Bungeni: 2016/18 Bodi ya Mikopo ilitoa Tsh. Bil 1.76 kwa wasio na sifa kwa maelekezo ya Serikali

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,117
Ukaguzi uliofanywa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) umebaini HESLB iliwapa Mikopo Wanafunzi ambao hawakuwa Vyuo Vikuu kwa maelekezo ya Serikali.

Pia, PAC imesema kati ya 2018/19 wanafunzi 2,852 walipangiwa mikopo chini ya kiwango kwa upungufu wa Tsh. Bilioni 1.14 huku Tsh. Bilioni 2.25 zikilipwa kwa wasiokuwa na uhitaji.

Aidha wanafunzi 6,182 walipangiwa mikopo zaidi ya kiwango kwa kiasi cha Tsh. Bilioni 5.66 wakati wanafunzi wapya wengi wakipangiwa chini ya 100%.

=======================

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (PAC) imebaini utoaji wa mikopo inayofikia Sh1.76 bilioni kwa wanafunzi wasiostahili katika kipindi cha kati ya mwaka 2016 hadi mwaka 2018.

Hayo yamesemwa leo Jumanne Novemba 2, 2022 na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Japhet Hasunga wakati akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo kuhusu ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka unaoishia Juni 30, 2021.

Amesema mikopo hiyo ilitolewa kati ya mwaka 2016 hadi 2018 kwa wanafunzi ambao hawakuwa kwenye vyuo vya elimu ya juu lakini walipewa mikopo kwa maelekezo ya Serikali

Amesema uchambuzi wa taarifa ufanisi kuhusu upangaji na ugawaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kumeonekana uwepo wa maboresho makubwa katika taratibu za utoaji wa mikopo na ongezeko la idadi ya wanufaika wa mikopo husika.

Amesema pia kumekuwa na ongezeko la wanufaika wa mikopo kutoka 116,706 (2016/2017) hadi 149,389 (2020/2021). Alisema upangaji wa mikopo usiotosheleza kwa wanafunzi wapya ambapo Bodi haikuweza kutoa mikopo kwa asilimia 100 kwa waombaji waliostahili.

Alisema walibaini pia waombaji kupangiwa ada chini ya kiwango na zaidi ya kiwango cha ada stahiki na kwamba mwaka 2018/2019 wanafunzi 6,182 walipangiwa mikopo zaidi ya kiwango kwa kiasi cha Sh5.66 bilioni.

Alisema wanafunzi 2,852 walipangiwa mikopo chini ya kiwango kwa upungufu wa Sh1.14 bilioni na upangaji wa mikopo inayofikia Sh 2.25bilioni kwa waombaji wasiokuwa na uhitaji.

“Kutowapangia mikopo wanafunzi wanaostahili kupata mikopo na usimamizi hafifu wa bakaa na fedha za wanafunzi wanaohama vyuo na uhamasishaji duni wa vyanzo vingine vya fedha kwa ajili ya mpango wa mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu,” amesema.

MWANANCHI
 
Ukaguzi uliofanywa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (PAC) umebaini HESLB iliwapa Mikopo Wanafunzi ambao hawakuwa Vyuo Vikuu kwa maelekezo ya Serikali.
Hehehe

Watu wakiamua lao huwa hawapoi hadi litimie.

Wenye akili wanag'amua mapemaaa
 
Ukaguzi uliofanywa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) umebaini HESLB iliwapa Mikopo Wanafunzi ambao hawakuwa Vyuo Vikuu kwa maelekezo ya Serikali.

Pia, PAC imesema kati ya 2018/19 wanafunzi 2,852 walipangiwa mikopo chini ya kiwango kwa upungufu wa Tsh. Bilioni 1.14 huku Tsh. Bilioni 2.25 zikilipwa kwa wasiokuwa na uhitaji.

Aidha wanafunzi 6,182 walipangiwa mikopo zaidi ya kiwango kwa kiasi cha Tsh. Bilioni 5.66 wakati wanafunzi wapya wengi wakipangiwa chini ya 100%.

=======================

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (PAC) imebaini utoaji wa mikopo inayofikia Sh1.76 bilioni kwa wanafunzi wasiostahili katika kipindi cha kati ya mwaka 2016 hadi mwaka 2018.

Hayo yamesemwa leo Jumanne Novemba 2, 2022 na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Japhet Hasunga wakati akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo kuhusu ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka unaoishia Juni 30, 2021.

