ITV, Mengi to be dealt with soon

Mmiliki wa vyombo vya habari anaruhusiwa kutumia vyombo vyake vya habari kutangaza habari zake yeye mwenyewe au haruhusiwi? Jambo hili linawahusu wamiliki wote au baadhi ya wamiliki?
Inategemea na mmiliki ni nani!.. ndio funzo nililopata hapa!
Unajua Mwanakijiji, tazama magazeti leo hii yanavyonfunika Mengi tena mengine ni ya serikali lakini sijui kama wanafuata sheria hiyo hiyo wanayozungumzia..
Kumbuka hata wewe uliwekwa ktk nafasi hiyo ulipokuwa ukimzungumzia Lowassa akiwa Waziri Mkuu..mbona hawakukutumia barua ya kukuonya na kukufungia - Ujinga mtupu..
 
Inategemea na mmiliki ni nani!.. ndio funzo nililopata hapa!

Thats sums up the whole controversy..

Maana hadi sasa sijaelewa ni kwanini mmiliki asitumie chombo chake manufaa yake binafsi! yawe ya kifedha, kujitangaza au vinginevyo. Nimebaki kujiuliza hivi wamiliki wote wa biashara hawataki manufaa binafsi? au ni manufaa gani ambayo hayatakiwi mtu kuyapata..

Maana serikali ina vyombo vyake vya habari na inavitumia kwa manufaa ya serikali!! Lakini sijasikia serikali ikijipinga na kujiandikia barua (ndiyo sababu TBC hawakupewa onyo) ya kujikataza manufaa binafsi.. !!
 
kweli kabisa lakini naona ni vizuri alivyofanya mengi kwani ni ujasiri mkubwa sana.tukiendelea kuogopa kusema maovu nchi haitoendelea.na kinachofanya idara za usalama kuangaika kiasi hiki ni kutokana na ukweli wa maneno ya mengi.kama maneno ya mengi yangekuwa ya uongo lingekuwa swala dogo sana kusolve na kumuadhibu mengi.

Na Watanzania tunafuatilia kwa karibu kuona 'dola' inataka kumsulubu vipi Mengi. Hadi hii leo hakuna hata fisadi mmoja aliyeitwa katika kamati ya ulinzi na usalama. Mapapa mafisadi wote ambao ndiyo wangestahili kuitwa kwenye kamati hiyo akina Rostam, Manji, Subhash, Jeetu, Chavda bado wanaendelea kupeta tu. Mafisadi ndani ya chama na serikali akina Chenge, Idrissa Rashid na wengineo hawajaitwa katika kamati hiyo lakini wamekuwa na speed ya kutisha kutaka kumuweka kiti moto mmoja wa mashujaa wa Tanzania bwana Mengi. Tunasubiri kusikia kitakachojiri katika kikao hicho.
 
Dola yaanza kumwandama Mengi


Aitwa kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama

Yeye ataka mahakama iachiwe ifanye kazi yake

Sheria ya kudhibiti umiliki vyombo vingi vya habari yaja

Mwandishi Wetu Mei 27, 2009

Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

KAULI na vitendo vya Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Limited, Reginald Mengi, zinazowagusa watu aliowaita mafisadi papa, vimemuingiza katika matata makubwa, na sasa ameanza kubanwa na vyombo vya dola, Raia Mwema imeambiwa.

Habari za uhakika kutoka serikalini zimethibitisha kwamba mara baada ya Mengi kutoa kauli iliyowataja wafanyabiashara wenzake watano kuwa ndio mafisadi papa, kumekuwa na matukio mazito ya mfululizo yanayolenga kumbana, la karibuni zaidi likiwa ni la mfanyabiashara huyo kuitwa na Kamati Ndogo ya Ulinzi na Usalama wa Taifa.

Ofisa Mwandamizi wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, aliithibitishia Raia Mwema wiki hii kwamba mara kadhaa wamekuwa wakimtaka Mengi kutoa ushirikiano na wamemfuata hadi nyumbani kwake, wilayani Kinondoni na kumuandikia barua mara mbili lakini yeye amekuwa akisita.

“Ni kweli wakubwa walimtaka atoe ushirikiano bila mafanikio, mara ya kwanza Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai (DCI) ilimwandikia barua kutaka apeleke ushahidi wa tuhuma alizozitoa, akagoma akieleza kwamba ushahidi huo atautumia mahakamani ambako kuna kesi mbili kuhusiana na tuhuma hizo na mara ya pili sasa Kamati Ndogo ya Ulinzi na Usalama wa Taifa ikamtaka aende kutoa ushirikiano,” alisema Ofisa huyo.

