ITV, Mengi to be dealt with soon

Jamani kwani kilichotangazwa na TBC kuwa mengi ni nyangumi ndicho kinaruhusiwa? au mkoma hakukiona?
 
I dont see any reason for crucifying reginald mengi.He is a patriot, a tanzanian businessman employed lots of Tanzanians, he pays taxes to the government and infact he is a senior citzen who can come out publicly to speak evils. It is quite unfortunate that poor corrurpt countreals tends to cooprate with foreigners than locals. This is a deadly syndrome of poor and corrupt government ..putting the locals for the last. Would you emaging an employee of ultimate security owned by somaiya earns only 60,000 monthly gross pay???.
 
I dont see any reason for crucifying reginald mengi.He is a patriot, a tanzanian businessman employed lots of Tanzanians, he pays taxes to the government and infact he is a senior citzen who can come out publicly to speak evils. It is quite unfortunate that poor corrurpt countreals tends to cooprate with foreigners than locals. This is a deadly syndrome of poor and corrupt government ..putting the locals for the last. Would you emaging an employee of ultimate security owned by somaiya earns only 60,000 monthly gross pay???.

Duu...

omarilyas
 
I’ve read all letters, ya TCRA na ITV Advocate!

don’t know why they’re here! Unless kama sijazielewa, otherwise there’s nothing burning here!!! Mnataka kutushawishi kwamba ITV (Mengi) inataka kuhujumiwa? If I can remember, Manji alipeleka malalamiko TCRA kwa kile alichoona (yeye Manji) kwamba Mengi anatumia nafasi yake kama mmiliki wa vyombo vya habari kutumia vyombo hivyo kuwadharirisha wenzake! Au kwa maana nyingine, anatumia vyombo vyake kwa maslahi yake binafsi.

Whether this’s true or not, ni kweli sheria za vyombo vya habari zinakataza kuweka mbele maslahi binafsi badala ya yale ya kitaifa!! Hii si mara ya kwanza kwa ITV kushutumiwa kwa jambo hili, kuna wakati ilisemwa kwamba hata muda anaopewa JK kama kiongozi wa nchi ni mdogo ukilinganisha na ule anaopata Mengi( am not sure abt this, and it’s none of my businesss)! Sasa kama TCRA walipelekewa hayo malalamiko na Manji, what could they do?!

Hawakutakiwa kuwaandikia ITV kwenda kuji-defend? Mbona kwenye hiyo order ya TCRA sijaona popote panapoonesha dalili za kutaka kuihujumu ITV? Au ni kwavile TCRA walipiga biti kwamba ITV wasipo-appear before Authority watakuwa punished? I don’t think kama kuna something wrong hapo. TCRA ni mamlaka inayotambulika kisheria hivyo order yake lazima iheshimike whether mtuhumiwa(Say ITV) kafanya kosa au hapana!!!

Kwangu mimi hii nayo ni ilele ya kutaka kumuonesha RM kwamba ni mtu anayehujumiwa!! Kila anapohisi kunafanyika mambo negative dhidi yake, anatafuta defensive mechanism ya kutaka kujionesha anaonewa!! Nakumbuka last year, or year before kuna wapuuzi fulani waliongea kwamba eti RM ni mbaguzi wa kidini!! Katika kutaka kuonesha yeye si mbaguzi, few days later ( if not hours) ITV wakarusha kipindi cha karibu nusu saa (kama sio saa nzima) ikimuonesha RM akila msosi na watoto wa Madrasa kule Kibaha kama sikosei! Katika maongezi yake hiyo siku, nakumbuka RM akisema “ …..watoto, kuna watu wanasema eti mimi nawabagua nyinyi……!” Nilicheka sana siku hiyo na kujiuliza how can such great man look for such cheap popularity!

Unataka kutushawishi yale ya TBC1 na RA ni ya kitaifa? Au kwa makusudi ume skip issue hii kuizungumzia kwenye details zako?

nafikiri hapa anaonyesha kwamba TCRA wanashughurikia barua ya Manji kiofisi ili waweze kuwa na majibu. ndiyo hivyo wana investigate, na kwa kuanzia wanaomba maelezo toka ITV. Sasa hapa huwezi kuzungumzia TBC1 kwani hakuna mtu aliyeandika barua TCRA kuilalamikia. jamani na sisi kama ni wazalendo kweli tuwe tunapeleka malalamiko yetu rasmi panapohusika mf. hayo makosa ya TBC1 yalipotiwe TCRA ili kama kuna kosa wachukue hatua.
 