Amesema mikopo hiyo ilitolewa kati ya mwaka 2016 hadi 2018 kwa wanafunzi ambao hawakuwa kwenye vyuo vya elimu ya juu lakini walipewa mikopo kwa maelekezo ya Serikali

Amesema uchambuzi wa taarifa ufanisi kuhusu upangaji na ugawaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kumeonekana uwepo wa maboresho makubwa katika taratibu za utoaji wa mikopo na ongezeko la idadi ya wanufaika wa mikopo husika.

Amesema pia kumekuwa na ongezeko la wanufaika wa mikopo kutoka 116,706 (2016/2017) hadi 149,389 (2020/2021). Alisema upangaji wa mikopo usiotosheleza kwa wanafunzi wapya ambapo Bodi haikuweza kutoa mikopo kwa asilimia 100 kwa waombaji waliostahili.

Alisema walibaini pia waombaji kupangiwa ada chini ya kiwango na zaidi ya kiwango cha ada stahiki na kwamba mwaka 2018/2019 wanafunzi 6,182 walipangiwa mikopo zaidi ya kiwango kwa kiasi cha Sh5.66 bilioni.

Alisema wanafunzi 2,852 walipangiwa mikopo chini ya kiwango kwa upungufu wa Sh1.14 bilioni na upangaji wa mikopo inayofikia Sh 2.25bilioni kwa waombaji wasiokuwa na uhitaji.

“Kutowapangia mikopo wanafunzi wanaostahili kupata mikopo na usimamizi hafifu wa bakaa na fedha za wanafunzi wanaohama vyuo na uhamasishaji duni wa vyanzo vingine vya fedha kwa ajili ya mpango wa mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu,” amesema.

MWANANCHI
Kwani watetezi wa Rais wa Wanyonge wao wanasemaje?
 
Tatizo la Tanzania ni Usiri na Unafiki...
Rais mpya alitakiwa atueleze Ripoti ya CAG baada ya kifo cha JPM

Aunde kamati huru kuchunguza kilichotokea kwenye ile Tril 1.5
 
Ukaguzi uliofanywa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) umebaini HESLB iliwapa Mikopo Wanafunzi ambao hawakuwa Vyuo Vikuu kwa maelekezo ya Serikali.

Pia, PAC imesema kati ya 2018/19 wanafunzi 2,852 walipangiwa mikopo chini ya kiwango kwa upungufu wa Tsh. Bilioni 1.14 huku Tsh. Bilioni 2.25 zikilipwa kwa wasiokuwa na uhitaji.

Aidha wanafunzi 6,182 walipangiwa mikopo zaidi ya kiwango kwa kiasi cha Tsh. Bilioni 5.66 wakati wanafunzi wapya wengi wakipangiwa chini ya 100%.

=======================

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (PAC) imebaini utoaji wa mikopo inayofikia Sh1.76 bilioni kwa wanafunzi wasiostahili katika kipindi cha kati ya mwaka 2016 hadi mwaka 2018.

Hayo yamesemwa leo Jumanne Novemba 2, 2022 na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Japhet Hasunga wakati akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo kuhusu ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka unaoishia Juni 30, 2021.

Amesema mikopo hiyo ilitolewa kati ya mwaka 2016 hadi 2018 kwa wanafunzi ambao hawakuwa kwenye vyuo vya elimu ya juu lakini walipewa mikopo kwa maelekezo ya Serikali

Amesema uchambuzi wa taarifa ufanisi kuhusu upangaji na ugawaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kumeonekana uwepo wa maboresho makubwa katika taratibu za utoaji wa mikopo na ongezeko la idadi ya wanufaika wa mikopo husika.

Amesema pia kumekuwa na ongezeko la wanufaika wa mikopo kutoka 116,706 (2016/2017) hadi 149,389 (2020/2021). Alisema upangaji wa mikopo usiotosheleza kwa wanafunzi wapya ambapo Bodi haikuweza kutoa mikopo kwa asilimia 100 kwa waombaji waliostahili.

Alisema walibaini pia waombaji kupangiwa ada chini ya kiwango na zaidi ya kiwango cha ada stahiki na kwamba mwaka 2018/2019 wanafunzi 6,182 walipangiwa mikopo zaidi ya kiwango kwa kiasi cha Sh5.66 bilioni.

Alisema wanafunzi 2,852 walipangiwa mikopo chini ya kiwango kwa upungufu wa Sh1.14 bilioni na upangaji wa mikopo inayofikia Sh 2.25bilioni kwa waombaji wasiokuwa na uhitaji.

“Kutowapangia mikopo wanafunzi wanaostahili kupata mikopo na usimamizi hafifu wa bakaa na fedha za wanafunzi wanaohama vyuo na uhamasishaji duni wa vyanzo vingine vya fedha kwa ajili ya mpango wa mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu,” amesema.