Ofisa huyo wa Polisi ameliambia Raia Mwema kwamba kamati hiyo inayoongozwa na Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Jeshi la Polisi (DDCI), Peter Kivuyo, ni kamati ya watendaji ambayo kwa sasa inahusisha vyombo vyote vya dola isipokuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambao walijitoa.
.

Hivi, mbona kamati ya Ulinzi na Usalama wa Taifa haijamfuata Chenge, Karamagi, Msabaha, Idrissa na hata Mwakyembe na Rostam na kuwahoji kuhusu tuhuma za Ufisadi zilizo juu ya vichwa vyao?

Kwa nini Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Taifa haijafanyia kazi mapendekezo ya Ripoti ya Warioba au Ripoti ya Amina Chifupa ya wenye kufanya biashara za kulevya?

Kwa nini kamati ya Ulinzi na Usalama wa Taifa haijafanya uchunguzi na kuwaita wale wote wanaoagiza vyakula na bidhaa mbovu pamoja na maafisa wa idara za Ushuru na Kodi ambao hukagua hizo bidhaa kabla hazijaingizwa nchini?

Kwa nini kamati ya Ulinzi na Usalama wa Taifa haijafanya kazi kwa umakini kuhusu suala la Maalbino kutolewa kafara?

Kamati hii ya Ulinzi na Usalama ilikuwa wapi Watanzania walipobambikwa magari ya wizi?

Kamati hii ya Ulinzi na Usalama imezubaa vipi kuwa mashirika ya umma yalioingizwa ubia na wawekezaji yanadidimia kimapato na karibu kulitia hasara ya kukata na shoka Taifa? Watu kama TRL iweje tusubiri BOT waamke na kukaripia?

Kamati ya Ulinzi na Usalama ilikuwa wapi Richmond na Dowans zilipotuingiza mkenge achilia mbali Kiwira?

Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Taifa itaanza lini kufanyia kazi Ripoti ya CAG ili kuhakikisha kuwa vitendo vya uhujumu na matumizi mabaya ya fedha hayaliingizi Taifa hasara na hata kutishia thamani ya Shilingi yetu?

Kama rafiki yangu Mmoja anavyosema, ni UNAFIKI mtupu na ni AIBU tupu kuwa leo Kamati hii ya Ulinzi na Usalama inamrukia Mengi na kumtaka atoe maelezo, lakini haijasema inamtaka Rostam ajieleze alipotoa habari za Mengi has kuhusu akaunti za Benki kitu ambacho ni kinyume na taratibu za kibenki (Bank Secrecy Act)!

Simtetei Mengi na si shabiki wake, lakini ni lazima haki itendeke na sheria zifuatwe siku zote na kila wakati si pale inapotokea maslahi ya kikundi kinachojidai ni Serikali kutumia nafasi yake kisiasa kujizatiti inapoona kuwa maslahi yao yako hatarini na kuleta kisingizio cha Ulinzi na Usalama wa Taifa!
 
Date::5/28/2009
Mfanyabiashara Reginald Mengi alibanwa na dola

Na Mwandishi Wetu

Mwananchi

MFANYABIASHARA maarufu wa jijini Dar es salaam, Reginald Mengi amedai kuwa alibanwa na vyombo vya dola baada ya kutangaza hadharani majina ya watu watano wanaotuhumiwa kwa vitendo vya ufisadi, akiwabatiza jina la mafisadi papa.

Mengi, ambaye anamiliki vyombo tofauti vya habari, alibainisha hayo jana wakati akitoa mchango wake juu ya sera mpya ya habari kwenye mkutano wa wadau wa habari ulioitishwa na Idara ya Habari (Maelezo) kwenye Ukumbi wa Karimjee.

"Baada ya kutangaza majina ya watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi, niliitwa na (Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa), Takukuru na kuambiwa kwa nini nisichukuliwe hatua kwa kitendo changu," alisema Mengi.

"Niliitwa pia na Maelezo na kuambiwa kwa nini nisichukuliwe hatua; niliitwa na (Mamlaka ya Mawasiliano) TCRA. Kote huko niliulizwa kwa nini nisichukuliwe hatua."


Mengi pia alisema kuwa alielezwa kwenye taarifa yake ya kutaja watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi kulikuwa na chembechembe za ubaguzi wa rangi na kutakiwa kutoa maelezo.

"Siku hiyo ndipo nilipojua kuwa kumbe ufisadi una rangi," alisema Mengi.

