Wafadhili, ila sitaenda mbali.Nijuavyo mimi Intarahamwe ni kundi ambalo lilihusika ktk mauaji ya kimbari(genocide) kule Rwanda,
Ni nini kimemsukuma Prof.LIPUMBA kuwaita wajumbe bunge la katiba wanaounga mkono serikali 2 kuwa ni Intarahamwe?
Kwa mtu anayeheshimika kuwa msomi , Prof Lipumba amejishushia hadhi mbele ya jamii.
Intarahamwe waliua na kukandamiza haki za watu wasiokuwa na Hatia,CCM na serikali yake kupitia BMK wameamua kuua mawazo, maoni na mapendekezo ya wananchi. Na kama hujasahau pale walipojitokeza wapigania hali za waliokandamizwa walivamiwa, kutekwa na kuuliwa na pengine kutupwa mabwepande. Kama walikuwa hawahusiki mbona hajakamatwa hata wa kusingizia kama yule mkenya? Nalishangaa Kanisa Katoliki waliigwa pale O;asiti mbele ya Ba;ozi wa Papa lakini kwa mshangao Kadinari anapigia chapua serikari ya CCM na sera ya serikali mbili....
Maoni ya Prof. Lipumba yanaweza kuwa na ukweli kwa kuangalia na kuijua Intarahamwe vema,,,
Lugha aliyoitoa Profesa Lipumba Bungeni akiongoza kususia Bunge la Katiba hakika imesitua wengi.
Siyo siri, ni lugha ya uchochezi.
Pengine Lipumba anasitiriwa kwa vile ni kiongoxi mwenye jina kuba katika upinzani na siasa za Tanzania, na amegombea urais miaka iliyopita.
wengi wetu tusio katika siasa huwa tunatazama mantiki ya argument na kuyaweka mambo yote kwenye mizania.
Kutofautiana katka siasa na wanasiasa ni jambo la kwaida, na hata kususia vikao kwa nchi yetu sasa hivi imezoeleka.
Hata hivyo kusikia kiongozi mkuu wa upinzani anatoa matamshi yanayotaka kuhamisha mauaji ya kimbari toka nchi jirani ya Rwanda na kuifananisha na nchi yetu, mimi naona si jambo la kuvumilika.
Lipumba inabidi atuambie kama kuna Intarahamwe humu nchini inayoongoza mauaji ya kimbari , basi atuambie Watusi naouwawa ni nani hao?
Na Wahutu waliokuwa wengi huko Rwanda wakiongoza mauaji ni nani?
Twaomba Lipumba atoe ufafanuzi, la sivyo achukuliwe hatua kwa kutoa uchochezi!
Prof.Lipumba na UKAWA kwa ujmla wenu mna makosa, tena huku mtaani sifa yenu sio nzuri kwa haya mnayoyasema na kufanya.
Kuhusisha Intarahamwe na ndugu zetu watanzania ni kosa kubwa sana.
Kumdhihaki Baba wa Taifa ni kosa kubwa sana kwani watanzania wengi wanamuenzi Nyerere, kumbuka Nyerere day 14/10 kola mwaka.
Kujitoa Bungeni ni kosa kubwa na imewauma watanzania wengi, hasa ukizingatia gharama zilizokwisha tumika.
Usione kwanini mnatoa matamko wananchi Wako kimya mkadhani ni bahati mbaya au hawajasikia, hii ni kwasababu mmekosea kwa mambo mengi mpaka sasa.
Jirudini mtubu la sivyo mtaishia kuaibika sana.
Umefanya Utafiti gani lini na sampuli yako ni kubwa kiasi gani isije ikawa sawasawa na kura za Jamaa za mwaka 2010 na sasa anapeperusha bendera kwa ziara za majuu tu. Acha uongo, hayo ni mawazo yako binafsi. CCM inasema kama watu wakinyamaza maana yake jambo hilo haliwasumbui? Nenda darasani kama umeunga unga shule yako, Mie naamini sasa ndo mmepata fursa ya kuleta ile rasimu mliyowakaririsha wajumbe wenu muipitishe fasta. Yaani mnawataka UKAWA ili kuhalalisha mbinu zenu chfu. Pigeni kazi kama mnavyohamisha meno ya tembo bila kikwazo, kama mnavyouza raslimali asilia kwa wachina na wamarekani bila vikwazo vyovyote. Pigeni kazi kama mnavyowarishisha watoto weny kwenye vyeo baba zao wanapostaafu ama kufariki kama Kalenga na Chalinze.
Kwa mtu anayeheshimika kuwa msomi , Prof Lipumba amejishushia hadhi mbele ya jamii.
Sina tatizo na yeye kutofautiana na CCM, tatizo langu nu kutoa ulinganishi, au analogy isiyo na msingi.
Interhamwe ni wauaji wa kimbari, yeye Lipumba yuko hai hajauwawa na katoka Bungeni kwa hiari, ili aweke shinikizo.
Lakini kuta wengine Interhamwe ni jambo la kipuuzi na kichochezi kwa mtu kama Lipumba.
Lugha aliyoitoa Profesa Lipumba Bungeni akiongoza kususia Bunge la Katiba hakika imesitua wengi.
Siyo siri, ni lugha ya uchochezi.
Pengine Lipumba anasitiriwa kwa vile ni kiongoxi mwenye jina kuba katika upinzani na siasa za Tanzania, na amegombea urais miaka iliyopita.
wengi wetu tusio katika siasa huwa tunatazama mantiki ya argument na kuyaweka mambo yote kwenye mizania.
Kutofautiana katka siasa na wanasiasa ni jambo la kwaida, na hata kususia vikao kwa nchi yetu sasa hivi imezoeleka.
Hata hivyo kusikia kiongozi mkuu wa upinzani anatoa matamshi yanayotaka kuhamisha mauaji ya kimbari toka nchi jirani ya Rwanda na kuifananisha na nchi yetu, mimi naona si jambo la kuvumilika.
Lipumba inabidi atuambie kama kuna Intarahamwe humu nchini inayoongoza mauaji ya kimbari , basi atuambie Watusi naouwawa ni nani hao?
Na Wahutu waliokuwa wengi huko Rwanda wakiongoza mauaji ni nani?
Twaomba Lipumba atoe ufafanuzi, la sivyo achukuliwe hatua kwa kutoa uchochezi!
Sasa mbona watu wako kimya hata baada ya wao Kutoka nje ya Bunge, Takwimu za Warioba zimewaponza sasa, wataishia kupata aibu isiyotarajiwa, kwani huoni appetite ya move yao imedoda.