MWANANCHI
Huu ujinga wa Serikali ya Samia kujificha kwenye kivuli cha Serikali ya Magufuli sijui utakwisha lini, Magufuli amekaa hapa zaidi ya miaka 6, hatukuwahi kusikia wanafunzi wakilalamika fedha kuchelewa wala kukosa kwa waliokidhi vigezo fedha zilienda kwa wakati mpaka wakati wa Covid,ampapo Uchumi wa nchi haukuwa mzuri, Sasahivi wakati wa Samia wanafunzi wanalalamika kukosa mikopo tena kwa uwiano, Maana mtoto wa masikini anapata % ndogo wa vigogo wanapata 100%, kamati uchwala zinaleta mambo ya 2016,Kwaiyo ela ya 2016 ndizo zimesababisha wanafunzi hawa kutopata mikopo yao wakati wamekidhi vigezo?Mkitaka kumchafua Magufuli haonekane hakufanya chochote,fanyeni zaidi yake, Sio kutafuta madhaifu ya Magufuli.
 
Huu ujinga wa Serikali ya Samia kujificha kwenye kivuli cha Serikali ya Magufuli sijui utakwisha lini, Magufuli amekaa hapa zaidi ya miaka 6, hatukuwahi kusikia wanafunzi wakilalamika fedha kuchelewa wala kukosa kwa waliokidhi vigezo fedha zilienda kwa wakati mpaka wakati wa Covid,ampapo Uchumi wa nchi haukuwa mzuri, Sasahivi wakati wa Samia wanafunzi wanalalamika kukosa mikopo tena kwa uwiano, Maana mtoto wa masikini anapata % ndogo wa vigogo wanapata 100%, kamati uchwala zinaleta mambo ya 2016,Kwaiyo ela ya 2016 ndizo zimesababisha wanafunzi hawa kutopata mikopo yao wakati wamekidhi vigezo?Mkitaka kumchafua Magufuli haonekane hakufanya chochote,fanyeni zaidi yake, Sio kutafuta madhaifu ya Magufuli.
Upende usipende Magufuli alikuwa mpigaji ile mbaya! Heri aliondoka vinginevyo ingekuwa majanga!
 
Huu ujinga wa Serikali ya Samia kujificha kwenye kivuli cha Serikali ya Magufuli sijui utakwisha lini, Magufuli amekaa hapa zaidi ya miaka 6, hatukuwahi kusikia wanafunzi wakilalamika fedha kuchelewa wala kukosa kwa waliokidhi vigezo fedha zilienda kwa wakati mpaka wakati wa Covid,ampapo Uchumi wa nchi haukuwa mzuri, Sasahivi wakati wa Samia wanafunzi wanalalamika kukosa mikopo tena kwa uwiano, Maana mtoto wa masikini anapata % ndogo wa vigogo wanapata 100%, kamati uchwala zinaleta mambo ya 2016,Kwaiyo ela ya 2016 ndizo zimesababisha wanafunzi hawa kutopata mikopo yao wakati wamekidhi vigezo?Mkitaka kumchafua Magufuli haonekane hakufanya chochote,fanyeni zaidi yake, Sio kutafuta madhaifu ya Magufuli.
Magufuli alikua mabutu wa tanzania, hizo hela alichukua pamoja na plea burgain na za akaunti za watu bureau de change na kupeleka chato, mwivi,muuaji mkubwa yule
 
Upende usipende Magufuli alikuwa mpigaji ile mbaya! Heri aliondoka vinginevyo ingekuwa majanga!
Alikuwa mpigaji sawa kwamujibu wa mawazo yako, Siwezi kukubishia, Sasahivi hawa ambao sio wapigaji mbona kila kitu kimesimama?kama kwa miaka 6 hatukuwahi kusikia wanafunzi wakilalamika fedha kuchelewa,leo huyu ndio mwaka matatizo kila secta,ukienda hospital madawa amna kwenye almashauli wizi huko usipime,maji/umeme tabu, Wakati wa Magufuli hayo mambo yalisahaulika kabisa, alafu mnasema alikuwa mpigaji,Samia ahache kutumia kujificha kwenye kivuli cha Magufuli tunaita kuona matokeo, Sio kuunda vikamati uchwala kuanza kutafuta report za 2016, Wakati Sasahivi ni 2023 uongo uo hautamsaidi.Watanganyika hatudanganyiki kilaisi hivyo.
 
Any mentally sound person will take this report with a grain of salt. A senile person will believe it outright.
Mnachofanya baadhi ya watumishi waliopo serikali hii mnamchafua Mh.Samia kwamba hawezi kuongoza anatumia mbinu za kumchafua mtangulizi wake kama sehemu ya kuficha mapungufu yake ya uongozi kitu ambacho si kweli. Hajawatuma.