Hata hivyo, Mengi hakueleza mazungumzo yake na vyombo hivyo vya dola yaliishaje na alijibu nini, lakini alijitetea kufanya hivyo si kutumia vibaya vyombo vya habari kwa kuwa ni kutetea nchi yako.

"Labda serikali ituorodheshee mambo gani yanamaanisha kutumia vibaya vyombo vya habari na mambo gani yanaonyesha kutumia vizuri vyombo vya habari," alisema mfanyabiashara huyo.

Mengi aliingia kwenye vita kubwa na wafanyabiashara wenzake baada ya kuwatangaza kuwa ndio wanaofilisi nchi, wote wakiwa ni wenye asili ya Asia. Baadhi walijitokeza na kujibu tuhuma hizo, huku wengine wakiibuka na tuhuma dhidi ya Mengi na kuziwasilisha Takukuru.

Serikali ilikemea kitendo cha Mengi, ikimtaka kuviachia vyombo vya dola kufanya kazi yake, sambamba na kumuonya mfanyabiashara Rostam Aziz akidaiwa pamoja na Mengi kwa kutumia vibaya vyombo vyao vya habari.
 
Ninasikitika kuona baadhi ya wabongo wanachukulia haya mambo katika hali ya ushabiki!! Mengi amelonga, RA amejibu na tuhuma kuzitoa dhidi ya Mengi, lakini cha ajabu ni kuona Serikali ilivyomshupalia Mengi! Kwanza alianza waziri wa bora utawala, then akaja waziri wa bahati, then katika kuonyesha kwamba kwenda shule sio kuelimika, wamekuja na muswaada wa kutoruhusiwa kwa mtu mmoja kumiliki zaidi ya chombo kimoja cha habari!! Bado watu wanaleta ushabiki katika masuala haya!! Sasa, kama mnataka kuleta ushabiki, basi kila mwana JF aseme amenufaika nini toka kwa Mengi, na amenufaika nini toka kwa RA & co. Iwe direct au indirect, wether ni wewe au jamaa yako, na isiwe lazima fedha, hapa ninazungumzia huduma, starehe na burudani. Nasubiri majibu!!!!
 
Dunia ipo inaangalia,watafunga ITV wakati coverage ya TBC1 ni less than 50%, na kwa vipi watafunga ,kwa kutumia sheria ipi,pana ngoma wamechelewa wenyewe walimpaisha kwa kumpa kichwa sasa mwache awahabarishe wananchi bila kuchuja au kuficha habari kama wanavyofanya TBC1 ,halafu wakifunga watamfanya mjamaa apaiishwe kishenzi kwenye nyaja za kimataifa ataonekana alikuwa ni mpambanaji atatumiwa ticketi kutoka dunia nzima akaeleze uonevu wa serikali na ndipo watakapochafuka zaidi waachane na woga
lakini wanasema what goes around comes around si JK na huyo muirani wake waliotumia magazeti na vyombo vingine kuwachafua wenzao kweli yamewafika watahangaika
 
Sitoshangaa kwani anatishia kuwatoa watu kwenye UTAMU, ambao unaweza kusababisha kuondolewa madarakani na hivyo kuvua nguo machafu yote waliyokuwa wanayafanya kwa karibu nusu karne!
 
Angekuwa Mengi alikubali kufa kiume mwaka 1995 kwa kupromote demokrasia leo asingebanwa. Maana tungekuwa na wabunge wengi wa upinzani na hivyo serikali isingekuwa na nguvu sana. Pia CCM wasingeweza kuwa wanashinda kwa kishindo. Lakini kwa kung'ang'ania utamu wa 1995 alisahau kuwa yatamkuta ya sasa. Hilo ni fundisho siyo kwa wafanyabiashara tu bali hata wanataaluma wengine wote. Wanasiasa hawana marafiki wa kudumu bali maslahi ya kudumu. Mwangalie Ulimwengu naye alikoma ubishi.
 
Fiksiman,

Unaposema inamtoa Mengi ktk sifa ya Mtanzania wa kawaida na kuwa mfanyabiashara una maana gani?.. yaani mfanyabiashara sii Mtanzania wa kawaida au kumiliki chombo cha habari ambacho unakitumia kutangaza habari hiyo huondoa Utanzania wa kawaida!..

