Introverts Vs Relationship

Same to me huwa wanasema nipo serious sana na ni kweli sinaga stori sana na watu nsiowafahamu na swagga zangu ni salamu mwisho.marafiki wachache pia hata mtaani huwa sifagilii kuonekana sana sio kwamba najitenga ila ndvo nilivyo naweza kaa mtaa mwezi mzima mpaka siku naondoka ndo nakutana na masela wa mtaa wakidhani ndo nimerud mtaa kumbe ndo naondoka
 
mimi ndio hata sijielewi niko wapi coz napenda kuwa private,demu nikichati nae ghafla na change nafuta hadi namba nakaa mwezi sihitaji mawasiliano.
kila demu nayekutana nae naanza kumchambua mpaka na imagination akiwa mama watoto naishia kustop.
naogopa sana kutendwa
 
Mi ndo naweza kufika tu wakati nikawa tu annoyed na kuonana au kufanya kitu na mtu yule yule kila mara. So hali hii ikikuangukia kama tulikuwa watu wa stori nakupiga ban kwa muda. Kama ilikuwa ni Ku chat kwa msg au kupiga simu naanza kukupotezea utapiga simu naiangalia tu na msg nazipotezea naweza kukutahadhalisha kwa kukwambia usipige wala kutuma sms simu imeharibika kioo, button zimeharibika nk. Kuna wale wakuja kugonga mlangoni mi niko zangu ndani, naweza tu kujisikia sitaki kuonana na yeyote siku hiyo au kwa kipindi flani so utagonga sana mlango mi ntaangalia kupitia dirishani who's knocking nikiona sio ndugu au mtu wa karibu sana naendelea na mambo yangu ndani hadi utakapojiongeza ukaamua kusepa. Pia kuna wale wageni wakuja stori zinakuwa nyingi kama niko na mwingine home ntakuacha nae mjendelee mi naenda room au nje na kama umenikuta mwenyewe kuna mawili aidha niongeze sauti ya TV au redio au nishike simu niendelee na mambo yangu huku we unajiongelesha.. life langu muda mwingine linanishangazaga mwenyewe
 
"Introvert ni mtu ambaye anahitaji muda wa kuwa pekee ili kurecharge mara kwa mara ili kuendelea na shughuli za duniani"Check this out on LinkedIn Learning: Managing Your Career as an Introvert

Hiyo nimeipata wakati nasoma kozi ya introvert.....anaweza akawa na rafiki lakini sometime anamuignore ili arecharge nguvu urafiki wao.
Nliteseka sana wakati wakuingia ukumbini kwenye harusi yangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
aisee

Mimi akija mgeni nyumbani Kama si wa muhimu Sana basi sitoki kumsalimia..nitakaa chumbani Hadi atakapoondoka.

Kuhusu kufungua mlango hiyo tabia nilikuwa nayo shule,nikiwa pekeyangu rum akaja kugonga mtu ambaye najua kabisa huyu Hana Cha maana Cha kuongea zaidi ya stories za hapa na pale Basi nilikuwa sifungui.
Nikikaa nikitulia huwa sitaki kubugudhiwa kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo uliingiaje mkuu
Tuhadithie kidogo Mambo yalivyokuwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Same here habari za kuchoreshana sipendi na sintofanya. Ni watu kadhaa wa msingi basi, kama nae muoa hata ridhika na hii then aandae sherehe ya peke yake ntaigharamikia
 
Same here habari za kuchoreshana sipendi na sintofanya. Ni watu kadhaa wa msingi basi, kama nae muoa hata ridhika na hii then aandae sherehe ya peke yake ntaigharamikia

Kwanza Mimi zile kelele kelele na shamra za sherehe huwa zinaniumiza kichwa..nitatoka hapo kichwa chote kinawaka Moto
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa hvo ndo nilivyo mimi!!!!! Dah umenigusa kumoyo, hv ww ni mwanamke au mwanaume??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hii Kama inawakuta wengi vile...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…