Dola yaanza kumwandama Mengi

Aitwa kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama

Yeye ataka mahakama iachiwe ifanye kazi yake

Sheria ya kudhibiti umiliki vyombo vingi vya habari yaja

Mwandishi Wetu Mei 27, 2009

Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

KAULI na vitendo vya Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Limited, Reginald Mengi, zinazowagusa watu aliowaita mafisadi papa, vimemuingiza katika matata makubwa, na sasa ameanza kubanwa na vyombo vya dola, Raia Mwema imeambiwa.

Habari za uhakika kutoka serikalini zimethibitisha kwamba mara baada ya Mengi kutoa kauli iliyowataja wafanyabiashara wenzake watano kuwa ndio mafisadi papa, kumekuwa na matukio mazito ya mfululizo yanayolenga kumbana, la karibuni zaidi likiwa ni la mfanyabiashara huyo kuitwa na Kamati Ndogo ya Ulinzi na Usalama wa Taifa.

Ofisa Mwandamizi wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, aliithibitishia Raia Mwema wiki hii kwamba mara kadhaa wamekuwa wakimtaka Mengi kutoa ushirikiano na wamemfuata hadi nyumbani kwake, wilayani Kinondoni na kumuandikia barua mara mbili lakini yeye amekuwa akisita.

"Ni kweli wakubwa walimtaka atoe ushirikiano bila mafanikio, mara ya kwanza Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai (DCI) ilimwandikia barua kutaka apeleke ushahidi wa tuhuma alizozitoa, akagoma akieleza kwamba ushahidi huo atautumia mahakamani ambako kuna kesi mbili kuhusiana na tuhuma hizo na mara ya pili sasa Kamati Ndogo ya Ulinzi na Usalama wa Taifa ikamtaka aende kutoa ushirikiano," alisema Ofisa huyo.

Ofisa huyo wa Polisi ameliambia Raia Mwema kwamba kamati hiyo inayoongozwa na Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Jeshi la Polisi (DDCI), Peter Kivuyo, ni kamati ya watendaji ambayo kwa sasa inahusisha vyombo vyote vya dola isipokuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambao walijitoa.

"Unajua haya mambo yana utata sana, maana hiyo kamati ya kina Kivuyo inahusika zaidi na kupambana na ujambazi na dawa za kulevya na ndiyo maana TAKUKURU walijitoa, sasa kama huyo mzee (Mengi) alizungumzia ufisadi, wanapaswa kuwaachia akina Hosea (Dk. Edward, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU) wafanye kazi yao," alisema.

Habari kutoka TAKUKURU zimethibitisha kwamba tayari chombo hicho kimekuwa kikifanyia kazi kile kilichopewa jina la "malumbano kati ya Mengi na Rostam" na kwamba wamekwishakupata ushirikiano kutoka pande zote zinazohusika.

Mengi mwenyewe alipotafutwa na Raia Mwema wiki hii alieleza kwamba hawezi kuzungumza lolote kwa kuwa yeye tayari amefungua kesi mahakamani na angependa mambo yaende kwa mujibu wa sheria si katika vyombo vya habari.

Kabla ya polisi kuingilia kati suala la Mengi, viongozi waandamizi wa Serikali wakiwamo mawaziri wawili Sophia Simba wa Utawala Bora na George Mkuchika wa Habari, Utamaduni na Michezo, walizungumzia matamshi yake na wote walionyesha wazi kumpinga mfanyabiashara huyo anayemiliki vyombo kadhaa vya habari.

Baada ya mawaziri hao kutoa kauli hiyo, mwanasiasa aliyejijengea heshima mbele ya jamii, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, alijitokeza kumpinga Mengi akisema kwamba mfanyabiashara huyo alikosea na kwamba alifanya hivyo kujipendekeza na kumsaidia Rais Jakaya Kikwete, na si kwa kutetea maslahi ya umma.

Mwangwi wa Lipumba ulipokewa na Mbunge wa chama chake, Hamad Rashid Mohamed, ambaye yeye aliuliza swali bungeni akitaka ufafanuzi kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuhusiana na matumizi ya vyombo vya habari kushambulia watu wengine.

