INTARAHAMWE WA Prof.LIPUMBA

INTARAHAMWE WA Prof.LIPUMBA

Lugha aliyoitoa Profesa Lipumba Bungeni akiongoza kususia Bunge la Katiba hakika imesitua wengi.
Siyo siri, ni lugha ya uchochezi.
Pengine Lipumba anasitiriwa kwa vile ni kiongoxi mwenye jina kuba katika upinzani na siasa za Tanzania, na amegombea urais miaka iliyopita.

wengi wetu tusio katika siasa huwa tunatazama mantiki ya argument na kuyaweka mambo yote kwenye mizania.
Kutofautiana katka siasa na wanasiasa ni jambo la kwaida, na hata kususia vikao kwa nchi yetu sasa hivi imezoeleka.

Hata hivyo kusikia kiongozi mkuu wa upinzani anatoa matamshi yanayotaka kuhamisha mauaji ya kimbari toka nchi jirani ya Rwanda na kuifananisha na nchi yetu, mimi naona si jambo la kuvumilika.

Lipumba inabidi atuambie kama kuna Intarahamwe humu nchini inayoongoza mauaji ya kimbari , basi atuambie Watusi naouwawa ni nani hao?
Na Wahutu waliokuwa wengi huko Rwanda wakiongoza mauaji ni nani?

Twaomba Lipumba atoe ufafanuzi, la sivyo achukuliwe hatua kwa kutoa uchochezi!

Hatua mchukulieni kwanza kikwete aliyetishia kuipindua nchi kijeshi. Na ukiandika uzi mwingine tumia kichwa sio makalio.
 
Lugha aliyoitoa Profesa Lipumba Bungeni akiongoza kususia Bunge la Katiba hakika imesitua wengi.
Siyo siri, ni lugha ya uchochezi.
Pengine Lipumba anasitiriwa kwa vile ni kiongoxi mwenye jina kuba katika upinzani na siasa za Tanzania, na amegombea urais miaka iliyopita.

wengi wetu tusio katika siasa huwa tunatazama mantiki ya argument na kuyaweka mambo yote kwenye mizania.
Kutofautiana katka siasa na wanasiasa ni jambo la kwaida, na hata kususia vikao kwa nchi yetu sasa hivi imezoeleka.

Hata hivyo kusikia kiongozi mkuu wa upinzani anatoa matamshi yanayotaka kuhamisha mauaji ya kimbari toka nchi jirani ya Rwanda na kuifananisha na nchi yetu, mimi naona si jambo la kuvumilika.

Lipumba inabidi atuambie kama kuna Intarahamwe humu nchini inayoongoza mauaji ya kimbari , basi atuambie Watusi naouwawa ni nani hao?
Na Wahutu waliokuwa wengi huko Rwanda wakiongoza mauaji ni nani?

Twaomba Lipumba atoe ufafanuzi, la sivyo achukuliwe hatua kwa kutoa uchochezi!

Lipumba hana tofauti na magazeti ya Rwanda yanayomchafua mh Kikwete kama wanyarwanda wanamtusi Rais wetu kwa kumwita Intarahamwe na Lipumba akasema hayo, unapata picha gani?
 
Prof.Lipumba na UKAWA kwa ujmla wenu mna makosa, tena huku mtaani sifa yenu sio nzuri kwa haya mnayoyasema na kufanya.

Kuhusisha Intarahamwe na ndugu zetu watanzania ni kosa kubwa sana.

Kumdhihaki Baba wa Taifa ni kosa kubwa sana kwani watanzania wengi wanamuenzi Nyerere, kumbuka Nyerere day 14/10 kila mwaka.

Kujitoa Bungeni ni kosa kubwa na imewauma watanzania wengi, hasa ukizingatia gharama zilizokwisha tumika.

Usione kwanini mnatoa matamko wananchi Wako kimya mkadhani ni bahati mbaya au hawajasikia, hii ni kwasababu mmekosea kwa mambo mengi mpaka sasa.

