hearly
JF-Expert Member
- Jun 19, 2014
- 51,622
- 74,008
sorry google translategoogle map??
sorry google translategoogle map??
Aisee . yaani ndani ya miezi 12 tu anakuwa sawa na mtu mwenye umri wa miaka 50... sasa mkuu hizi nchi zilizoendelea sizitakuwa na wanausalama wengi sana ambao ni human cloning " kwa mantik hiyo neno hasara ya rasilimali watu pindi itakapo tokea maafa kwao itakuwa ni msamiati tu
hiyo ni Bio frofile ya Jim acosta...nguli wa Mwanahabari white house mbishi ,kichwa wa kuchambua habari za white house ,mpiga maswali mazito maraisi wanaoingia Ikulu huwa wanamwogopa huyu jamaa..Ohppsss .. kichwa chote kizito "
nimekuelewa vyema mkuu " salute
Aisee Kazi kweli kweli ... lmfaohiyo ni Bio frofile ya Jim acosta...nguli wa Mwanahabari white house mbishi ,kichwa wa kuchambua habari za white house ,mpiga maswali mazito maraisi wanaoingia Ikulu huwa wanamwogopa huyu jamaa..
Ila sasa ukisoma profile yake utashindwa kutrace familia yake..
hahaa " inafikirisha sana .. hiyo Tech imekuja kuleta kizaa zaa kikubwa sana duniani "... hili ni zaidi ya balaamkuu watu walishaaanza kitambo haya mambo..wakiona wew ni mtu muhimu kwao ni kutengeneza clone yako ambayo wataisubject mahala ambapo pataifaaa ili ikafanye kazi zingine mbadla bila kupoteza maarifa ya recipient( original ) yake..
Tumebaki tu sisi huku kuhangaika na kusoma eti ukawe usalama wa taifa ...ha ha ha utasubiri sana labda kuwa barozi wa nyumba kumi huku kwetu ndo usalama wa taifa.. 😕 😕
We ni geniuslifecoded ahsante mkuu ubarikiwe sana nimesoma comments zote nimefatilia mwanzo mwisho halafu wewe baba swalehe acha kunigombanisha na mkubwa wa nchi
Ooh mi ni replica wa nanhahaa lifecoded ni mzimu wa tesla ... jamaa ni bigger mind haswaa ", pongezi kwake
hauna tofauti na jiweOoh mi ni replica wa nan
hauna tofauti na jiwe
hahaa pumbavuDna helicase wewe
Ntakufumua kamahahaa pumbavu
Habari za weekend wana JF, kuna swali nimekua nikijiuliza muda mrefu sana na kuna mada iliwekwa humu JF ambapo wachangiaji wengi kina Wick na Malcom Lumumba waliijadili hii issue ila kwa kugusia tu maana haikuwa kiini cha mada.
Ukweli mchungu: Pasipo anguko la Malaika (Sons of Gods/Watchers/Anunnakis/Aliens), Mwanadamu angeendelea kubaki kilaza. - JamiiForums
Humo ndani kuliibuka debate kama akili za binadamu ni hereditary/genetic au ni mazingira. Baada ya kusoma tafiti /makala kadhaa nikaona nilete mada humu ili tuweze kujadili suala hili kwa upana zaidi na niweze kupata conclusive answer kwa mjadala ule. Na source yangu kubwa ni study hii ya huyu neurosurgeon niliyeambatanisha pdf yake hapo chini.
View attachment 919915
UTANGULIZI
Akili kwa kifupi tu tunaweza kusema ni uwezo wa kufikiri au kuchanganua masuala mbalimbali yanayotuzunguka na kwa mingi wanasayansi wamejaribu kupima hiyo "akili" kati ya mtu na mtu ili kuweza kufahamu sababu halisi za kuwepo utofauti huo yaani mtu kuwa na akili ''ndogo'' au ''kubwa'' kuliko mwenzake.
Mnamo mwaka 1905 serikali ya ufaransa ilitaka kuanzisha mfumo wa "elimu kwa wote" hivyo ikataka kugundua watoto wenye ''akili ndogo'' ili wapewe elimu maalum kuwawezesha kusoma kwa spidi yao kuliko kuwabakisha nyumbani tu au kuitwa "wehu". Mtihani huu uliitwa stanford-simon test ambapo ulikuwa unapima vitu vikuu vitano ambako na sisi ningependa tutumie tunapoendelea na mjadala huu sababu hizi factors ndio zimeweka msingi wa IQ tests na mbinu karibu zote duniani za kupima akili ya mtu.
