William ni mmoja wa Watanzania waliobahatika kuona sehemu tofauti na Tanzania ingawa sina uhakika kama exposure hiyo inamsaidia.
Ni mtoto wa Mzee Malecela aliyeshika nyadhifa nyingi serikalini ikiwa ni pamoja na uwaziri wa mambo ya nje,uwaziri mkuu na makamu wa kwanza wa Rais na mgombea mtarajiwa wa Urais CCM mara mbili
Nashawishika kusema William ana mtukana mzee wake kwa sababu za kuthibitika kutokana na maandishi yake
Si kawaida kumjibu kwa kutambua ufinyu na maono yake, ninachotaka kufanya ni jamvi kumuelewa na kuelewa upotoshaji na matusi kwa wazee akiwemo baba yake.
Hoja ya serikali 3 ilianza siku nyingi na kundi la G55 liliifikisha bungeni.
Kundi hili lilikuwa na wabunge 55 wa chama tawala CCM kilichokuwa na wabunge zaidi ya 200.
Kiongozi wa serikali bungeni alikuwa baba yake william mzee J.S.Malecela.
Hoja ya G55 ilikataliwa na Nyerere kwasababu kuu mbili, kwanza haikuwa sera ya CCM na haiwezi kufanyika bila wananchi kuulizwa. Nyerere alitambua kuwa kubadili katiba ilihitaji ridhaa ya wananchi na si CCM.
Nyerere alimtuhumu Malecala kwa kumshauri rais vibaya.
William anaposema sera ya CCM ni serikali 2, wakati baba yake ambaye ni mwanzilishi wa CCM alitaka serikali 3 Kupitia idadi ya wabunge 55 kama ambavyo wapo 47 wa upinzani sasa ni kutoelewa anaongelea nini.
Hapa William hamtukani Warioba anamtukana baba yake mzazi. Hii kama si laana sijui ni nini.
William na kofia ya degree na kuishi nje ya nchi hajui kuwa katiba si ya chama ni ya wananchi.
Hatambui kuwa katiba haina chama kwasababu vyama vinapita katiba inabaki.
KANU na UNIP hazipo tena lakini Kenya na Zambia zipo.
Sasa kuaminisha kuwa CCM ndio wanaandika katiba, inasikitisha sana!!
Aasema wabunge wa CCM wana haki ya kuandika katiba. Hilo tu linaonyesha jinsi asivyojua katiba ni kitu gani. Lakini pia hajui hata sera za chama chake.
CCM haina sera wala haikuwa na ilani ya kuandika katiba.Hakuna kikao chochote kiwe cha NEC, CC au kamati ya wabunge kilichojadili suala la katiba.'Haki ya kuandika katiba'' wanaipata wapi?
Willy, CCM kupitia tume ya Jaji Nyalali, Kisanga na Warioba zimeshawahi kuleta maoni ya serikali 3.
Hakuna mahali katika rekodi CCM imewakemea kwa hilo. Warioba kama baba yako Malecela ndio wenye chama na wanaijua nchi kabla hujazaliwa. Kuwatukana wakiwemo akina Kisanga, Nyalali n.k. ni laana, ungama sasa hivi.
Willy, anasema kazi ya tume ya Warioba ni kukusanya maoni. Tume ya Warioba si makarani ni watu wenye weledi wa kueleza watu nini maana ya katiba ili watoe mawazo kulingana na hadidu za rejea.
Hadidu za rejea wamepewa na JK ambaye ni mwenyekiti wa CCM, kumtukana Warioba ni kumtukana JK, laana hiyo!
Willy anasema Warioba asiandike katiba aachie wananchi. Wakati huo huo haelezi wapi Warioba amelazimisha mawazo yake. Amesahau kuwa mawazo ya wananchi aliyokusanya Warioba ndiyo yale ya G55 ambayo baba yake alisimama Kidete kutetea akiwa na CCM ya wabunge 55.
Vipi amtukane baba yake kupitia Warioba kama si laana.
Williama na Bulembo hawaelezi wapi Warioba na tume yake wamelazimisha mawazo yao.
Wanasema wananchi wamekataa maoni ya Warioba, hawaelezi ni kigezo gani kimetumika kusema wananchi 'wamekataa' hata kabla ya kura ya maoni achilia mbali bunge la katiba.
Willy anasema kazi ya Warioba imekwisha kilichofikishwa bungeni mswada.
Mungu wangu! huyu ni kiongozi ambaye hajui kuwa kilichofikishwa si mswada wa rasimu ni marekebisho ya mswada ambao ulianzisha tume ya Warioba. Hajui kipi kimeanza kipi kinafuta na kitamalizika kipi. jamani!
Anasema wabunge wa CCM wanapaswa kuandika katiba, aibu kubwa!
wabunge wapi kwasababu hiyo si kazi ya chama na hata hao wabunge hawajui ni kitu gani kwasababu haipo katika ilani yao wala sera, sijui kama Willya anajua anachoandika.
Nia si kumjibu kwasababu hana hoja, ninachotaka Wanajamvi wafahamu ni kuwa huyu ipo siku utamsikia ni mjumbe wa NEC au CC. Unaweza kumsikia ni waziri, balozi wetu nchi za nje au mwenyekiti wa bodi ilimradi tu anaweza kuwa sehemu ya maamuzi yanayowahusu Watanzania.
Kwa mtu asiyejua kwanini Tanzania ni masikini basi ajiulize tena.