Jamaa yangu ananitesa kisa alinitafutia kazi, ni haki?

Nipo private sector pia nazungumza namna utaratibu inavyotakiwa kuwa, kama wasipoufuata ndio hapo Sasa ujue haki zako na wajibu wako, hakuna wakukupeleka kizembe. Lakini kama huwezi kubeba majukumu yako utaogopa watu nakuwanyenyekea sehem ambapo wao ilitakiwa ndio wakunyenyekee.
Hapo Sasa Ili kutimiza wajibu na haki yako,inabidi ujifunge kibwebwe maana unaenda kupambana na maboss zako!

Huo ubavu unao?

Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
 
Si haki, chukua shillingi elfu 50 mwambie kaka asantee Kwa mchango wako sina kikubwa chakukupa lakini hiki kinatosha. Kisha baada yahapo mkatae, kwani lazima utoke nae out?. Akikuambia mtoke ukamuambia hauko vizuri kifedha atakulazimisha?.

Jifunze kusema hapana.
Nadhani uzi uishie hapa msimamo ndio swala la msingi
 
Hapo Sasa Ili kutimiza wajibu na haki yako,inabidi ujifunge kibwebwe maana unaenda kupambana na maboss zako!

Huo ubavu unao?

Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
Pia hakuna boss anaetaka kumfukuza mfanyakazi anaemletea faida. Ndio maana nikasema kama Jamaa anayabeba majukumu yake vizuri basi aondoe hofu amwambie ukweli jamaa. Lakini kama mpaka kwenye kazi haziwezi basi acha aendelee kutumia.
 
Paying the goodwill has known no end. Bila huyo jamaa usingekuwa na hii mada. Sisi wengine mbona tunaendelea kulipa fadhila kwa miaka sasa ingawa si kwa pesa ya kila mwezi. Ila siku ukijipata unamkumbuka mtu aliyekufanya uwe hapo ulipo.
Onesha ukomavu wa maisha.
shida ni kwamba mwamba anataka kumfanya jamaa kiraka kisa kampa conneee
 
Siku moja umnunulie bia za kutosha ili Kila mara umkumbushie kwamba bila wewe, yeye asingepata bia za kutosha itabidi na yeye akushukuru pia
 
Paying the goodwill has known no end. Bila huyo jamaa usingekuwa na hii mada. Sisi wengine mbona tunaendelea kulipa fadhila kwa miaka sasa ingawa si kwa pesa ya kila mwezi. Ila siku ukijipata unamkumbuka mtu aliyekufanya uwe hapo ulipo.
Onesha ukomavu wa maisha.
Ila sio kila mkitoka uwe unamaliza shida zake na huyo aliekutoa sio kujitapa kila mahali japo tunatofautiana ila kila mtu kujua umemsaidia fulani sidhani kama ni kitu poa bora upige kimya akikusahau unakausha
 
Siku moja umnunulie bia za kutosha ili Kila mara umkumbushie kwamba bila wewe, yeye asingepata bia za kutosha itabidi na yeye akushukuru pia
Ah nikajua amnunulie beer nyingi akilewa akamfi&e kumbe kumkumbusha na yeye ashukuru dah
 
Kila mwezi Vipi punguza utoto.

Thanks unampa mtu mara moja imetoka, sidhani mtu mwenye akili timamu eti akutegemee wewe kisa amekuconnect kazi.

Kitendo cha wewe kumpa Thanks 30,000/= tayari inaonesha wewe ni mtu wa hovyo tu.

Hiyo amount tunapeana hapa JF bila kujuwana.
Hata mimi nimefikilia hiki kitu, hapo ungempa 500000/= unaachana nae, siku wamekutimua hapo uanze kumsumbua akutafutie kazi
 
Wasalaam,

Nilikuwa down bad, yaani nimepigika kinoma, yaani apeche alolo, yaani mbombo ngafu, yaani moja haikai mbili haikai, Yani nmechina mweupe pee. Kula ya mashaka, kulala kama ndege. Ila Kuna huyu jamaa angu tulisoma ote Olevel akaniconnect kwenye ajira inalipa fresh sio haba.

Sasa tatizo, imekuwa kama kero, Kila siku anajimwambafy kuwa bila yeye nsingetoboa anasema natakiwa niwe namshukuru kila mshahara ukitoka. Tukienda out Kila siku

Mimi tu ndo anataka nimnunulie bia. Wote tuna mshahara ila yeye anataka na shida zake Mimi nimtatulie.

Mimi naona imekuwa kama manyanyaso sasa.

Nifanyaje?
Wasalaam,

Nilikuwa down bad, yaani nimepigika kinoma, yaani apeche alolo, yaani mbombo ngafu, yaani moja haikai mbili haikai, Yani nmechina mweupe pee. Kula ya mashaka, kulala kama ndege. Ila Kuna huyu jamaa angu tulisoma ote Olevel akaniconnect kwenye ajira inalipa fresh sio haba.

Sasa tatizo, imekuwa kama kero, Kila siku anajimwambafy kuwa bila yeye nsingetoboa anasema natakiwa niwe namshukuru kila mshahara ukitoka. Tukienda out Kila siku Mimi tu ndo anataka nimnunulie bia. Wote tuna mshahara ila yeye anataka na shida zake Mimi nimtatulie.

Mimi naona imekuwa kama manyanyaso sasa.

Nifanyaje?
Sio haki ushaur anza kumkataa kisiasa mkiwa mnatoka out wewe usitoke mwambie kaka sipo freshi kimwili na kifedha now kuna majukumu nimejipa kuna deni nalilipa nilikopa kwa ajili ya kumkwamua mdogo wangu yupo mkoa anasoma na wazee walibanana naomba nitulie tu hadi takapomaliza
 
Back
Top Bottom