1.Maarifa (knowledge) ambapo hapa wanapima kama mtoto ana uwezo wa kuelewa mambo yanayomzunguka mfano mtoto aliulizwa kushiba au kuchoka ndio nini?
2. uchanganuzi wa hesabu (Quantitative reasoning) ; Hapa mtoto anaulizwa masuala ya hesabu ili kupima uwezo wa akili yake mfano kujumlisha,kutoa,kugawanya n.k
3. Working memory yaani Kumbukumbu ya muda mfupi ambapo hapa wanapima kama mtoto ana uwezo wa kutunza mambo aliyofundishwa au kuyashuhudia muda mfupi tu uliopita mfano kama unawaonyesha picha basi unawauliza picha ya kwanza kuwaonyesha ilikuwa ya nani.
4. Visual-spatial processing yaani utambuzi wa vitu kwa kuangalia mfano uhusiano baina ya picha na zaidi inayotumika ni puzzle ambapo mtoto alitakiwa kupanga vipande tofauti ili vitengeneze picha moja.
View attachment 919908
5.Ya mwisho ni uwezo wa kuchanganua (fluid reasoning) yaani uwezo wa kufikiri na kupata suluhisho kwa jambo ambalo halitegemei kitu ulichowahi fundishwa au kukutana nacho huko nyuma mfano kuunganisha dots za suala fulani fulani ili upate picha kamili mfano hapa chini ambapo mtoto ataulizwa umbo gani ndio sahihi kuwekwa kwenye alama ya kiulizo??
View attachment 919909
NADHARIA
Baada ya kujua baadhi ya vitu tunavyopima kwenye uwezo wa akili ya mtu.... Basi tuangalie nadharia mbalimbali zilizoletwa juu ya mjadala huu.
1. Akili hurithishwa /Heritability.
Kwenye nadharia hii baadhi ya wanasaikolojia wamejaribu kufanya tafiti mbalimbali kuonyesha kuwa akili ya mtu hurtishishwa kutoka kwa mzazi hivyo uwezo wa akili za wazazi ndio utaamua uwezo wa wanaye kwa kiasi kikubwa. Kwa mujibu wa tafiti nilioambatanisha hapo chini inaonyesha mapacha wakufanana wana wana akili (IQ) zinazofanana kuliko mapacha wasiofanana ikimaanisha jenetiki zina nafasi ya kucheza kwenye kuamua akili ya mtoto. Vilevile utafiti mwingine ukaonyesha ndugu waliokuzwa kwenye nyumba moja wana akili zinazofanana kuliko watoto wasio na undugu waliokuzwa eneo moja ikimaanisha genetics za kifamilia ndio huamua akili ya mtoto na sio makuzi/malezi n.k
Nadhari nyingine inayotumika humu ni wilson effect ambayo inasema mtu anapozidi kukua basi uwezo wa akili yake unakuwa umechangiwa na akili za kurithi kuliko sababu zingine zozote na alihitimisha kwa utafiti unaoonyesha 60% mpaka 80% ya akili ya mtu mzima huwa imerithiwa kutoka kwa kizazi chake na zilizobaki ndio sababu zingine kama elimu,makuzi,mazingira,uzoefu,afya n.k
2. Mazingira/makuzi
Nadharia ya pili inadai mtoto huzaliwa na uwezo wa akili wa kawaida ila mazingira au makuzi atayakayopata ndio yataamua akili yake hapa duniani. Tafiti mbalimbali zimefanyika mfano weinberg (1989) unaonyesha mapacha wanaofanana waliokuzwa mazingira tofauti kabisa uwezo wa akili zao haukufanana ikimaanisha uwezo wa akili huamuliwa na mazingira ambayo mtoto anakulia na sio kurithi akili za mzazi. Mfano mtoto ambaye baba na mama yake wana akili ila amekulia mazingira ya umaskini hivyo kula yake ni ya shida na hapati lishe bora hasa udogoni inaathiri size ya ubongo wake hasa ubongo wa mbele (frontal lobes) hivyo itasababisha uwezo wake wa akili kupungua sana. Ama mtoto mwenye uwezo mdogo wa akili akikulia mazingira ambayo wazazi wanamjengea uwezo wa kufikiri kama kumpa maarifa kadha wa kadha toka akiwa mdogo,kusoma vitabu,mitihani ya kimaisha ya kumfanya afikiri basi mtoto huyu akili yake (IQ) itapanuka muda unavyozidi kusogea.
View attachment 919916
Tabula rasa
Hii ni nadharia iliyoanzishwa na John locke (1690) inayodai mtoto akizaliwa huwa ni MWEUPE kichwani ila uwezo wake wa akili utaamuliwa na mazingira,uzoefu,maarifa atakayopata kwenye makuzi,mazingira au uzoefu anavyozidi kukua. Hivyo kwa kiujumla nadharia hii inasema haijalishi mtoto kazaliwa na akili gani ila makuzi yake ndio yataamuwa kama atakuwa na akili ''kubwa'' au ''ndogo''.