Hamad hakumtaja Mengi, japo alibainisha kuwa na lengo hilo kwa kuhoji; "Je, Mheshimiwa Waziri Mkuu ni halali kwa mmiliki wa vyombo vya habari kutumia chombo cha habari, kuwahukumu watu kwa chombo chake cha habari, hiyo ni sehemu ya sera za utawala bora?"

Katika majibu yake, Waziri Mkuu Pinda alikuwa makini zaidi kuliko mawaziri wake kwa kusema; "Niseme kwamba kwa hili ambalo hasa unalizungumzia tunaweza tukalitazama kwa namna mbili; moja, sawa ametumia uhuru ule amesema alichosema. Sasa jukumu ni la yule aliyesemwa katika mazingira yale kama anaona ameonewa, hakutendewa haki vyombo vya sheria vipo anaweza kabisa akaenda mahakamani akafungua kesi kulingana na aina ya matamshi ambayo yeye kayapata. Alitumia fursa ile upande mmoja ni sawa kama Hamad Rashid Mohamed ambaye angeweza kutumia chombo kingine chochote."

Hata pale Hamad alipotaka Waziri Mkuu azungumzie hatua, Waziri Mkuu alisema, "Ni jambo ambalo linatakiwa lifanyiwe kazi kwa umakini mkubwa na vyombo vile ambavyo vimekabidhiwa dhamana hiyo, wakifika mahali wakaridhika wakaona iko kosoro na kwa sababu Wizara yenyewe ya habari ipo. Kwa hiyo, mimi matumaini yangu ni kwamba hatua stahiki zitachukuliwa kwa kadri itakavyowezekana."

Kwa upande wake, Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohamed Shein, ambaye alikuwa akisoma hotuba ya Rais Kikwete wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani (Mei Mosi), aligusia suala la mapambano dhidi ya ufisadi na kusema kwamba haki ya kutoa maoni isitumike kuathiri haki za wengine na uhuru wa mahakama. Hata hivyo hakuingia undani wa sakata la Mengi na Rostam, pamoja na kuonekana kuligusia.

Mlolongo huo wa viongozi wa juu wa Serikali na wanasiasa ndio ulioelezwa kupokewa kwa vitendo na watendaji wa vyombo vya dola ikiwamo Polisi, huku Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) nayo ikiingilia kati na kuiandikia telivisheni ya ITV inayomilikiwa na Mengi, ikiitaka ijitetee kwa kuvuruga ratiba za vipindi vyake wakati wa kutoa taarifa iliyowatuhumu wafanyabiashara watano walioitwa mafisadi papa.

Raia Mwema imeambiwa kwamba tayari hatua hiyo ya TCRA imepingwa na wanasheria wa ITV ambao mbali ya kutoa maelezo, waliamua kulifikisha suala hilo mahakamani wakiegemea kuwapo kwa kesi mbili zinazohusiana na kipindi hicho, zote zikiwa zinamhusu Mengi na wafanyabiashara waliotajwa naye kuwa ni mafisadi papa.

Mbali ya Polisi na TCRA, katika hali isiyotarajiwa, Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Elieza Feleshi, alinukuriwa na gazeti la Serikali la Daily News, akisema kwamba ofisi yake inachunguza tuhuma zilizotolewa na Rostam dhidi ya Mengi, tuhuma ambazo zilikuwa zimewasilishwa TAKUKURU siku chache kabla ya tamko hilo. Kwa kawaida DPP hupokea majalada kutoka vyombo vya dola na kuyatolea uamuzi kabla ya kufikishwa mahakamani ama kutupiliwa mbali.

Katika hatua nyingine Serikali inadaiwa imeanza mchakato wa kuandaa sera ya habari ambayo itatungiwa sheria ikizuia mtu yeyote kumiliki aina tofauti ya vyombo vya habari, sera ambayo inaonekana wazi kulenga kumpunguzia nguvu Mengi anayemiliki vyombo vingi vya habari, ikiwa ni pamoja na televisheni, redio na magazeti kadhaa.

Kwa mujibu wa sera hiyo, mtu anayemiliki vyombo zaidi ya kimoja atapewa muda wa miaka mitano kujiondoa, muda ambao umeelezwa kulenga uchaguzi wa mwaka 2015, ambao mfanyabiashara huyo anaelezwa kuwa anaweza kuwa tishio kwa wanasiasa ambao wamekuwa wakitofautiana.

