J. Samwel Malecela ni mgonjwa

J. Samwel Malecela ni mgonjwa

Pole sana Mzee JSM.........tunakuombea ili upone haraka........Familia ya Mzee........Its going to be fine.......tupo pamoja sana......
 
Pole sana Mzee Mungu akuponye .Ukisha pona uje kuwasumbua watanzania kuwaongezea umasikini kwa jina la CCM . Sitasahau maneno ya huyu mzee kwa kweli . Mungu ampe afya njema in Jesus name.

Mkulu Lunyungu,
Ninafurahi kuona kuwa sasa unaandika tena hapa JF..........ulikuw aunaumwa....wana JF tulikuombea na tunazidi kukuombea.....pamoja na tofauti zetu za kimitizamo......tunaendelea kukuombea..........naona ume-recover vyema kabisa.........Mungu Mkubwa na Tumshukuru sana.........
......Vivyo hivyo kwa Mzee wetu JSM.......tumtakie kheri ya afya njema.........
 
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"]Malecela azungumzia afya yake
[/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"] Send to a friend
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"] Wednesday, 22 June 2011 21:40
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]digg

Boniface Meena
MWANASIASA mkongwe na kada maarufu wa CCM, John Malecela, amezungumzia afya yake kutokea nchini Uingereza, akieleza kuwa inaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo katika Hospitali ya Wellington North nchini humo.

Hata hivyo, taarifa za kitaalamu zilizolifikia gazeti hili zinaonyesha kuwa Malecela alipata tatizo la kuvimba kwa mishipa inayotoa damu moyoni kwenda mwilini na kusababisha mtiririko wa damu kuyumba kwa kiasi.

Taarifa zilisema kutokana na hali hiyo, njia pekee ya kuondoa tatizo hilo ilikuwa kumfanyia upasuaji mkubwa wa moyo ambapo madaktari walilazimika pia kuchukua mishipa kutoka katika mguu wake na kuweka kwenye moyo wake.

Lakini jana, Malecela mwenyewe aliyezungumza na Mwananchi kutoka Uingereza alikolazwa baada ya kufanyiwa upasuaji huo, alisema kuwa madaktari wamemshauri afanye mazoezi kwa muda wa wiki tatu hadi sita ili waangalie hali yake na baada ya hapo wataweza kumpa ruhusu ya kurudi nchini.

"Ninaendelea vizuri na madaktari wameniambia nifanye mazoezi kwa muda wa wiki tatu hadi sita kuiangalia hali ikoje ili waweze kunipa certificate (cheti) ya kuweza kurudi nyumbani,"alisema Malecela.
.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Mpiganaji ..tuko PAMOJA tena PAMOJA saana kwenye hili Mkuu .......Mungu awabariki !!!
 
One of the genious leaders. Lakini Tanzania kama tuijuavyo, ukizaliwa genius ' it is a bad news'. They will hunt you, attack you, lie about you, destroy you and what have you....

All in all, may you get well soon mzee wetu, a true hero of our land.

I know things from the truth not from corrupted ccmanic media.
 
umri aliofikisha unamtosha sana hata akifa hakuna hasara kwa taifa coz ni mzigo toka zamani
du kumbe hata humu JF kuna vichaa,kweli mtu mwenye akili timamu unaweza kumuombea binaadamu mwenzako kifo?huyu mzee kakufanya nini mpaka umuombee kifo au wewe umekuwa jiwe ,kumbuka ndugu wote tu wapita njia na marehemu watarajiwa,tunapishana tu kupata mauti,kila mtu ikifika zamu yake ataaicha dunia,kwa utamaduni wa kitanzania hatujafikia katika hayo unayofikiria,wasiwasi wangu wewe huenda umezaliwa miaka ya 2000 ndio maana huujui mchango wa Mzee Malecela katika nchi hii,na kama hujui Mzee Malecela ni moja ya watu wanaokufanya uandike na utoe maneno yasio na busara hapa JF,kwani ndio viongozi wa mwanzo wasaidizi wa Mwl J.K Nyerere ambao wameifanya Tanzania iwe nchi yenye misingi imara ya umoja,upendo n.k. namalizia kwa kusema kwa mila na desturi za kiafrika tunatakiwa tuwaheshimu walio tuzidi umri,na mwisho wewe ambaye ni kijana je una faida gani kwenye taifa hili,tujaribu kuwa waungwana na tuone aibu kwa maneno ya sio na busara
 