NB: tunapoongelea akili hatumaanishi za darasani na hatumaanishi jinsi mtu anavyozitumia bali tunamaanisha UWEZO wa juu zaidi ambao anaweza kutumia kufikiri hata kama bado hajaamua kuutumia ipasavyo. Kiufupi tunaangalia brain CAPACITY sio PERFORMANCE. Maana kuna wengine wana akili kubwa ila hawajawekewa mazingira ya kuzitumia kwa ukamilifu wake so tunapojadili tuwe nalo hili kichwani.
Naomba kuwasilisha
Cc
Mchawi Mkuu Malcom Lumumba Elungata Da'Vinci Mshana Jr Eiyer Kudo900 Vi rendra N J subi Bujibuji Kipanga boy Kiranga Che mittoga Ip man 3 mitale na midimu Mzee wa Torano Blaki Womani Grahnman za chembe jimmykb197 911sep11 afsa Francis3 mtu chake NJOLO Msolo Shubiri Pori Pendael24 Mr Miller Elli Khalifavinnie Kennedy Son of Gamba Kanungila Karim Mgambilwa ni mntu Mr FCB Mr Q geesten66 Jerry Ekky Mnabuduhe Chrisvern Dabby Jr kibuyu180 IGWE SALA NA KAZI
Wick Dukeson lifecoded Daimler monde arabe mtu watu
Shukran mkuu, umeongelea factor mbali mbali zinaweza kuleta hayo matatizo ya vichocheo vya kulisha ubongo kukosekana na kuleta hizo mental disability. Na vipi haya ma chromosomal disorder, kama mutation na mengine kwenye hii inteligency issue. Sijui ni gene gani zina husika kutengeneza bongo zetu, lakini hii brain ina tokana na gene pairing during meiosis kama sikosei, na sayansi ya embriology haisemi ni nini au genes zipi zinaunda ubongo au sijui ndio akili, wao husema tu viungo mbali mbali hutengenezwa during differentiation ya mesenchymal sterm cells, humo ndimo hutokea deletions, invertion, translocation na mengine hadi tuna pata hayo ma disabilities mbalimbali.ha ha ha ha inawezekana kabsa kuzaa au kupata mtoto taahira katika mazingira yote haijalishi nyumbani kwenu kuna natural history ya mental disorders among familiy members au laaa...
Lakini kuna study nyingi zimeshafanyika kuhusu kuzaaa watoto wenye mental disability huku wazazi wao wakiwa wazima kabsaa bila hata kuwa na family history ya ugonjwa huo.
kwa mfano mama anapokuwa na stress za kufaaa mtu wakati akiwa mjamzito anakuwa anazuia baadhi ya vichocheo( hormones) kusafirishwa kwenda kwa mtoto hasa vichocheo vinavyohusika na brain formation vinapokuwa haba kwa mtoto ,hapo mtoto lazima azaliwe na mental disorder flani..
Mama akiwa na depression( msongo wa mawazo) akiwa mjamzito lazima apate effects kubwa sana mtoto wake..
lakini pia inawezekana kabisa professor mzima akapata watoto taahira kama msomi huyu atapata mental disconfiguration akiwa mzima( namanisha akiwekwa kwenye mazingira ambayo yatachange au ku alter mental status yake ) hapo percent ya kupata mtoto taahira ni 25% .
Kwa hiyo Intelligence inabaki ni multifactorial continnum hasa katika inheritance yake..
Lakini haimanishi kuwa mtoto akiwa taahira tayari anakuwa na uwezo mdogo wa akili hapana..
kuna watu ni vichaaa lakini wana intelligence kubwa,inategemea na eneo gani kwenye ubongo( mind) limekuwa disfigured na enveronmental factors...
Intelligence ipo vice versa na mental disability...tena inasemekana kwamba kadri mtu anavyozidi kuwa na IQ kubwa ndipo anazidi kuwa na symptoms ( Dalili) za ukichaaa kuliko mtu anayejiheshimu zaidi!!
Fuatilia maisha ya akina Tesla,Isaac newton,Galileo Gallilei na Albert Einsten na wengine kibao ,yani maisha yao yalikuwa ni kujitengetenga na jamii na unakuta sometimes mambo ambayo jamaaa imekubaliana tusiyafanye wao ndo walikuwa wanayafanya na ndo mana walikuwa wanaonekana kituko simply because their sense of cognition ipo katika dimension kubwa sana kuanzia 6D huko kuliko Ng'ng'ona wengine wenye 2D recognition view..