Chanzo cha habari ndani ya Serikali na ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kinaeleza kwamba Mengi anaonekana kama tishio kubwa kwa baadhi ya wanasiasa ambao wamekuwa wakitafuta kila mbinu kumpunguzia nguvu ikiwa ni pamoja na kufanyia mbinu za kijasusi katika harakati zake na kwa watu wanaomzunguka.

Tayari Mengi anahusishwa na harakati za vyama vya upinzani hususan Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) huku ikifahamika wazi kwamba yeye na televisheni yake ya ITV ikiwa inajihusisha na kuisaidia CCM kwa miaka mingi sasa na anatajwa kuwa karibu na Rais Jakaya Kikwete.

Mengi amekuwa akijihusisha na harakati za kusaidia makundi ya kijamii katika baadhi ya majimbo ya uchaguzi nchini akiambatana na wabunge wa CCM, kitendo ambacho pia kimeanza kutafsiriwa kuwa ni harakati zenye malengo ya kisiasa zaidi na si za kijamii japo yeye mwenywe amekuwa akisema ya kuwa haoni ya kuwa ana wito wa siasa.
 
hii nchi yetu kiboko.mtu huna uhuru wa kufanya kitu chochote watu wanatumia nguvu ya kuwa serikalini kufanya maovu.swala la mengi kutaka mambo yamalizwe mahakamani ni swala zuri sana kwani hao wote wanaoajaribu kuzima huu mjadala wanaogopa kuumbuka.
 
Nadhani kuna tatizo hapa!
Kila kitu kinachukuliwa kama ni siasa.

TCRA ni chombo kinachojitegemea na ndani ya TCRA kuna CCC; hawa jamaa ukitukanwa kwenye mtandao au kwenye nyanja yoyote ya ICT, au service provider akilamba salio lako kwenye simu etc na mengi mengine unawapelekea... wakishapelekewa wana mwita aliyetuhumiwa kumsikiliza.

Sasa katika hili sijui kwamba wanatakiwa waendelea hata kama kuna hoja mahakama au lah!.

Lakini kule hamna siasa.

Let be serious, kwa sheria za nchi Mengi alichemsha kwa sympathy ya wananchi na kwa kuwa tumekata tamaa huenda hana kosa.

Turudi nyuma gavana wa Benk juzi tu amekataa wabunge wasiwe wajumbe wa bodi wa bank ambapo serikali ina shea... hii ilikuwa kilio cha watu wabunge wa upinzani na chama tawala lakini rais ameendelea kuwateua na mawaziri wameendea kuteua wabunge wenzao, Ndulu mteuliwa wa Rais amekataa... lakini hawezi fanywa lolote kwa kuwa BOT inajitegemea... anayefuata maelekezo ya serikali ambapo sio lazima ni udhaifu wake... na wala sio matatizo ya serikali.

Sasa mimi naona tukubali msumeno unakata pande zote.
 
Mengi kajipalia makaa chachandu,
Hakujua kuwa alipomgusa Rosta Aziz alikuwa anaugusa mtandao mkubwa sana wa watuhumiwa vitendo vya ufisadi,ambao kama kweli Mengi ana ushahidi zidi ya Rosatam tu, basi ni sawa kuwa mlolongo huo wote anaohusiana nao unaweza kuwa hatarini na kupelekea balaa kwa serikali ya awamu ya nne kabla ya hata uchaguzi wa 2010, ndo maana idara za usalama zinajaribu kupata kile ambacho Mengi anakusudia kukisema mahakamani kabla hakijafika huko.
 
But the thing is why only ITV??
Mbona Fisadi papa RA alivo enda TBC haijakemewa? yaani sielewi watu wazima wenye akili zao wanapo weza kufanya blanda kama hizi kwa ajili ya kumlinda fisadi mmoja tu!

