila majibu rasmi.
Chanzo kimoja kutoka ndani ya halmashauri, ambacho hakikutaka kutajwa jina kwa sababu za kiusalama, kilidai kuwa timu mbalimbali zilifika kufanya uchunguzi kuhusu mwenendo wa fedha hizo, jambo linaloongeza uzito wa tuhuma zinazomkabili kiongozi huyo wa zamani wa afya wilayani humo.
Pamoja na hayo, hadi sasa hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kueleza:
1. Nani anawajibika kati ya DMO au mtumishi aliyeagizwa na DMO?
2. Kwa nini akaunti binafsi ya mke wa mtumishi ilitumika?
3. Na kama uchunguzi ulikuwa unaendelea, kwa nini mtuhumiwa ahamishwe kabla ya kesi kukamilika?
Suala hili linaendelea kuzua mjadala mkubwa huku macho yakielekezwa kwa mamlaka za uchunguzi kuona kama haki itatendeka au sakata hilo litamalizwa kimya kimya kwa uhamisho wa kawaida.
Pia soma:
1. DOKEZO - Inawezekanaje Mganga Mkuu wa Halmashauri Mpimbwe Mwenye Tuhuma za Wizi wa Fedha Ahamishwe Kabla Uchunguzi Kukamilika, Au Ni Njia ya Kumlinda?
2. KERO - Halmashauri ya Mpimbwe inawatesa Wazabuni kwa kutolipa madeni
UPDATE: :
Kwa mujibu wa taarifa zinazozunguka miongoni mwa watumishi wa halmashauri hiyo, fedha hizo zinadaiwa kukusanywa kwa utaratibu wenye utata.
Kila incharge wa kituo ambacho kina mapato makubwa alipewa maelekezo ya kutoa pesa mbichi nje ya mfumo, huku kazi ya ukusanyaji akipewa mtumishi mwingine ambaye fedha hizo zinadaiwa kuwekwa kwenye akaunti binafsi inayohusishwa na mke wa mtumishi huyo.
Kinachozua maswali makubwa kwa watumishi ni hatua ya mamlaka kuishia kumhamisha mtuhumiwa mkuu wakati uchunguzi wa vyombo mbalimbali, ukiwemo wa TAKUKURU, ulidaiwa kuanza kufanyika kabla ya hatua hiyo ya uhamisho.
TAKUKURU walishafika na kuhoji watumishi wote waliohusika katika kupokea maelekezo ya kutoa pesa hizo, na kuna watumishi walikiri kuingiziwa pesa na kuombwa zirudishwe na DMO huyo.
Watumishi wengi sasa wanahoji:
1. Je, kuhamishwa ndio adhabu mpya ya matumizi mabaya ya fedha za umma?
Wengine wanaamini kuwa uhamisho huo wa haraka unaweza kuwa njia ya kuzima mjadala huku ukweli wa tuhuma hizo ukiachwa gizani bila majibu rasmi.
Chanzo kimoja kutoka ndani ya halmashauri, ambacho hakikutaka kutajwa jina kwa sababu za kiusalama, kilidai kuwa timu mbalimbali zilifika kufanya uchunguzi kuhusu mwenendo wa fedha hizo, jambo linaloongeza uzito wa tuhuma zinazomkabili kiongozi huyo wa zamani wa afya wilayani humo.
Pamoja na hayo, hadi sasa hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kueleza:
1. Nani anawajibika kati ya DMO au mtumishi aliyeagizwa na DMO?
2. Kwa nini akaunti binafsi ya mke wa mtumishi ilitumika?
3. Na kama uchunguzi ulikuwa unaendelea, kwa nini mtuhumiwa ahamishwe kabla ya kesi kukamilika?
Suala hili linaendelea kuzua mjadala mkubwa huku macho yakielekezwa kwa mamlaka za uchunguzi kuona kama haki itatendeka au sakata hilo litamalizwa kimya kimya kwa uhamisho wa kawaida.
Pia soma:
1. DOKEZO - Inawezekanaje Mganga Mkuu wa Halmashauri Mpimbwe Mwenye Tuhuma za Wizi wa Fedha Ahamishwe Kabla Uchunguzi Kukamilika, Au Ni Njia ya Kumlinda?
2. KERO - Halmashauri ya Mpimbwe inawatesa Wazabuni kwa kutolipa madeni
UPDATE: :
Nawapongeza TAKUKURU Wilaya ya Mlele halmashaur ya Mpimbwe kwa kazi kubwa wanayoendelea kuifanya katika kuchunguza tuhuma mbalimbali za ubadhirifu na matumizi mabaya ya rasilimali za umma katika Idara ya Afya.
Hatua zilizochukuliwa dhidi ya aliyekuwa DMO wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe na sasa ni DMO Halmashauri ya mji Nanyamba, Dkt. Mahmoud, zinaonesha kuwa hakuna aliye juu ya sheria na kwamba taasisi zetu zinaendelea kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria.
Watumishi wengi wamefurahi kuona kuwa angalau kwa kiwango fulani haki inaanza kutendeka na kwamba malalamiko na tuhuma...
Hatua zilizochukuliwa dhidi ya aliyekuwa DMO wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe na sasa ni DMO Halmashauri ya mji Nanyamba, Dkt. Mahmoud, zinaonesha kuwa hakuna aliye juu ya sheria na kwamba taasisi zetu zinaendelea kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria.
Watumishi wengi wamefurahi kuona kuwa angalau kwa kiwango fulani haki inaanza kutendeka na kwamba malalamiko na tuhuma...
- Anonymous
- kufuata kusimamia mpimbwe pongezi sheria takukuru uwajibikaji wake
- Replies: 1
- Forum: Jukwaa la Siasa