Ndo mana unaweza uka asses intelligence spectrum range ya mtoto wako akiwa mdogo kabsaa...
Key factor ya kwanza ni mtoto kujitenga na wenzie..yani unakuta anapenda kucheza peke yake..ukiona hivyo jua mtoto wako ni bonge la genius wa kutupa usimwachanize mazingira yakamharibu..kaa naye makini sana.
Keys factor nyingine kudetermine mtoto wako ni intelligence ni utundu wa kutupa huku akiwa lonely muda mwingi hawa tunawaweka kwenye Autistic spectrum disorders japo study nyingi zinasema watoto watundu wanakuwa na IQ ndogo kwa sababu wanakosa concentration ya kusikiliza lakini 25% ya watoto ambao ni Autistic ( wana Autism) wana IQ kubwa sana...
Kwa hiyo intelligence bado inaonekana kuwa ni multifactorial continnum kabsaa...japo gene ndo zinabaki kuwa wahusika wakuu sana wa kuleta intelligence ya mtu..
Hii hatari had Tanzania tuje tufike hii level ya wenzetu tutakuwa hatuwezi tena ku fikiria tena aisee.Fuatilia namna ya kuajili wataalamu wa intelligensia nchi zilizoendelea utakuta bioprofile data zao zinachekesha kama sio kuchanganya...
Utakuta baba yake kaandikwa kuwa ni mzawa wa Israel na mamake ni mzawa wa Australia ili iwe ngumu kumtrace zaidi..
ndo mana inakuwa ngumu sana kujua originality ya Intelligence officers...
fuatilia utakuja kunambia...
nasikia hata ikulu maalumu zimeanza kuwa na Artificial Intelligence officers..
Kwa mfano ikulu ya marekani inamshitukia sana mwanahabari wa CNN Abilio James "Jim" Acosta ambaye juzi kama sio jana kapigwa marufuku kuingia white house huku kwa kuwa na kibuli cha kubishana na jiwe( Trump) 😀 akiwa na nature ya kuwa clone...jamaa inasemekana ni clone na kapandikizwa pale white huse kuwa reporter wa CNN lakini inasemekana jamaa ni replica clone wa mtu ..
Na ukifuatilia uraia wake jamaa unashangaza mara baba yake sijui ni nani na mamake taifa gani ...
Aise wenzetu wapo level zingine kabsa sasa hivi...
Juzi juzi tu nchi ya tunisia imepewa Ma Intelligence officers kutoka Israel lakini inasemekana ni ma clone kabssa na lengo lao ni kuchota taarifa muhimu...
Nadhani hii ya cloning kafanyiwa pia Kanye West maana kichwa chake siku hizi pia ma star wa kubwa ni ma cloning ka kina Oprah nilisoma hizi habari za cloning zikanichaganya Ila ufafanuzi wako umenifunua akilianakuwa ni replica Intelligence...ila ananyimwa kumbukumbu ...ne needs memory booster kumrejeshea ya nyuma but after that anakuwa sawa...
Mammbo mazito chief...
Hahaha hii JF unauliza wataelewa wangapi?! Kwa taarifa yako humu kila mtu genius, JF bana ukieleza issue shallow utapondwa sana, mi nakubali lifecoded anavyoeleza, hizi ID fake za JF nyuma yake kuna watu wa kila aina, na interest tofauti. Unaweza mdharau mtu kumbe lecturer wa cell biology huko havard. Uwe unasoma tu na kupita, ni kweli wapo tusioelewa lakini kwa like alizopata lifecoded ina maana wameelewa hao.Duh umeeleza sana katika molecular level/proffesional explanation...sasa sijui wataelewa wangapi
Hahaha hili swala la sorrogate mothers linaweza kulisha swali langu la taahira aliyebakwa na kuzaa mtoto mzima, sijui huyu mama ana mchango gani ikuwa embryology ikiishatokea kinachofuata ni mesenchymal cell differentiation mpaka kuzaliwa?! Vipi watoto wa chupa yaani IVF baby wanapata wapi vichocheo hivi kutengeneza brain zao ikiwa zaidi ya 6 weeks w ako nje mama?!lakini pia kuna ukakasi sana juu ya kutumia Surrogate mother kwenye human cloning ambapo tunaona kuwa watu wanatak kutoa specie au clone yenye uelewa ule ule na mhusika ila wanampandikizia mother ( surrogate) na anakuja kedeliver product ile ile desired....
sasa hapa najiuliza tena mchango wa mama unakosekana....ha ha ha hatari snaa...