Labda niungane na Mwanakijiji kuuliza hivi RA hizi nguvu alizo nazo mbona ni za ajabu sana? anazitoa wapi? hivi ni kawaida kweli? ama kuna sayansi za ajabu zinaendelea juu yake kumfanya awe na utiisho juu ya binadamu wenzake? I dont get it!..
Mengi angeenda kulalamika kwenye tume ya mawasiliano nauhakika nao wangeandikiwa hivyo bye the way RA hakulalamika aliyelalamika kwenye tume hiyo ni Manji
 
I dont see any reason for crucifying reginald mengi.He is a patriot, a tanzanian businessman employed lots of Tanzanians, he pays taxes to the government and infact he is a senior citzen who can come out publicly to speak evils. It is quite unfortunate that poor corrurpt countreals tends to cooprate with foreigners than locals. This is a deadly syndrome of poor and corrupt government ..putting the locals for the last. Would you emaging an employee of ultimate security owned by somaiya earns only 60,000 monthly gross pay???.

mmmhhhh... hebu nikumbushe tena kifundi cha katiba kinachosema senior citizen achukue mamlamlaka ya mahakama?
 
Mengi kajipalia makaa chachandu,
Hakujua kuwa alipomgusa Rosta Aziz alikuwa anaugusa mtandao mkubwa sana wa watuhumiwa vitendo vya ufisadi,ambao kama kweli Mengi ana ushahidi zidi ya Rosatam tu, basi ni sawa kuwa mlolongo huo wote anaohusiana nao unaweza kuwa hatarini na kupelekea balaa kwa serikali ya awamu ya nne kabla ya hata uchaguzi wa 2010, ndo maana idara za usalama zinajaribu kupata kile ambacho Mengi anakusudia kukisema mahakamani kabla hakijafika huko.

kweli kabisa lakini naona ni vizuri alivyofanya mengi kwani ni ujasiri mkubwa sana.tukiendelea kuogopa kusema maovu nchi haitoendelea.na kinachofanya idara za usalama kuangaika kiasi hiki ni kutokana na ukweli wa maneno ya mengi.kama maneno ya mengi yangekuwa ya uongo lingekuwa swala dogo sana kusolve na kumuadhibu mengi.
 
"Mengi kajipalia makaa chachandu,
Hakujua kuwa alipomgusa Rosta Aziz alikuwa anaugusa mtandao mkubwa sana wa watuhumiwa vitendo vya ufisadi,ambao kama kweli Mengi ana ushahidi zidi ya Rosatam tu, basi ni sawa kuwa mlolongo huo wote anaohusiana nao unaweza kuwa hatarini na kupelekea balaa kwa serikali ya awamu ya nne kabla ya hata uchaguzi wa 2010, ndo maana idara za usalama zinajaribu kupata kile ambacho Mengi anakusudia kukisema mahakamani kabla hakijafika huko."


_______________________

Junius: Kama kweli wanafanya hayo kwa niaba dhati ya serikali kwa nini hawamkamati mzalendo huyo? Hizi ni harakati za akina RA na EL za kuwatumia wakuu fulani fulani ktk vyombo husika -- bila shaka kwa kuwanunua kwa pesa za EPA n.k. -- na kuwaamrisha kumuandikia barua za onyo, kumwita kwa mahojiano, etc ili tu kuonyesha eti kafanya jinai.

Jinai gani kafanya? Amani gani anahatarisha zaidi ya ile inayohatarishwa na hao wezi wa wananchi? Mfano huyo RA, anatumia majina ya bandia ktk kampuni zake na hao aliowanunua akina Mkuchika, Sophia Simba, maafisa wa Brela na wengine wanajifanya vipofu, mabubu etc. Inasikitisha! Inahatarisha amani!

Hivi RA ana dhamira njema kweli kwa wazalendo wa nchi hii anapotumia majina mbali mbali ktk biashara zake ambayo mengine ni ya bandia? Anaogopa nini? Anaficha nini? Atueleze. Aache kutegemea pesa za wizi kuwavuruga wakuu wa serikali kumremba, kumbeba, kumjenga!

Mengi hawamwezi katu, kwani umma wa wazalendo uko nyuma yake. Hawa wanajua hivyo na ndiyo maana hawatathubutu kumkamata. Watabakia kila kukicha kupikapika tu mambo dhidi yake.
 
A.W,
Labda niweke wazi kuwa NYUMBA KUBWA INATIKISWA, watu wanahangaikia nusra, mbona Rostam hawambugudhi?
 
Nadhani kuna tatizo hapa!
Kila kitu kinachukuliwa kama ni siasa.