Mengi amekosea hakukosea, swala la kutaka kulihukumu shirika kwa sababu yeye ndiye mmliki haina kichwa kabisa!.. Kwanza unaanza na makosa ya Mengi na kesi inaingia mahakamani. Je, maneno haya asingeyasema Mengi, kayasema Mkandara bado sheria ingelifungia ITV hata kama kuna ukweli..Je, Vyombo vya habari haviruhusiwi kurusha tuhuma zozote za Ufisadi?..na kwa nini tunatumia makosa ya Mengi kulihukumu shirika lake, nini makosa ya shirika hilo ktk utoaji habari tukimweka Mengi kando na nje ya habari hii.. Hakuna!

Siku zote sheria za Media na maadili hazina tofauti na sheria nyingine zote.. Sheria inayomhusu Mengi inatakiwa kumhusu pia Mkandara ktk swala husika, hakuna sheria iliyotungwa kwa ajili ya mtu au baadhi ya kundi la watu na kuwa applied tofauti kwa kundi jingine..
Mengi kafanya kosa mpelekeni mahakama.. chombo cha habari hakina makosa kwa sababu mwenye ushahidi ni Mengi na hakuzungumza yale maneno akiwa kama mmiliki wa ITV bali mwnaanchi anayezungumzia Ufisadi..
...


Mkuu, usiwe mgumu wa kuamka...sasa si muda muafaka wa kuanzisha ligi za kisiasa hapa tunazungumzia"professional view". Sheria na maadili ya vyombo vya habari ni tofauti na sheria zingine na vile vile mfano wako wa Dogo Muddy hapa si mahala pake.

Ni hivi: 1) Mfanyabiashara ni nani na anatabia gani? kabla hujaanza kuleta hoja zako ni vema unachokizungumza, kwa mfano mfanyabiashara hawezi kupewa sifa moja na mwananchi kwa kuwa yeye hulenga kutengeneza faida zaidi badala ya kutoa huduma, ndo maana Mwalimu Nyerere alisita mtu huyu kujihusisha na siasa au ufanyaji wa maamuzi bila kuangalia upande wake. Kwa bwana Mengi hakuna anayejua lengo lake la dhati katika mambo anayoyafanya. Sasa ni muhimu kumtengenesha yeye na wewe hasa linapokuja suala la maslahi ya kitaifa

2) kitendo alichofanya Mengi kuwatuhumu watanzania wengine kwenye chombo chake ni sahihi, dosari inakuja kwenye maadili ya habari. Kawaida unapomtuhumu mtu yeyote awe mhalifu au laa ni lazima utoe nafasi kwa mtu yule ajieleze kwa upande wake ili watazamaji au wasomaji waamue nani anasema ukweli. Sasa mengi hakuwahi kufanya hivyo na kibaya zaidi hata vyombo vyake hakuthubutu kuwatafuta waliotuhumiwa wajieleze. Kutokana na ujinga wa kufahamu sheria, wahusika walishindwa kumwajibisha Mengi na badala yake wakaamua kutumia vyombo vingine kujitetea. Pamoja na jitihada hizo Mengi aliendelea na madai yake kwa kuwatumia wanasheria wake na hata waandishi wake ambao walionekana wazi wazi kuegemea upande wake. Hapa ndipo palipo leta hiyo kitu hapo juu....Compliance order

3) Pia nakushauri pitia vitabu hata vya Biashara usome utaelewa kwanini Mengi anawajibika kwa alichokifanya pamoja na kituo chake. Kwa lugha ya biashara, mmiliki wa kampuni anaweza kufilisiwa endapo atashindwa kufikia kiwango fulani cha utendaji wake. Kwa maana nyingine Mengi is part and parcel of ITV kwasababu hiyo maamuzi anayoyafanya yanaweza au yanaathiri moja kwa moja utendaji wa kituo hicho. Kwa kuamini kuwa waandishi wa ITV wasingeweza kumhoji Bosi au Mwaajiri wao, Mhavile ambaye ndiye Mtendaji Mkuu wa ITV na kituo kizima (waandishi) wanabeba msalaba wa kutomshauri vizuri mwaajiri wao huku waikijua umuhimu wa kuzingatia maadili na uhuru wenye mipaka.