Jirudini mtubu la sivyo mtaishia kuaibika sana siku sio nyingi.

Tuacheni unafiki hivi mlikuwa hamjui kuwa rasimu ni ya serikali tatu?
 
Inawezekana unajaribu kudhani ukiwa nje ya bunge na u mwananchi wa kawaida.

Ila najaribu kutafuta link iliyopo kati ya maneno ya Prof. Lipumba na mchakato wote wa katiba kama viliendana na uliyoyasema wewe, nadhani hata Lipumba mwenyewe haamini iwapo aliyasema yale maneno
Intarahamwe waliua na kukandamiza haki za watu wasiokuwa na Hatia,CCM na serikali yake kupitia BMK wameamua kuua mawazo, maoni na mapendekezo ya wananchi. Na kama hujasahau pale walipojitokeza wapigania hali za waliokandamizwa walivamiwa, kutekwa na kuuliwa na pengine kutupwa mabwepande. Kama walikuwa hawahusiki mbona hajakamatwa hata wa kusingizia kama yule mkenya? Nalishangaa Kanisa Katoliki waliigwa pale O;asiti mbele ya Ba;ozi wa Papa lakini kwa mshangao Kadinari anapigia chapua serikari ya CCM na sera ya serikali mbili....

Maoni ya Prof. Lipumba yanaweza kuwa na ukweli kwa kuangalia na kuijua Intarahamwe vema,,,
 
Ccm hawajaenda kwa wananchi wakakusanya maoni ya serikali mbili.aliye kwenda kwa wananchi ni warioba na tume yake na wananchi wakasema tatu sasa kama wanatumia ubabe kupinga maoni halali kwa nini tusiwaite INTERAHAMWEEEEEEE!!
 
Nadhani jazba ilitawala kuliko hekima. Personality yake ni 0%. Mi kwanza huwa simpendi, hana mvuto wa kisiasa wala hana ushawishi. Ki muonekano na hata kama akiwa jukwaani hafananii na kuwa mwanasiasa. Nadhani walikosea waliomdanganya kuingia siasa, tunasema aliingia choo cha kike angali ni mwanaume! Pole zake, ataendelea kuwapigia saluti watu wasiokuwa hata na digirii.
 
Shida ya Lipumba kabebwa na siasa za kihuni naye kabebeka mwacheni atatukuta mwakani sijui kama hata kura elfu kumi atapata.

Hivi bado anagombeaga yeye tuuuuuu?

HUYU NDIYE
HASWAAA KOFIA YA 'INTERAHAMWE' INAMTOSHA!
(HEBU WOTE WANAOJIFANYA 'UKAWA' WAAZIMIE KWA PAMOJA KWAMBA MGOMBEA WAO WA URAIS AWE LISSU TUWAAMINIAMINI KIDOGO!)

 
ccm wengi wao hawatumii akili zao,wameambiwa na wakuu wao serikali mbili na wao wameng'ng'ania.
 
Tatizo la wana CCM ni maneno ya kuambiwa, Kama Lipumba Kajishushia hadhi inakuathirije wewe? Nime kuomba takwimu za Utafiti wako huo umeshindwa , sasa unakuja na longolongo ya kujishushia hadhi Lipumba. Ndugu zangu wana CCM mnapaswa kujua kwamba kila enzi na kitabu chake, enzi za kuishi kwa uongo na ujanja ujanja sasa basi.
UKAWA wamewapisha mpitishe Katiba yenu ya serikali mbili, na sasa tena mnazunguka zunguka, Sasa mnataka mfanyiwe nini? Sasa mmetumwa na Lumumba Project kujitafutia uhalali humu jamvini, nadhani hapa sio mahali pake. Pesa za kuhonga mnazo, Usalama wa Taifawapo kuwalinda, TCCCM ipo kuwapa coverage, Jeshi lipo kupindua iwapo ikibidi ziwe serikali tatu maana kumbe nako huko wameshapenyezwa makada wa chama. Sasa Mungu awape nini,
Kwenye Raslimali mnaruhusiwa kusaini mikataba na yeyote hata kama ni 17 usiku wa manane.
Wauza Unga wanapita bila shida yeyote hata kama scanner za Airport ni nzima au mbovu, Twiga wanaruhusuwa kupanda ndege kwenda Uarabuni,
Orodha ya Majambazi mnayo na wala haiwapi shida. Orodha ya wauza Unga pia ipo na hakuna linaloharibina maana chama kimeshika patamu

Umewapigilia msumali mkali.