TCRA ni chombo kinachojitegemea na ndani ya TCRA kuna CCC; hawa jamaa ukitukanwa kwenye mtandao au kwenye nyanja yoyote ya ICT, au service provider akilamba salio lako kwenye simu etc na mengi mengine unawapelekea... wakishapelekewa wana mwita aliyetuhumiwa kumsikiliza.

Sasa katika hili sijui kwamba wanatakiwa waendelea hata kama kuna hoja mahakama au lah!.

Lakini kule hamna siasa.

Let be serious, kwa sheria za nchi Mengi alichemsha kwa sympathy ya wananchi na kwa kuwa tumekata tamaa huenda hana kosa.

Turudi nyuma gavana wa Benk juzi tu amekataa wabunge wasiwe wajumbe wa bodi wa bank ambapo serikali ina shea... hii ilikuwa kilio cha watu wabunge wa upinzani na chama tawala lakini rais ameendelea kuwateua na mawaziri wameendea kuteua wabunge wenzao, Ndulu mteuliwa wa Rais amekataa... lakini hawezi fanywa lolote kwa kuwa BOT inajitegemea... anayefuata maelekezo ya serikali ambapo sio lazima ni udhaifu wake... na wala sio matatizo ya serikali.

Sasa mimi naona tukubali msumeno unakata pande zote.

Mkulu Kasheshe, I think that is a theoretical assumption, particularly, hapa Bongo!
 
Kuna wakati ni ngumu kukaa ukiona mjadala unavurugwa kwa makusudi. Ngojeni niwapeni dondoo kidogo hasa kwa wale wanaokurupuka bila kujua namna shughuli za media zinavyofanya kazi na maadili yake.

Mengi si mtu wa kawaida, kitendo cha kumiliki vyombo vya habari na makampuni kadhaa imemtoa katika sifa ya mtanzania wa kawaida na kuwa mfanyabiashara. Hapa kimaadili ndipo linapokuja tamko la TCRA kwa ITV. Kiufupi bwana mengi amekosea kwasababu yeye ametumia vyombo vyake kutuhumu watu wengine regardless kuwa anaushahidi au laa....waandishi wa habari wanamaadili mengi lakini moja kuu ni lile la kutochagua upande na kusema ukweli kama ulivyo.

Sasa kwa nguvu alizo nazo mengi isingekuwa rahisi kwa wafanyakazi wake kumhoji uhalali au ukweli wa taarifa alizotoa na labda wangejitahidi kuwapa nafasi watuhumiwa kujitetea au kurespond tuhuma hizo. Hapa ndipo ilipoingilia kati TCRA kwani walijua fika hakuna wa kumbana mengi juu ya ukweli wa tuhuma hizo na pia mjue kuwa kuna watu katika jamii huuamini kila kinachosemwa kwenye TV ni UKWELI, hata humu JF wapo wanaoshabikia kitendo cha mengi kwa mapenzi yao binafsi pengine waliwahi kusaidiwa na mjamaa huyo au ni kweli wanaushahidi wa aliyosema mengi, FINE let them join hands with HIM...ila ukweli unabakia kuwa hawapaswi walazimishe wote kuamini mengi alikuwa sahihi.

Kwanini TBC haikupewa order kama ya mengi...ni hoja na swali muhimu la kujiuliza. Kama wapo wanaopenda majibu ya kweli bila kuleta ubishi wa Man na Barca, ni hivi, baada ya tuhuma RA alitambua umuhimu wa kusema upande wake na ni wazi waandishi wa mengi hawakuonyesha nia ya kufanya hivyo aliwajibika kutafuta kituo kisicho na upande wowote na chenye kuaminika na wananchi (wapo wenye mtizamo tofauti), na TBC pia waliamini kuwa hiyo ilikuwa habari muhimu kwa wananchi kufahamu upande wa pili wa watuhumiwa, kwa kituo chochote makini na chenye kufuata misingi ya uandishi bora na wenye weledi wasingeweza kukataa kurusha hewani taarifa hiyo. Na pia walikuwa na uwezo wa kuchambua hoja na kuueleza umma nini kilikuwa kikiwasilishwa na Mtuhumiwa.

Tuache kumshabikia Mengi wakati anavuruga utaratibu na kama kweli anataka kumsaidia rais angeanzia mahakamani na kwa kuwa alikuwa na ushahidi basi isingekuwa rahisi kwa mahakama kupindisha sheria na kama ingefanya hivyo basi ndipo angetumia rungu lake kuuelezea umma kilichokuwa kinaendelea.