4) Ndugu ya Mukandara nafahamu fika msimamo wako kwenye sakata hili, hata mimi pia ninao wa kwangu, hebu tujaribu kuweka pembeni hii na tuwe wa kweli kwa watanzania wenzetu. Ni ushahidi gani ambao Mengi aliutoa wakati anawataja watuhumiwa hawa zaidi ya maneno yenye kujenga chuki kati yetu na watanzania wengine. Kama kweli alikuwa na haja ya kumsaidia Rais, je unataka kuniambia njia ile ilikuwa sahihi? Mimi, wewe na Mengi nani mwenye uwezo wa kuonana na Rais na kukaa nae pamoja kunywa gahawa, ni kweli mengi anania ya dhati ya kumpa tafu Kikwete kwa staili ile? Yaani hata kutumia ushawishi wake ameshindwa kumkabidhi kikwete ushahidi kwa kuwa haviamini vyombo vyake vya dola? Mi siamini kama kweli alikuwa na lengo hilo, okay tuseme kweli alikuwa na lengo hilo sasa kama serikali imeshindwa kuwachukilia hatua yoyote pamoja na uwezo na nguvu za kijeshi na kisheria ilizonazo, kitu gani kimemshawishi yeye angeweza? Yapo maswali mengi ya kujiuliza kama mjadala huu ila nia yangu si kufufua msiba huu bali ni kuwekana swa katika mambo ya msingi na yasiyo ya ubishi.

Ukweli wa yote anaujua yeye mwenyewe mimi na wewe ni washabiki kama ilivyo Man na Barca...mwisho wa siku rekodi zetu ziko sawa.
 
Kila mtu anaelewa wazi kuwa ITV iko chini ya Bw. Mengi lakini sina hakika watanzania wa leo watakubali serikali kuleta upumbavu huu wa ku-shut down IPPMEDIA outlets kwa sababu ambazo serikali inataka kuwalaghai watanzania. Nyie subirieni, hapo ndipo mtajua kuwa watanzania si wapumbavu.
 
Hivi, mbona kamati ya Ulinzi na Usalama wa Taifa haijamfuata Chenge, Karamagi, Msabaha, Idrissa na hata Mwakyembe na Rostam na kuwahoji kuhusu tuhuma za Ufisadi zilizo juu ya vichwa vyao?

Kwa nini Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Taifa haijafanyia kazi mapendekezo ya Ripoti ya Warioba au Ripoti ya Amina Chifupa ya wenye kufanya biashara za kulevya?

Kwa nini kamati ya Ulinzi na Usalama wa Taifa haijafanya uchunguzi na kuwaita wale wote wanaoagiza vyakula na bidhaa mbovu pamoja na maafisa wa idara za Ushuru na Kodi ambao hukagua hizo bidhaa kabla hazijaingizwa nchini?

Kwa nini kamati ya Ulinzi na Usalama wa Taifa haijafanya kazi kwa umakini kuhusu suala la Maalbino kutolewa kafara?

Kamati hii ya Ulinzi na Usalama ilikuwa wapi Watanzania walipobambikwa magari ya wizi?

Kamati hii ya Ulinzi na Usalama imezubaa vipi kuwa mashirika ya umma yalioingizwa ubia na wawekezaji yanadidimia kimapato na karibu kulitia hasara ya kukata na shoka Taifa? Watu kama TRL iweje tusubiri BOT waamke na kukaripia?

Kamati ya Ulinzi na Usalama ilikuwa wapi Richmond na Dowans zilipotuingiza mkenge achilia mbali Kiwira?

Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Taifa itaanza lini kufanyia kazi Ripoti ya CAG ili kuhakikisha kuwa vitendo vya uhujumu na matumizi mabaya ya fedha hayaliingizi Taifa hasara na hata kutishia thamani ya Shilingi yetu?

Kama rafiki yangu Mmoja anavyosema, ni UNAFIKI mtupu na ni AIBU tupu kuwa leo Kamati hii ya Ulinzi na Usalama inamrukia Mengi na kumtaka atoe maelezo, lakini haijasema inamtaka Rostam ajieleze alipotoa habari za Mengi has kuhusu akaunti za Benki kitu ambacho ni kinyume na taratibu za kibenki (Bank Secrecy Act)!

Simtetei Mengi na si shabiki wake, lakini ni lazima haki itendeke na sheria zifuatwe siku zote na kila wakati si pale inapotokea maslahi ya kikundi kinachojidai ni Serikali kutumia nafasi yake kisiasa kujizatiti inapoona kuwa maslahi yao yako hatarini na kuleta kisingizio cha Ulinzi na Usalama wa Taifa!

Ndugu yangu Rev. Kishoka, Kamati ipi unayoulizia uwepo wake? Hii hii tunayoijua? mbona hii kamati ni ya serikali hii hii - serikali ambayo ni pango la wanyang'anyi? unategemena nini hapo. unataka wafuatilie Richmond,ripoti za Warioba na CAG?!! Hata siku moja! Labda ungesema wamfuatilie Warioba na CAG sio report zao.
 