Sasa kukomesha tabia hii tunaomba watendaji wa wizarani na bodi ya mikopo walio husika kutoa mikopo kwa wasio stahili washitakiwe na kupewa adhabu kali ikithibitika wametenda kosa kisheria. Kama hafungwi mtu tutajua huu ni uongo na unafiki.
Akifungwa mtu pia tunataka majibu Mh.Samia na Waziri mkuu kwanini wasiwajibike wakati walikuwepo kwenye mamlaka za juu zilizo ruhusu pesa hizo zitolewe kimakosa?
 
Alikuwa mpigaji sawa kwamujibu wa mawazo yako, Siwezi kukubishia, Sasahivi hawa ambao sio wapigaji mbona kila kitu kimesimama?kama kwa miaka 6 hatukuwahi kusikia wanafunzi wakilalamika fedha kuchelewa,leo huyu ndio mwaka matatizo kila secta,ukienda hospital madawa amna kwenye almashauli wizi huko usipime,maji/umeme tabu, Wakati wa Magufuli hayo mambo yalisahaulika kabisa, alafu mnasema alikuwa mpigaji,Samia ahache kutumia kujificha kwenye kivuli cha Magufuli tunaita kuona matokeo, Sio kuunda vikamati uchwala kuanza kutafuta report za 2016, Wakati Sasahivi ni 2023 uongo uo hautamsaidi.Watanganyika hatudanganyiki kilaisi hivyo.
Ulikuwa unaishi wapi wakati wa Magufuli? Sasa kwa kukumbusha wakati huo vilio vilikuwa kila mahali, wananchi, wafanyakazi wa umma, wafanyabiashara wote walikuwa hoi. Silaha yake ilikuwa kuua au kukufunga ikiwa utaonekana unadadisi serikali yake hivyo watu wakabaki kusifia tu.

Fedha za mikopo zimepigwa sana enzi zake kwa manufaa yake binafsi!
 
Hapa ukiomba maelezo ya kina utagundua pesa hazikutoka kwa makosa wala hazikuliwa kiufisadi bali kuna mchezo wa kutumia maneno kiufundi ili kuwachafua watu watumike kama mbuzi wa kafara kuficha tatizo la watu wanao stahili mikopo kukosa mikopo mwaka huu 2022/2023. Watu wanajaribu kuzima mjadala huu wa kukosa mikopo kwa majibu mepesi.
 
Ulikuwa unaishi wapi wakati wa Magufuli? Sasa kwa kukumbusha wakati huo vilio vilikuwa kila mahali, wananchi, wafanyakazi wa umma, wafanyabiashara wote walikuwa hoi. Silaha yake ilikuwa kuua au kukufunga ikiwa utaonekana unadadisi serikali yake hivyo watu wakabaki kusifia tu.

Fedha za mikopo zimepigwa sana enzi zake kwa manufaa yake binafsi!
Wewe ilikuwa na cheti feki au fisadi, maana hao ndio waliopata tabu enzi za Magufuli,akina Mo walitangazwa bilionea kijana enzi za Magufuli,Bakresa hatukuona akiyumba wakati wa Magufuli tena enzi za Magufuli ndipo Tanzania ilikuwa na mamilionea wengi kupita Kenya tafuta riport zimo humu,labda wafanyabiara na Wafanyakazi wajanjawanja wazembe na wakwepa kodi ndio walipata shida enzi za Magufuli.
 
Wewe ilikuwa na cheti feki au fisadi, maana hao ndio waliopata tabu enzi za Magufuli,akina Mo walitangazwa bilionea kijana enzi za Magufuli,Bakresa hatukuona akiyumba wakati wa Magufuli tena enzi za Magufuli ndipo Tanzania ilikuwa na mamilionea wengi kupita Kenya tafuta riport zimo humu,labda wafanyabiara na Wafanyakazi wajanjawanja wazembe na wakwepa kodi ndio walipata shida enzi za Magufuli.
Mo alitekwa na kupelekwa kusikojulikana kwa siku tatu enzi za Magufuli! Mo hana hamu na Magufuli. Viroba vya watu waliouawa vilipatikana majini enzi za huyo mwehu Magufuli! Fedha 1.5 trilion zilitokomea kusikojulikana enzi zake. PhD fake alipata akiwa madarakani kwa kulazimisha UDSM. Mambo ni mengi ya kifisadi aliyafanya kwa vitisho!

Huyo ndiye Magufuli tunayemfahamu!
 
Back
Top Bottom