Aende tu kujibu kwani anaogopa nini.
 
Kuna wakati ni ngumu kukaa ukiona mjadala unavurugwa kwa makusudi. Ngojeni niwapeni dondoo kidogo hasa kwa wale wanaokurupuka bila kujua namna shughuli za media zinavyofanya kazi na maadili yake.

Mengi si mtu wa kawaida, kitendo cha kumiliki vyombo vya habari na makampuni kadhaa imemtoa katika sifa ya mtanzania wa kawaida na kuwa mfanyabiashara. Hapa kimaadili ndipo linapokuja tamko la TCRA kwa ITV. Kiufupi bwana mengi amekosea kwasababu yeye ametumia vyombo vyake kutuhumu watu wengine regardless kuwa anaushahidi au laa....waandishi wa habari wanamaadili mengi lakini moja kuu ni lile la kutochagua upande na kusema ukweli kama ulivyo.

Sasa kwa nguvu alizo nazo mengi isingekuwa rahisi kwa wafanyakazi wake kumhoji uhalali au ukweli wa taarifa alizotoa na labda wangejitahidi kuwapa nafasi watuhumiwa kujitetea au kurespond tuhuma hizo. Hapa ndipo ilipoingilia kati TCRA kwani walijua fika hakuna wa kumbana mengi juu ya ukweli wa tuhuma hizo na pia mjue kuwa kuna watu katika jamii huuamini kila kinachosemwa kwenye TV ni UKWELI, hata humu JF wapo wanaoshabikia kitendo cha mengi kwa mapenzi yao binafsi pengine waliwahi kusaidiwa na mjamaa huyo au ni kweli wanaushahidi wa aliyosema mengi, FINE let them join hands with HIM...ila ukweli unabakia kuwa hawapaswi walazimishe wote kuamini mengi alikuwa sahihi.

Kwanini TBC haikupewa order kama ya mengi...ni hoja na swali muhimu la kujiuliza. Kama wapo wanaopenda majibu ya kweli bila kuleta ubishi wa Man na Barca, ni hivi, baada ya tuhuma RA alitambua umuhimu wa kusema upande wake na ni wazi waandishi wa mengi hawakuonyesha nia ya kufanya hivyo aliwajibika kutafuta kituo kisicho na upande wowote na chenye kuaminika na wananchi (wapo wenye mtizamo tofauti), na TBC pia waliamini kuwa hiyo ilikuwa habari muhimu kwa wananchi kufahamu upande wa pili wa watuhumiwa, kwa kituo chochote makini na chenye kufuata misingi ya uandishi bora na wenye weledi wasingeweza kukataa kurusha hewani taarifa hiyo. Na pia walikuwa na uwezo wa kuchambua hoja na kuueleza umma nini kilikuwa kikiwasilishwa na Mtuhumiwa.

Tuache kumshabikia Mengi wakati anavuruga utaratibu na kama kweli anataka kumsaidia rais angeanzia mahakamani na kwa kuwa alikuwa na ushahidi basi isingekuwa rahisi kwa mahakama kupindisha sheria na kama ingefanya hivyo basi ndipo angetumia rungu lake kuuelezea umma kilichokuwa kinaendelea.

Aende tu kujibu kwani anaogopa nini.

Mkuu,
Tuko pamoja katika hili, Mengi amekosea sana. Nimevutiwa pale ulipo hoji kuwa ni nani katika ITV anayeweza kumkatalia Mengi hata kama anachokifanya ni kinyume na maadili ya uandishi wa habari? Tumeona mambo Mengi yanayofanywa kinyume kabisa bila hata utawala wa ITV kumkatalia boss wao.
Kwa mfano Mengi alipokuwa katika ugomvi na yule Sheikh (nadhani wa msikiti mmoja hapa Dar) ITV haikumtendea haki ya kutaka kujua chanzo cha malalamiko yake na badala yake walikuwa wakimwonesha kwa kumdhihaki na huku wakimwonesha Mengi akimshambulia bila ya yule mzee kuwa na defence yeyote. Kana kwamba haitoshi, Mengi akaanda chakula na watoto wa moja kati madrasa na kuchukua muda mwingi kuonesha tukio lile na wakati huohuo kuendelea kumdhihaki yule mzee watu masikini asiye kuwa na nguvu hata ya kuita press conference.
Ni lazima kwa serikali iliangalie hili suala na kuweka sheria zitakazo linda jamii dhidi ya watu wachache wenye tabia kama ya Mengi.
 