Mfanyabiashara Reginald Mengi alibanwa na dolaNa Mwandishi Wetu

MFANYABIASHARA maarufu wa jijini Dar es salaam, Reginald Mengi amedai kuwa alibanwa na vyombo vya dola baada ya kutangaza hadharani majina ya watu watano wanaotuhumiwa kwa vitendo vya ufisadi, akiwabatiza jina la mafisadi papa.

Mengi, ambaye anamiliki vyombo tofauti vya habari, alibainisha hayo jana wakati akitoa mchango wake juu ya sera mpya ya habari kwenye mkutano wa wadau wa habari ulioitishwa na Idara ya Habari (Maelezo) kwenye Ukumbi wa Karimjee.

"Baada ya kutangaza majina ya watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi, niliitwa na (Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa), Takukuru na kuambiwa kwa nini nisichukuliwe hatua kwa kitendo changu," alisema Mengi.

"Niliitwa pia na Maelezo na kuambiwa kwa nini nisichukuliwe hatua; niliitwa na (Mamlaka ya Mawasiliano) TCRA. Kote huko niliulizwa kwa nini nisichukuliwe hatua."

Mengi pia alisema kuwa alielezwa kwenye taarifa yake ya kutaja watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi kulikuwa na chembechembe za ubaguzi wa rangi na kutakiwa kutoa maelezo.

"Siku hiyo ndipo nilipojua kuwa kumbe ufisadi una rangi," alisema Mengi.

Hata hivyo, Mengi hakueleza mazungumzo yake na vyombo hivyo vya dola yaliishaje na alijibu nini, lakini alijitetea kufanya hivyo si kutumia vibaya vyombo vya habari kwa kuwa ni kutetea nchi yako.

"Labda serikali ituorodheshee mambo gani yanamaanisha kutumia vibaya vyombo vya habari na mambo gani yanaonyesha kutumia vizuri vyombo vya habari," alisema mfanyabiashara huyo.

Mengi aliingia kwenye vita kubwa na wafanyabiashara wenzake baada ya kuwatangaza kuwa ndio wanaofilisi nchi, wote wakiwa ni wenye asili ya Asia. Baadhi walijitokeza na kujibu tuhuma hizo, huku wengine wakiibuka na tuhuma dhidi ya Mengi na kuziwasilisha Takukuru. Serikali ilikemea kitendo cha Mengi, ikimtaka kuviachia vyombo vya dola kufanya kazi yake, sambamba na kumuonya mfanyabiashara Rostam Aziz akidaiwa pamoja na Mengi kwa kutumia vibaya vyombo vyao vya habari.
 
I think closing ITV is just taking Mengi to several steps higher and JK will face an international community criticism. JK will not allow it to happen unless someone is running the country for him.
 
I think closing ITV is just taking Mengi to several steps higher and JK will face an international community criticism. JK will not allow it to happen unless someone is running the country for him.

Didn't you now this? Had it been that he was himself running the country the fisadis like Kagoda's (rostam) would have been taken to task and all the boastings and assumed powers of these fisadis wouldn't be there. Actually JK is remotedly controlled.
 
Ni hivi: 1) Mfanyabiashara ni nani na anatabia gani? kabla hujaanza kuleta hoja zako ni vema unachokizungumza, kwa mfano mfanyabiashara hawezi kupewa sifa moja na mwananchi kwa kuwa yeye hulenga kutengeneza faida zaidi badala ya kutoa huduma, ndo maana Mwalimu Nyerere alisita mtu huyu kujihusisha na siasa au ufanyaji wa maamuzi bila kuangalia upande wake. Kwa bwana Mengi hakuna anayejua lengo lake la dhati katika mambo anayoyafanya. Sasa ni muhimu kumtengenesha yeye na wewe hasa linapokuja suala la maslahi ya kitaifa

naona kama una komplicate situation. yeye alisema mafisad ni hawa. yaani alisema wezi wetu ni hawa. na akataja na makashfa yawahusuyo. sasa kwanin tuanze kuangalia huyu mengi anashughulika na nini? haya chukulia ni mshindani wao katka biashara au anataka uraisi baada ya jmk. kwahiyo tusimsikilize au hana haki ya kusema ukweli?