CCM fisadi, wauza unga na majangiri wa tembo kuwang'oa madarakani kidemokrasia ni kazi ngumu...na bado watazalisha interahamwe zaidi ya ilivyokuwa Rwanda...

It's very abnormal kuona siasa inavyoendeshwa Tanzania. Uongo uongo kila mahali. Nini kinachowazungusha ccm sasa na propagada zao serikali3?
 
Nanukuu tafadhali kulingana na maneno ya Mh Lipumba wale wote wasiopenda haki nakutetea masirahi yao kama ccm ni Intarahamwe....
mi Ukawa jamani na Intarahamwe sijui mwenzangu.
Natetea masirahi ya wananchi wenzangu!!
Nakuunga mkono serikali 3!!
 
Umefanya Utafiti gani lini na sampuli yako ni kubwa kiasi gani isije ikawa sawasawa na kura za Jamaa za mwaka 2010 na sasa anapeperusha bendera kwa ziara za majuu tu. Acha uongo, hayo ni mawazo yako binafsi. CCM inasema kama watu wakinyamaza maana yake jambo hilo haliwasumbui? Nenda darasani kama umeunga unga shule yako, Mie naamini sasa ndo mmepata fursa ya kuleta ile rasimu mliyowakaririsha wajumbe wenu muipitishe fasta. Yaani mnawataka UKAWA ili kuhalalisha mbinu zenu chfu. Pigeni kazi kama mnavyohamisha meno ya tembo bila kikwazo, kama mnavyouza raslimali asilia kwa wachina na wamarekani bila vikwazo vyovyote. Pigeni kazi kama mnavyowarishisha watoto weny kwenye vyeo baba zao wanapostaafu ama kufariki kama Kalenga na Chalinze.
Hebu fikiria ktk secta moja tu ya BENK KUU tunawakuta watoto wa vigogo1.FILBET SUMAYE 2.BEATRICE BOMANI3.PAMELA LOWASA4.ZACHARIA KAWAWA5.SALAMA MWINYI6.RACHEL MSEKWA7.SALAMA MAHITA 8.JANE SITA9.JASMIN KARUME 10.JUSTINA NCHIMBI11.BLASIA W.MKAPA12.RADHIA SHEIN13.JEROME DIALO 14.LIKELE NGASONGWA 15.ANDY MAGUFULI-16.THOMAS MONGELA17.JABIR KIGODA 18.MARY MRAMBA


Hawana aibu nguruwe hawa sijuwi watanzania tumelogwa na nani
 
Lipumba hana tofauti na magazeti ya Rwanda yanayomchafua mh Kikwete kama wanyarwanda wanamtusi Rais wetu kwa kumwita Intarahamwe na Lipumba akasema hayo, unapata picha gani?
Kwa matamshi aliyotoa Lipumba anaanza kukosa sifa za Kitaifa!
Sana sana anamsarandia Lissu, amejidowngrade kweli kweli.
 
Nanukuu tafadhali kulingana na maneno ya Mh Lipumba wale wote wasiopenda haki nakutetea masirahi yao kama ccm ni Intarahamwe....
mi Ukawa jamani na Intarahamwe sijui mwenzangu.
Natetea masirahi ya wananchi wenzangu!!
Nakuunga mkono serikali 3!!

mimi natetea masilahi ya wananchi wenzangu naunga mkono serikali moja!
 
Back
Top Bottom