... ndio maana huujui mchango wa Mzee Malecela katika nchi hii,na kama hujui Mzee Malecela ni moja ya watu wanaokufanya uandike na utoe maneno yasio na busara hapa JF,kwani ndio viongozi wa mwanzo wasaidizi wa Mwl J.K Nyerere ambao wameifanya Tanzania iwe nchi yenye misingi imara ya umoja,upendo n.k.
Hii ni opinion yako wewe kuhusu Malecela. Legacy ya Malecela ni "go to hell" statement aliyowaambia wananchi akiwa kiongozi. Sio kila mtu anadhani Malecela ana mchango mkubwa kwa nchi hii.
 
Malecelamzee.jpg
 
Samahani kama nitakuwa nimewaudhi, kwa nini hawa wanasiasa wetu hawatibiwi Muhimbili au Mwanayamala kama sisi wengine?
 
Arigold: Let us use common sence and let us not critisize everything.
1. Heart surgery is one of the complicated operations and can not be handled in a centre like mwananyamala
2. THis guy serverd this nation in the high post (PM) and he deserver this service ( I assume he enjoy govt benefits)
3.Ningeshangaa kama serikali ingeshindwa kuwahudumia watumishi/viongozi wa kitaifa wakiwa ktk hali mbaya kiafya
 
Mwananyamala wanafanya operation ya moyo? Clear your mind.

Ametaja Mwananyamala au Muhimbili...Mwananyamala hawafanyi operation ya moyo, Muhimbili wanafanya zaidi ya mwaka sasa na matokeo ni mazuri tu, kwa nini hakwenda hapo?
 
Ametaja Mwananyamala au Muhimbili...Mwananyamala hawafanyi operation ya moyo, Muhimbili wanafanya zaidi ya mwaka sasa na matokeo ni mazuri tu, kwa nini hakwenda hapo?
Dunia ya sasa ni vigumu sana kumchagulia mtu sehemu anayohitaji kupata huduma. Huu ni ulimwengu wa kibepari, mteja anafuata panapomfaa. Pamoja na hayo Mh. Malecela ni mmoja wa mawaziri wakuu wastaafu, nadhani ana stahili anazopokea ambazo zinamwezesha kutibiwa nje
 
Hizo hospitali za Mwananyamala na Mhimbili ni za wazawa.
 
Mwananyamala hawafanyi upauaji wa moyo; Muhimbili bado wapo kwenye majaribio! Kufanay upasuaji (ambao siyo complicated) kwa miaka miwili tu hakutoshi kuifanya hospitali ya Muhimbili kuwa "qualified" kumtibu Retired PM, Makamu wa Mwenyekiti wa Ruling Party, etc

Si Malecela tu, mbona watanzania wengi kil amwaka wanapelekwa India kwa ajili ya upasuaji wa moyo? tena hawa ni watanzania wa kawaida tu, na wanakwenda kwa gharama za serikali, mbona hujalalamikia hili??
Mh Malecela alikuwa na haki 100%, na kwa hili Serikali imewajibika ilivyostahili!
 
Dunia ya sasa ni vigumu sana kumchagulia mtu sehemu anayohitaji kupata huduma. Huu ni ulimwengu wa kibepari, mteja anafuata panapomfaa.
"Mteja" anatumia hela yake, huyu Malecele anatumia hela yetu, ingekuwa ya kwake yasingetuhusu.

Sisi walipa kodi tuna protest kwamba ( 1 ) hatuna hela ya kutibu tibu hawa wazee nje ya nchi ( 2 ) sio fair kutibu watu fulani fulani kana kwamba wao uhai wao ndio muhimu zaidi ( 3 ) Wazee hawa ndio walipewa dhamana ya kujenga misingi ya infrastructure za huduma za jamii, wakashindwa, kwa nini wao ndio wakajitibu nje?
 
Bado hatujasomesha madaktari wa kuweza kufanya upasuaji wa moyo
 
Back
Top Bottom