yaani, wafanyabiashara wote tusiwasikilize wakiwashutumu wenzao kuwa wanalihujumu taifa. tuwadharau kabisa. tuseme kwenda huko kwanza wewe mwenyewe ni mfanyabiashara kama hao wezi. tuseme tunataka mfanyakazi wa kuajiriwa au mkulima ndo atupe habari za sisi kuibiwa na wafanyabiashara?
kwanini?
hapana. tumsikilize kila mtu. la muhimu iwe usahihi wa hizo habari. then vyombo vya dola vifuatilie. after all tunawalipa kwa hilo
afande kova kila mara anasema anaomba 'ulinzi shirikishi'. ambapo raia watatoa taarifa kwa polis na polis watafuatilia. alichofanya mengi ni kumuunga mkono kova

hata kama angekuwa anataka urais bado anastahili kusikilizwa. asikilizwe na vyombo vinavyohusika vifuatilie. akija kuanza kugombea urais tuje tumhukumu kwa matendo yake na michango yake kwa tz

4) Ndugu ya Mukandara nafahamu fika msimamo wako kwenye sakata hili, hata mimi pia ninao wa kwangu, hebu tujaribu kuweka pembeni hii na tuwe wa kweli kwa watanzania wenzetu. Ni ushahidi gani ambao Mengi aliutoa wakati anawataja watuhumiwa hawa zaidi ya maneno yenye kujenga chuki kati yetu na watanzania wengine. Kama kweli alikuwa na haja ya kumsaidia Rais, je unataka kuniambia njia ile ilikuwa sahihi? Mimi, wewe na Mengi nani mwenye uwezo wa kuonana na Rais na kukaa nae pamoja kunywa gahawa, ni kweli mengi anania ya dhati ya kumpa tafu Kikwete kwa staili ile? Yaani hata kutumia ushawishi wake ameshindwa kumkabidhi kikwete ushahidi kwa kuwa haviamini vyombo vyake vya dola? Mi siamini kama kweli alikuwa na lengo hilo, okay tuseme kweli alikuwa na lengo hilo sasa kama serikali imeshindwa kuwachukilia hatua yoyote pamoja na uwezo na nguvu za kijeshi na kisheria ilizonazo, kitu gani kimemshawishi yeye angeweza? Yapo maswali mengi ya kujiuliza kama mjadala huu ila nia yangu si kufufua msiba huu bali ni kuwekana swa katika mambo ya msingi na yasiyo ya ubishi.

kuna namna nyingi za kumsaidia mtu kufanya kazi yake ipasavyo.
nionavyo na nifikiriavyo mimi vyombo vya serikali vina ushahid na uwezo mzuri zaid ya mengi katka hili. kwa hiyo kwa mengi zaid ilikuwa - ebanaeee, mbona hufanyi kazi yako!
hata maskin kabisa hapendi kuibiwa au kudhulumiwa. hata asiyejua kuwa anaibiwa pia hapendi kuibiwa. kwangu alichofanya mengi ni kuungana na mamilion ya watz wengine kupiga kelele, kulalamika. na makelele haya yanaweza kuwa very effective. na huo ni mchango bora kabisa pia

Ukweli wa yote anaujua yeye mwenyewe mimi na wewe ni washabiki kama ilivyo Man na Barca...mwisho wa siku rekodi zetu ziko sawa.

si kweli kuwa mkandara na wewe au mimi na wengineo suala la mengi na rostam ni kama ushabiki kwa man na barca. si kweli kabisa. suppose man au barca inashinda, mkandara kama mshabiki wa timu inayoshinda kikawaida atapata nini? kwa upande mwingine chukulia mkandara ni mtz na anamuunga mkono au kumshabikia kama unavyoita bwn mengi. je mengi akishinda - na hapa kushinda ni kuwa mkweli na kuchukuliwa hatua kwa hao mafisad, je mkandara kama mtz hatanufaika kivyovyote?
au unataka kutufundisha hapa kuwa anachosema mengi si kwa manufaa ya taifa?
hilo somo mi siwezi kulielewa. labda unifafanulie zaid.
haiwezekani mtu anakuja anasema, ebanaeee, tunaibiwa, halafu wewe hapa useme hasemi hayo kwa faida yetu sote. sikatai inaweza kuwa inamnufaisha directly au indirectly, leo au kesho but still hainiumi kama sie, kama watz inatusaidia pia

mapesa ya serikali au kama yale ya epa ilikuwa yatusaidie sisi sote. yakiibwa tumeibiwa sote
 
Mwenye taarifa aniambie kama huyu Nkoma alishakubalika kwamba ni M-Tanzania.