Fiksiman,
Mengi si mtu wa kawaida, kitendo cha kumiliki vyombo vya habari na makampuni kadhaa imemtoa katika sifa ya mtanzania wa kawaida na kuwa mfanyabiashara. Hapa kimaadili ndipo linapokuja tamko la TCRA kwa ITV. Kiufupi bwana mengi amekosea kwasababu yeye ametumia vyombo vyake kutuhumu watu wengine regardless kuwa anaushahidi au laa....waandishi wa habari wanamaadili mengi lakini moja kuu ni lile la kutochagua upande na kusema ukweli kama ulivyo
Unaposema inamtoa Mengi ktk sifa ya Mtanzania wa kawaida na kuwa mfanyabiashara una maana gani?.. yaani mfanyabiashara sii Mtanzania wa kawaida au kumiliki chombo cha habari ambacho unakitumia kutangaza habari hiyo huondoa Utanzania wa kawaida!..

Mkuu wangu hata Mohammed Interprise akiamua kuendesha bus huitwa dereva kwa wakati huo..Makosa yake yatatokana na sheria zinazofungamana na sheria za Uderava wa bus na sii sababu za Umiliki wake, basi hizo sheria zinageuka... sheria zinabakia palepale ila makosa yanaweza kuongezeka kutokana na makosa yake kama dereva wa bus... unless gari lile halina vibali vya kuwa barababani au kubeba abiria..

Huwezi kulihukumu shirika zima kwa sababu Mohammed akiendesha bus kapata ajali na kusababisha wajeruhi. waathirika watamshitaki Mohammed kama dereva na makosa aloyafanya kama dereva, hivyo ushahidi utahusiana zaidi na ajali ile kama dereva kwanza kisha yanatazamwa makosa ya gari kuwepo barabani nje ya ajali hiyo.
.
Mengi amekosea hakukosea, swala la kutaka kulihukumu shirika kwa sababu yeye ndiye mmliki haina kichwa kabisa!.. Kwanza unaanza na makosa ya Mengi na kesi inaingia mahakamani. Je, maneno haya asingeyasema Mengi, kayasema Mkandara bado sheria ingelifungia ITV hata kama kuna ukweli..Je, Vyombo vya habari haviruhusiwi kurusha tuhuma zozote za Ufisadi?..na kwa nini tunatumia makosa ya Mengi kulihukumu shirika lake, nini makosa ya shirika hilo ktk utoaji habari tukimweka Mengi kando na nje ya habari hii.. Hakuna!

Siku zote sheria za Media na maadili hazina tofauti na sheria nyingine zote.. Sheria inayomhusu Mengi inatakiwa kumhusu pia Mkandara ktk swala husika, hakuna sheria iliyotungwa kwa ajili ya mtu au baadhi ya kundi la watu na kuwa applied tofauti kwa kundi jingine..
Mengi kafanya kosa mpelekeni mahakama.. chombo cha habari hakina makosa kwa sababu mwenye ushahidi ni Mengi na hakuzungumza yale maneno akiwa kama mmiliki wa ITV bali mwnaanchi anayezungumzia Ufisadi..

Je, Kikwete akizungumza haya haya itabidi Ikulu ifungwe kwa sababu anatumia vibaya madaraka yake na kwamba kama alikuwa na ushahidi kwa nini asiende mahakamani?..Hizi ni tuhuma na sii kazi ya Kikwete, Mengi wala Mkandara ni kazi ya vyombo vya Usalama kutafuta ushahidi unawahusisha wahusika kulingana na statement ya Mengi. Kama hakuna ushahidi basi serikali au wahusika wanaruhusiwa kabisa kumshtaki Mengi kwa kupotosha Umma na kuharibu majina ya wahusika, na Sii chombo HURU cha habari kilichorusha habari hizo...
 
Mmiliki wa vyombo vya habari anaruhusiwa kutumia vyombo vyake vya habari kutangaza habari zake yeye mwenyewe au haruhusiwi? Jambo hili linawahusu wamiliki wote au baadhi ya wamiliki?
 
Back
Top Bottom