Prof. Nkoma haionyeshwi alizaliwa wapi lakini tangu alipoletwa nchini kutoka huko Botswana, ilieleweka yeye ni raia wa Malawi. Kusoma hapa na kuajiliwa hapa ilikuwa ni makosa ya ujamaa wa enzi hizo. Ano ndugu pia walioko nchini bila uraia wetu na wanaishi maeneo ya Kunduchi.

Pamoja na suala hilo kuzimwa na ikulu, je alishakuwa M-Tz? Isije ikawa tunasumbuliwa na raia wa nchi jirani.

Nafikiri hili la Prof.Nkoma ni la muhimu kulifuatilia ili kujua Utanzania wake ni wa namna gani,kwani kwa kweli kwa jinsi hili jambo la ITV linavyopelekwa inaonekana wazi kuwa wana nia ya kukifunga hiki kituo cha ITV.

Kama Prof.Nkoma ni mmalawi sitoshangaa kwani wamalawi ni wengi tuu hapa kwetu Tanzania wengine wao ni mahouse girls and boys kwenye baadhi ya mitaa tunayoishi.

Sasa kwa hali inavyokwenda kuna kila sababu kwa mtanzania halisi kuinuka tena kwa pamoja ili tuikomboe nchi yetu.Tumechoka kunyanyaswa na wageni waliokuja kwa nia moja tuu nayo nikupora urithi wa nchi yetu kwa kutumia baadhi ya viongozi vibaraka tuliowaweka madarakani.
 
Yaani badala ya kumpongeza our hero Mengi wanampotezea mda wake kwa kumlazimisha ku deal na non-issues kama hizi!!!!?? Kweli Rostam na Manji nchi ni yao, ndiyo waongoza nchi.

Yaani nimeamini hata kama kiongozi wa idara/department ni Proffesor but hana sauti ya kutumia elimu yake ku deal na issues, wanakaa mezani kusubiri order za mafisadi na serikali yao. Unajua wananchi watanzani tunasema tunakaribia milion 40 lakini ........

Jamani kwa nini tusiandamane kupinga Mengi kughasiwa. Huyu ndiye mzalendo pekee aliyeweza kuthubutu kutaja mafisadi wa kweli hadharani tofauti na mimi nabwabwaja hapa na anonimity yangu. Tumuunge mkono jamani. Hii ni kwa faida yako na vizazi vijavyo kwani nahofia si muda mrefu tutakuwa wakimbizi ndani ya nchi yetu, apartheid ya South Africa inaingia Tza doubled!!! Kina RA watakapofanikiwa kushinda ubunge tena na Manji naamini anajipanga kuwania, basi tumekwisha, tutaendelea kudharauliwa mno na watajiona vijogoo kabisa. Tusikubali kuwa mtetea tuamke tupambane.

Nakubaliana na wewe kwa asilimia 100 lakini tatizo lililopo ni kwamba ingawa kuandamana ni haki ya kikatiba kwa watanzania,mafisadi kwa kuwatumia polisi watazuia hayo maandamano kwa visingizio mbalimbali.

Napendekeza uandaliwe mkakati maalum wa kuwatokomeza mafisadi na mtandao wao wote ndani ya serikali.Hili likikamilika ndipo tunaweza kuwashirikisha wananchi kwa ujumla wao wale wanaopinga ufisadi na kuzishirikisha asasi za kiraia.

Napenda kukumbusha pia kwamba marehemu Mwalimu Julius Nyerere yeye na wenzake walishirikiana bega kwa bega kuhakikisha kuwa wanaikomboa Tanganyika toka mikononi mwa mkoloni.Walitumia nguvu zao,ushawishi na elimu yao yote na hatimaye walishinda.

Kizazi hiki kinachopingana na ufisadi kinadeni kwa Tanzania ya leo,tuna kila sababu ya kuikomboa Tanzania dhidi ya mtandao wa ufisadi ambao umejipanga kuinyonya nchi yetu na wananchi wake.Tuna kila sababu ya kutumia elimu yetu,ushawishi wetu na nguvu yetu yote na wote kwa pamoja kuupinga ufisadi na hatimaye tutashinda.
 
kweli hii inatia hasira ukitaja mafisadi badala ya vyombo husika kuwafanyia kazi uliyetaja ndio unachunguzwa ikiwa jk mwenyewe katamka kuwa tuwataje mafisadi sijui ana maanisha nini?

Tz ndio mana hata ukimkuta mtu barabarani kagongwa unamuacha hapo2 mana ukimsaidia kwenye gari lako we ndio utaisaidia police.
 
Back
Top Bottom